Roman Abramovich: Utajiri wa Damu, Risasi na Umafia

Roman Abramovich: Utajiri wa Damu, Risasi na Umafia

ROMAN ABRAMOVICH: MABILIONI YA DAMU, RISASI NA UMAFIA




FINALE




Safari ya Abramovich kwenda London ilikuwa mahususi kwa ajili ya kwenda kuonana na mentor wake huyo wa zamani akiwa na maagizo kutoka juu kwa bwana mkubwa… Putin. Maagizo haya yalikuwa ‘straight’ bila kupiga piga chenga. Kwamba Berezovsky anafahamu kuwa hakuna mahala ambako anaweza kujificha na mkono wa Putin ukashindwa kumfikia. Kwa hiyo Putin alikuwa anampa sharti moja tu… kwamba Berezosky amuuzie Roman Abramovich kituo cha televsheni na akikubali kufanya hivyo Putin atamuacha aishi.
Kituo hiki cha televisheni kilikuwa na thamani ya mabilioni ya dola lakini Abramovich alimuambia Berezosvky kwamba atakinunua kwa dola milioni 150 tu. Berezovsky akakataa.

Abramovich akarudi Russia kupeleka mrejesho kwa Putn kwamba Berezovsky amekataa. Putin akamtuma tena Abramovich kwenda London na ofa nyingine mpya.
Safari hii alipokutana na Berezovsky alimueleza kwamba yeye mwenyewe yuko tayari kupandisha kidogo dau lake la kununua kituo cha televisheni na atampa dola milioni 175. Na si hivyo tu bali pia kama atakubali kumuuzia kituo hicho cha televisheni basi Putin atamuachia huru rafiki yake kipenzi Glushkov ambaye tayari alikuwa anatumikia kifungo jela.
Kitendo cha kusikia kuwa rafiki yake kipenzi Glushkov ataachiwa huru, Berezovsky hakuwa na nguvu tena ya kukataa ofa ya Abramovich, akakubali kumuuzia kituo chake cha televisheni. Na huo ndio ukawa mwisho wa uhuru wa habari nchini Rusia mpaka leo hii maana kituo cha Berezovsky ndio kilikuwa na ushawishi zaidi nchini Russia. Na Abramovich baada tu ya kukinunua kutoka kwa Berezovsky alikikabidhi mikononi mwa Putin akitumie anavyotaka.

Jambo baya zaidi ile ahadi yao ya kumuachia Glushkov hawakuitimiza. Glushkov akaendelea kusota jela. Kuna kipindi akawekewa mtego akiwa amepelekwa hospitali kutibiwa maaskari magereza wakamuacha chumbani peke yake na akataka kutoroka. Akakamatwa tena na kuongezewa kifungo. Maoligarch kadhaa nao wakakamatwa kwa tuhuma za kupanga njama ya kumtorosha Glushkov. Ule mtandao wa maoligarch uliokuwa unaongozwa na Berezosvky ambao ulikuwa unampiga vita Putin na Abramovich ukasambaratishwa wote. Maoligarch wengine waliosalia wakaelewa somo… ukitaka kusurvive kibiashara ndani ya Russia kuna mtu mmoja haupaswi kumgusa… Roman Abramovich.

Nilikuwa natamani niishie hapa lakini kuna kionjo kidogo wacha nikisimulie pia ili uone uwezo wa Abramovich kucheza na ‘system’ ya dunia. Hata ‘wazungu’ wa magharibi amewahi kuwafanyia uhuni ambao hata sasa hawaamini macho yao.

