Rehma na amani ziwafikie Muhammad na Yesu Kristo

Rehma na amani ziwafikie Muhammad na Yesu Kristo

Ivi ukalibu ulioko baina ya MUNGU+MUHAMMAD+YESU+MARIA+ISLAEL+SAUDIA palikuwa panahitajika dua ya mtenda dhambi kama mimi ili kuweka Amani na Rehma katika huo ukalibu wao?.
 
Hebu tuiache Biblia itueleze:

Yesu akaondoka huko, akaenda kando pande za Tiro na Sidoni. Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo. Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu. Akajibu, akisema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Naye akaja akamsujudia, akisema, Bwana, unisaidie. akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani za bwana zao. Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile.

Mathayo 15.21-28

Kwa maneno yasiotatanisha Yesu Kristo anasema kuwa yeye hakutumwa ila kwa "kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli."

Hakuwajia Waarabu, wala Wazungu, wala Wahindi, wala Waafrika, wala Machina.

Kama hayo hayakutosha kuonyesha kuwa yeye hakuwajia wasio Mayahudi anazidi kufahamisha kwa mfano wa kumkata mtu kiu:

Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa."

Ikiwa ipo shaka yo yote katika akili ya mtu kuwa maana ya maneno hayo ni kuwa Yesu anasema kuwa hakutumwa kwa kabila nyengine zo zote ila Waisiraili tu na atazame mwenye shaka tafsiri kubwa kabisa ya Wakristo inayoeleza maana wazi maneno ya Biblia, The Interpreter's Bible, sahifa 441 jalada VII ambamo imeandikwa hivi:

"Yaonekana wazi kuwa Yesu hakika aliamini kuwa ujumbe wake kwanza na khasa ni kwa watu wake mwenyewe." Ndio maana alisema:

Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua.

Mathayo 7.6

Mbwa na nguruwe ni watu wa mataifa yasiyokuwa wana wa Israili. Ukristo haufai kufundishwa watu wo wote isipokuwa Mayahudi.
Soma YOHANA 10:16

Ujifunze acha kutukuza tamaduni za waarabu mtumish

YESU KRISTO anakupenda sana
 

Attachments

  • Screenshot_20241220-221210.png
    Screenshot_20241220-221210.png
    183.1 KB · Views: 4
Wasomi na watumishi wa dini hizi mbili yaani (Uislamu na njia ya Kristu), naomba jibu ya swali langu hili dogo tu,.

Kila linapotajwa jina la YESU au la MUHAMMAD
Huwa mnaongezea na maneno tena kwa unyenyekevu au kwa molali ya hali ya juu huwa mnasema

(REHMA NA AMANI ZIMFIKIE)
Swali langu kwa waislamu
Je, ni Amani gani mnayotaka Muhammad imfikie?
Je, ni Rehma gani hizo mnazomuombea Muhammad kwa Mungu ili ZIMFIKIE?
Na je ni nani huyo aliyetoa ilo agizo?
Yaani ni Muhammad mwenyewe akitaka kuombewa Rehma kutoka kwetu, au ni Mungu mwenyewe ndio anataka tuwaombee mitume yake mwenyewe?

Je kati ya Muhhammadi na sisi yupi wa kumuombea mwenzie REHMA na AMANI kwa Mungu.?

Ukisoma biblia na quran tukufu imetanabaisha kuwa
MUHAMMAD na YESU ni binadamu watakatifu na ni binadamu wasio wahi kutenda dhambi katika maisha yao yote ya duniani.
Maana yake ni watu wa peponi moja kwa moja.

Alafu hiki kipengele cha kuweka neno (REHMA NA AMANI ZIMFIKIE)
Je ni Muhammad mwenyewe kakiweka ili apate amani au ni Mungu ndie kaweka mumuombee amani kiongozi wenu maana hayuko kwenye amani, au mumeweka kwa utashi wenu kwa kuhisi hao viongozi wenu hawako kwenye amani?

Sasa kuna haja gani ya kuwaombea REHMA NA AMANI.?
Je huko waliko kwani wanahitaji Rehma au Amani?

Nawasilisha.,

Sio kwa ubaya wala kubeza nahitaji kupata tu elimu.

Yesu haitaji rehma na amani kutoka kwa mwanadamu. Labda huyo aliyeko huko tusipopatamani kufika!
 
[emoji28]
Sio unacheka jaribu kufikiria hata kwa akili yako ndogo.

