Riwaya ya Kijasusi; Mtoto wa Rais

Riwaya ya Kijasusi; Mtoto wa Rais

RIWAYA; MTOTO WA RAIS
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU 0652 212391

SEHEMU YA KUMI NA TISA

"Sipendi kukutesa Salum. Sitaki Aisha akakosa baba pia. Aisha hastahili kuwa yati.." Daniel hakumaliza alichotaka kusema.

"Nooo! Usiseme chochote kuhusu Aishaaa.." Salum aliongea huku akidondosha machozi.

"Salum, niambie ulifata nini nyumbani kwa Donald Tengo?" Daniel hakujari kama Salum alikuwa analia.

"Sijui nianzie wapi Daniel kukueleza" Salum aliongea huku machozi yakimdondoka.
"Ni kweli mimi ninaitwa Salum Taiwan. Nilikuwa meneja wa tawi la benki la LDB huko Muheza. Nilikuwa meneja nzuri sana katika benki hiyo. Na mara kadhaa nimepewa tuzo ya mfanyakazi bora. Pengine uchapakazi wangu ndio ulioniponza. Maana kama miezi miwili hivi nyuma nilipokea barua ya kuhamishwa kutoka Muheza, na kuletwa katika tawi letu la Mlimani city. Mimi niliukataa uteuzi huo. Na sababu ikiwa ni moja tu, sikutaka kuwa mbali na mke wangu, Merina!.
Nilikuwa nampenda sana Merina. Nilimpenda kuliko kitu chochote kile hapa duniani. Nilimpenda kwasababu alinipa sababu milioni za kumpenda. Barua ile ya uhamisho, kwangu ilikuwa sawa na kutenganishwa na Merina, mkewangu.
Unaweza ukasema si ningehama na Merina na kuhamia jijini Dar es salaam? Hiyo ilikuwa ngumu, na kama tungetaka iwe hivyo ilimpasa Merina aache kazi! Kwa maana Merina alikuwa ni katibu muktasi katika shamba la miti huko Longuza. Nilipeleka hoja hiyo kwa afisa rasilimali wetu wa mkoa, lakini wala haikusikilizwa. Ilikuwa ni lazima mimi nihame Muheza. Na nilipoonekana mbishi kuhama Muheza kwa sababu ya Merina, ndiposa walipoamua kumuua Merinaaa!" Salum aliangua kilio kikubwa.

Daniel alimwangalia Salum kwa huruma. Aliujua uchungu wa mke ingawa yeye alikuwa hajaoa.

"Pole sana Salum. Ninajaribu kuvaa viatu vyako lakini havinitoshi. Walimuua mkeo kwa sababu ndogo kama hiyo?" Daniel aliuliza kwa wahka mkubwa.

"Ndio, walimuua Merina! Vijana wa Bahari nyekundu walimuua Merina! Ili tu lengo lao litimie la mimi kuhama Muheza"

"Bahari nyekundu walimuua Merina, ni kina nani hao vijana wa Bahari nyekundu?" Daniel aliuliza. Kwa mara nyingine tena alisikia kuhusu Bahari nyekundu.

"Nitakueleza. Nitakuekeza kila kitu Daniel. Baada ya Merina kuuwawa sikuwa na sababu ya kukaa Muheza. Kumbukumbu za Merina zilikuwa haziishi kunijia ndani ya mji ule. Nilikubaliana na matakwa yao ya kuhamia Dar es salaam.

Wiki moja iliyopita ndio niliingia hapa mjini, jumatatu niliwasili kazini, ndipo nilipokutanishwa na meneja Hashim. Mambo niliyoyakuta Dar es salaam ni tofauti kabisa na kazi yangu. Kitaaluma mimi ni afisa mikopo, ambapo kule Muheza nilipanda cheo na kuwa Meneja. Lakini jukumu alilonipa meneja Hashim halikuwa la uafisa mikopo na wala halihusiani na mambo ya kibenki" Salum alisema.

"Ulipewa kazi gani?" Daniel aliuliza kwa hamu kubwa sana.

"Nilipofika hapa, kazi yangu kuu ilikuwa ni kila siku jioni kupeleka pesa katika duka moja la Kilimo.
Mwanzoni niliikataa kazi hii, nikisema sicho nilichosomea. Sicho nilichokuja kufanya Dar es salaam. Sicho kilichonitoa Muheza. Lakini sikusikilizwa hata kidogo. Nilitishiwa kuuwawa kama mke wangu Merina. Hapo ndipo nikajua kwamba ajari ya Merina ilikuwa ni ya kupangwa. Pamoja na hivyo bado nilikataa kuwa mtumwa kwa kutishiwa kifo. Hapo ndipo walipomteka mwanangu, Aisha..." Salum alianza kulia tena.