Pale ulaya wana benki yao, European Bank. Mwishoni mwa mwaka 1998 kuna benki ya kirusi inaitwa SBS Agro ilichukua mkobo wa hela nyingi sana, mabilioni ya Euro. Ikapita kama miaka miwili hivi pasipo SBS Agro kulipa deni lake. Baada ya kuona deni hilo halilipwi European Bank wakahitaji dhamana ya mkopo huo kutoka kwa SBS Agro. Kama dhamana, SBS Agro wali-plegde deni la dola milioni 14 ambalo wanadai kwa kampuni inaitwa RUNICOM S.A. ambayo imesajiliwa nchini Uswisi. Na hapa ndipo ambapo jina la Abramovich linatokea… kampuni hii ya RUBICOM S.A faida yake kubwa walikuwa wanaipata kwa kuuza mafuta ya kampuni ya Sibneft kwenye nchi za ulaya. Katika kipindi hiki pia benki ile ya SBS Agro ilitangaza kufilisika. Lakini European Bank hawakuwa na wasiwasi kwa sababu deni lao lilikuwa ‘guaranteed’ na RUNICOM S.A… sijui kama naeleweka sawasawa…

Sasa basi,

European Bank wakaanza kuwadai RUNICOM S.A. Wakadai sana bila mafanikio… ikabidi uitishwe uchunguzi kuangalia mali za kampuni ili wajue namna gani wanaweza kurudisha fedha zao. Katika uchunguzi wao huu mkazo mkubwa uliwekwa kwenye kuingalia biashara ya mafuta ambayo RUNICOM walikuwa wanaifanya kwa sababu nyaraka zilionyesha kwamba faida yao kubwa ilitoka huko. Hawakuamini macho yao walipogundua kuwa biashara ile ya mafuta ya Sibneft kama miezi sita iliyopita ilikuwa imehamishiwa kwenye kampuni nyingine iliyosajiliwa nchini Cyprus ikiitwa RUNICOM LIMITED.

European Bank wakafura kweli kweli… hii ndio ile kwa umombo wanaita ‘sleight of hand’. Ushawahi kuona mchezo wa karata tatu… anazivuruga vuruga unahisi umeona sawia kuwa shupaza iko pale mkono wa kulia lakini akifunua unakuta kuna dume la kopa. Hii iliyokuwa inafanyika twaweza kusema ilikuwa ‘financial sleight of hand’… abracadabra.

Kuna kitu gani ambacho kinafanana kwenye huu msululu wote? SBS Agro waliokopa awali ni kampuni ya kirusi (Roman Abramovich ni mrusi). Walio gurantee huo mkopo RUNICOM S.A faida yao kubwa walikuwa wanaipata kwa kuuza mafuta ya sibneft kwenye nchi za ulaya (Roman Abramovich ndiye mmiliki wa Sibneft). RUNICOM LIMITED walirithishwa biashara ya mafuta ya sibneft kutoka RUNICOM S.A (Sibneft… Abramovich).

European Bank wakafura zaidi… ilikuwa wazi kwamba ujanja huu walikuwa wanafanyiwa na Roman Abramovich lakini ubaya ni kwamba huwezi kumshtaki kwa kuwa siye uliyemkopesha… walimkopesha nani? SBS Agro… European Bank wakaenda mhakamani. Kesi ikaunguruma kwa miaka miwili. Hukumu ikatolewa kwamba European Bank walipwe kiasi cha dola milioni 24. Lakini nani akulipe?? SBS Agro walishatangaza kufilisika miaka miwili iliyopita na kampuni haipo tena… nani atakulipa hela hizo? Mpaka leo hii ninapoandika makala hii deni hilli halijalipwa na kamwe halitolipwa na ubaya ni kwamba muhusika mkuu na aliyenufaika na mkopo unamjua lakini huwezi kumshitaki kwa sababu hakuna jina lake halijatokea popote kwenye nyaraka na wala hukumkopesha. Tangu kipindi hicho wazungu wanalijua vyema jina la Abramovich na ni mtu wa namna gani.

