Habibu B. Anga
JF-Expert Member
- May 7, 2013
- 6,557
- 25,717
- Thread starter
- #1,101
ROMAN ABRAMOVICH: MABILIONI YA DAMU, RISASI NA UMAFIA
FINALE
Safari ya Abramovich kwenda London ilikuwa mahususi kwa ajili ya kwenda kuonana na mentor wake huyo wa zamani akiwa na maagizo kutoka juu kwa bwana mkubwa… Putin. Maagizo haya yalikuwa ‘straight’ bila kupiga piga chenga. Kwamba Berezovsky anafahamu kuwa hakuna mahala ambako anaweza kujificha na mkono wa Putin ukashindwa kumfikia. Kwa hiyo Putin alikuwa anampa sharti moja tu… kwamba Berezosky amuuzie Roman Abramovich kituo cha televsheni na akikubali kufanya hivyo Putin atamuacha aishi.
Kituo hiki cha televisheni kilikuwa na thamani ya mabilioni ya dola lakini Abramovich alimuambia Berezosvky kwamba atakinunua kwa dola milioni 150 tu. Berezovsky akakataa.
Abramovich akarudi Russia kupeleka mrejesho kwa Putn kwamba Berezovsky amekataa. Putin akamtuma tena Abramovich kwenda London na ofa nyingine mpya.
Safari hii alipokutana na Berezovsky alimueleza kwamba yeye mwenyewe yuko tayari kupandisha kidogo dau lake la kununua kituo cha televisheni na atampa dola milioni 175. Na si hivyo tu bali pia kama atakubali kumuuzia kituo hicho cha televisheni basi Putin atamuachia huru rafiki yake kipenzi Glushkov ambaye tayari alikuwa anatumikia kifungo jela.
Kitendo cha kusikia kuwa rafiki yake kipenzi Glushkov ataachiwa huru, Berezovsky hakuwa na nguvu tena ya kukataa ofa ya Abramovich, akakubali kumuuzia kituo chake cha televisheni. Na huo ndio ukawa mwisho wa uhuru wa habari nchini Rusia mpaka leo hii maana kituo cha Berezovsky ndio kilikuwa na ushawishi zaidi nchini Russia. Na Abramovich baada tu ya kukinunua kutoka kwa Berezovsky alikikabidhi mikononi mwa Putin akitumie anavyotaka.
Jambo baya zaidi ile ahadi yao ya kumuachia Glushkov hawakuitimiza. Glushkov akaendelea kusota jela. Kuna kipindi akawekewa mtego akiwa amepelekwa hospitali kutibiwa maaskari magereza wakamuacha chumbani peke yake na akataka kutoroka. Akakamatwa tena na kuongezewa kifungo. Maoligarch kadhaa nao wakakamatwa kwa tuhuma za kupanga njama ya kumtorosha Glushkov. Ule mtandao wa maoligarch uliokuwa unaongozwa na Berezosvky ambao ulikuwa unampiga vita Putin na Abramovich ukasambaratishwa wote. Maoligarch wengine waliosalia wakaelewa somo… ukitaka kusurvive kibiashara ndani ya Russia kuna mtu mmoja haupaswi kumgusa… Roman Abramovich.
Nilikuwa natamani niishie hapa lakini kuna kionjo kidogo wacha nikisimulie pia ili uone uwezo wa Abramovich kucheza na ‘system’ ya dunia. Hata ‘wazungu’ wa magharibi amewahi kuwafanyia uhuni ambao hata sasa hawaamini macho yao.