"Pole sana Salum. Mimi sijabahatika kupata mtoto lakini najua maumivu unayoyapitia.."

"Daniel, hawa watu ni wabaya sana. Bahari nyekundu sio watu hata kidogo. Walimrudisha kwangu Aisha, lakini hakuwa Aisha yule. Wamemtia Aisha ugonjwa wa ajabu sana. Ugonjwa ambao inampasa Aisha anywe vidonge maalum kila siku. Bila hivyo vidonge basi Aisha naye naenda kumpoteza.
Atakufa mwanangu!!!"

"Pole sana Salum. Hivyo vidonge maalum unavitoa wapi?" Daniel aliuliza.

"Wanavyo wao. Wao tu. Mimi wananipa vidonge vya kutumia kwa wiki moja kwa malipo ya kwenda kuwachukulia kemikali zao kila siku jioni"

"Wapi unapoenda kuchukua hizo kemikali?"

Huwa nafungwa kitambaa usoni nikielekea lilipo hilo duka. Meneja Hashim hunipa mkoba wenye hela kutoka benki. Nafunguliwa mita chache kabla sijafika dukani. Lakini nikipelekwa sasahivi au nikipita karibu na hilo duka, nitalikumbuka"

"Ushaenda mara ngapi katika hilo duka?"

"Kila siku jioni, na jana ni siku ya sita"

"Unahisi wanataka kufanyia nini hizo kemikali?"

"Kwakweli sifahamu. Lakini ninavyoamini wanataka kufanya kitu kikubwa sana. Maana wanatumia gharama kubwa sana kununua hizo kemikali"

"Na pale kwa Donald Tengo ulifata nini?"

"Inavyoonesha jana ndio ilikuwa siku ya mwisho kuchukua hizo kemikali. Na leo asubuhi tulipokea ujumbe kuwa tunatakiwa tukapewe shukrani, tukielekezwa tuende kwenye nyumba ile. Lakini cha kushangaza haikuwa shukrani, tumepewa kazi nyingine"

"Kazi gani mliyopewa?"

"Tumepewa kazi ya kumuua Mtoto wa Rais!"

"Mumue nani, Aneth au Moses?" Daniel alishangaa.

"Yule mzee alisema anaitwa Aneth.."

"Mpango wao wa kumuua Aneth, ukoje?" Daniel aliuliza.

"Najua unajua kuwa Aneth ni mwanafunzi wa shahada ya uzamivu ya sheria katika chuo kikuu cha Dar es salaam. Aneth ni mwanafunzi mahiri sana katika uga huo. Aneth amekuwa makini katika masomo pia katika mambo yake binafsi. Maisha yake ameyafanya kuwa siri ijapokuwa yeye ni Mtoto wa Rais. Lakini cha kushangaza maisha ya Aneth sio siri kwa watu wale. Wanajua kila kitu kuhusu Aneth. Wanajua analala saa ngapi?, anaamka saa ngapi? anakula nini? Na atavaa nini?. Kitu walichotuambia leo ni kuwa Mh. Rais ana mpango wa kumuachia madaraka Aneth pindi muda wake utakapokwisha. Sote tunajua kuwa Rais Mark amebakisha miaka mitatu ili muda wake wa kukaa madarakani uishe. Hivyo Rais anamtengeneza Aneth aje kuwa mrithi wake. Jambo hilo linapingwa kwa nguvu zote na wale watu. Hawataki Aneth aje kuwa Rais!!"

"Kwanini hawataki Aneth awe Rais? Kwa sababu ni mtoto wa Rais?"

"Hapana, sababu sio hiyo. Hata mimi niliuliza swali hilo, yule jamaa alikataa kwa kichwa. Lakini pamoja na kumdadisi sababu, katu hakutuambia sababu ya wao kupinga Aneth arithi madaraka ya baba yake" Salum alisema.

"Na mpango wa kumuua Aneth upoje?"

"Jamaa alinambia kuwa Aneth ni mteja wa benki ya LDB pale Mlimani city. Na kila jumatatu asubuhi amekuwa akienda pale ofisini kupeleka marejesho ya mkopo wake. Na hapo ndipo mimi nilipangwa niwe kama Mhudumu wa kupeleka kahawa yenye sumu wakati Aneth akiwa katika ofisi ya afisa mikopo"

"Wana uhakika angekunywa hiyo kahawa? Na je isingegundulika kama pale benki ndio mliomnywesha hiyo sumu Aneth?"