Kuna watu ukiwasimulia upande huu wa pili wa Abramovich ambao hawajawahi kuusikia watakwambia kuhusu miradi mikubwa ya kijamii ambayo aliifanya akiwa kama gavana wa Chukokta. Jibu langu siku zote ni kweli kwamba Abramovich alitumia fedha zake binafsi karibia dola blioni 3 kwa muda wote aliokuwa gavana wa Chukokta… lakini je unafahamu alinufaikaje?
Baada ya Putin kuwa Rais akampa Baraka Abramovich kuingia kwenye siaisa. Ukitoka pale Kremlin, mwendo wa ndege kama masaa tisa hivi kuna jimbo masikini mno mno linaitwa Chukokta. Hili ndilo ambalo Abramovich aligombea ugavana na kushinda. Alitumia mabilioni ya hela zake kwa ajili ya maendeleo lakini wengi wasichojua ni kwamba alinufaika zaidi. Akiwa kama gavana alikuwa anashawishi sheria ndogo za kodi na misamaha ya kodi kwa kampuni wanazoziona zinafaa. Sasa ile kampuni yake ya Sibneft visima vyake vya mafuta viko Siberia. Walichokuwa wanafanya walikuwa wanauza mafuta yao ya Sibneft kwa bei ya kutupa kwa kampuni ambazo walizisajili kwenye jimbo la Chukokta. Kisha kampuni hizi za Chukokta wanauza mafuta hayo nje ya Russia kwa kampuni dada ya Sibneft kama vile RUNICOM S.A. na walifanya hivi kwa kuwa mafuta haya yakitokea Chukokta yalikuwa na msamaha wa kodi.

Kwa hiyo ni kweli Abramovich alikuwa anasadia lakini papo papo alikuwa ananufaika zaidi.


Wale ‘maswahiba’ wake wa zamani wako wapi?

Mentor wake Boris Berezovsky ambaye alikuja kuwa adui mkubwa siku ya March 23 mwaka 2013 alikutwa amefariki bafuni nyumbani kwake Barkshire, Uingereza. Kifo chake bado kina ubishani mkubwa baadhi ya wachunguzi wa masuala ya post mortem wakisema amejiua wengine wakisema ameuwawa. Wengine wanadai alijiua baada ya kuandamwa na madeni kutokana na kushindwa kesi ambayo alimfungulia Abramovich kugombea umiliki wa Sibneft akitaka kulipwa fidia ya dola bilioni 6 kesi ambayo ilisikilizwa nchini Uingereza na Abramovich kushinda. Hili suala la kugombea Sibneft sijalieleza humu… ila kwa kifupi tu Abramovich alimpiga mchanga wa macho mentor wake… unakumbuka nilieleza kwamba enzi zile za utawala wa Yeltsin Abramovich na Berezovsky walinunua kwa pamoja Sibneft kwenye mnada wa ulaghai ambao wao pekee ndio walikuwa ‘bidders’. Nadhani tunakumbuka vyema… sasa baada ya Berezovsky kukimbia Urusi, Abramovich akafanya janja janja na kumuondoa Berezovsky kwenye umiliki. Berezosvky akafungua kesi.

Abramovich alishinda kesi.

Wanadai kwamba kesi ile ilimfilisi Berezovsky kwa kulipa gharama kubwa za mawakili.

Lakini tukitazama nyuma kidogo tuna pata picha ya tofauti na pengine kutupa dalili kuwa Berezovsky aliuwawa. Novemba mwaka 2006 mshirika wake wa karibu sana Alexander Litvinenko aliuwawa kwa Polonium hapo hapo Uingereza.
Miaka miwili baadae yule rafiki yake Badri ambaye kipindi wako Russia alikuwa anasimamia televisheni yake alikutwa amefariki chumbani kwake hapo hapo Uingereza.
Kama hiyo haitoshi yule rafiki yake kipenzi Nikolai Glushkov alimaliza vifungo vyake na kutoka jela na kukimbilia nchini Uingereza. Huyu naye mwaka jana tu hapa 2018 mwezi March amekutwa amefariki nyumbani kwake hapo hapo Uingereza.

Kwa hiyo maoligarch wote ambao walianzisha vita dhidi ya Putin na Abramovich wote wamefariki vifo vya utata wakiwa na afya njema kabisa… lakini wale wote ambao walikuwa wapole na kumuunga mkono Abramovich kama vile akina Deripaska wako hai hata sasa na utajiri wao ukizidi kupaa kila uchwao.

