RC Makonda: Watu wanafunga maduka, wanajifungia majumbani kisa Corona, mtakufa na njaa

RC Makonda: Watu wanafunga maduka, wanajifungia majumbani kisa Corona, mtakufa na njaa

Na ole wako uropoke eti nyumba fulani kuna mgonjwa wa Corona au amekufa kwa Corona kama utaona Makonda akikutetea mbele ya shtaka la kutoa taarifa za uchochezi.
 
Mh tumekusikia waswahili wanamsemo...akili zakuambiwa changanya na zako...ndio tumechanya akili tayari na majibu umeyaona katika ziara uliyofanya tukirejea taarifa za mataifa mengine wanachofanya siamini watakuwa hawakuliona ulilotamka hususan nchi za dunia ya tatu tusicheze kamali na maisha kama mfanya biashara au taasisi imeamua kufunga shughuli zake kwa mda usilazimishe/shawishi jambo zito liwe jepesi...
 
Wakati wa vita kuna kitu kinaitwa commanding post ambapo mashambuliz na mipango yote hufanyika.
Corona ni vita,commanding post imeshatangazwa.Ni wajibu wetu wote tufuate maagizo toka commanding post.
Tuombe Mungu,sijui itakuwaje tukifikiwa na hali kama ya Italy,Allah aepushie mbali!!
NANI? Bashite? Huyo ni chui waliemlea wenyewe. Hao wote pamoja na mkubwa wao anaelalalala kwenye mawe, sasa wanamwogopa.
 
Tanzania wananchi wanajifungia ndani lakin Serikal inawahamasisha watoke Nje wafanye kazi

Kwingineko Duniani Wananchi wanataka kutoka nje kuchapa kazi Serikal zao zinawazuia kwa hofu ya Corona

Maana yake Wananchi wa TZ ni waoga na wavivu wakati Serikal yao ni ya kijasiri na kichapa kazi

Kwingineko Serikal zao za kivivu na kioga wakati wanancho wao ni wachapakazi na majasiri



Sent using Jamii Forums mobile app

..walioamua kuchukua tahadhari za ZIADA wasilaumiwe au kusumbuliwa.

..kwa mfano, mtu aliyefunga duka lake kwa kuogopa Corona, hana athari, au hatishii afya za wengine. Hakuna haja ya kumsumbua mtu aliyechukua tahadhari hizo.

..wanaotakiwa kuandamwa ni wale wasiochukua tahadhari kabisa.

..Kwa mfano, wafanya biashara wasioweka maji ya kunawa, au sanitizer, ktk maeneo yao ya biashara. Au wenye daladala wanaojaza abiria kupita kiasi.

..Serikali inatakiwa kushughulika na wale wasiochukua tahadhari, na siyo kuandama wanaochukua tahadhari za ziada.
 
"Tokeni kafanyeni kazi eti Watu wanafunga maduka, wanajifungia majumbani kisa Corona, mtakufa na njaa, ndio maana leo nawafuatilia wakandarasi, sasa nimkute mkandaraai hayupo site kisa corona, kuna wapuuzi huko wanasema Serikali inadanganya idadi imeongezeka, kwenu kuna Mtu amekufa na corona?, kuna Mtu kwenu anaumwa corona?, hiyo idadi imetoka wapi?" - Paul Makonda, RC DSM

Good work our focused leader

======

Wananchi wanaingia hasara kwa kukwepa majukumu yao huku mambo yakienda tofauti wanaanza kuilalamikia serikali ili iweze kupatia msaada.

Amesema hayo leo mkuu wa mkoa wa Dar es Salaaam Mh Paul Makonda wakati akikagua mradi wa TARURA katika eneo la Kinondoni shamba ambapo kumekuwa na mgogoro baina ya TARURA na wananchi wa eneo hilo.

Pia amewataka wananchi kuacha kujifanya wajuaji wakati tatizo linapokuwa kubwa kwasababu wakati watu wanaingia katika eneo la mradi ambalo hawatakiwi kuvamia.

