Rekodi yangu bora kimasomo haijaniwezesha kupata ajira. Naathirika Kisaikolojia

Rekodi yangu bora kimasomo haijaniwezesha kupata ajira. Naathirika Kisaikolojia

Kitu kama hicho rafiki, wekapo miaka 7 kabla ya s/msing na miaka 7 baada ya s/m hapo aseme anaelekea 40yrs.

Halafu wakat anamalza chuo nna uhakika kwa kiwango chake cha ufaulu na rekod yake tangu s/m, migod mikubwa kama GGM na Buzwag wangekua washa mgongea/ kumwekea oda kabla hata hajamaliza chuo labda kama fields zake alikua anazifanyia kwenye tumigod tudogo tudogo coz najua walokua wanapga fd migod mikubwa na wakaonyesha uwezo mkubwa walikua wanakua booked mapema sana.

Kitu kimoja tuwekane sawa hapa, practical sio theory na theory sio practcal so unaweza kua mzuri kwenye makaratas halafu ukawa wa hovyo unapopewa mashine ufanye kaz.

Ushauri, kuna watu hawana hata chet cha la7 ila n wakemia migod midogo ya uchenjuaji madn (dhahabu) maarufu kana migod ya kuozesha (vat reaching plants) nenda kajifunze hyo fan for free kikubwa uwe na hela yako ya kula wskat wa mafunzo. Migod mingine mtu kama wewe unaweza kwenda kujfunza ni elution plants na sp plants.

Geology mnasoma miamba halafu unakua na njaa kweli?? Kwahyo hujui jinsi ya kuipata miamba ya dhahabu eti? Au umesomea miamba ya chumvi? Tafta mashine za kufanyia survey ya miamba (we unajua mnafanyaje) ukipata hyo mashine nenda machakani huko katafte miamba ukiipata nenda ofis za madini omba resen ya kuchimba umiliki claim (kilempu, kwa kibongo bongo). Then tafta mtu mwenye mtaji mkachimbe hizo dhahabu. Kumbuka uki claim eneo hata la kituo cha afya au police unaweza kuwalipa wenye eneo wakahama we ukapiga kaz kama huwez kuwalipa bas mtagawana dhahabu. NB NB NB Vipimio vya miamba vipo had vya laki na nusu
Bila shaka we ni mchimbaji mdogo. Ama la umekaa sana na wachimbaji wadogo. Yoote uliyoyaongea, kwakuwaza tuu yanawezekana yote. Ukiyaingiza katika uhalisia huambulii hata moja.
 
Wew msomi ama mpumbavu yaani kusoma kote huko hukutambua lengo la elimu ya kiafrika ni kuwafunza raia kusoma&kuandika then wajiendeleze wenyewe ktk kazi za mikono? Na baadhi yao kwa uchache wanachukuliwa kama cheap labour/wafanyakazi wa serikali ktk secta mbalimbali.

Nyie wasomi wa kukalili mambo mtaendelea kusota na maisha mpka mtakapogundua lengo la elimu si kukupa maisha mazuri wala kukupa ajira, bali kukupa mwanga wa wewe kupambana na changamoto ktk mazingira.

Hakuna ajira muelewe na mtambue kuwa serikali haiwezi kumfuraisha kila mtu, matokeo yako darasani hayakupi uhalali wa maisha mazuri wala kupredict future yako, bali maono yako na kujituma kwako ktk shughuli za uzalishaji&biashara&sanaa.

Narudia tena, enyi wasomi vilaza muelewe kuwa, lengo la elimu hasa ya kibongo, si kukupa maisha bora wala si jukumu la serikali kukupa maisha bora, hilo ni jukumu la mzazi wako na wewe mwenyewe.

Shule tulienda kujifunza vitu vichache vitusaidie kuyaelewa mazingira&namna ya kuwasiliana na jamii , na kwa wachache sana kuwafanya wajakazi wa kuwatumikia raia wengine ktk nyanja mbalimbali.