"Kama nilivyokwambia awali. Jamaa wanajua kilakitu kuhusu Aneth. Wanajua kwamba Aneth ni mpenzi mkubwa sana wa kahawa. Na amekuwa na utaratibu wa kunywa kahawa kila anapofika katika ofisi ile. Afisa mikopo na Aneth wana urafiki tangu zamani, hivyo huwa hana wasiwasi wowote kutumia chochote mle ofisini. Kuhusu kugundulika hata mimi nilimuuliza yule jamaa, alinambia kwamba sumu hiyo ingemuua taratibu. Ingemchukua mwezi mzima ndipo afe, hivyo isingekuwa rahisi watu kuitilia shaka benki ya LDB kuhusika na mauaji ya Aneth"

"Unadhani mpango wa kumuua Aneth utaendelea hata baada ya nyinyi kukamatwa?" Daniel aliuliza.

"Wale jamaa wana dhamira ya kweli kumuua Aneth. Naamini mpango wa kumuua Aneth utaendelea. Ingawa sina hakika kama wataendelea na namna hiihii waliyoipanga ya kumuua Aneth" Salum alisema.

Daniel alitafakari, kisha akasema "Salum ninashukuru sana kwa ushikiriano wako. Kwa ushirikiano huu ulionipa ninakuahidi nami nitakusaidia. Nitahakikisha mwanao hafi kwa kupata hizo dawa maalum siku zote utakapokuwa hapa, kisha tutampeleka nje ya nchi kumtibu kabisa"

"Kweli Daniel?" Salum alikuwa analia.

"Chukua maneno yangu. Utakuwa salama, na mwanao atakuwa salama!" Daniel alisema kwa kujiamini.

Salum alinyanyuka kwenye kiti na kumkumbatia Daniel.

"Usijari, ni katika jukumu langu. Haya twende ukumbini tukaungane na wenzetu" Daniel alisema.

Daniel na Salum waliongozana hadi ukumbini. Waliwakuta wakina Amini wakiongea mambo mbalimbali. Wakati Hannan akichezea tarakilishi yake. Alipofika Daniel, wote walikaa kimya.

Daniel akashika usukani. Akawasimulia kila kitu alichoambiwa na Salum. Wote pale ukumbini walisikitika sana, walimpa pole Salum kwa madhila yaliyomkuta.

"Sasa tuna kazi mbili mbele yetu" Daniel alisema. Ukumbi ukachukua tena utulivu wake. Kazi ya kwanza tutaifanya kuanzia sasahivi, hadi usiku iwe imekamilika. Kuhakikisha tunapata dawa maalum za mtoto wa Salum!" Daniel alinyamaza akiwaangalia wote mle ukumbini kwa zamu. "Tuna njia moja tu ya kupata hizo dawa maalum, ni kumteka yule jamaa aliyewapa kazi wakina Salum ya kumuua Aneth! Yule ndiye atakuwa funguo yetu wapi hizo dawa maalum zinawekwa. Kazi yetu ya pili tutaifanya kesho asubuhi, nayo ni kufatilia nyendo zote za Aneth, na endapo ataenda katika benki ya LDB ni lazima tuhakikishe usalama wake." Daniel alisema. Huku vijana wote walikubaliana naye.

"Daniel," Hannan aliita. Daniel akamwangalia Hannan
"Wakati ukiwa unamhoji Salum, kuna vitu viwili vimetokea. Kwanza nimegundua kwamba simu za kina mzee Rwekwaza zimetoka katika orodha yangu ya simu ninazozifatilia. Hii ni ishara kwamba wamegundua kwamba simu zao zilikuwa zimedukuliwa" Hannan alimeza mate huku akihakikisha taarifa hizo zinapenya vizuri katika masikio ya kina Daniel.

"Jambo la pili, kuna meseji mbili zimeingia katika simu ya Robin. Namshukuru Mungu kwani niliweka mfumo maalum wa kuhifadhi meseji zote zitakazoingia katika simu hii. Kwani baada ya meseji hizo kuingia simu ya Robin ilipoteza taarifa zake zote. Na kwasasa hatuwezi tena kunasa meseji zozote zitakazoingia. Nina imani nao wamegundua kwamba simu ya Robin haipo katika mikono salama" Hannan alinyamaza kidogo. Ukumbi ulikuwa kimya, masikio yote walimpa Hannan.

"Meseji ya kwanza ilisema hivi 'Ukimya wako inamaanisha kwamba ZAK amekunyima mzigo. Na amechukua mzigo wako'. Meseji hiyo ilifatiwa na meseji nyingine iliyoandikwa 'Nenda kwa balozi wa 21.19.1 kama kuna tatizo' na baada ya meseji hiyo ndipo simu ikazimwa" Hannan alimaliza.

Itaendelea...
 
Sometimes stori ziwe zina reflect mazingira ya eneo husika. Mfano stori inaongelea Tanzania lkn una kuta mambo ya teknolojia ambayo hata marekani hawajafikia.


Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
Naamini komenti hii ni ya memba ambaye shule hakwenda ila alijifunza kusoma na kuandika akiwa mtaani.

