Ripoti ya CAG 2021/2022. ATCL, NHIF, Deni la Taifa, Vyura wa Kihansi, risiti za kielektroniki, Biswalo. Vyazua Mjadala

Ripoti ya CAG 2021/2022. ATCL, NHIF, Deni la Taifa, Vyura wa Kihansi, risiti za kielektroniki, Biswalo. Vyazua Mjadala

Hivi yule Zito Zuberi Kabwe, MWAMI inamaana Hadi sasa hajaipata Ripoti ya CAG?
 
Hatimae kichaka cha hayati Magufuli kimeisha sasa wizi wao, ufisadi wao, uongo wao, unafiki wao upo hadharani sasa.
Bora hata Hawa wanaweka hadharani kuliko wale waliokuwa wanaiba harafu wakiwekwa hadharani wanafukuza CAG 😁😁
 
Waandishi na hao uliowaita "wapashaji" hasingeweza kufanya uchambuzi wa ripoti wasiyonayo, leo ndio imekuwa wazi kwa umma hivyo itachambuliwa sasa. Na kuhusu maswali, hasa hiyo ripoti ndiyo maswali yenyewe. Wanaotakiwa kuulizwa ili wajibu ni serikali.
Katika nchi ambazo watu wake wajitambua na wawajibikaji hiyo ripoti baada ya kusomwa na mkaguzi vyombo vya habari vyote (vile vinavyoheshimika) hupewa nakala ili wajiandae kwa uchambuzi na masuali.

Kisha baada ya hapo huandaliwa mkutano wa mkaguzi na waandishi wa habari ili kuwepo uwazi na ufafanuzi wa masuala mengi tu.
 
Waandishi aina Moloto, mbona aongelei na kuchambua report ya awamu ya sita
 
Hatimae kichaka cha hayati Magufuli kimeisha sasa wizi wao, ufisadi wao, uongo wao, unafiki wao upo hadharani sasa.
Kwa hiyo ripoti ya CAG mwakani itakuwa swaaaafi au siyo? Hiyo ni ndoto. Acha kujidanganya
 
Nchi yetu ina waandishi mahiri wa habari wachache sana, yaani top class na Jenerali Uliomwengu aongoza kundi hili.

Pia nchi yetu ina waandishi wa habari ambao ni mchanganyiko wa umahiri na uhuni na ndo hao unowasema wamenunuliwa na ndo huitwa "chequebook journalists" hawa wapowapo tu mara hapa mara pale.

Kicha kuna wale wapashaji habari ambao ndo wengi wao wana vibuyu vya asali.
Pascal Mayalla unakubaliana na hili ?..
 
Mkaguzi mkuu ndio aje aongelee uchakavu wa miundombinu ya Choo uwanja wa ndege?

Hakuna Menejimenti huko Airport. Sio swali hili, nasema Hakuna Menejmenti huko Airport kwa sababu ndio picha anayotoa CAG.

.... naamini kuna miongozo ya CAG katika kuwakilisha picha nzima ya ukaguzi anaofanya -kwamba mambo muhimu ya uhakiki huo ni ya kweli na ya haki-hapa naona mambo muhimu ya uhakiki kuwa ni ya kweli lakini sio ya haki-ni kama amepuuza sehemu ya haki na huo ndio mtazamo wangu yaani, si haki kuweka picha nzima ya usimamizi kama ile ya miundombinu ya choo ni chakavu- na sio kwamba nasema miundombinu ya choo ni mbaya per se lakini, again kwa maoni yangu ni -kama kuna harufu ya upigaji na ni mbaya kana harufu ya choo.
 
Leo April 06, 2023 mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali, Charles Kichere ameongea na waandishi wa habari kuhusu ripoti ya ukaguzi wa hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha 2021/22.

Miongoni mwa mambo muhimu
CAG amewashukuru waandishi wa habari, wenyeviti na makamu wenyeviti wa kamati za Bunge kwa kujimuika katika uwasilishaji wa taarifa hiyo. CAG amesema aliwasilisha ripoti ya ukaguzi kwa Rais kwa mujibu wa katiba na leo zimewasilishwa Bungeni hivyo kuzifanya kuwa nyaraka zinazoweza kusambazwa kwa umma. Leo anatoa taarifa ya yaliyomo kwa ufupi.

Ripoti 22
CAG amesema aliwasilisha kwa Rais jumla ya ripoti 22 zikijumuisha mambo mambo mbalimbali kwa taasisi zilizokaguliwa na CAG miongoni zikiwemo ripoti ya Serikali kuu, TAMISEMI, mashirika ya umma, miradi ya maendeleo na nyinginezo.

Hati 1010 kati ya 1045 zinaridhisha(96.6%)
CAG ametoa jumla ya hati 1045 kwa mwaka wa fedha 2021/22. Katika hizo, hati zinazoridhisha ni hati 1010 sawa na asilimia 96.6, hati zenye shaka ni 29(2.78%) na hati mbaya ni 3(0.29%) na hati tatu zilizoshindikana kutoa maoni.

Malipo ya Bilioni 25.95 hayana risiti za kielektroniki
CAG ameona malipo bila kuomba risiti za kielekroniki ya Bilioni 25.95 kwenye maeneo mbalimbali ndani ya Serikali, CAG amesema inadhohofisha juhudi za Serikali katika kukusanya kodi, wafanyabiashara wanaweza kutumia mwanya huu kukwepa kodi.