Mwanzoni mwa makala hii nilijenga hoja kwamba si jambo jepesi sana kuwa bilionea. Unaweza kuwa tajiri… milionea, hakuna shida wala shaka. Lakini kutengeneza utajiri wa kufikia dola bilioni moja na zaidi ni lazima ukubali mikono yako kuchafuka ‘vumbi’ kidogo. Muulize Mo Dewji, msome Gates na alichowafanyia IBM na Steve, chunguza vifo vilivyotokea mwanzoni kwa kuanzishwa kwa Facebook na alichokifanya Mark, muulize Aliko Dangote, teta na akina Motsepe na familia ya Gupta pale Afrika Kusini.
Wote hawa hawawezi kukataa kwamba “behind every great fortune lies a great crime.” Kila utajiri una ukafiri nyuma yake.





MWISHO




H.B ANGA “THE BOLD”
To Infinity and Beyond
 
FINALE..



Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij addenbwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo shedede kamtu33 SteveMollel ngushi Donald stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush mossad 03 white wizard xtaper Mzigua90 Ollachuga Oc Gidbang Mateja M.G Yango jipu abaa4all DIBAJI Agenda1 Grahnman The MaskmaN Slim5 Xubzero agprogrammer JoJiPoJi Architectus blance86 Mamtolo monde arabe Ngao Ya Imani stardust JK naiman64 Dharra seledunga ABB SHAMMA Richard Waziri wa Kaskazini Mwinjuma1 Kanungila Karim baracuda Mwamba028 besaro Pyepyepye Bilionea Asigwa ibn Kiti Chema Tugas Royal Warrior mederii mmangO manzi james LIKUD adrenaline Royal Son Mhadzabe salaniatz Natasha Ismail jiwe jeusi chibalangunamchezo
John Mloy conjuget Van Pauser great G Mtoto wa nzi Zeus1 hindustan Sci-Fi MAN OF PEACE kashata emnly danny baraka bb MTOTELA kbosho TEMLO DA VINCA
 
si jambo jepesi sana kuwa bilionea. Unaweza kuwa tajiri… milionea, hakuna shida wala shaka. Lakini kutengeneza utajiri wa kufikia dola bilioni moja na zaidi ni lazima ukubali mikono yako kuchafuka ‘vumbi’ kidogo. Muulize Mo Dewji, msome Gates na alichowafanyia IBM na Steve, chunguza vifo vilivyotokea mwanzoni kwa kuanzishwa kwa Facebook na alichokifanya Mark, muulize Aliko Dangote, teta na akina Motsepe na familia ya Gupta pale Afrika Kusini.
Wote hawa hawawezi kukataa kwamba “behind every great fortune lies a great crime.” Kila utajiri una ukafiri nyuma yake.





MWISHO




H.B ANGA “THE BOLD”
To Infinity and Beyond

Sawa sawa
 
Habib ww ni nyoko, ww n nouma, ww n kiboko, kudadeki zako uwa unanifurahisha sana hakuna uzi wako uliowahi kuniangusha hongera sana dadeki zako, achana na hao wanga wanaosema ujinga na wao wakacopy watuletee kama awajaleta vi definition vyao vya kingereza hata ku translate wanashindwa😂😂😂 Ishi miaka kibwena ndugu natarajia utakuja mzigo mzito baada ya huu
 
The bold,sweettablet ,
Mwanzoni mwa makala hii nilijenga hoja kwamba si jambo jepesi sana kuwa bilionea. Unaweza kuwa tajiri… milionea, hakuna shida wala shaka. Lakini kutengeneza utajiri wa kufikia dola bilioni moja na zaidi ni lazima ukubali mikono yako kuchafuka ‘vumbi’ kidogo. Muulize Mo Dewji, msome Gates na alichowafanyia IBM na Steve, chunguza vifo vilivyotokea mwanzoni kwa kuanzishwa kwa Facebook na alichokifanya Mark, muulize Aliko Dangote, teta na akina Motsepe na familia ya Gupta pale Afrika Kusini.
Wote hawa hawawezi kukataa kwamba “behind every great fortune lies a great crime.” Kila utajiri una ukafiri nyuma yake.