Nakushauri utafute nukuu za fasihi andishi halafu chambua kipengele cha Riwaya, naamini ukifanya hivyo utakuwa umejinasua kwenye kundi la wasema ovyo.
 
Naamini komenti hii ni ya memba ambaye shule hakwenda ila alijifunza kusoma na kuandika akiwa mtaani.

Nakushauri utafute nukuu za fasihi andishi halafu chambua kipengele cha Riwaya, naamini ukifanya hivyo utakuwa umejinasua kwenye kundi la wasema ovyo.
Achana naye huyo....
 
RIWAYA; MTOTO WA RAIS
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU 0652 212391

SEHEMU YA ISHIRINI

"Meseji ya kwanza ilisema hivi 'Ukimya wako inamaanisha kwamba ZAK amekunyima mzigo. Na amechukua mzigo wako'. Meseji hiyo ilifatiwa na meseji nyingine iliyoandikwa 'Nenda kwa balozi wa 21.19.1 kama kuna tatizo' na baada ya meseji hiyo ndipo simu ikazimwa" Hannan alimaliza.

Daniel alishusha pumzi, huku watu wote ukumbini walikuwa wakimwangalia yeye. Ni yeye, ndiye alikuwa tumaini lao mle ndani. Pamoja na kuwa na kazi mbili ngumu mbele yao, lakini pia iliwapasa kuuchakata ubongo wao kujua maana ya meseji zile.

Daniel aliukumbuka ule ujumbe wa awali aliotumiwa Robin, kutoka katika shirika la ujasusi la Marekani kama walivyoamini.

'Robin vipi umejua mahali mzigo wa ZAK ulipo?'

"Kabla ya kuujua huo mzigo lazima tujiulize huyu ZAK ni nani?" Daniel alikuwa ananong'ona, kwa sauti ambayo ilisikiwa na wote mle ndani. "Tuna watu wengi sana tunawafatilia katika uchunguzi wetu, lakini ni mmoja tu ambaye jina lake linaanzia na herufi 'Z', naye ni Zayiid" Daniel alikuwa kama anaongea peke yake.

"Anaitwa Zayiid nani?" Daniel aliuliza akimwangalia Hannan. Harakaharaka Hannan alicheza na tarakilishi yake.

"Zayiid Ally Khalifa" Hannan alisema.

Daniel alitafakari kidogo, kisha akasema... "Ndio! Na huyo ndiye ZAK. Wamechukua herufi moja kutoka katika jina lake, la baba yake na babu yake. Zayiid Ally Khalifa!" Alivyosema hivyo watu wote waliibuka na shangwe, huku wakimpigia makofi Daniel, alikuwa ameanza kulifumbua fumbo.

"Jamaa walikuwa wanamuuliza Robin Johnson" Daniel alianza kuongea baada ya utulivu kurejea

' Vipi umejua mahali mzigo wa ZAK ulipo?" Hii ni sentensi ya kijajusi. Ni ngumu kidogo kuielezea, lakini mnabidi mjue tu hapa hakuna kinachoitwa mzigo wa ZAK, bali ZAK mwenyewe ndio mzigo"

"Sijakuelewa Daniel," Martin alidakia.

"C.I.A walikuwa wanamuuliza Robin. Je amefahamu mahali Zayiid alipo?" Daniel alisema kwa uhakika.

"Ndio, sasa inaleta maana" Martin alisema.

"Hii meseji ya leo inasema 'Ukimya wako inamaansha ZAK amekunyima mzigo. Na amechukua mzigo wako' Meseji hii inamaanisha kwamba jamaa wanahisi Robin ameuwawa au amekamatwa na ZAK. Na ndio maana wakamuuliza au amechukua mzigo wako?. Hii imetokana na kuona meseji yao ya awali haijajibiwa. Ndio maana wakatuma tena hii kumuuliza. Na walipohisi pengine yupo mashakani ndio wakatuma hiyo nyingine 'Nenda kwa balozi wa 21.19.1'. Hili ni fumbo lengine." Daniel alisema, jasho lilikuwa linamtiririka.

"Hannan naomba maji ya baridi. Halafu nenda maktaba kule uje na lile bango lenye mpangilio wa herufi A mpaka Z.." Daniel alisema.

Hannan aliacha tarakilishi yake na kutokomea ndani. Baada ya kama dakika tatu alirudi. Alikuwa na maji mkononi na bango lenye herufi zote, kuanzia A mpaka Z. Daniel alichukua yale maji na kuyanywa funda moja moja mpaka yakaisha. Akampa ile bilauri Hannan. Akalipokea lile bango lenye herufi. Akalitandaza juu ya meza.

"Njooni muangalie hapa" Daniel alisema. Wote wakasogea wakiwa wameizunguka meza yenye bango la herufi.