Mtaisoma namba, mlidhani kufaulu darasani ni tiketi ya kufaulu maisha? Wake up and change your mind, dunia haina huruma, acha kujilizaliza na kutaka huruma hapa, ukweli mchungu, rudi mtaani tafuta uhalisia wako wa maisha yako utaukuta huko, uzuri wa mtaa njoo na akili zako tu, ujuzi utaukuta huku huku.

Shame on you.
 
Ndiyo maana mi mtoto wangu nimempangia asome mwisho form 4 then peleka SUA akasomee KILIMO NA UFUGAJI then akiwa anaingia Degree namuanzishia duka la pembejeo akimaliza nauza viwanja viwili namfundisha kufuata madawa ya mifugo na shambani KENYA NA CHINA likiwa pumbafu shauri lake nahamia kwa mdogo ake.
KAMA UMEPENDA HUU MPANGO WANGU GONGA LIKE TWENDE WOTE
Safi
 
Ndiyo maana mi mtoto wangu nimempangia asome mwisho form 4 then peleka SUA akasomee KILIMO NA UFUGAJI then akiwa anaingia Degree namuanzishia duka la pembejeo akimaliza nauza viwanja viwili namfundisha kufuata madawa ya mifugo na shambani KENYA NA CHINA likiwa pumbafu shauri lake nahamia kwa mdogo ake.
KAMA UMEPENDA HUU MPANGO WANGU GONGA LIKE TWENDE WOTE
Watu bado hawajatambua kuwa zama zimebadirika, inashangaza msomi wa marks nzuri nayeye analialia ajira ngumu, mtu huyu kama aliweza kuelewa michezo ya darasani alishindwa vipi kuusoma mchezo wa maisha ya uhalisia kuwa mahitaji ya waajiriwa yanahitajika kwa watu wa Elimu ipi, nafasi ipi, na secta zipi zilizo na magape ya kutoa ajira&mahitaji ya taifa ni yapi?

Vijana wengi wakishafanikiwa kufaulu vizuri basi hata hawafikilii tena mambo ya baadae wao wanabeti maisha kuwa chochote atakachokisomea ilimladi kafaulu basi atatoboa na yalivyo majinga yanachagua zile course ngumu zenye majina ya kutisha, kumbe deep down yanajikomoa yenyewe.

Wasomi wetu bado hawajui kuusoma mchezo wa maisha unaenda vipi, wao wanaishi kwa kubeti na kutegemea bahati
 
Habari wana jukwaa. Kwa kweli hivi sasa bila connection ni ngumu kupata kazi, vinginevyo Mungu aingilie kati. Binafsi kwa neema ya M/Mungu nimefanikiwa kuwa nahistoria ya kufanya vizuri darasani, na kuwa mwanafunzi bora kuanzia nilipokuwa shule ya msingi mpaka chuo kikuu. Historia yangu kwa ufupi ipo hivi.

Primary

Ufaulu mzuri nikapangiwa kwenda sekondari, japo ni ya kata, wakati huu ndo shule za kata zimeanzishwa kwa wingi, hivyo hata wenye ufaulu mzuri walipelekwa shule hizi ili kufidia gap la wanafunzi

Sekondari

Nilifanya vizuri sana. Nimekuwa mwanafunzi namba moja darasani tangu kidato cha kwanza mpaka cha nne na nikafanikiwa kuzawadia cheti cha mwanafunzi bora na uongozi baada ya kufanya vizuri kwa miaka yote minne ya sekondari.

Nikafaulu kwa ufaulu wa daraja la kwanza, nikiwa mwanafunzi pekee darasa nzima la wanafunzi 138 mwenye daraja la kwanza na nikapangiwa kwenda Advance kwa mchepuo wa PCM (Physics, Chemistry, Advance Math)

Advance

Hapa napo sikukaa kizembe, katika darasa la wanafunzi 38, kidato cha tano na cha sita vyote nilikuwa mwanafunzi namba moja ama namba mbili kwenye mitihani ya terms na kikanda. Katika wanafunzi 38 wa PCM, wanafunzi 2 pekee tukafanikiwa kupata Div I. Hivyo moja kwa moja tukapangiwa chuo kikuu, na wote tulikwenda chuo kimoja, UDSM (University of Dar Es Salaam)

Chuo Kikuu.

