Ridhiwani Kikwete: Asilimia kubwa ya waandishi wa Habari ni makanjanja

Ridhiwani Kikwete: Asilimia kubwa ya waandishi wa Habari ni makanjanja

Kweli Vyuo Vikuu sasa vimekosa thamani ......................... yaani magraduate wazima wanamwalika Riz kuja kuwahutubia!! Hata kama ni njaa lazima ujali your dignity. Ingawa ni mambo ya kichama but I still insist that was too low for the graduates!!
 
Waandishi ni kama Waalim katika nchi hii wanatukanwa, wanadhalilishwa lakini hatimaye wakiitwa kula ubwabwa na kupewa shilingi kidogo unaona wanapayuka kupamba watu hata wasio na sifa. Acha Riz awatukane maana jioni atawapoza na ubeche halafu kesho wanaanza kumpamba
 
Waandishi ni kama Waalim katika nchi hii wanatukanwa, wanadhalilishwa lakini hatimaye wakiitwa kula ubwabwa na kupewa shilingi kidogo unaona wanapayuka kupamba watu hata wasio na sifa. Acha Riz awatukane maana jioni atawapoza na ubeche halafu kesho wanaanza kumpamba

Mkuu nakubaliana na wewe kwa asilimia zote kuwa walimu na wanahabari wamekua kama tambara la deki, hutumika kusafisha wanasiasa wachafu lakini baadaye wanakuja kukanyagwa. Walimu na wanahabari wabadilike sasa wakati ni huu.
 
Haya maneno ya huyu mtoto yanamuumbua Pasco na kupenda bahasha za khaki na kuzigawa .Pasco yuko humu humu muumini mzuri wa bahasha ili kuandika ukanjanja .Haya kazi kwenu akina Pasco .

Em jifunze sasa unapo reply with quote post ndefu kama hiyo unaiounguxa, tunachoka kupita kwenye wall story ileile inajirudia wee afu ndefu ati kisa mtu umequote yote, sio maana ya hiyo button kuwepo hapo
 
Huenda anapoona hawanunuliki tena anawageuka, alipowahitaji aliwanyenyekea, na sasa baada ya kupata kile alichokichuchumia hana haja nao na hata zile bahasha za kaki hawapi tena.


2015 siyo mbali, atarudi kwa maknjanja hao hao. Na mbaya zaidi makanjanja kwa njaa zao watampigia magoti. Acha watukanwe tu na IQ zao za kuunga.
 
Riz yupo sahihi kabisa waandishi ni makanjanja asilimia kubwa
Kweli yupo sahihi kuita makanjanja maana yeye mwenyewe ni miongoni mwa watu wanaowatumia wanasiasa kwa masilahi yao yaani kama upo kwenye msafara wake lazima uandike ya kumpamba kwa kuwa amekulipa na ndio maana vyombo vya habari hasa magazeti yanatakiwa wajitegemee kila kitu pindi wanapokwenda kuandika habari ili ku-balance, mfano mzuri waandishi wa magazeti ya mwananchi walikuwa wanafukuzwa kwenye kampeni za JK those days na kulikuwa na mratibu ambae anafanya uhakiki
 
Ridhiwan-Kikwete-June18-2014.jpg

Mbunge wa Chalinze (CCM),Ridhiwani Kikwete

Mbunge wa Chalinze (CCM), Ridhiwani Kikwete, amewashambulia wanahabari nchini kuwa asilimia kubwa ni makanjanja na kwamba wanapoandika habari wanasukumwa na weledi wa jinsi wanavyofikiria vichwani na itikadi zao za kisiasa.

Ridhiwani alitoa kauli hiyo hivi karibuni wakati wa mahafali ya wanafunzi ambao ni wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika vyuo vikuu vya mjini Morogoro yaliyofanyika katika ukumbi wa bwalo la Umwema mjini humo.

“Asilimia kubwa ya waandishi tuliokuwa nao ni makanjanja, ni ukweli kabisa wanapokaa kwenye meza zao wanaandika vitu tu, wanapokaa kwenye ofisi zao wanaandika vitu tu, yaani mtu anapikapika tu vitu,” alisema.

Alisema siyo dhamira yake kuwasema vibaya wanahabari, lakini waandishi wengi hapa nchini wanasukumwa sana na weledi wa siasa zao jinsi wanavyofikiria vichwani mwao na itikadi ya siasa.

Aliongeza kuwa wakati mwingine hata jambo zuri likifanyika hawezi kulisifia badala yake kazi yake kubwa ni kuandika mambo ya ovyo ovyo tu.

“Mimi ningependa sana kuwasihi waandishi wetu hebu kidogo tuandike vitu vinavyofanana na hali halisi, hatusemi kuwa watu wanapofanya mabovu wanyamaziwe, hapana, wabovu waandikwe na mabovu yao, wanapofanya mazuri wasifiwe ili kuendelea kutiana moyo katika kulijenga taifa,” alisema.

