Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mwaka wa Fedha 2019/2020

Na kubadilisha mfumo ndo tatizo.
Hii sheria ya HESLB kiboko mwaka juzi niliomba loan statement yangu deni likawa million 7 juzi nimeomba loan statement deni limekuwa milion 9 nikajiuliza hili deni litaisha lini maana nalipa ila ninazidi baada ya kupungua, so hili linaitaji ufumbuzi wa haraka sana ni mzigo
 
Hyo ni Sheria ya wizi ndio maana nimeona CAG kwenye report, hata waliokopa biashara huwa haiwi hivi, toka lini mkopo wa elimu ukawa na marejesho makubwa kuliko wa biashara na ingetakiwa mtu akianza kulipa hyo retention fee ikome, imagine Sasa maelfu ya watu wasio na ajira Deni linaongezeka tu, na huyo kabudi aliyekuja na hii Sheria walisomaga bure kabisa na hawadaiwi
 
Millioni 34 Na Laki 4 zimetumika kwa chakula cha vikao 20, halafu haitoshi wakapewa Posho Ya Kujikimu Millioni 799 na Laki 9. Ndio maana watu vitambi vilikua vinawatoka wakati wa utawala wa Magufuli.

Wangepewa Mama Ntilie hicho kibarua cha chakula isingefikia hata gharama ya Millioni 5.
 
Ilo jeduali niliisi kikao cha harusi aisee!!! Yani posho milioni mia700 hakiyamungu kuna raia zinakula maisha aisee... Alafu posho mia700 na bado kuna pesa ya malazi apo na usafiri.... Sasa sijui iyo posho ni kwaajili ya kitu gani walahi? Rais Magufuli namkubali sana ila hii sijui alikuwa wapi mpaka raia zinapiga pesa ndefu kiasi icho yani vikao20 na semina ndo bilion daaah. Ngoja nisomeshe mwanangu
 
Daah kweli aisee
Hawa waliokuwa wanalipwa posho ndefu ndio walikuwa praise team wazuri kisa walikuwa wanapata green pasture. Bongo hii wanaopata mteremko huona ujinga kutetea masilahi ya wengine
 
Kuna watu wanadhani haya tunawaonea
 
Mwizi ni mwizi tu
 
mishahara isipopanda mwaka huu ndio ntaamini kuwa shetani ni watu.
 
TUNA safari ndefu sana kama taifa kufikia maendeleo ya kweli kila
awamu huwa yanaibuliwa madudu serikalini ila hakuna anayewajibishwa
wala kuwajibika tunishia kulalamika tu na kukosoa je sisi kama wananchi nini
wajibu wetu
 
kama kawaida yetu tujiulize kama wananchi tulichukua hatua gani yalipotokea haya
MEREMETA
KAGODA
DOWANS
KIWIRA
RICHMOND
RADAR
ESCROW
EPA
Na mengine mengi nani aliwajibishwa au kuwajibika inavyotakiwa
 
Ulikuja kama mkombozi kwa maneno yako mwenyewe eti mtetezi wa wanyonge
watanzania walio wengi kwa unyonge wao wakakushangilia
ukasema wewe msema kweli ukajificha kwenye mgongo wa dini kwa imani zote wenye dini zao wakakuamini
kumbe baba ulikuwa mwizi jambazi wa kuzima wengine wasiseme mjomba huku mambo yote hadharani

nilitamani sana umalize muhula wako halafu madudu yako yaibuliwe tukusute mchana kweupe
 
Na next election wataaambiwa ahadi zile zile.. mambo yalele na bado watawapigia kura.
 
Ulikuja kama mkombozi kwa maneno yako mwenyewe eti mtetezi wa wanyonge
watanzania walio wengi kwa unyonge wao wakakushangilia....
Kabisa unyonge na ujinga wa watanzania ulimfanya Magufuli aonekane shujaa kumbe alikuwa shujaa wa mambo yake binafsi.
 
Hayo mambo yaliyoorodheshwa kama 'mafanikio' hayahusiani kabisa na ubadhirifu wa mali za umma ulioibuliwa na CAG. Kuna tishio kubwa la kiwango duni cha kufikiri na kujenga hoja zinazoeleweka.
 
hii ripoti ni alarm kwa Viongozi wetu wote wenye dhamana ya Kutongoza na kututumikia sisi wananchi.

1. Lazima wawe wakali ktk kusimamia fedha za wananchi walipa kodi.

2. ufuatiliaji wa mara kwa mara wa miradi ya wananchi,

3. Kuchukua hatua mara moja bila kusita pindi inapo bainika kuna harufu ya ubadhirifu wa mali ya umma.

4. mashirikiano kati ya wizara na wizara zingine ktk kutenda kazi.

5. Taasisi ya kupambana na kuzuia Rushwa iongeze umakini na weledi ktk kutekeleza majukumu yake, haswa ktk kitengo cha upelelezi, lkn pia kitengo cha F.I.U kinahitaji Lowe na watu weledi wenye uzoefu wa kupambana.

6.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…