Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 47
Wote wale sita walikuwa wamevaa nguo zilizochafuka. Wawili wao walivaa viatu vya mpira na wengine walikuwa miguu wazi. Hii ilikuwa ni ajabu kubwa kwa Kijakazi. Maisha yake yote, tangu uhai wa Bwana Malik, hakupata kuona watu kama wale wakiingia ukumbini mle mlimopambwa kwa mapambo ya kila aina. Miguu ya wale watu ililichafua lile zulia zuri lililotandikwa juu ya sakafu ya ukumbi huo.
Baada ya kukaa vitini wale wageni wasiojulikana kwa yule waliyemtembelea, kwanza walitazamana na mara mmoja wao akaanza kusema.
“Nafikiri unaelewa kuhusu sheria mpya ya ardhi?”
“Sheria ya ardhi? Sheria gani?” Fuad aliuliza huku roho ikimwenda mbio.
“Sheria inayosema kwamba ardhi yote ni mali ya serikali.”
“Naam! Nimeisikia, Bwana!” Fuad alijibu, wakati umemgeukia na sasa naye anajua kuita ‘Bwana’.
“Basi sisi tumekuja kukujuvya kwamba, ijapokuwa wewe mwenyewe utakuwepo hapa, inakupasa ujue kwamba ardhi yote ile iliyokuwa chini ya milki yako ni mali ya serikali. Kwa hivi sasa unaweza kuendelea na kazi zako mpaka tutakapokuletea taarifa nyingine,” alieleza yule mtu.
“Nimesikia, Bwana! Nimesikia!”
“Basi sisi tumekuja kukuarifu tu tunakwenda zeut.”
Wale watu walitoka na kuingia ndani ya magari yao wakaondoka.
Baada ya kuondoka tu. Fuad alitoka nJe ya nyumba. yake amekasirika sana, uso umemwiva mwekundu kama papai akinung’unika peke yake.
“Wezi wakubwa!” alijisemea.
Ilikuwa wakati wa asubuhi kiasi ya saa nne. Kijakazi alikuwa anafagia uwanja ulioko mbele ya jumba la Fuad. Fuad alikuwa chumbani mwake amelala na mara ilifika gari moja mbele ya nyumba yake.
Ilikuwa ni moja katika zile gari mbili zilizokuja siku ile. Baada ya kufika tu gari hiyo, alishuka mtu mmoja na kumwuliza Kijakazi, “Fuad tumemkuta?”
“Bwana? Si ... sijui, ngojea nikamtazame ndani.” Kijakazi alijibu.
Fuad aliyekuwapo chumbani mwake alimsikia yule mtu alipokuwa akiuliza na mara alitoka nje mbio.
“Nipo! Nipo Bwana! Je mnataka kuonana na mimi?” Fuad aliuliza huku akijifunga vizuri kikoi cha Jabir alichokuwa amevaa wakati ule.
“Tuna haja ya kuonana na wewe kidogo,” alisema yule mtu.
“Karibuni, piteni ndani!” Fuad alijibu huku akijidai kucheka kama mtu aliyefurahi kweli kufikiwa na wageni wale.
Watu wengine wawili waliteremka kutoka kwenye lile gari na wote watatu waliingia ukumbini kwa Fuad pamoja na Fuad mwenyewe.
Kijakazi hakuwa mbali na aliweza kusikia wazi wazi yaliyokuwa yakizungumzwa.
“Je, khabari za toka siku ile?” aliuliza mmoja wa wageni wale.
“Nzuri! Nzuri Bwana!” Fuad alijibu.
“Tumekuja kuonana na wewe kuhusu ile habari tuliyozungumza siku ile. Je unakumbuka tulizungumza nini?”
“Nakmbuka! Nakumbuka vizuri!”
Wote wale sita walikuwa wamevaa nguo zilizochafuka. Wawili wao walivaa viatu vya mpira na wengine walikuwa miguu wazi. Hii ilikuwa ni ajabu kubwa kwa Kijakazi. Maisha yake yote, tangu uhai wa Bwana Malik, hakupata kuona watu kama wale wakiingia ukumbini mle mlimopambwa kwa mapambo ya kila aina. Miguu ya wale watu ililichafua lile zulia zuri lililotandikwa juu ya sakafu ya ukumbi huo.
Baada ya kukaa vitini wale wageni wasiojulikana kwa yule waliyemtembelea, kwanza walitazamana na mara mmoja wao akaanza kusema.
“Nafikiri unaelewa kuhusu sheria mpya ya ardhi?”
“Sheria ya ardhi? Sheria gani?” Fuad aliuliza huku roho ikimwenda mbio.
“Sheria inayosema kwamba ardhi yote ni mali ya serikali.”
“Naam! Nimeisikia, Bwana!” Fuad alijibu, wakati umemgeukia na sasa naye anajua kuita ‘Bwana’.
“Basi sisi tumekuja kukujuvya kwamba, ijapokuwa wewe mwenyewe utakuwepo hapa, inakupasa ujue kwamba ardhi yote ile iliyokuwa chini ya milki yako ni mali ya serikali. Kwa hivi sasa unaweza kuendelea na kazi zako mpaka tutakapokuletea taarifa nyingine,” alieleza yule mtu.
“Nimesikia, Bwana! Nimesikia!”
“Basi sisi tumekuja kukuarifu tu tunakwenda zeut.”
Wale watu walitoka na kuingia ndani ya magari yao wakaondoka.
Baada ya kuondoka tu. Fuad alitoka nJe ya nyumba. yake amekasirika sana, uso umemwiva mwekundu kama papai akinung’unika peke yake.
“Wezi wakubwa!” alijisemea.
Ilikuwa wakati wa asubuhi kiasi ya saa nne. Kijakazi alikuwa anafagia uwanja ulioko mbele ya jumba la Fuad. Fuad alikuwa chumbani mwake amelala na mara ilifika gari moja mbele ya nyumba yake.
Ilikuwa ni moja katika zile gari mbili zilizokuja siku ile. Baada ya kufika tu gari hiyo, alishuka mtu mmoja na kumwuliza Kijakazi, “Fuad tumemkuta?”
“Bwana? Si ... sijui, ngojea nikamtazame ndani.” Kijakazi alijibu.
Fuad aliyekuwapo chumbani mwake alimsikia yule mtu alipokuwa akiuliza na mara alitoka nje mbio.
“Nipo! Nipo Bwana! Je mnataka kuonana na mimi?” Fuad aliuliza huku akijifunga vizuri kikoi cha Jabir alichokuwa amevaa wakati ule.
“Tuna haja ya kuonana na wewe kidogo,” alisema yule mtu.
“Karibuni, piteni ndani!” Fuad alijibu huku akijidai kucheka kama mtu aliyefurahi kweli kufikiwa na wageni wale.
Watu wengine wawili waliteremka kutoka kwenye lile gari na wote watatu waliingia ukumbini kwa Fuad pamoja na Fuad mwenyewe.
Kijakazi hakuwa mbali na aliweza kusikia wazi wazi yaliyokuwa yakizungumzwa.
“Je, khabari za toka siku ile?” aliuliza mmoja wa wageni wale.
“Nzuri! Nzuri Bwana!” Fuad alijibu.
“Tumekuja kuonana na wewe kuhusu ile habari tuliyozungumza siku ile. Je unakumbuka tulizungumza nini?”
“Nakmbuka! Nakumbuka vizuri!”