Regional Per Capita GDP: Hii ndio Mikoa 7 ambayo Wananchi wake wana kipato cha Uchumi wa kati Tanzania Bara

Regional Per Capita GDP: Hii ndio Mikoa 7 ambayo Wananchi wake wana kipato cha Uchumi wa kati Tanzania Bara

Mnazo ila mumeshindwa kuzitumia kwenye mazingira yenu na kuinua maisha yenu na ya Mkoa na nchi kiujumla.Kiifupi nyie ni chawa
Wahaya wengi wanathamini kuajiriwa kuliko kufanya biashara ndio maana unaona mkazo wao kwenye 'kukusanya' vyeti uko juu sana.

Mentality hiyo imewadumaza sana, ndizi wanalima wao vijana wanatoka Tabora, Shinyanga, Singida hadi Dom wananunua kwa bei chee wqnaenda kupiga hela. Wao na elimu zao hata kusaka wapi soko zuri lipo hawawezi.
 
Swala sio watawala ni tu watanzania wengi vichwa vibovu kikiwemo chako

Japan haina raslimali yeyote na ni tajiri hasa sababu private sekta watu wana akili sana

Fikiria familia moja ya TOYOTA inajaza magari Tanzania nzima kila uendapo unakutana na TOYOTA

Wewe na familia yako cha maana mlichogundua na kuzalisha ni nini?
Japan haina rasilimali?
Coal, iron ore, zinc, lead, copper, sulfur,gold, and silver are among the most abundant minerals (in relative terms), with lesser quantities of tungsten, chromite, and manganese. Japan also has large deposits of limestone.

Huwa sipendi kujadili mambo na empty headed kama wewe.
 
Kumbuka hii kitu inahusisha GDP against population sasa hili la mzunguko wa pesa halina mashika hapa.Inawezekana watu wa mijini wakawa na pesa kuliko wengi wa vijijini.

Maisha ya watu wa Nyanda za juu hayategemei maeneo machache ya mijini kama ilivyo kanda ya ziwa.Kwa mfano halmashauri za Iringa na Mbeya unakuta zote zina mapato zaidi ya 3.5b wakati kwa Mikoa ya kanda ya ziwa ni miji ichache ina makusanyo makubwa wakati sehemu zingine hakuna kitu.

Hizi ni takwimu sahihi na mara kadhaa imeripotiwa kanda ya ziwa kuwa na idadi kubwa ya maskini kulinganisha na mnachozalisha na kasi kubwa ya kuzaana inayosababishwa na utamaduni uliopitwa na wakati.Sasa kukubali au kutokubali halinihusu mimi unaweza fanya utafiti wako uka refute huu wa NBS.
mzee mimi ni mtu wa nyanda za juu kusini, lakini nimeishi pia kaskazini na kanda ya ziwa. chukua mfano mmoja tu KAHAMA na Geita, sijaelewa ni kwanini mapato yanakuwa machache, labda watu wa maeneo hayo hawatoi kodi/kodi au mapato yao hayakusanywi. ila tukiongelea kwenye ground, huwezi k ulinganisha umasikini wa iringa au njombe na Geita na shinyanga. wasukuma kule wanalima balaa kuliko hata mahindi yetu hayo, na kuna biashara sana kwasababu ya machimbo ya dhahabu. i understand only one thing, kwamba wanagawanya kwa idadi ya watu wa eneo hilo, jambo ambalo halitaleta jibu lenye uhalisia sasa kwenye maisha ya kawaida, ndio maana nasema mahesabu ya kwenye makaratasi ni tofauti na maisha halisi kwenye ground. sikubaliani kwamba watu wa huko wamekuwa masikini wakati wanamiliki mifugo mingi sana na nyanda za juu mnamiliki mahindi na viazi tu. wao wanalima mpunga na wana makundi makubwa ya ng'ombe. au hayo ninyi wachumi huwa hampimi?
 
Takwimu za nchi hii huwa siziamini hata kidogo maana most of them huwa ni za "kupika data".
Mkuu nilishiriki katika zoezi hili na tulikuwa tunachukua data za miaka 3 mwaka 2017,2018,2019 .
Kulikuww na questionnaires ambazo tulipita kwenye biashara tofauti tofauti kuanzia kwa muuza Nyanya mpaka kwwa makampuni makubwa ndani ya Mkoa.

Kuna vigezo vingi sana vinatumika,lakini kikubwa na uwezo wa Wananchi wa Mikoa husika kushiriki katika uzalishaji Mali ikiwemo uwezo wa ukopaji wa mitaji na urejeshaji kutoka taasisi za kifedha.

Mfano takwimu za mwaka 2018,Kilimanjaro na Njombe zilikuwa nafasi ya 2 na 3 lakini hizi za 2019 zipo nafasi ya 4 na 7 maana yake kila mwaka kuna mikoa watu wanaamka.