Vilevile amewataka wananchi kufanya kazi huku wakichukua tahadhari ya ugonjwa wa Corona wasikae ndani watafute hela ili wasije wakafa na njaa.

“Tokeni ndani mkafanye kazi Corona isiwe kigezo cha kujifungia ndani tumepambana na magonjwa mengi ikiwemo kipindupindu na magonjwa mengine tufanye kazi huku tukichukua tahadhari’amesema Makonda.

Aidha Makonda amekukagua miradi ya barabara inayotekelezwa na TARURA katika wilaya ya Ilala na Kinondoni kujua maendeleo ya miradi hiyo.

“Barabara ni ahadi ya muda mrefu ya Mh Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli ijengwe kutoka makao makuu wa Bakwata hadi Biafra”amesema Makonda.

Hatahivyo amepokea taarifa ya mgogoro kutoka kwa wananchi wa eneo lile kwa kutaka kuvunjiwa nyumba zao bila kupata fidia na walio lipwa wapo na hawajipotiwa na barabara hiyo.

Aidha amewataka wananchi kuwa atatuma kamati yake ifanye ukaguzi na wataanza jumatatu ili walete majibu kamili ili mradi huo uende kwa haraka.


Sent using Jamii Forums mobile app

Makonda ni mmoja ya viongozi bora wa awamu hii.
 
Mkuu wa mkoa wa Dar Makonda amewashangaa wananchi kujifungia ndani kisa Corona.

Makonda amesema watu watoke wakafanye kazi taratibu za kujikinga na corona ziko wazi, hivyo kujifungia ndani kisa Corona ni uzembe.

Amewashangaa wafanyabiara kufunga maduka kisa Corona.

Pia ameonya wanaosambaza habari kuwa kuna wagonjwa wengi ila wanafichwa, amehoji kwenye familia yako kuna mtu anaumwa corona ama amekufa na corona serikali imeficha.

NB. Kwa hizi kauli za viongozi ikitokea Corona ikatupiga sawasawa sidhani kama kuna Taifa litatia mguu kutusaidia.

Hata kama serikali ina msimamo wake kuhusu hili wangefanya kimya kimya, kutangaza hadharani hivi ni hatari kwa mstakabali wa Taifa letu.




Bwashee kodi isipolipwa mishahara na marupurupu ya watumishi wa umma utalipa wewe?!

Kama hukubaliani na data za serikali basi tuletee ushahidi!
 
Bwashee kodi isipolipwa mishahara na marupurupu ya watumishi wa umma utalipa wewe?!

Kama hukubaliani na data za serikali basi tuletee ushahidi!

..hivi nchi hii haina AKIBA?

..so far tumepata wagonjwa 20 tu, na wananchi bado wako makazini na biashara ziko wazi, kwanini tunatishana kwamba serikali itashindwa kulipa mishahara?
 
Tanzania wananchi wanajifungia ndani lakin Serikal inawahamasisha watoke Nje wafanye kazi

Kwingineko Duniani Wananchi wanataka kutoka nje kuchapa kazi Serikal zao zinawazuia kwa hofu ya Corona

Maana yake Wananchi wa TZ ni waoga na wavivu wakati Serikal yao ni ya kijasiri na kichapa kazi

Kwingineko Serikal zao za kivivu na kioga wakati wanancho wao ni wachapakazi na majasiri



Sent using Jamii Forums mobile app
Hii ni komenti yangu bora ya mwezi!
 
Naunga mkono hoja watu wanaweka siasa kila mahala ooo serikali inadanganya wao watuambie wameshakutana na wagonjwa wa covid-19 wangapi.
 
Na ole wako uropoke eti nyumba fulani kuna mgonjwa wa Corona au amekufa kwa Corona kama utaona Makonda akikutetea mbele ya shtaka la kutoa taarifa za uchochezi.
Jitoe muhanga kusaidia wengine kama yule daktari wa China.
 
Oooh namlaani Makonda, asifanye siasa! kiko wapi? ndiyo kwaanza anakagua miradi, laani zina warudia
 
Back
Top Bottom