"Meseji yao ya tatu inasema 'Nenda kwa Balozi wa ishirini na moja, nukta, kumi na tisa, nukta, moja' Sasa angalieni herufi ya ishirini na moja katika huu mpangilio wa herufi ni ipi?" Vijana wote wakaanza kuhesabu.

"U" wakasema kwa pamoja.

"Na herufi ya kumi na tisa?" Daniel akauliza tena.

"S" Walijibu baada ya kuhesabu tena.

"Na herufi ya kwanza?" Daniel akauliza.

"A" Sasa walijibu kwa haraka.

"21.19.1 ina maanisha ni U.S.A. C.I.A walikuwa wanamwambia Robin aende kwa Balozi wa Marekani. Sasa lazima twende sisi kujua kuna taarifa gani huko kwa balozi wa Marekani?" Daniel alisema.

"Wewe jamaa ni hatari sana!" Leonard aliropoka kwa nguvu.

Kwa mara nyingine tena wote walimpigia makofi Daniel, wakati Daniel akitabasamu.

"Jiandaeni, tunaenda nyumbani kwa Donald kumchukua yule jamaa. Lengo ni kujua mahali zilipo dawa maalum za mtoto Aisha. Karim, utamsindikiza Salum nyumbani kwake kwenda kumchukua mtoto, mumlete hapa.."

Daniel hakuyajari makofi yao. Kwani yeye alijua kwamba, kazi ndio kwanza ilikuwa inaanza.

Baada ya nusu saa, gari la kina Daniel lilikuwa limepaki mahali palepale lilipokuwa limepaki awali. Ndani ya gari walikuwa watu watatu kama awali, lakini safari hii walikuwa wamejipanga zaidi. Lengo lao lilikuwa ni moja, kumchukua Mzee Kizito akawaoneshe mahali ambapo kuna hifadhi ya dawa maalum kwa ajili ya mtoto wa Salum, Aisha.

Mbele ya usukani alikuwepo Daniel Mwaseba. Pembeni yake alikuwepo Martin Hisia, wakati katika siti ya nyuma alikuwepo Leonard. Wakati huo alikuwa akimweka sawa Kipepeo wake, ili amtume tena kama awali, bila shaka Kipepeo naye atumike.

Umbali kama wa mita mia moja hivi, kulikuwa na gari nyingine, ndani yake kulikuwa na Amini na Amani. Wadunguaji mahiri ambao hawakuwahi kukosa shabaha. Katika masikio yao waliweka visikilizio ili kuwasiliana na kina Daniel, na kina Daniel nao walivaa vivo hivyo.

Nyumbani, walimuacha Hannan na watoto wa Donald Tengo. Kila dakika Hannan alikuwa anaomba dua wakina Daniel warejee salama. Alikuwa na hofu sana na usalama wao.

"Leonard, mrushe Kipepeo tuone mazingira yapoje? Pia tujue kama shabaha yetu ipo ndani?" Daniel alisema akimgeukia Leonard.

Leonard alimshika Kipepeo wake. Safari hii alimnong'oneza kisha akamuachia. Akaanza kumuongoza kuelekea katika nyumba ya Donald Tengo.

"Fanya kama nilivyokutuma mpenzi wangu" Leonard akasema kwa sauti ndogo.

Kipepeo aliruka juu ya geti. Huku picha zikipokelewa na simu ya Leonard. Hakukuwa na mlinzi yoyote yule pale getini. Palikuwa peupe pe, tofauti na walivyokuja awali.

"Mbona hakuna walinzi?" Leonard aliuliza kwa mshangao.

"Mzungushe kipepeo kwa nyuma" Daniel alisema.

Leonard alifanya kama alivyoambiwa. Kipepeo alizunguka ile nyumba. Hakukuwa na mtu yoyote yule hata huko nyuma. Na palikuwa kimya sana.

"Jaribu kumpeleka kipepeo mlangoni" Martin alisema.

"Huoni mlango umefungwa?" Leonard aliuliza kwa mshangao.

"Twendeni tukaingie ndani" Daniel alishauri.

"Hapana!" Martin alipinga. "Mgusishe mlangoni kipepeo" Alisisitiza.

"Mgusishe.." Daniel naye alisema.

Leonard akafanya kama alivyoelekezwa. Alimpeleka Kipepeo usawa wa mlango. Akamgusisha.

Kilichotokea...

Ulisikika mlipuko mkubwa sana! Ikifatiwa na kishindo kisicho na mfano. Kisha ukafata moshi na vumbi kubwa sana.

"Walitega bomu!" Daniel alisema kwa sauti mkubwa huku aking'oa gari. Na gari la kina amini nalo lilifata kwa nyuma.

