Ripoti ya CAG juu ya kutohuisha upembuzi yakinifu mradi wa JNHPP ni upotoshaji mkubwa, kuna uwezekano CAG anatumika kisiasa

Ripoti ya CAG juu ya kutohuisha upembuzi yakinifu mradi wa JNHPP ni upotoshaji mkubwa, kuna uwezekano CAG anatumika kisiasa

Huo mradi wa Bwawa la Nyerere unapingwa na vigogo wa awamu ya nne sababu kuu wana hisa kwenye gesi ya mtwara wanataka kuuza gesi yao kwa Tanesco na pia wana hisa kwenye mikampuni yenye mitambi ya umeme ya IPTL Dowans nk hawataki tujitegemee kwenye umeme watupige kwa kutuuzia wa mitamvo yao.Hizi kelele zote ni za mijizi na mifisadi ya serikari ya awamu ya nne imeona akaunti zao waluzoficha uswisi salio haliongezeki linapungua tu kila siku.Ndio maana u akuta wameshupalia hilo na bandari ya bagamoyo

Mama Samia akae sawa hawa watu ni mafia hawana woga wala aibu wala woga wala huruma kwa watanzania walio wengi na wako tayai kwa lolote kutimiza agenda zao akae nao mbali
Kama nakuelewa hivi
 
hayo manunuzi ya ndege na utekelezaji wa fedha za miradi ya maendeleo na ya kimkakati yanahusisha wizara ya kilimo na umwagiliaji sio?!...
Miradi ya Mazingira iliyotajwa ilikuwa Ofisi ya Zimamoto.
Mbona hawaulizi ilipo ripoti ya ofisi ya Magufuli kama kweli CAG alikuwa na nia ya kumchafua Malaika wao?
 
Ukiisoma kwa umakini ripoti ya CAG miradi ya maendeleo ukurasa wa 98 utagundua kuwa kuna upotoshaji mkubwa kuwa upembuzi yakinifu haukuhuishwakabisa na hivyo data zinazotumika kutekeleza huu mradi ni za mwaka 1970 na mwaka 1980. Jambo ambalo sio kweli.

Huu mradi unaosimamiwa na TANESCO kupitia kitengo chake cha ushauri wa kihandisi una umuhimu kwa taifa letu.

Ni kweli upembuzi yakinifu ulifanyika mwaka 1970 na ule wa utalaamu wa kiufundi ulifanyika mwaka 1980. Kampuni ya Ms Norconsult na M s Norplan zote za Norway.

Lakini taarifa aliyotoa CAG kuwa upembuzi yakinifu haukuhuishwa na sasa watu wanajua ule wa mwaka 1970 na 1980 unatumika sio kweli.

Kwa mujibu wa ripoti ya CAG huu mradi unatakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia sheria ya umeme ya mwaka 2008, sheria usimamizi vyanzo vya maji ya mwaka 2009 na sheria ya mazingira ya mwaka 2004. Hivyo kuutekeleza bila kuhuisha upembuzi yakinifu ilikuwa ni vigumu.

Kwa uharaka wa mradi wenyewe vipengere muhimu vya upembuzi yakinifu kama, tathimini ya mazingira,usanifu wa kiufundi,utafiti wa kitaamamu na ufanisi wa miamba ulihuishwa. Hivyo vipengere vingine kama umuhimu wa kiuchumi na uwezo wa kutekelezeka vilibaki kama awali sababu ni mambo ambayo yanaonekana kuwa yapo vilevile. Hii ipo ukurasa wa 98 wa ripoti ya CAG miradi ya mendeleo.

Kwa mantiki hii hivi inaingia akilini kuwa watalaamu wa CAG mlienda kufanya ukaguzi na kudai kuwa kwa sababu upembuzi yakinifu wote haukuhuishwa kwa vipengele vyote hivyo huu mradi hauwezi kutekelezeka?

Yaani kwa akili ya kawaida mnataka kampuni ipewe kazi ya kufanya feasibility study kujua kama maji yatatosha kuzalisha umeme mto rufiji? Kwamba huu mradi una umuhimu gani kwa uchumi wa taifa letu?

Hata kama ni fitina za kisiasa muwe na aibu.
Mbona unashindwa kusema huo upembuzi yakinifu uliohuishwa ulifanywa na kampuni gani na Ni ya nchi gani? Au wewe ndio umelipwa kuja kutetea ujinga hapa?
 
Nimesoma, lakin mbona yuko sahihi bado.
Hoja iko pale pale hii feasibility study ni ya 1970s as a whole, kilichohuishwa ni vipengele vichache lakin study yenyewe ni ya miaka hiyo.
Unaelewa feasibility study ni kitu gani? Inakuwa na vipengele gani? Katika ile study ya mwaka 1970 vipengele viwilii tu ambavyo ni umuhimu wa kiuchumi wa mradi na uwezekano wa mradi kuendeshawa ndio havikuhuishwa. Kwa sababu hivi vipo Constant maana huwezi kusema vimebadilika. Vipengele vingine kama walivyomjibu vilihuishwa tatizo wapi?
 
Mbona unashindwa kusema huo upembuzi yakinifu uliohuishwa ulifanywa na kampuni gani na Ni ya nchi gani? Au wewe ndio umelipwa kuja kutetea ujinga hapa?
Ungekuwa unajua upembuzi yakinifu ni kitu gani usingehangaika. Kwa ufupi ulifanyika tena mara mbili na baadhi ya wapinzani walidai huu mradi utaharibu mazingira kumbe kiuhalisia unatumia eneo dogo sana la Selous
 
Hivi arobaini lini mkuu!?
Niulize tu, hivi mbona hatusomi chochote kuhusu report ya CAG kutoka ofisi mbili, ofisi ya makamu wa raisi na ofisi ya waziri wa fedha?