Nikasomea program ya engineering (Engieering Geology), ni program ya miaka minne. Kwa ufupi hapa shule ilikuwa ngumu sana, ukijumlisha na changamoto za kifedha, lakini historia ya nyuma ya shule ilinibeba nikapata mkopo wa serikali 100%. Chuoni tulianza wanafunzi 14, lakini tuliobahatika kumaliza mpaka mwaka wa mwisho ni wanafunzi 6, na katika hao sita, ni mimi pekee nilifanikiwa kufaulu kwa kiwango cha juu kidogo ukilinganisha na wenzangu cha Second class honors, Upper division ambacho na hakika si kiwango haba kutokana na ugumu wa program husika.

Hio ndo historia yangu ya shule kwa ufupi sana, nimeelezea matokeo tuu, sijaelezea matukio. Lakini nasikitika kuona kwamba rekodi hio haijawa na mchango chanya kuniwezesha kupata kazi. Mpaka sasa kijana natangatanga, hapa na pale. Nipo wazi kufanya kazi kwenye migodi ya uchimbaji, kampuni za ujenzi wa majengo na barabara. Na kwa sasa nina leseni ya ulipuaji (blasting licence for both Open pit & Underground mining)
Hahah! Ama hakika kupata kazi zama hizi connection... Wakuu nipeni CONNECTION!! Umri ni miaka 27.
Nenda Ajiraportal omba hizi nafasi then uendelee na kutafuta vijiwe vya kupata hela ya kula.
Screenshot_20241113-192358.jpg
 
Pambana
kuna jamaa namjua alihustle kitaa,mara afundishe Tuition,mara aajiriwe kibarua kwa wahindi ila kaja kupata ajira ya maana akiwa 35,muda huu Mambo yanamuendea sawa

Mwanaume pambana,hakuna atakae kuhurumia,ukikata tamaa umekwisha

Mwanamke ndio anaeonewa huruma,yakimzidi anatafuta bwana wa kumuoa
Mimi namjua mmoja aliajiriwa akiwa na 34, maisha si mchezo kwa mwanaume.
 
Ndiyo maana mi mtoto wangu nimempangia asome mwisho form 4 then peleka SUA akasomee KILIMO NA UFUGAJI then akiwa anaingia Degree namuanzishia duka la pembejeo akimaliza nauza viwanja viwili namfundisha kufuata madawa ya mifugo na shambani KENYA NA CHINA likiwa pumbafu shauri lake nahamia kwa mdogo ake.
KAMA UMEPENDA HUU MPANGO WANGU GONGA LIKE TWENDE WOTE
Hahahaa.

Jamaa umeburudisha ila ni ukweli mchungu sana uliousema.

Niongezee tu hapa, Mzazi kama unajiweza hakikisha unamtengenezea mwanao mazingira ya kuchomoka mapema, kusoma kwa mfumo wetu huu ili baadae uje ujikwamue ni jau sana, Dunia imebadilika
 
Njoo hapa tufanye kazi kijana usilalamike sana..

Mchongo upo hivi. Kampuni yetu unafanya kazi kwa siku ni 15000 hyo kwa ajili ya kula..

Akini pia mwisho mwezi unapewa chako kama kawaida yaani mshahara..

Sasa kazi ipoje.. kuwa mpole...
Kwanza hii kampuni yetu unajihusisha na uuzaji wa blue band. Na biadhaa nyingine kama mafuta pamoja na majiko ya gesi.

Kazi unafanya vipi. Utapata maelekezo ofisini.
Je ukiulizwa nyumbani unafanya nini jibu ni..... Bussness manager

Mkuu pesa ipo huku hatuzunguki sana mda mwingi upo kwa gari.

Ikitokea root ya mkoani utainjoi sana sana sana tena sana.

Kama ni mtu wa totoz mkuu hapa ndo.mahari pake mkuu..