Ndani ya gari ilikuwa kimya. Hakuna aliyeamini kwamba walikuwa wamekikaribia kifo kwa kiasi kile. Ushauri wa Daniel ulikuwa ni ushauri wa kukifata kifo. Lakini hisia za Martin zilikuwa zimewaokoa. Walikikwepa.

"Ulijuaje kama wametega bomu mlangoni?" Leonard aliuliza akimshangaa Martin.

"Hisia zangu" Martin alijibu. "Hisia zangu katu hazijawahi kunidanganya"

"Tunashukuru sana Martin kwa kutuokoa. Tulikuwa tunaenda kufa kifo kibaya sana. Bila shaka jamaa walijua kama tutarudi tena hapa. Hivyo wakatega bomu. Pamoja na kunusurika kifo lakini tumerudi nyuma hatua nyingi sana katika uchunguzi wetu. Hapa ndipo mahali pekee tukipopategemea kumpata yule jamaa, tutampata wapi sasa?" Daniel aliuliza.

"Ule mpango wa pili unaweza kutufikisha katika jibu. Sasa ni muda wa kuanza kumfatilia Aneth, ni yeye pekee ndiye atatuweka karibu na hawa watu" Martin alisema.

"Ndio, Leonard hebu angalia hapo Aneth anaishi wapi?" Daniel alisema akimgeukia Leonard.

Leonard akaanza kubonyaza tarakilishi yake aliyoilaza katika siti ya pembeni. "Kipepeo wangu ameuwawa" akasema kwa sauti ndogo.

"Unasema?" Daniel akauliza.

"Aneth anakaa Ikulu" Leonard akasema. Kina Daniel hawakugundua kuwa Leonard hakusoma kwenye tarakilishi taarifa ile.

"Tutaenda kuweka makazi yetu nje ya Ikulu kuanzia kesho alfajiri. Tutafata nyendo zake zote kutokea hapo. Kwa sasa turudi nyumbani" Daniel alisema.

Itaendelea..
 
RIWAYA; MTOTO WA RAIS
Imeandikwa na Halfani Sudy
Sinu 0652 212391

Sehemu ya Ishirini na Moja

"Tutaenda kuweka makazi yetu nje ya Ikulu kuanzia kesho alfajiri. Tutafata nyendo zake zote kutokea hapo. Kwa sasa turudi nyumbani" Daniel alisema.

***

Ni saa moja ilikuwa imepita tangu wamkose Mzee Kizito nyumbani kwa Donald Tengo. Walirudi maskani kwao. Wakina Karim walikuwa wamerudi na mtoto Aisha. Wote walikula na kuoga, kila mmoja akaenda kupumzika.

Chumbani kwa Daniel alipumzisha mwili tu, lakini akili ilikuwa kazini.

"Bado sijapata mwanga juu ya mkasa huu. Tangia mwanzo yametawala mafumbo tu ambayo ni magumu sana kuyafumbua. Pengine kesho tutapata kitu kwa kufatilia nyendo za Aneth. Bila shaka Aneth ana kitu ambacho kinawafanya wamsake na kutaka kumuua, ni kitu gani hiko? Lazima kesho nifahamu. Utata mwengine upo katika hadithi ya Salum Taiwan. Alisema jamaa wananunua kemikali kwa bei kubwa sana, je nini kazi ya kemikali hizo? Wamepanga kuzifanyia nini? Na wapi?. Fumbo lengine lipo kwa Zayiid Khalifa. Nadhani bado sijapata taarifa nyingi kumhusu huyu mtu. Taarifa alizonipa Hannan pekee sidhani kama zinatosha. Hadi sasa najua kwamba Zayiid anasakwa na C.I.A, pia zaidi ameletwa hapa nchini na wakina Donald Tengo. Kwa kazi gani? Yupo wapi kwasasa? Anafanya nini?. Maswali ni mengi, na yatupasa kuyatafuta majibu. Huu sio muda wa kupumzika!" Daniel alisema akinyanyuka kitandani. Akaanza kutembea taratibu akirejea ukumbini.

"Lazima tujue zaidi kuhusu ZAK, lazima tujue sababu ya kumuua Aneth. Lakini, kwanini nisiende kuongea na Aneth hukohuko Ikulu? Pia nimtahadharishe na nyendo zake ingawa tutakuwa tunamlinda kwa siri. Nafikiri ni wazo zuri" Daniel alifika sebuleni. Alibonyaza swichi moja ukutani. Ndani ya dakika moja wote walifika ukumbini mbiombio.

"Muda wa mapumziko umeisha" Daniel alisema akiwatazama usoni.

Watu wote walimshangaa.

"Niliwaambia mkapumzike. Sasa muda wa kupumzika umeisha. Huu ni wakati wa kazi" Daniel aliongea utani ukiwa mbali na yeye.