CAG amerejea ushauri wa awali wa maafisa masuuli wanapaswa kufanya shughuli na wafanyabiashara ambao wana mashine za risiti na kudai risiti za kielektroniki kwa mujibu wa sheria za kodi.

Ucheleweshaji malipo umesababisha riba ya bilioni 418.77
CAG amesema alibaini ucheleweshaji wa malipo na kuzaa riba ya bilioni 418.77 katika taasisi mbalimbali za Serikali. CAG amesema haya ni malipo yasiyo na tija na kuiingiza Serikali hasara. Sababu za ucheleweshaji inajumuisha mchakato wa malipo kuchukua muda mrefu bila kuzingatia mkataba.

Dawa za bilioni 3.5 muda wa matumizi ulikwisha bila kutumika
CAG alibaini baada ya kukagua rejesta katika hospitali dawa na vifaa tiba vyenye thamani ya bilioni 3.5, hatari yake kuangukia kwa watu wasio waaminifu.

Pia bohari kuu ya dawa ina dawa zenye thamani ya milioni 235.84 zilizokwisha muda wake kabla ya kusambazwa.

Magari yenye thamani ya bilioni 35.29 hayajapokelewa
Magari yenye thamani ya bilioni 35.29 yaliyonunuliwa kupitia wakala wa huduma wa ununuzi Serikalini yalikuwa hayajapokelewa mpaka mwezi wa 12 wakati wanamalizia ukaguzi.

Mfuko wa wanawake, vijana na wenye ulemavu - Bilioni 88. 4 hazijakusanywa
Mfuko wa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, mamlaka 180 za Serikali za mitaa zimeshindwa kukusanya bilioni 88.42 za mikopo iliyotolewa kutokana na kukosekana ujuzi, udhaifu kwenye upembuzi, udhaifu katika ufuatiliaji wa mikopo.

Mifumo ya usalama na utambuzi wa moto haifanyi kazi Uwanja wa Mkapa
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (#CAG), Charles Kichere amesema “Nimebaini mapungufu kadhaa kuhusiana na utendaji wa Uwanja wa Mkapa, ambayo yanahitaji usimamizi makini.”

Ameongeza “Nimebaini miundombinu na vifaa duni, viti vimevunjika na havijarekebishwa, hali isiyoridhisha kuhusu miundombinu ya choo, hii inaweza kuleta athari za kiafya kwa watumiaji na kuathiri mapato."

Amesema “Viyoyozi hazifanyi kazi vizuri, usambazaji wa maji na mfumo wa usafi haufanyi kazi kwa njia inayoridhisha, mifumo ya usalama haifanyikazi kama wa utambuzi wa moto na wa tahadhari haifanyi kazi.”




Wizara ya fedha kwenye mambo ya fedha waziri anayehusika hatoshi ktk hyo nafasi,awajibishwe
 
Muungwana huchutama wambile wale wa kale, na walau pamoja na madudu mengi yaliyomo kwenye report ya CAG, Muungwana kachutama.

Nasema nini!!? Kwa Siasa za nchi nyingi za Kiafrika na hata Tanzania, Rais anayo mamlaka kubwa na ikiwa ataamua kuitumia vibaya, taasisi hazitafanya kazi zake kwa Uhuru, na hivyo ikiwa Rais Samiah angetaka kuficha madudu yaliyomo kwenye report ya CAG na hasa kwa kuzingatia ukweli kwamba idadi ya Wabunge wa chama chake ndiyo kubwa Bungeni, madudu hayo yangebakia kuwa minong'ono tu. Kaamua kuchutama na huu ni Uungwana.

Hata hivyo, ni makosa ya kimantiki kuacha report hii itaje madudu yote haya na bado ipite tu bila kuchukua hatua dhidi ya uzembe, usaliti na ufisadi mbaya kabisa unaotajwa humo. Hii itakuwa alama ya dharau kwa Watanzania, ama ishara ya kwamba kuna "the untouchables" ndani ya nchi hata kwa Mkuu wa Nchi na Amiri Jeshi Mkuu, hili litakuwa jambo la kutisha sana.

Yaani kama kumekuwa na hasara, uzembe na ufisadi mkubwa namna hii na hadi sasa hakuna hata anayehofia nafasi yake, hii inamaanisha it's just business as usual, na hii ni mbaya.

Binafsi ni muumini wa kwamba siyo lazima wote tumpende mtu anqyekalia kiti cha Rais, lakini tunawajibika wote kumheshimu; na wakati watendaji wanapofanya mambo ya hovyo without any fear or remorse, ni dalili mbaya sana ya dharau. Najiuliza tunamdharau kwanini!!?

Sina ninalojua Nanga miye, nawaza tu kibanangabananga!!!
 
Hizo zilizoshindikana kutolea maoni ziwekwe hapa wanajukwaa watatoa maoni
 
Chawa Lucas Mwashambwa tangu itoke ripoti ya CAG hajaonekana, sijui ni hasira ya kukosa mgao wa ile 80 b iliyotengwa katika kampeni ya kumsifia Mama. Chawa wameadimika sana wiki hii

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Anayejua sehemu sahihi ya kuipata Hii report aseme hapa.

Au kama MTU anayo, share it here maana inaonekana kuna madudu Mengi Ambayo hatuyajui.
 
Magufuli alikuwa anamchukia Assad. Sasa Magufuli ameondoka tuone jambo gani litawafika hawa watu wanaotiliwa mashaka na CAG.
Je,watu wanayo appetite ya hawa vigogo kusakwa mmoja baada ya mmoja na kutiwa pingu?
Mambo ya Magufuli haya
 
Back
Top Bottom