Pale ulaya wana benki yao, European Bank. Mwishoni mwa mwaka 1998 kuna benki ya kirusi inaitwa SBS Agro ilichukua mkobo wa hela nyingi sana, mabilioni ya Euro. Ikapita kama miaka miwili hivi pasipo SBS Agro kulipa deni lake. Baada ya kuona deni hilo halilipwi European Bank wakahitaji dhamana ya mkopo huo kutoka kwa SBS Agro. Kama dhamana, SBS Agro wali-plegde deni la dola milioni 14 ambalo wanadai kwa kampuni inaitwa RUNICOM S.A. ambayo imesajiliwa nchini Uswisi. Na hapa ndipo ambapo jina la Abramovich linatokea… kampuni hii ya RUBICOM S.A faida yake kubwa walikuwa wanaipata kwa kuuza mafuta ya kampuni ya Sibneft kwenye nchi za ulaya. Katika kipindi hiki pia benki ile ya SBS Agro ilitangaza kufilisika. Lakini European Bank hawakuwa na wasiwasi kwa sababu deni lao lilikuwa ‘guaranteed’ na RUNICOM S.A… sijui kama naeleweka sawasawa…
Sasa basi,
European Bank wakaanza kuwadai RUNICOM S.A. Wakadai sana bila mafanikio… ikabidi uitishwe uchunguzi kuangalia mali za kampuni ili wajue namna gani wanaweza kurudisha fedha zao. Katika uchunguzi wao huu mkazo mkubwa uliwekwa kwenye kuingalia biashara ya mafuta ambayo RUNICOM walikuwa wanaifanya kwa sababu nyaraka zilionyesha kwamba faida yao kubwa ilitoka huko. Hawakuamini macho yao walipogundua kuwa biashara ile ya mafuta ya Sibneft kama miezi sita iliyopita ilikuwa imehamishiwa kwenye kampuni nyingine iliyosajiliwa nchini Cyprus ikiitwa RUNICOM LIMITED.
European Bank wakafura kweli kweli… hii ndio ile kwa umombo wanaita ‘sleight of hand’. Ushawahi kuona mchezo wa karata tatu… anazivuruga vuruga unahisi umeona sawia kuwa shupaza iko pale mkono wa kulia lakini akifunua unakuta kuna dume la kopa. Hii iliyokuwa inafanyika twaweza kusema ilikuwa ‘financial sleight of hand’… abracadabra.
Kuna kitu gani ambacho kinafanana kwenye huu msululu wote? SBS Agro waliokopa awali ni kampuni ya kirusi (Roman Abramovich ni mrusi). Walio gurantee huo mkopo RUNICOM S.A faida yao kubwa walikuwa wanaipata kwa kuuza mafuta ya sibneft kwenye nchi za ulaya (Roman Abramovich ndiye mmiliki wa Sibneft). RUNICOM LIMITED walirithishwa biashara ya mafuta ya sibneft kutoka RUNICOM S.A (Sibneft… Abramovich).
European Bank wakafura zaidi… ilikuwa wazi kwamba ujanja huu walikuwa wanafanyiwa na Roman Abramovich lakini ubaya ni kwamba huwezi kumshtaki kwa kuwa siye uliyemkopesha… walimkopesha nani? SBS Agro… European Bank wakaenda mhakamani. Kesi ikaunguruma kwa miaka miwili. Hukumu ikatolewa kwamba European Bank walipwe kiasi cha dola milioni 24. Lakini nani akulipe?? SBS Agro walishatangaza kufilisika miaka miwili iliyopita na kampuni haipo tena… nani atakulipa hela hizo? Mpaka leo hii ninapoandika makala hii deni hilli halijalipwa na kamwe halitolipwa na ubaya ni kwamba muhusika mkuu na aliyenufaika na mkopo unamjua lakini huwezi kumshitaki kwa sababu hakuna jina lake halijatokea popote kwenye nyaraka na wala hukumkopesha. Tangu kipindi hicho wazungu wanalijua vyema jina la Abramovich na ni mtu wa namna gani.
Kuna watu ukiwasimulia upande huu wa pili wa Abramovich ambao hawajawahi kuusikia watakwambia kuhusu miradi mikubwa ya kijamii ambayo aliifanya akiwa kama gavana wa Chukokta. Jibu langu siku zote ni kweli kwamba Abramovich alitumia fedha zake binafsi karibia dola blioni 3 kwa muda wote aliokuwa gavana wa Chukokta… lakini je unafahamu alinufaikaje?
