Roma Mkatoliki amwibua Mwakyembe, adai hana elimu ya kumshauri yeye mwenye digrii 4. Kama anapenda siasa aanzishe chama cha siasa

Wakina Nandy na Harmonaize walipoimuimba Magufuli hawajachanganya siasa na sanaa kwa kuwa wamesifia ila Roma kuimba kwa kuelezea matatizo ya wananchi na kuikosoa serekali yeye ndiyo inaonekana kachanganya siasa na mziki

DOUBLE STANDARDS.


#NO BODY CAN STOP ROMA.
 
Mwakyembe asitutishe na digrii, kwani uongozi mpaka uwe na digrii au mtu kutoa mawazo yake lazima kuipongeza serikali? Kama kweli ni msomi akubali kukosolewa na ajibu wakosoaji kwa hoja za kisomi wananchi tu chambue wenyewe asijifiche nyuma ya digrii wakishindwa kwa hoja na darasa la 4 kwa mujibu wake wanaingia kwenye Kichaka cha usomi. Hata Mtume Mohammad na Yesu hawakusoma hata darasa 1 na ndo tuna aamini na kufuata busara na mafundisho yao.
 
Hili babu mwakyembe halijapona hili
Ila mdogo angu roma asipotekwa tena basi nitajua kuwa majambazi yanaanzia kuingiwa woga
 
Hata akiwa na digrii miamoja kama Elimu Yake haisaidii watu au elimu Yake anatumia kujenga Taifa. Lisilo na upendo. Ni afadhali ya mtu asiyesoma hata darasa la kwanza.Elimu zetu zisaidie kujenga umoja wa kitaifa na mambo ya kihuni ktk Taifa.
 
Msomi never stop learning. Huo ndio ukweli. Sio kwa vile una Madegree ishirini ndio unasema sihitaji kujifunza tena, hapana. Tunajifunza kila siku kupitia kuingiliana na watu wengine. Na tunajifunza kutoka kwa watu mbalimbali wanaotuzunguka. You don't expect every one kuwa educated or clever as you are..?!...kwa hio alitaka kusikia ushauri wa nani wa mtu mwenye degree tano? mnhh
 
Waafrika wengi bado tuna colonial mentality, ni ngumu sana kumtambua mwafrika alielimika na ambae hajaelimika!! Anae jiita msomi utamkuta kwenye foleni ya babu wa loliondo akisubiri apewe kikombe kilichojaa maji, akiamini eti hayo maji yanatibu na kumaliza kabisa magonjwa ya kansa,ukimwi,kisukari na mengine yote sugu!!! Ambae hajaelimika utamkuta anakata mauno kwenye viwanja vya mikutano akishangilia na kuamini porojo za yule "msomi" alietoka kunywa maji ya kikombe loliondo!! kuwa atamletea neema na kumaliza matatizo yake yote aliyonayo!!! Wengine utawakuta wakilia makanisani wakimlilia Mungu, wanatafuta wanaume wa kuwaoa,na maisha mazuri kwa njia za kimiujiza!!! Ni ngumu sana kumuelewa mwafrika,huyo waziri ni sample tu,huoni mwingine anajiona katika watu milioni zaidi ya hamsini yeye peke yake ndio mwenye akili kuliko wote,hao Wakoloni hawakuondoka hivi hivi waliacha wamepanda mbegu kichwani mwetu,sasa wanavuna taratibu wakiwa uko kwao.
 
Kufaulu sio akili
Maisha yangu ya kuanzia o level mpaka chuo kikuu nilikuwa sisomi,muda wa prepo nipo nje ya shule nakula bata,chuo kikuu ndio usiseme ila nimewapita watu wengi tu,
Asante "MWAKYEMBE" kwa kuupa "PROMO MWIMBO WA TAIFA (Anaitwa Roma).

Ila tukukumbushe; Asilimia 90% wananchi wa Tanzania hawana elimu ya darasani kama wewe, hivyo hayo matusi yako ni "YETU SOTE TUSIO NA ELIMU"

Pili, Kua na elimu ya "DEGREE 4" au "KUFUNDISHA CHUO KIKUU" sio kua na "MAARIFA" au "MAENDELEO" katika maisha.

1) Bill Gates - Aliacha kusoma chuo.

2) Said Salim Bakhressa - Hajasoma hata chekechea.

3) Jack Ma (Tajiri wa kwanza China, mwenye Alibaba) - Alifeli primary school mara 4, alifeli mpaka "INTERVIEW" yakua mhudumu wa KFC kwasababu alikua zuzu.

#Mwakyembe huu mchezo hautaki hasira.
 
Co kwa mawe yale lazma wale timu kusifu na kuabudu wachukie c unajua tena lazma tulinde tumbo
 
Kwa hiyo Magufuli na ka PhD kake ka kemistre hawezi kumkosoa Mwakyembe mwenye degree nne?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…