Karibu sana mkuu.
Your warmly welcome
 
Miaka 27 bado mkuu! Wengine tumepata kazi serikalini tukiwa above 30 yrs! Wengi wanajichanganya kwenye kuchagua course mavyuoni, kwa ufaulu wako ungekuwa umesomea course zingine mfano civil, mechanical, Electrical, IT hizo course hata usipoajiriwa na serikali huwezi kulala na njaa!!

Note: mimi sio muumini wa connection toka nafanya usaili pale utumishi nimepiga saili nyingi sana mpaka nakuja kupata kazi ilikuwa nafasi moja na nikaenda nikapiga nikachukuliwa kwa hiyo usiamini kwenye connection pambana sema wewe ulichagua course zenye nafasi za ajira chache ndo maana unaangaika mkuu! Ila kuwa na subira siku yako ikifika utafidia miaka yote uliokaa mtaani
Aombe hizi nafasi
Screenshot_20241113-192358.jpg
 
Point mkuu
Ukiona kama hujiwezi jaribu kijinyenyekeza kwa mwenyezi mungu anaweza kufungulia njia sehemu yoyote ile sio lazima uajiriwe.
Ika kama unahisi bado una nguvu na vyeti unaweza kujipambania mwenyewe endelea
 
Njoo hapa tufanye kazi kijana usilalamike sana..

Mchongo upo hivi. Kampuni yetu unafanya kazi kwa siku ni 15000 hyo kwa ajili ya kula..

Akini pia mwisho mwezi unapewa chako kama kawaida yaani mshahara..

Sasa kazi ipoje.. kuwa mpole...
Kwanza hii kampuni yetu unajihusisha na uuzaji wa blue band. Na biadhaa nyingine kama mafuta pamoja na majiko ya gesi.

Kazi unafanya vipi. Utapata maelekezo ofisini.
Je ukiulizwa nyumbani unafanya nini jibu ni..... Bussness manager

Mkuu pesa ipo huku hatuzunguki sana mda mwingi upo kwa gari.

Ikitokea root ya mkoani utainjoi sana sana sana tena sana.

Kama ni mtu wa totoz mkuu hapa ndo.mahari pake mkuu..

Karibu sana mkuu.
Your warmly welcome
Inachukua mtu yeyote au vigezo ni vipi mkuu nije na Mimi hapo
 
Njoo hapa tufanye kazi kijana usilalamike sana..

Mchongo upo hivi. Kampuni yetu unafanya kazi kwa siku ni 15000 hyo kwa ajili ya kula..

Akini pia mwisho mwezi unapewa chako kama kawaida yaani mshahara..

Sasa kazi ipoje.. kuwa mpole...
Kwanza hii kampuni yetu unajihusisha na uuzaji wa blue band. Na biadhaa nyingine kama mafuta pamoja na majiko ya gesi.

Kazi unafanya vipi. Utapata maelekezo ofisini.
Je ukiulizwa nyumbani unafanya nini jibu ni..... Bussness manager

Mkuu pesa ipo huku hatuzunguki sana mda mwingi upo kwa gari.

Ikitokea root ya mkoani utainjoi sana sana sana tena sana.

Kama ni mtu wa totoz mkuu hapa ndo.mahari pake mkuu..

Karibu sana mkuu.
Your warmly welcome
Umerogwa?
 
Miaka 27 bado mkuu! Wengine tumepata kazi serikalini tukiwa above 30 yrs! Wengi wanajichanganya kwenye kuchagua course mavyuoni, kwa ufaulu wako ungekuwa umesomea course zingine mfano civil, mechanical, Electrical, IT hizo course hata usipoajiriwa na serikali huwezi kulala na njaa!!

Note: mimi sio muumini wa connection toka nafanya usaili pale utumishi nimepiga saili nyingi sana mpaka nakuja kupata kazi ilikuwa nafasi moja na nikaenda nikapiga nikachukuliwa kwa hiyo usiamini kwenye connection pambana sema wewe ulichagua course zenye nafasi za ajira chache ndo maana unaangaika mkuu! Ila kuwa na subira siku yako ikifika utafidia miaka yote uliokaa mtaani
Watiaji moyo hamkosekani mwamba anataka channel yenye connection sio kumtia moyo mpigieni pande hilo
 
Back
Top Bottom