Juzi nimeona waumini wa dini kadhaa zikiombea amani saudia na wengine ISLAEL ivi ni kweli akili zetu zina akili.
Yaani mimi wa kumuombea mtoto wa mama samia ela kwa mama ake kweli?
 
Yesu haitaji rehma na amani kutoka kwa mwanadamu. Labda huyo aliyeko huko tusipopatamani kufika!
Sio kweli. Kuna dua huwa mnamuombea yesu na mama yake baraka jaribu kuuzulia kanisani. Pia hata yesu mwenyewe aliomba tumuombee kwa baba yake juu ya kile kikombe
 
Mwenye dhambi huombewa msamaha si rehma
Sasa Muhhammadi namuombeaje msamaha kutoka kwa Mungu wakati simu ya kiama ile wakati wa jua kali Muhammad yeye anakaa kivulini na Mungu ?
 
Ewaaa ni Mungu mwenyewe katuambia tumtakie rehma, na yeye Hadi mitume wengine tunawatakia rehma Hadi masahaba nao wanatakiwa rehma
Ivi sisi na mitume nani alipaswa kumuombea mwenzie kwa Mungu? Nani aliye kalibu zaidi na Mungu
 
Yesu haombewi amani.
yeye ndiye mtoa amani.

Yohana (Joh) 14:27
Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo.
Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.
Peace I leave with you, my peace I give unto you: not as the world giveth, give I unto you. Let not your heart be troubled, neither let it be afraid.
 
Yaani niache kujiombea mimi mwenyewe Rehma niache kuombea kizazi changu nianze kuombea na mitume Rehma hayo ni matumizi mabaya ya kuomba.

Mfano musa alikuwa anaongea na Mungu moja kwa moja sasa ashindwe kumuomba Mungu mwenyewe nimuombee mimi, Muhammad alikuwa analetewa wajihi na Mungu moja kwa moja si ndio palikuwa pahala pa kuomba hapo nije niombe mimi na pombe yangu kichwani?
 
Yesu haombewi amani.
yeye ndiye mtoa amani.

Yohana (Joh) 14:27
Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo.
Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.
Peace I leave with you, my peace I give unto you: not as the world giveth, give I unto you. Let not your heart be troubled, neither let it be afraid.
Tatizo lako huendi kanisani.

Kanisani tunaanza kuwaombea wana wa Israel tunafata Maria tunamalizia na yesu mwenyewe.

Pia hatuishii hapo na bado tunafanya happy birth day ya (YESU, MARIA, NA MUHHAMMADI (inaitwa mauridi.

Yaani akili zetu sijui zimekwama wapi?
 
Ivi sisi na mitume nani alipaswa kumuombea mwenzie kwa Mungu? Nani aliye kalibu zaidi na Mungu
Yeye kashatuombea Kwa Mungu Alituombea Mungu asishushe Tena gharika dhidi yetu Kama ilivyokuwa Kwa MANABII wa mwanzo, hivyo ukitenda dhambi unasubiriwa mpaka siku ya mwisho.
Alituombea tusamehewe dhambi muda wote mpaka siku ya umauti ukiweza tunaomba mshamaha.

Kumbuka mtume ni binadamu Mungu kafanya hivyo ili kumpunguza ego asijekujiona yeye ni Mkubwa na kujawa na kiburi akati tofauti yake na sisi ni cheo TU Cha utume.

Ndio maana ishu ya Yesu itamgarimu maswali siku ya mwisho Kwa kua wafuasi wake walimwita Mungu. Hivyo itambidi ajieleze mbele ya Mola wake kiushahidi na kuwakana waliomwita hivyo kwa ushahidi wa maandiko
 
Yeye aeleze mbele ya Mola wake kiushahidi na kuwakana waliomwita hivyo kwa ushahidi wa maandiko
Kwani Mungu si anayajua hata yaliyo mioyoni mwetu? Kwanini atataka na ushahidi?
 
Tatizo lako huendi kanisani.

Kanisani tunaanza kuwaombea wana wa Israel tunafata Maria tunamalizia na yesu mwenyewe.

Pia hatuishii hapo na bado tunafanya happy birth day ya (YESU, MARIA, NA MUHHAMMADI (inaitwa mauridi.

Yaani akili zetu sijui zimekwama wapi?
ndio kanisa lako linavyofanya ?
linaitwaje ?
mimi umenijulia wapi hadi unisemee wewe?
 
Back
Top Bottom