MWISHO

H.B ANGA “THE BOLD”

To Infinity and Beyond



Nilikuandikia kuwa ukiwa muongo, au ukiwa na maarifa na taarifa kidogo,, Jifunze sana kutunza kumbukumbu.
REJEA COMMENT YANGU NO. 1022.


Uliandika kuwa mauji hayapo Ulaya, Afrika, kama ilivyokuwa huko Russia kwa ulimwengu wa sasa ila sehemu yako hii ya mwisho umeonyesha waziwazi kuwa Uingereza, watu wanauawa, na unahitimisha kwa kutaja majina na nchi ambako mambo hayo yanafanyika.

Wewe ni uchwara katika intelijensia na hauna connection yoyote na mtu wa intelijensia bali wewe ni mlamba viatu vya watu ili wakupe taarifa ila unapewa taarifa uchwara.

Eti ,, unajinadi kwamba una taarifa zote za kiintelijensia ya nchi za Afrika Mashariki.

Boy, remember ; "Always, I don't acknowledge the mess"
 
manonawire, post: 33266332, member: 470499"]
Aisee Habibu B. Anga asante sana mkuu
Nadhani utuwekee na hzo za kina gupta maana na mm najiandaa kufanya ukafiri ili nifike huko
[/QUOTE]

Ukifanya ukafiri ili upate mali, ni lazima moto ukuchome.

Tutakunyofoa kabisa na genge lako la kutaka kufanya ukafiri.
 
manonawire, post: 33266332, member: 470499"]
Aisee Habibu B. Anga asante sana mkuu
Nadhani utuwekee na hzo za kina gupta maana na mm najiandaa kufanya ukafiri ili nifike huko

Ukifanya ukafiri ili upate mali, ni lazima moto ukuchome.

Tutakunyofoa kabisa na genge lako la kutaka kufanya ukafiri.
[/QUOTE]

Poise
Ila ww n mkali khaaa
Nn kubishana na watu vile , ila uko vzur boss unajua vitu kutokana na position yako
 
Habibu kazi unayofanya ni kubwa nasema hili kutoka ndani kabisa ya moyo wangu maana nimejaribu kufatilia mwenyewe kwa mwanga uliotoa hapa hata haikuwa rahisi sawa napata maana lakini ule udambwi dambwi wa simulizi ni haupo kabisa nikaacha kwa wanaobeza ni kawaida yao kufanya hawfanyi na hawapendi wengine kufanya
Asante sana mkuu kwa kuniunga mkono na kunitia moyo. Means alot kwangu niendelee kwa juhudi, uwezo na maarifa yangu yote
 
manonawire, post: 33269260, member: 470499"]
Ukifanya ukafiri ili upate mali, ni lazima moto ukuchome.

Tutakunyofoa kabisa na genge lako la kutaka kufanya ukafiri.
[/QUOTE]

Poise
Ila ww n mkali khaaa
Nn kubishana na watu vile , ila uko vzur boss unajua vitu kutokana na position yako
[/QUOTE]


Huwa sipendi mtu anayejionesha kuwa yeye ni mtu wa intelijensia ; halafu ni muongo.

Sipendi kulea watu wa hovyo hovyo ambao watasababisha Taifa kuwa na kizazi cha hovyo cha kusifu na kuabudu bila kutathimini ukweli, uongo na propaganda.

Any way, I don't acknowledge the mess.
 
manonawire, post: 33269260, member: 470499"]
Ukifanya ukafiri ili upate mali, ni lazima moto ukuchome.

Tutakunyofoa kabisa na genge lako la kutaka kufanya ukafiri.