"Leonard na Hannan ninahitaji taarifa zaidi kuhusu Zayiid Khalifa. Ninawapa nusu saa. Mpekue mnavyoweza kutoka katika vyanzo vyenu vyote vya taarifa. Mje na taarifa hapa Zayiid ni nani hasa? Nendeni mkajifungie katika kile chumba cha mwisho" Daniel alisema, na wakina Leonard wakaelekea katika chumba alichowaonesha Daniel.

"Timu ya wadunguaji, Amin na Amani. Mimi pamoja nanyi" Daniel alisema akiwaonesha mkono Karim na Martin "Tunaenda kazini sasahivi. Kazi yetu ya kwanza ni kwenda kumsaka Aneth popote pale alipo. Aneth ni mtu muhimu sana kwetu kwa'sasa. Bila shaka ana taarifa ambazo zinamfanya atafutwe kwa udi na uvumba. Lazima tuwe wakwanza kumpata Aneth ili tuzipate taarifa hizo. Tunaingia mtaani sasahivi" Daniel alisema akiwatolea macho Karim na Martin.

"Wazo zuri Daniel, huu haukuwa muda sahihi wa kupumzika. Lakini kwanini tusimtumie Hannan kunasa simu ya Aneth ili tujue mahali alipo? Hii ni nzuri kuliko kwenda kuzurura tu huko mtaani" Martin alisema.

"Upo Sahihi Martin. Karim kamwite Hannan, mwambie aje na tarakilishi yake" Daniel alisema. Karim alienda katika chumba walichokwenda wakina Hannan.

Ndani ya dakika moja Hannan na Karim walirejea. Hannan akiwa na tarakilishi mkononi.

"Samahani kwa kuwakatisha kazi yenu. Kuna kazi ya dharura imejitokeza hapa" Daniel alisema akimwangalia Hannan.

"Kazi gani Daniel?"

"Tunataka utafute mahali alipo Aneth sasahivi. Tunataka tumfate hapohapo alipo" Daniel alisema.

Hannan hakuongea kitu. Aliiweka tarakilishi yake juu ya meza na kuanza kuichezea.

"Anaitwa Aneth Mark Mwazilindi" Hannan alisema.

"Ndio" Daniel alijibu.

"Sawa, nimeipata namba yake" Hannan alisema huku akiwa ameiinamia tarakilishi.

Ukumbi ulikuwa kimya, wote wakimwangalia Hannan akifanya mambo yake.

"Kwasasa Hannan yupo Masaki, katika nyumba namba hamsini na tisa. Najaribu kuangalia mmiliki wa nyumba hii" Hannan alisema huku akiendelea kubonyaza tarakilishi yake kwa kasi kubwa sana.

Baada ya muda mfupi akasema "Kwa mujibu wa taarifa kutoka mamlaka ya nyumba. Hii nyumba namba hamsini na tisa iliyopo Masaki, inamilikiwa na mtu anayeitwa Joash Mtoto..."

"Yule mbunge kijana machachari?" Daniel aliuliza.

"Bila shaka ni huyohuyo. Joash Mtoto ni mbunge mdogo zaidi bungeni. Joash akijipatia umaarufu mkubwa sana bungeni baada ya kupeleka mswaada binafsi juu ya namna ya kuzuia biashara ya madawa ya kulevya hapa nchini. Ingawa mswaada ule ulikataliwa bungeni, lakini Joash Mtoto alikubalika sana kwa wananchi. Hadi leo wananchi wanashangaa kwanini mswaada ule ulikataliwa?" Hannan alisema.

"Yatupasa twende huko Masaki. Nahisi kuna kitu kinaendelea kati ya Aneth na Joash" Daniel alisema.

"Wazo zuri. Nitawaambia endapo simu ya Aneth itahama eneo" Hannan alisema.

"Sawa Hannan, kaendelee kufanya kazi ya kumchunguza Zayiid, lakini pia usiache kuangalia mienendo ya simu ya Aneth" Daniel alikubali.

Hannan alirudi chumbani. Hakukumkuta Leonard. Alipochungulia dirishani alimwona akiongea na simu bustanini. Akaendelea na kazi.

Wakati Martin, Daniel, Amini, Amani na Karimu walitoka nje. Safari ya kuelekea Masaki nyumbani kwa Joash Mtoto ilianza. Walitoka na gari mbili, ya mbele ilikuwa imepandwa na Daniel Mwaseba, Martin na Karim. Wakati nyuma walifuatiwa na wakina Amini.

Kutokana na foleni waliyokutana nayo barabarani iliwachukua wakina Daniel saa zima kufika Masaki, nyumbani kwa Joash Mtoto. Wakiwa njiani mara kwa mara waliwasiliana na Hannan, na mara zote Hannan aliwaambia kuwa simu ya Aneth bado ilikuwa ndani ya nyumba namba hamsini na tisa, Masaki.