Baada ya Putin kuwa Rais akampa Baraka Abramovich kuingia kwenye siaisa. Ukitoka pale Kremlin, mwendo wa ndege kama masaa tisa hivi kuna jimbo masikini mno mno linaitwa Chukokta. Hili ndilo ambalo Abramovich aligombea ugavana na kushinda. Alitumia mabilioni ya hela zake kwa ajili ya maendeleo lakini wengi wasichojua ni kwamba alinufaika zaidi. Akiwa kama gavana alikuwa anashawishi sheria ndogo za kodi na misamaha ya kodi kwa kampuni wanazoziona zinafaa. Sasa ile kampuni yake ya Sibneft visima vyake vya mafuta viko Siberia. Walichokuwa wanafanya walikuwa wanauza mafuta yao ya Sibneft kwa bei ya kutupa kwa kampuni ambazo walizisajili kwenye jimbo la Chukokta. Kisha kampuni hizi za Chukokta wanauza mafuta hayo nje ya Russia kwa kampuni dada ya Sibneft kama vile RUNICOM S.A. na walifanya hivi kwa kuwa mafuta haya yakitokea Chukokta yalikuwa na msamaha wa kodi.
Kwa hiyo ni kweli Abramovich alikuwa anasadia lakini papo papo alikuwa ananufaika zaidi.
Wale ‘maswahiba’ wake wa zamani wako wapi?
Mentor wake Boris Berezovsky ambaye alikuja kuwa adui mkubwa siku ya March 23 mwaka 2013 alikutwa amefariki bafuni nyumbani kwake Barkshire, Uingereza. Kifo chake bado kina ubishani mkubwa baadhi ya wachunguzi wa masuala ya post mortem wakisema amejiua wengine wakisema ameuwawa. Wengine wanadai alijiua baada ya kuandamwa na madeni kutokana na kushindwa kesi ambayo alimfungulia Abramovich kugombea umiliki wa Sibneft akitaka kulipwa fidia ya dola bilioni 6 kesi ambayo ilisikilizwa nchini Uingereza na Abramovich kushinda. Hili suala la kugombea Sibneft sijalieleza humu… ila kwa kifupi tu Abramovich alimpiga mchanga wa macho mentor wake… unakumbuka nilieleza kwamba enzi zile za utawala wa Yeltsin Abramovich na Berezovsky walinunua kwa pamoja Sibneft kwenye mnada wa ulaghai ambao wao pekee ndio walikuwa ‘bidders’. Nadhani tunakumbuka vyema… sasa baada ya Berezovsky kukimbia Urusi, Abramovich akafanya janja janja na kumuondoa Berezovsky kwenye umiliki. Berezosvky akafungua kesi.
Abramovich alishinda kesi.
Wanadai kwamba kesi ile ilimfilisi Berezovsky kwa kulipa gharama kubwa za mawakili.
Lakini tukitazama nyuma kidogo tuna pata picha ya tofauti na pengine kutupa dalili kuwa Berezovsky aliuwawa. Novemba mwaka 2006 mshirika wake wa karibu sana Alexander Litvinenko aliuwawa kwa Polonium hapo hapo Uingereza.
Miaka miwili baadae yule rafiki yake Badri ambaye kipindi wako Russia alikuwa anasimamia televisheni yake alikutwa amefariki chumbani kwake hapo hapo Uingereza.
Kama hiyo haitoshi yule rafiki yake kipenzi Nikolai Glushkov alimaliza vifungo vyake na kutoka jela na kukimbilia nchini Uingereza. Huyu naye mwaka jana tu hapa 2018 mwezi March amekutwa amefariki nyumbani kwake hapo hapo Uingereza.
Kwa hiyo maoligarch wote ambao walianzisha vita dhidi ya Putin na Abramovich wote wamefariki vifo vya utata wakiwa na afya njema kabisa… lakini wale wote ambao walikuwa wapole na kumuunga mkono Abramovich kama vile akina Deripaska wako hai hata sasa na utajiri wao ukizidi kupaa kila uchwao.
Mwanzoni mwa makala hii nilijenga hoja kwamba si jambo jepesi sana kuwa bilionea. Unaweza kuwa tajiri… milionea, hakuna shida wala shaka. Lakini kutengeneza utajiri wa kufikia dola bilioni moja na zaidi ni lazima ukubali mikono yako kuchafuka ‘vumbi’ kidogo. Muulize Mo Dewji, msome Gates na alichowafanyia IBM na Steve, chunguza vifo vilivyotokea mwanzoni kwa kuanzishwa kwa Facebook na alichokifanya Mark, muulize Aliko Dangote, teta na akina Motsepe na familia ya Gupta pale Afrika Kusini.
Wote hawa hawawezi kukataa kwamba “behind every great fortune lies a great crime.” Kila utajiri una ukafiri nyuma yake.