Kwamba ofiri aliyokuwepo SSH ilikuwa safi au ofisi aliyokuwepo mpango ilikuwa safi? Nchi ngumu sana hii.
 
View attachment 1748957
Soma vizuri ukurasa wa 98 ripoti ya CAG majibu mazuri aliyopewa CAG.
Sasa hapo kuna msaada gani kwenye point yako ya kitoto? CAG kawauliza wataalamu wa TANESCO, mmetumia upembuzi gani kuanza mradi? Wao wamemjibu, "tumetumia upembuzi yakinifu wa mwaka 1970 na 1980, kwa sababu ya uharaka wa kuanza mradi". Hiyo sababu ya uharaka wewe unaona inakuingia akilini kama siyo ufinyu wa mawazo? Umepiga hesabu ya kujenga nyumba kwenye Kiwanja mwaka 1980 unaanza ujenzi 2019 unatumia hesabu zilezile bila kujali kama humo kwenye Kiwanja kuna jirani alichimba shimo la taka, kuna miti mikubwa imeota, hali ya hewa imebadilika badala ya baridi kuna joto kwa hiyo paa linapaswa kuwa refu, wewe unapuyanga tu sababu ya uharaka? Mpingeni CAG kwa hoja siyo huu utopolo wa vioja.
 
Kazi ya kuhuisha baadhi ya vipengele ilifanywa na kampuni gani na mwaka gani? Tupe hizo taarifa kama ulizisoma mkuu, kama ni kweli tujue CAG anatumika kisiasa kama hauna basi unatumika kueneza propaganda za kisiasa ili kumchafua CAG
Mlishazoea kushibisha kampuni zenu za kifisadi
 
Sasa hapo kuna msaada gani kwenye point yako ya kitoto? CAG kawauliza wataalamu wa TANESCO, mmetumia upembuzi gani kuanza mradi? Wao wamemjibu, "tumetumia upembuzi yakinifu wa mwaka 1970 na 1980, kwa sababu ya uharaka wa kuanza mradi". Hiyo sababu ya uharaka wewe unaona inakuingia akilini kama siyo ufinyu wa mawazo? Umepiga hesabu ya kujenga nyumba kwenye Kiwanja mwaka 1980 unaanza ujenzi 2019 unatumia hesabu zilezile bila kujali kama humo kwenye Kiwanja kuna jirani alichimba shimo la taka, kuna miti mikubwa imeota, hali ya hewa imebadilika badala ya baridi kuna joto kwa hiyo paa linapaswa kuwa refu, wewe unapuyanga tu sababu ya uharaka? Mpingeni CAG kwa hoja siyo huu utopolo wa vioja.
Pole sana, kosa lako ni kukosa elimu bora.
 
View attachment 1748957
Soma vizuri ukurasa wa 98 ripoti ya CAG majibu mazuri aliyopewa CAG.
Sasa huoni vipengele ambavyo Ni muhimu zaidi havikufanyiwa upembuzi yakinifu..
1. Kipengele cha uchumi wa mradi ( gharama za mradi)
2. Uwepo wa maji ya kutosha kuendesha mradi.
Kila mtu anajua mvua zilizokuwa zinanyesha miaka ya 70(miaka 50 iliyopita) Ni tofauti na mvua za Sasaiv.. na matumizi ya watu ya maji ya wakati ule Ni tofauti na sasa.
Sasa unatetea nini hapa. Na kwanini unakuwa mjinga kiasi hiki hata usiweze kuona vitu hivi waziwazi?
 
Huo mradi wa Bwawa la Nyerere unapingwa na vigogo wa awamu ya nne sababu kuu wana hisa kwenye gesi ya mtwara wanataka kuuza gesi yao kwa Tanesco na pia wana hisa kwenye mikampuni yenye mitambi ya umeme ya IPTL Dowans nk hawataki tujitegemee kwenye umeme watupige kwa kutuuzia wa mitamvo yao.Hizi kelele zote ni za mijizi na mifisadi ya serikari ya awamu ya nne imeona akaunti zao waluzoficha uswisi salio haliongezeki linapungua tu kila siku.Ndio maana u akuta wameshupalia hilo na bandari ya bagamoyo

Mama Samia akae sawa hawa watu ni mafia hawana woga wala aibu wala woga wala huruma kwa watanzania walio wengi na wako tayai kwa lolote kutimiza agenda zao akae nao mbali

Wote hao ni CCM,

Ujinga na upumbavu mwingi kutetea walewale
 
Ungekuwa unajua upembuzi yakinifu ni kitu gani usingehangaika. Kwa ufupi ulifanyika tena mara mbili na baadhi ya wapinzani walidai huu mradi utaharibu mazingira kumbe kiuhalisia unatumia eneo dogo sana la Selous
Najua upembuzi yakinifu Ni feasibility study..mi nimesoma mambo ya miradi hivyo usitake kunifundisha vitu usivyovijua. Tunajua kabisa upembuzi yakinifu uliofanywa na Mashirika makubwa ulionyesha uharibifu utakaofanywa na huo mradi Ni sawa na kukata miti eneo lote la mkoa wa Dar es Salaam na ripot hiyo ilikataliwa na Jiwe akisema Ni wa mabeberu..na akaenda kumchukua professor uchwara hapo UD ili aandike kitu kinachomfurahisha
 
Back
Top Bottom