Hata hivyo Jaribu kusafiri wewe mwenye sehemu hizo utaona utofauti wa maisha ya watu.
 
mzee mimi ni mtu wa nyanda za juu kusini, lakini nimeishi pia kaskazini na kanda ya ziwa. chukua mfano mmoja tu KAHAMA na Geita, sijaelewa ni kwanini mapato yanakuwa machache, labda watu wa maeneo hayo hawatoi kodi/kodi au mapato yao hayakusanywi. ila tukiongelea kwenye ground, huwezi k ulinganisha umasikini wa iringa au njombe na Geita na shinyanga. wasukuma kule wanalima balaa kuliko hata mahindi yetu hayo, na kuna biashara sana kwasababu ya machimbo ya dhahabu. i understand only one thing, kwamba wanagawanya kwa idadi ya watu wa eneo hilo, jambo ambalo halitaleta jibu lenye uhalisia sasa kwenye maisha ya kawaida, ndio maana nasema mahesabu ya kwenye makaratasi ni tofauti na maisha halisi kwenye ground. sikubaliani kwamba watu wa huko wamekuwa masikini wakati wanamiliki mifugo mingi sana na nyanda za juu mnamiliki mahindi na viazi tu. wao wanalima mpunga na wana makundi makubwa ya ng'ombe. au hayo ninyi wachumi huwa hampimi?
Mkuu Kuwa na madini sio hoja ndio maana unaona Tz tuna Madini but bado ni masikini,Madini hayo yanachimbwa na Makampuni Makubwa hamna Mtanzania hata moja ana miliki mgodi mkubwa kama wa North Mara.

Hii maana yake ni kuwa revenue yote inayopatikana wankwenda kutumia wamiliki wa migodi hiyo ambayo wapo Nje ya Nchi.
 
mzee mimi ni mtu wa nyanda za juu kusini, lakini nimeishi pia kaskazini na kanda ya ziwa. chukua mfano mmoja tu KAHAMA na Geita, sijaelewa ni kwanini mapato yanakuwa machache, labda watu wa maeneo hayo hawatoi kodi/kodi au mapato yao hayakusanywi. ila tukiongelea kwenye ground, huwezi k ulinganisha umasikini wa iringa au njombe na Geita na shinyanga. wasukuma kule wanalima balaa kuliko hata mahindi yetu hayo, na kuna biashara sana kwasababu ya machimbo ya dhahabu. i understand only one thing, kwamba wanagawanya kwa idadi ya watu wa eneo hilo, jambo ambalo halitaleta jibu lenye uhalisia sasa kwenye maisha ya kawaida, ndio maana nasema mahesabu ya kwenye makaratasi ni tofauti na maisha halisi kwenye ground. sikubaliani kwamba watu wa huko wamekuwa masikini wakati wanamiliki mifugo mingi sana na nyanda za juu mnamiliki mahindi na viazi tu. wao wanalima mpunga na wana makundi makubwa ya ng'ombe. au hayo ninyi wachumi huwa hampimi?
Unavyoongea utadhani Nyanda za Juu hakuna hiyo mifugo,sasa kama hakuna viwanda vya kusindika maziwa vilivyojengwa Iringa,Njombe na Tukuyu hivi ni vikibwa vidogo vidogo kila sehemu unadhani vinaagiza maziwa kutoka huko usukumani au?

Unashangaza sijui huko Kanda ya ziwa kuna kilimo gani cha kuzidi Nyanda za Juu ambako kilimo ni asili.

Wewe utakuwa umekulia huko Dar basi na unaendaga kusalimia bibi zako Highlands na wakwe zako huko Kanda ya ziwa sasa unajifanya kujua kuliko watafiti.

Kwa taarifa yako huko usukumani hakuna malisho ya kutosha mifugo imehamia Katavi,Rukwa, Songwe,Mbeya, Morogoro,Kigoma nk nk

Kama hata hujui Nyanda za Juu wanalima Mazao gani makuu hutakiwi kubisha kitu ambacho huna ufahamu nacho
 
Wahaya wengi wanathamini kuajiriwa kuliko kufanya biashara ndio maana unaona mkazo wao kwenye 'kukusanya' vyeti uko juu sana.

Mentality hiyo imewadumaza sana, ndizi wanalima wao vijana wanatoka Tabora, Shinyanga, Singida hadi Dom wananunua kwa bei chee wqnaenda kupiga hela. Wao na elimu zao hata kusaka wapi soko zuri lipo hawawezi.
Yaani jamaa hao wanapenda kazi laini, nafikiri imechangiwa na historia yao ya siku hizo kua walikua wanakuwa na wapagazi kwa kazi zote nyumbani toka nchi jirani kwa kina waliowaita' washuti', sasa labda imepelekea kuwa wazito wa kuhangaika....ni maoni tu,na mie najaribu kuwa messenger tu kwa jinsi ninavyoona wala nisishambuliwe kwa mawe.....
 