MWISHO
H.B ANGA “THE BOLD”
To Infinity and Beyond
FINALE
Safari ya Abramovich kwenda London ilikuwa mahususi kwa ajili ya kwenda kuonana na mentor wake huyo wa zamani akiwa na maagizo kutoka juu kwa bwana mkubwa… Putin. Maagizo haya yalikuwa ‘straight’ bila kupiga piga chenga. Kwamba Berezovsky anafahamu kuwa hakuna mahala ambako anaweza kujificha na mkono wa Putin ukashindwa kumfikia. Kwa hiyo Putin alikuwa anampa sharti moja tu… kwamba Berezosky amuuzie Roman Abramovich kituo cha televsheni na akikubali kufanya hivyo Putin atamuacha aishi.
Kituo hiki cha televisheni kilikuwa na thamani ya mabilioni ya dola lakini Abramovich alimuambia Berezosvky kwamba atakinunua kwa dola milioni 150 tu. Berezovsky akakataa.
Abramovich akarudi Russia kupeleka mrejesho kwa Putn kwamba Berezovsky amekataa. Putin akamtuma tena Abramovich kwenda London na ofa nyingine mpya.
Safari hii alipokutana na Berezovsky alimueleza kwamba yeye mwenyewe yuko tayari kupandisha kidogo dau lake la kununua kituo cha televisheni na atampa dola milioni 175. Na si hivyo tu bali pia kama atakubali kumuuzia kituo hicho cha televisheni basi Putin atamuachia huru rafiki yake kipenzi Glushkov ambaye tayari alikuwa anatumikia kifungo jela.
Kitendo cha kusikia kuwa rafiki yake kipenzi Glushkov ataachiwa huru, Berezovsky hakuwa na nguvu tena ya kukataa ofa ya Abramovich, akakubali kumuuzia kituo chake cha televisheni. Na huo ndio ukawa mwisho wa uhuru wa habari nchini Rusia mpaka leo hii maana kituo cha Berezovsky ndio kilikuwa na ushawishi zaidi nchini Russia. Na Abramovich baada tu ya kukinunua kutoka kwa Berezovsky alikikabidhi mikononi mwa Putin akitumie anavyotaka.
Jambo baya zaidi ile ahadi yao ya kumuachia Glushkov hawakuitimiza. Glushkov akaendelea kusota jela. Kuna kipindi akawekewa mtego akiwa amepelekwa hospitali kutibiwa maaskari magereza wakamuacha chumbani peke yake na akataka kutoroka. Akakamatwa tena na kuongezewa kifungo. Maoligarch kadhaa nao wakakamatwa kwa tuhuma za kupanga njama ya kumtorosha Glushkov. Ule mtandao wa maoligarch uliokuwa unaongozwa na Berezosvky ambao ulikuwa unampiga vita Putin na Abramovich ukasambaratishwa wote. Maoligarch wengine waliosalia wakaelewa somo… ukitaka kusurvive kibiashara ndani ya Russia kuna mtu mmoja haupaswi kumgusa… Roman Abramovich.
Nilikuwa natamani niishie hapa lakini kuna kionjo kidogo wacha nikisimulie pia ili uone uwezo wa Abramovich kucheza na ‘system’ ya dunia. Hata ‘wazungu’ wa magharibi amewahi kuwafanyia uhuni ambao hata sasa hawaamini macho yao.