Ridhiwani alisema Watanzania jambo kubwa wanalolihitaji ni amani na kwamba wasomi watambue kuwa nchi ipo mahali pazuri sana na amani inazidi kutawala tofauti na inavyoripotiwa na magazeti.

Alisema wakati wa mjadala wa bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini ya mwaka 2014/15, mambo yaliyofanywa na wizara hiyo katika kipindi cha 2013/2014 ni mazuri sana, lakini cha ajabu siku moja kabla ya kuanza kwa mjadala wa wizara hiyo, magazeti yaliandika Waziri Muhongo kikaangoni.

“Kikaango hicho kipi, haya ndiyo magazeti tuliyonayo, yanaandika andika tu yaani mpaka wakati mwingine nashindwa kuelewa,” alisema Ridhiwani.

Aliongeza kuwa wakati wa mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kulizuka kelele kwa baadhi ya watu kwamba wanataka waandishi wawe huru, lakini yeye (Ridiwani) akawa anajiuliza moyoni hivi huo muswada wa habari ukipelekwa Bungeni hawatalia?

Wakati Ridhiwani akiwashambulia waandishi wa habari, amekuwa mwanasiasa kijana ambaye kila anakokwenda kwenye shughuli za kisiasa anafuatana na msururu wa waandishi ambao humpamba kwa habari nzuri.

Miongoni mwao, ni kikosi kikubwa cha waandishi alichokuwa nacho wakati wa kampeni za uchaguzi katika jimbo la Chalinze Aprili mwaka huu.

Katika harakati zake za kisiasa amekuwa akitumia waandishi wa habari kumpamba kwa nia ya kujijenga kisiasa kama ambavyo wamekuwa wakifanya wanasiasa wengi, wakiwamo ambao anawachukulia kama mfano wa kuigwa.

Source: Nipashe


kibaya zaidi ni kwamba waandishi wa habari wanafanywa kama ni toilet paper,yaani ukisha itumia na kumaliza matatizo yako basi huitaki tena na inakuwa haina dhamani tena kwako.
Huu ni ukweli ulivyo na hata wenyewe waandishi wa habari wanalielewa hili na kila siku tumekuwa tukisia wakisemwa vibaya na bado kesho utawakuta wapo na mtu yule yule na wanampamba kweli kweli.mambo kama haya yanawafanya watu kuichezea fani ya uandishi wa habari.
Waandishi wa habari ni watu muhimu sana ktk taifa lolote lile,ni vyema heshima hii kwao ikaendelea kulindwa na kuheshimiwa na hii iendane sambamba na wao wenyewe kujiheshimu,kujidhamini na kuipenda kazi yao na kutoruhusu wachache kuwatumia kwa matakwa ya kisiasa na baada ya mafanikio muhusika huwakana waandishi wa habari na kuwaona si lolote lile.
waandishi wa habari ni wakati wenu sasa wa kubadilika na kuacha kuwa wepesi,mjitahidi sana kuwa mwiba na ikiwezekana mridhike na kile mkipatacho,hii itasaidia sana kupunguza sana kuitwa makanjanja.
Mungu aendelee kuwapa nguvu na moyo wa upendo,lakini chonde chonde msiwe kama mshumaa kuungua huku mkiwamulikia wasio ona nini maana ya mwanga muutoao
 
Ridhiwan-Kikwete-June18-2014.jpg

Mbunge wa Chalinze (CCM),Ridhiwani Kikwete

Mbunge wa Chalinze (CCM), Ridhiwani Kikwete, amewashambulia wanahabari nchini kuwa asilimia kubwa ni makanjanja na kwamba wanapoandika habari wanasukumwa na weledi wa jinsi wanavyofikiria vichwani na itikadi zao za kisiasa.

Ridhiwani alitoa kauli hiyo hivi karibuni wakati wa mahafali ya wanafunzi ambao ni wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika vyuo vikuu vya mjini Morogoro yaliyofanyika katika ukumbi wa bwalo la Umwema mjini humo.

“Asilimia kubwa ya waandishi tuliokuwa nao ni makanjanja, ni ukweli kabisa wanapokaa kwenye meza zao wanaandika vitu tu, wanapokaa kwenye ofisi zao wanaandika vitu tu, yaani mtu anapikapika tu vitu,” alisema.

Ohooo!
Ukweli unauma ,
Lakini Bwana mdogo anata ligi na waandishi makanjanja!
 
Haya maneno ya huyu mtoto yanamuumbua Pasco na kupenda bahasha za khaki na kuzigawa .Pasco yuko humu humu muumini mzuri wa bahasha ili kuandika ukanjanja .Haya kazi kwenu akina Pasco .

Pasco njoo huku njaa yako imeanikwa.
 
Waandishi wa tanzania makanjanja wengi na wala sio siri wanafanyakazi kwa maslahi ya watu tu tena tumewachoka sana wanatakiwa wajue hilo . Wanafanyakazi kwa kununuliwa , angalia NIPASHE , Mwananchi hayafai kabisa .Ukitaka uandikwe habari zako lazima uwape Fedha ni rushwa rushwa tu

kama maslahi ya boss wako
 
Back
Top Bottom