Unavyoongea utadhani Nyanda za Juu hakuna hiyo mifugo,sasa kama hakuna viwanda vya kusindika maziwa vilivyojengwa Iringa,Njombe na Tukuyu hivi ni vikibwa vidogo vidogo kila sehemu unadhani vinaagiza maziwa kutoka huko usukumani au?

Unashangaza sijui huko Kanda ya ziwa kuna kilimo gani cha kuzidi Nyanda za Juu ambako kilimo ni asili.

Wewe utakuwa umekulia huko Dar basi na unaendaga kusalimia bibi zako Highlands na wakwe zako huko Kanda ya ziwa sasa unajifanya kujua kuliko watafiti.

Kwa taarifa yako huko usukumani hakuna malisho ya kutosha mifugo imehamia Katavi,Rukwa, Songwe,Mbeya, Morogoro,Kigoma nk nk

Kama hata hujui Nyanda za Juu wanalima Mazao gani makuu hutakiwi kubisha kitu ambacho huna ufahamu nacho
Mkuu kweli kabisa usemayo Kagera hasa karagwe Kuna ufugaji na maziwa Sana tu na nyama sana Lita moja ya maziwa leo hii 500/600 chá ajabu Hakuna viwanda vya kusindika maziwa pamoja na ujuaji wote kma ilivyo iringa ambako Sasa Kuna usindikaji kibao nmeona mama mmoja mnyarwanda anajenga benaco pale ngara but karagwe no
 
Nyanda za juu Kusini, ukiacha miji, ipo juu sana kuliko vijiji vya kanda ya ziwa kwa ubora wa maisha na maendeleo.

Usukumani wanafuga, lakini quality ya mifugo ni duni sana ukilinganisha na mifugo inayofugwa nyanda za juu. Kanda ya ziwa wanalima, lakini ni vishamba vidogo, na hawajui ukulima wa kisasa. Lakini pia kanda ya ziwa wanazaana sana, na familia nyingi ni duni. Sorry to say this - ukimpata mwanakijiji wa kanda ya ziwa ambaye hajasoma kabisa, na wa namna hiyo hiyo wa Nyanda za juu kusini, uelewa wao katika mambo mengi, ni mbingu na nchi. Kanda ya ziwa, mpaka leo hii, wapo watu ambao hawajui hata kusalimia tu, kwa Kiswahili.

Kuna wakati nilikuwa nakagua baadhi ya maeneo, wilayani Bukombe, tulikuwa tunatumia chopa, tukatua kijiji kimoja karibu sana na hifadhi ya Kigosi, kwenye programu hiyo ya siku 2 ilihusisha kuchukua sampuli, tukawachukua vibarua wa hapo kijijini, na wengine toka Ushirombo. Jioni baada ya kazi, walikuwa wakiongea mambo ya kawaida. Kukawa na mjadala wa kidini, kijana mmoja wa kisukuma, baada ya kusikiliza kwa muda mrefu, aliuliza, "huyo Yesu ina maana ni mkubwa kuliko Mwanamalunde?". Nilisoma habari za Mwanamalunde nikiwa shule ya msingi, nilicheka na kutafakari sana. Yule kijana, karne hii, hajui habari ya ukristo, wala uislam. Kwa kumjaribu tu, nilimwuliza kama anamjua Rais wa Tanzania (wakati ule alikuwa Kikwete), alinijibu, 'Unyerere".

Kanda ya ziwa, suala la elimu, hasa maeneo ya vijijini, achilia mbali elimu ya darasani, hata ile elimu tu ya mazingira wanayoyaishi, bado sana. Yapo maeneo, mpaka leo hii, mtu anajisikia ufahari kumiliki fisi wa kishirikina.

Umaskini wa Tanzania ni reflection ya kiwango cha elimu cha watu wa eneo husika.
 
Unavyoongea utadhani Nyanda za Juu hakuna hiyo mifugo,sasa kama hakuna viwanda vya kusindika maziwa vilivyojengwa Iringa,Njombe na Tukuyu hivi ni vikibwa vidogo vidogo kila sehemu unadhani vinaagiza maziwa kutoka huko usukumani au?

Unashangaza sijui huko Kanda ya ziwa kuna kilimo gani cha kuzidi Nyanda za Juu ambako kilimo ni asili.

Wewe utakuwa umekulia huko Dar basi na unaendaga kusalimia bibi zako Highlands na wakwe zako huko Kanda ya ziwa sasa unajifanya kujua kuliko watafiti.

Kwa taarifa yako huko usukumani hakuna malisho ya kutosha mifugo imehamia Katavi,Rukwa, Songwe,Mbeya, Morogoro,Kigoma nk nk

Kama hata hujui Nyanda za Juu wanalima Mazao gani makuu hutakiwi kubisha kitu ambacho huna ufahamu nacho
nyanda za juu kusini kuna mifugo gani mzee, zaidi ya nguruwe na misukule?
 
Back
Top Bottom