Pale ulaya wana benki yao, European Bank. Mwishoni mwa mwaka 1998 kuna benki ya kirusi inaitwa SBS Agro ilichukua mkobo wa hela nyingi sana, mabilioni ya Euro. Ikapita kama miaka miwili hivi pasipo SBS Agro kulipa deni lake. Baada ya kuona deni hilo halilipwi European Bank wakahitaji dhamana ya mkopo huo kutoka kwa SBS Agro. Kama dhamana, SBS Agro wali-plegde deni la dola milioni 14 ambalo wanadai kwa kampuni inaitwa RUNICOM S.A. ambayo imesajiliwa nchini Uswisi. Na hapa ndipo ambapo jina la Abramovich linatokea… kampuni hii ya RUBICOM S.A faida yake kubwa walikuwa wanaipata kwa kuuza mafuta ya kampuni ya Sibneft kwenye nchi za ulaya. Katika kipindi hiki pia benki ile ya SBS Agro ilitangaza kufilisika. Lakini European Bank hawakuwa na wasiwasi kwa sababu deni lao lilikuwa ‘guaranteed’ na RUNICOM S.A… sijui kama naeleweka sawasawa…
Sasa basi,
European Bank wakaanza kuwadai RUNICOM S.A. Wakadai sana bila mafanikio… ikabidi uitishwe uchunguzi kuangalia mali za kampuni ili wajue namna gani wanaweza kurudisha fedha zao. Katika uchunguzi wao huu mkazo mkubwa uliwekwa kwenye kuingalia biashara ya mafuta ambayo RUNICOM walikuwa wanaifanya kwa sababu nyaraka zilionyesha kwamba faida yao kubwa ilitoka huko. Hawakuamini macho yao walipogundua kuwa biashara ile ya mafuta ya Sibneft kama miezi sita iliyopita ilikuwa imehamishiwa kwenye kampuni nyingine iliyosajiliwa nchini Cyprus ikiitwa RUNICOM LIMITED.
European Bank wakafura kweli kweli… hii ndio ile kwa umombo wanaita ‘sleight of hand’. Ushawahi kuona mchezo wa karata tatu… anazivuruga vuruga unahisi umeona sawia kuwa shupaza iko pale mkono wa kulia lakini akifunua unakuta kuna dume la kopa. Hii iliyokuwa inafanyika twaweza kusema ilikuwa ‘financial sleight of hand’… abracadabra.
Kuna kitu gani ambacho kinafanana kwenye huu msululu wote? SBS Agro waliokopa awali ni kampuni ya kirusi (Roman Abramovich ni mrusi). Walio gurantee huo mkopo RUNICOM S.A faida yao kubwa walikuwa wanaipata kwa kuuza mafuta ya sibneft kwenye nchi za ulaya (Roman Abramovich ndiye mmiliki wa Sibneft). RUNICOM LIMITED walirithishwa biashara ya mafuta ya sibneft kutoka RUNICOM S.A (Sibneft… Abramovich).
European Bank wakafura zaidi… ilikuwa wazi kwamba ujanja huu walikuwa wanafanyiwa na Roman Abramovich lakini ubaya ni kwamba huwezi kumshtaki kwa kuwa siye uliyemkopesha… walimkopesha nani? SBS Agro… European Bank wakaenda mhakamani. Kesi ikaunguruma kwa miaka miwili. Hukumu ikatolewa kwamba European Bank walipwe kiasi cha dola milioni 24. Lakini nani akulipe?? SBS Agro walishatangaza kufilisika miaka miwili iliyopita na kampuni haipo tena… nani atakulipa hela hizo? Mpaka leo hii ninapoandika makala hii deni hilli halijalipwa na kamwe halitolipwa na ubaya ni kwamba muhusika mkuu na aliyenufaika na mkopo unamjua lakini huwezi kumshitaki kwa sababu hakuna jina lake halijatokea popote kwenye nyaraka na wala hukumkopesha. Tangu kipindi hicho wazungu wanalijua vyema jina la Abramovich na ni mtu wa namna gani.
Kuna watu ukiwasimulia upande huu wa pili wa Abramovich ambao hawajawahi kuusikia watakwambia kuhusu miradi mikubwa ya kijamii ambayo aliifanya akiwa kama gavana wa Chukokta. Jibu langu siku zote ni kweli kwamba Abramovich alitumia fedha zake binafsi karibia dola blioni 3 kwa muda wote aliokuwa gavana wa Chukokta… lakini je unafahamu alinufaikaje?
Baada ya Putin kuwa Rais akampa Baraka Abramovich kuingia kwenye siaisa. Ukitoka pale Kremlin, mwendo wa ndege kama masaa tisa hivi kuna jimbo masikini mno mno linaitwa Chukokta. Hili ndilo ambalo Abramovich aligombea ugavana na kushinda. Alitumia mabilioni ya hela zake kwa ajili ya maendeleo lakini wengi wasichojua ni kwamba alinufaika zaidi. Akiwa kama gavana alikuwa anashawishi sheria ndogo za kodi na misamaha ya kodi kwa kampuni wanazoziona zinafaa. Sasa ile kampuni yake ya Sibneft visima vyake vya mafuta viko Siberia. Walichokuwa wanafanya walikuwa wanauza mafuta yao ya Sibneft kwa bei ya kutupa kwa kampuni ambazo walizisajili kwenye jimbo la Chukokta. Kisha kampuni hizi za Chukokta wanauza mafuta hayo nje ya Russia kwa kampuni dada ya Sibneft kama vile RUNICOM S.A. na walifanya hivi kwa kuwa mafuta haya yakitokea Chukokta yalikuwa na msamaha wa kodi.