Walifika Masaki, walipaki gari mita chache nje ya nyumba ya Joash Mtoto. Na kama kawaida wakina Amini wao walipaki kwa mbali kidogo wakifatilia kila kitu.

"Timu ya wadunguaji wametuambia kila kitu kipo sawa. Sasa tunaenda kuingia katika hii nyumba, ambayo tunaamini Aneth yupo ndani yake. Umakini unahitajika kama ilivyo ada ya Mpelelezi yeyote yule duniani" Daniel aliwapa tahadhari.

"Tunaingiaje? Kwa kuvamia au kistaarabu?" Karim aliuliza.

"Tutaingia kistaarabu kwa kwenda kugonga geti. Mbinu itabadilika kutokana na tutakavyopokelewa huko ndani. Lengo la kwanza la misheni hii ni kumpata Aneth akiwa hai. Lengo la pili la misheni hii ni kumpata Aneth akiwa hai. Na lengo la tatu la misheni hii?" Daniel aliuliza.

"Ni kumpata Aneth akiwa hai" Martin na Karim walijibu kwa pamoja.

Walishikana mikono huku Daniel akigawa majukumu. Na misheni ilianza. Karim alibana upande wa kushoto wa geti. Daniel alibaki upande wa kulia, wakati Martin alienda kugonga geti. Kila mmoja alikuwa karibu sana na bastola yake. Hawakujua nini kitatokea katika sekunde inayofuata.

"Ngo ngo ngo" Martin aligonga geti kwa mkono wake wa kushoto.

"Ngo ngo ngo ngo" Aligonga tena kwa mara ya pili baada ya ile ya kwanza kupokelewa na ukimya. Lakini bado iliendelea kupokelewa na ukimya.

"Jaribu kusukuma geti" Daniel alisema kwa sauti ndogo iliyofikiwa na masikio ya Martin Hisia.

Martin akasukuma geti dogo. Geti likafunguka. Martin aliutumia upenyo huo kuchungulia ndani. Hakuona kitu chochote zaidi ya maua yaliyopangiliwa kwa mpangilio mzuri.

"Ingia ndani, kuwa makini sana Martin" Daniel alisema kwa kunong'oneza.

Martin alinyata taratibu, bastola ikiwa mbele. Aliingia mle ndani na kwa kasi alielekea katika kibanda cha mlinzi. Ilianza kufika bastola yake kibandani kabla ya yeye. Akiwa kibandani aliangalia mazingira yote ya mle ndani. Kulikuwa kimya kabisa, kimya, kimya, kimya.

"Mnaweza kuja kuko salama" Martin aliongea kwa kutumia vifaa walivyovaa masikioni. Wakina Daniel nao wakaingia ndani na bastola zao mikononi. Wote wakichukua tahadhari kubwa sana. Walielekea pale katika kibanda cha Mlinzi.

"Haujakuta mtu hapa?" Daniel aliuliza naye alipofika.

"Hapana, hakuna mtu" Martin alijibu.

"Yatupasa kwenda ndani. Bila shaka Aneth yupo ndani ya nyumba hii. Hannan kanitumia meseji kusisitiza bado simu yake ipo humuhumu ndani" Daniel alisema kwa uhakika.

"Sawa, tunaenda ndani kwa kulindana. Tuhakikishe hakuna anayefanya kosa lolote lile, kosa moja tu litaamua hatma ya mwengine" Martin alisema akitoa tahadhari.

Alianza Daniel Mwaseba, alijibiringisha kwa namna ya ajabu hadi mlangoni. Ilikuwa ni mithili ya tairi la gari likisukumwa na mtoto mdogo. Martin naye akafata kwa mtindo uleule, mwisho Karim alienda, lakini hakuweza kuwaiga wale wanaume wawili. Wakipekee. Yeye alitambaa kama nyoka wa kijani.

"Tunaingia ndani, umakini zaidi unahitajika. Nitapiga hodi, isipojibiwa tutaingia kwa namna yetu" Daniel alisema.

Alijaribu kupiga hodi. Lakini kulikuwa kimya. Akabisha tena hodi, bado kulikuwa kimya. Akajaribu kuufungua ule mlango. Ulikuwa umefungwa. Akatoa rundo la funguo mfukoni. Akajaribu funguo ya kwanza, ikakataa. Akajaribu ya pili, ikakataa, akajaribu funguo ya tatu, mlango uliitika. Mlango uliwachekea.

Daniel alitangulia kuingia ndani akifatiwa na Karim, kisha Martin. Wote bastola zilikuwa zimetangulia mbele ya vifua vyao. Walikuwa makini sana.


Itaendelea...
 
Back
Top Bottom