Roho inaniuma nimetimiza miaka 35 sina mtoto wala maisha

Roho inaniuma nimetimiza miaka 35 sina mtoto wala maisha

Uko Kama Mimi mdogo wangu...tuliza boli utapata Kama uliandikiwa...kikubwa uhai na ibada....mtaani kwetu kuna Jamaa Ana hela maisha ya kifahari lakini hazai kabisa Bora hata wewe hujasema Kama unamatatizo ya uzazi...yeye kapewa pesa kanyimwa watoto lakini anayafurahia maisha Yake kwake anaishi na ndugu tu..shukuru kwa kila jambon uzidishe ibada.
 
pole sana mkuu lakini pia hongera kwa kushtuka na kujutia, hiyo ni ishara tosha wewe ni mpambanaji na mpambanaji siku zote hakati tamaa,wengine hushtukia washashika mkongojo.endela kupambana mkuu, kwani kuna mahali uliona pameandikwa kila mtu atafanikiwa ndani ya miaka yake 35 ?, jibu ni hapana.
kila mtu ana muda wake mkuu. pambanaa pambanaa na tena pambanaa. ushauri wangu ni huu, sali sana na pia jitathmini wewe mwenyewe ujue wapi unakosea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We tafuta tu hela mkuu hata ukiwa na miaka hamsini Bora kuzeeka ukiwa na ela sio watoto
 
USIKATE TAMAA USIOGOPE, KUHUSU MTOTO UKIPATA MTU WA KUBEBA MIMBA YAKE AU KUMPA MIMBA MPE TU...
KUHUSU MAISHA ENDELEA KUMTUMAINIA MUNGU IPO SIKU YAKO VERY SOON KIKUBWA USIJIFUNGIE NDANI...
 
Roho inaniuma jamani leo nimetimiza miaka 35 kamili sina mtoto wala sina maisha licha ya kutumia miaka 10 katika kupambana na maisha.

Uzee sasa umepiga hodi taratibu hapa nilipo nahisi naanza kuchanganyikiwa kwa umri huu mpaka leo hii naishi maisha ya kubangaiza nipate hela ya kula miaka 35 yote hii.
Na waliokuwa hospital wanataman angalau wangekuwa na afya kama yako wasemeje?
 
Mungu akubariki sana kwa shuhuda ulizotoa hapa Chifu.
Binadamu tunataabika sana kwa kujifanyia ulinganifu katika maisha na watu wengine. MUNGU kila mja amempangia mapito yake.Wakati yeye anasikitika hana watoto na maisha yanayoeleweka, kuna mtu anapigania walau apone tu na dalili haipo! Tushukuru kwa kila jambo mkuu
 
Roho inaniuma jamani leo nimetimiza miaka 35 kamili sina mtoto wala sina maisha licha ya kutumia miaka 10 katika kupambana na maisha.

Uzee sasa umepiga hodi taratibu hapa nilipo nahisi naanza kuchanganyikiwa kwa umri huu mpaka leo hii naishi maisha ya kubangaiza nipate hela ya kula miaka 35 yote hii.
Hongera kwa uhai ulionao
 
Maisha ndio haya haya. Magumu alafu atunywi sumu kujiua. Kilicho mbele ndio tunafanya. Usitake kuishi maisha ya mipango ya ndotoni kumbe huna, imenitesa Sana hii hali ya kutamani maisha ya mtu. Soma vitabu vingi vinavyofundisha kutunza pesa na kutumia pesa japo ikiwa ndogo.
 
Mimi nina miaka 31 sasa hivi, niko kama wewe ila niko MAKINI.

Ni bora uwe na familia lakini usiwe na hela. Utapambana hata kuilisha kwa GENGE. Elimu watoto watapata hata ELIMU BURE.

Jambo la msingi tu usizae watoto wengi.

Punguza matarajio, oa mwanamke wa kawaida uanze maisha.

Tatizo letu vijana tuna matarajio na ndoto kubwa sana, mwisho wa siku umri unatutupa mkono wakati PESA HATUNA na FAMILIA hatuna.

Tunabaki kuzurula kwenye familia za watu kupiga stori za MAJUNGU.
Ushauri bora wa Mwaka huu!!
 
Si kila sehemu lazima uwe fundi kujua. Ulichofanya hapa ni ufundi kujua.

Mtu ana shida, anahitaji msaada na wewe unaleta ngonjera zisizokuwa na kichwa wala miguu.

Ndivyo ulivyofundishwa kwenu, mtu akiwa na matatizo suluhu ni kumchamba. Nimeshangaa sana mwanaume unachamba.

Kama ulikuwa huna cha kusema kumsaidia, akheri ungekaa kimya, wala usingepungukiwa chochote.

Inakuaje unaandika barua yote hii kumuharibia mtu siku, kumtonesha kidonda, kuongeza mzigo juu ya mzigo, kuongeza msiba juu ya msiba.

Wewe binadamu gani unaona fasheni kutokuwa na huruma dhidi ya binadamu mwenzio. Unasaidia watu kweli wewe?