Poise
Ila ww n mkali khaaa
Nn kubishana na watu vile , ila uko vzur boss unajua vitu kutokana na position yako
[/QUOTE]


Huwa sipendi mtu anayejionesha kuwa yeye ni mtu wa intelijensia ; halafu ni muongo.

Sipendi kulea watu wa hovyo hovyo ambao watasababisha Taifa kuwa na kizazi cha hovyo cha kusifu na kuabudu bila kutathimini ukweli, uongo na propaganda.

Any way, I don't acknowledge the mess.
[/QUOTE]
Ok dhamira yako n mzuri
 
Hongera sana mwandishivwa Nalala hii "The Bold" ubatikwe sana . wengine tumeongeza ufahamu tu lkn hatuna Mawazo na uwezo wa kumiliki chochote kikubwa zaidi ya familia yangu.
Mimi nilimpenda huyu Abromovich badala ya kuiinua Chelsea. Kimsingi nilikuwa siipendi Man u, arsenal na Liverpool's KUTOKANA na Maneno mengi ya wapenzi wao. Napo ukiweza tuwekee kwa uchache alipataje inunua chelsea
 
The bold,sweettablet ,
Mwanzoni mwa makala hii nilijenga hoja kwamba si jambo jepesi sana kuwa bilionea. Unaweza kuwa tajiri… milionea, hakuna shida wala shaka. Lakini kutengeneza utajiri wa kufikia dola bilioni moja na zaidi ni lazima ukubali mikono yako kuchafuka ‘vumbi’ kidogo. Muulize Mo Dewji, msome Gates na alichowafanyia IBM na Steve, chunguza vifo vilivyotokea mwanzoni kwa kuanzishwa kwa Facebook na alichokifanya Mark, muulize Aliko Dangote, teta na akina Motsepe na familia ya Gupta pale Afrika Kusini.
Wote hawa hawawezi kukataa kwamba “behind every great fortune lies a great crime.” Kila utajiri una ukafiri nyuma yake.

MWISHO

H.B ANGA “THE BOLD”

To Infinity and Beyond



Nilikuandikia kuwa ukiwa muongo, au ukiwa na maarifa na taarifa kidogo,, Jifunze sana kutunza kumbukumbu.
REJEA COMMENT YANGU NO. 1022.


Uliandika kuwa mauji hayapo Ulaya, Afrika, kama ilivyokuwa huko Russia kwa ulimwengu wa sasa ila sehemu yako hii ya mwisho umeonyesha waziwazi kuwa Uingereza, watu wanauawa, na unahitimisha kwa kutaja majina na nchi ambako mambo hayo yanafanyika.

Wewe ni uchwara katika intelijensia na hauna connection yoyote na mtu wa intelijensia bali wewe ni mlamba viatu vya watu ili wakupe taarifa ila unapewa taarifa uchwara.

Eti ,, unajinadi kwamba una taarifa zote za kiintelijensia ya nchi za Afrika Mashariki.

Boy, remember ; "Always, I don't acknowledge the mess"
Poise, najua mwimbaji ni wewe. Aliyetunga taarabu yako nani? Aliyetia muziki nani! Wenzako akina Mzee Yusuph huwa wanawataja!
 
sweettablet, post: 33270389, member: 259334"]
Poise, najua mwimbaji ni wewe. Aliyetunga taarabu yako nani? Aliyetia muziki nani! Wenzako akina Mzee Yusuph huwa wanawataja!
[/QUOTE]

Ufahamu wangu ni wa kusimamia na kuongoza watu 1 Billioni wasomi wa ngazi ya uzamivu (PhD) na wenye sifa ya kiprofesa katika taaluma.

Kwa hiyo mtu yeyote aliye na unyafuzi wa kiakili hawezi kuona ninachokiona au kuandika ninachokiandika hapa.

Wewe endelea kumezeshwa chibuku ; tatizo lako ni unyafuzi wa kiakili ulioupata wakati unazaliwa!
 
Back
Top Bottom