Kwa hiyo ni kweli Abramovich alikuwa anasadia lakini papo papo alikuwa ananufaika zaidi.
Wale ‘maswahiba’ wake wa zamani wako wapi?
Mentor wake Boris Berezovsky ambaye alikuja kuwa adui mkubwa siku ya March 23 mwaka 2013 alikutwa amefariki bafuni nyumbani kwake Barkshire, Uingereza. Kifo chake bado kina ubishani mkubwa baadhi ya wachunguzi wa masuala ya post mortem wakisema amejiua wengine wakisema ameuwawa. Wengine wanadai alijiua baada ya kuandamwa na madeni kutokana na kushindwa kesi ambayo alimfungulia Abramovich kugombea umiliki wa Sibneft akitaka kulipwa fidia ya dola bilioni 6 kesi ambayo ilisikilizwa nchini Uingereza na Abramovich kushinda. Hili suala la kugombea Sibneft sijalieleza humu… ila kwa kifupi tu Abramovich alimpiga mchanga wa macho mentor wake… unakumbuka nilieleza kwamba enzi zile za utawala wa Yeltsin Abramovich na Berezovsky walinunua kwa pamoja Sibneft kwenye mnada wa ulaghai ambao wao pekee ndio walikuwa ‘bidders’. Nadhani tunakumbuka vyema… sasa baada ya Berezovsky kukimbia Urusi, Abramovich akafanya janja janja na kumuondoa Berezovsky kwenye umiliki. Berezosvky akafungua kesi.
Abramovich alishinda kesi.
Wanadai kwamba kesi ile ilimfilisi Berezovsky kwa kulipa gharama kubwa za mawakili.
Lakini tukitazama nyuma kidogo tuna pata picha ya tofauti na pengine kutupa dalili kuwa Berezovsky aliuwawa. Novemba mwaka 2006 mshirika wake wa karibu sana Alexander Litvinenko aliuwawa kwa Polonium hapo hapo Uingereza.
Miaka miwili baadae yule rafiki yake Badri ambaye kipindi wako Russia alikuwa anasimamia televisheni yake alikutwa amefariki chumbani kwake hapo hapo Uingereza.
Kama hiyo haitoshi yule rafiki yake kipenzi Nikolai Glushkov alimaliza vifungo vyake na kutoka jela na kukimbilia nchini Uingereza. Huyu naye mwaka jana tu hapa 2018 mwezi March amekutwa amefariki nyumbani kwake hapo hapo Uingereza.
Kwa hiyo maoligarch wote ambao walianzisha vita dhidi ya Putin na Abramovich wote wamefariki vifo vya utata wakiwa na afya njema kabisa… lakini wale wote ambao walikuwa wapole na kumuunga mkono Abramovich kama vile akina Deripaska wako hai hata sasa na utajiri wao ukizidi kupaa kila uchwao.
Mwanzoni mwa makala hii nilijenga hoja kwamba si jambo jepesi sana kuwa bilionea. Unaweza kuwa tajiri… milionea, hakuna shida wala shaka. Lakini kutengeneza utajiri wa kufikia dola bilioni moja na zaidi ni lazima ukubali mikono yako kuchafuka ‘vumbi’ kidogo. Muulize Mo Dewji, msome Gates na alichowafanyia IBM na Steve, chunguza vifo vilivyotokea mwanzoni kwa kuanzishwa kwa Facebook na alichokifanya Mark, muulize Aliko Dangote, teta na akina Motsepe na familia ya Gupta pale Afrika Kusini.
Wote hawa hawawezi kukataa kwamba “behind every great fortune lies a great crime.” Kila utajiri una ukafiri nyuma yake.
MWISHO
H.B ANGA “THE BOLD”
To Infinity and Beyond