Huenda husaidii, sio kwa kuibua huko dhana usiyo na uhakika nayo kama ina uhusiano na mtoa mada basi tu upenyeze mipasho! Halafu unamshauri afanye maamuzi asilie.

Seriously kuna mwanadamu hafanyi maamuzi! Tatizo la mtoa mada sio kutofanya maamuzi bali anafanya maamuzi yasiyo muongezea thamani anayoitaka. Ulipaswa umshauri afanyeje hayo maamuzi baada ya kuacha kulia.

Halafu Baba, Mtoa mada kasema anapambana na maisha na wewe unaibuka na ushauri wa "pambana watu wakupe hongera wanapoona mafanikio". Inaleta tofauti gani? Nicheke 🤣.

Mkuu C kama hutojali nicheki PM tushirikishane mawazo. Usimsikilize huyu fundi kujua ambaye kaokota kapoint huko anadhani kanaapply kila mahali. Lipo tumaini kumpata C unayemtaka. Kama hutoboi maana yake kuna mahali unazingua. So you need to take good care of it.

Nisamehewe mimi🙏, nimetuma kama nilivyopokea.
Mkuu sio kweli kwamba jamaa "kamchamba" .. ila kaanua kuchangia tu maoni yake kama wewe unavyochangia sasa...
 
Kama una afya njema shukuru MUNGU , kuna ndoa zipo na maisha unakuta wana 45 na hawana watoto, watoto ni zawadi toka kwa mwenyezi MUNGU , tafuta binti wakukufaa kama unauwezo wakulipa kodi oa, lakini kusema mpaka ujenge nyumba sijui gari zuri utakwama tafuta binti wakuendana naye oa, baraka nyingine hupatikana kwa mke na mme!

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
Hapo kWa kusema hana mtoto ndo anakosea.watu wana miaka 30 kwenye ndoa Sasa na hawana hata mtoto wa ngama.
Anaweza aoe na asipate hao watoto anaowawaza.
Kila sehemu mitihani. Au Unaweza uwapate na wa kaondoka wote kama yule maza Akiondoka na watoto wote 4 kwenye msiba wa magufuli.
We shukuru Mungu u yu hai... Hayo mengine yatajiseti.
Jua wakati u napanga na Yeye anapanga.
Na ya kwake ndio mara zote yanatimia.
Au uanweza ukawapata na wote wakawa mateja... Kama jirani yangu hapa... Mpk alikuwa analaamika kwamba Yeye ndio mtu Mwenye mkosi Dunia nzima. Haiwezekani Ana watoto 5 wa kiume na wote mateja/bangi mpk wanamshikia kisu Yeye.
 
Mimi nina miaka 31 sasa hivi, niko kama wewe ila niko MAKINI.

Ni bora uwe na familia lakini usiwe na hela. Utapambana hata kuilisha kwa GENGE. Elimu watoto watapata hata ELIMU BURE.

Jambo la msingi tu usizae watoto wengi.

Punguza matarajio, oa mwanamke wa kawaida uanze maisha.

Tatizo letu vijana tuna matarajio na ndoto kubwa sana, mwisho wa siku umri unatutupa mkono wakati PESA HATUNA na FAMILIA hatuna.

Tunabaki kuzurula kwenye familia za watu kupiga stori za MAJUNGU.

Moja kati ya ushauri wa hovyo kuwahi kutolewa JF
 
Hapo kWa kusema hana mtoto ndo anakosea.watu wana miaka 30 kwenye ndoa Sasa na hawana hata mtoto wa ngama.
Anaweza aoe na asipate hao watoto anaowawaza.
Kila sehemu mitihani. Au Unaweza uwapate na wa kaondoka wote kama yule maza Akiondoka na watoto wote 4 kwenye msiba wa magufuli.
We shukuru Mungu u yu hai... Hayo mengine yatajiseti.
Jua wakati u napanga na Yeye anapanga.
Na ya kwake ndio mara zote yanatimia.
Au uanweza ukawapata na wote wakawa mateja... Kama jirani yangu hapa... Mpk alikuwa analaamika kwamba Yeye ndio mtu Mwenye mkosi Dunia nzima. Haiwezekani Ana watoto 5 wa kiume na wote mateja/bangi mpk wanamshikia kisu Yeye.
Ndiyo hivyo yule mama wawili walikuwa wakwake na wawili washeji yake na mdada wa kazi naye akifariki pia piga picha kama hiyo mmewe kabaki na shemeji yake na mkewe wamebaki hawana watoto, mambo mengine nikumshukuru MUNGU tu ukiwa na afya mengine MUNGU anafanya mwenyewe, watu tuna misiba ila unamwachia MUNGU tu akusaidiye.
 
Mkuu ulifanikiwa kuhama kwa baba Mkubwa..? Kitu unapaswa kushukuru Mungu ni kua na Afya njema. Hayo mengine yanakuja tu ukipambana. Shukuru Mungu kwa zawadi ya maisha, badili mitazamo na misimamo yako kaa pekeyako au tafuta mtu (mentor) akuongoze katika kujua nn unapaswa kufanya. Wakati mwingine haufanikiwi kwasababu unafanya sana kazi bali kwa kufanya kazi sahihi.
 
Back
Top Bottom