Rich gang members wamwaga mamilioni ya pesa kaburini kwa Ivandon

Rich gang members wamwaga mamilioni ya pesa kaburini kwa Ivandon

Mhuu! Sidhani kama ni pesa zilizopatikana kwa njia halali.
 
upumbavu huu Uganda kwao watu wanakufa kwa njaa mpaka wanachemsha majani ili wasife wao wanafukia pesa ili zioze

Hivi kuchana noti au kuchoma kwa nini ni kosa la kisheria wakati ni zako? Nadhani ni kwa vile unazitoa kwenye mzunguko na fedha hizo ni mali ya umma. Jee kuzika ardhini pesa na kuziondoa kwenye mzunguko sio kosa la jinai?
 
Wanatambika hao...
Waafrika shida sana...sipati jamaa angekua na pesa mfano kama Billgates...?

Inawezekana kweli wanatambika maana Ivan alikuwa sangoma, tunaweza tukawa tunaona maburungutu ya noti kumbe vichwa vya watoto wachanga
 
Mwenye kujuwa haya makaburi yako sehemu gani tafadhali anipe picha kamili maana huu ukata nilionao lazima nishughulikie hizi pesa. Niko hapa Kagera nasubiri meli ya leo usiku kuelekea Kampala.
 
Sasa familia ngapi wenye hali duni wangenufaika na hizo hela. Ningefurahi Museveni angelizungumzia hilo, na wote waliofanya hivyo kuchunguzwa walivyo zipata hizo hela, maana hawana uchungu nazo na sio watu wenye huruma ama imani
Acha kuzipangia matumizi Pesa za mwanaume mwenzio
 
Mwenye kujuwa haya makaburi yako sehemu gani tafadhali anipe picha kamili maana huu ukata nilionao lazima nishughulikie hizi pesa. Niko hapa Kagera nasubiri meli ya leo usiku kuelekea Kampala.
Yapi njia ya kwenda Kabellele, njia panda ya kwenda Jinja, mita 200 toka round about.
 
Nimesikia Jack Pemba alikatazwa kusogelea hilo kaburi-nia yake ilikuwa kuweka historia mpya Uganda-boot ya gari yake ilijaa pounds za UK-yaani hata nafasi ya kuweka coffin ingekuwa taabu
 
Sasa familia ngapi wenye hali duni wangenufaika na hizo hela. Ningefurahi Museveni angelizungumzia hilo, na wote waliofanya hivyo kuchunguzwa walivyo zipata hizo hela, maana hawana uchungu nazo na sio watu wenye huruma ama imani
Kiongozi watu wana hela wacha watumie.
Usiwapangie matumizi.
Tutafute zetu tukumbukwe.
 
Back
Top Bottom