RPC Kinondoni aliyemwambia Mbowe hachomoki ndiye alimwambia Lema hashindi Arusha

RPC Kinondoni aliyemwambia Mbowe hachomoki ndiye alimwambia Lema hashindi Arusha

Kumbe huyu RPC ambaye alimtolea maneno mabaya Mbowe kuwa "this time huchomoki tutakupiga na kesi ya ugaidi(kwa maneno ya John Mrema) "vile vile aliwahi kumwambia Lema akiwa RCO Arusha kuwa hatashinda uchaguzi kwa sababu yeye ni Kada. Maneno haya aliyasema ndugu Godbless Lema mbunge mstaafu Arusha mjini kupitia kipindi cha mtandaoni cha Maria Space.

Hili ndio jeshi letu la polisi, kiongozi wake anafanya kazi kwa kusukumwa na siasa kuumiza wengine makusudi. Jeshi linaendeshwa kwa misukumo ya kisiasa tuseme kuwa Tanzania tunailinda upendo na mshikamano wetu? Hawa si ndio polisi wavuruga amani?

IGP Simon Siro hili ndio jeshi lako linalofanya kazi na kujawa kibri kufikia hatua hii. Si ajabu hii taarifa iliyosomwa na jeshi la polisi ilikua na maneno ya huyu RPC.

Ni dhambi kubwa sana kumtuhumu mtu kesi nzito kiasi hicho ikiwa hajawahi hata kutishia mtu mabati.

Itakuwa ni a aibu sana kwa Jeshi la Polisi siku akigundulika hana hatia maana kesi yoyote ile ni ushahidi.
Ni aibu hata kutamka kuwa ni jeshi. Jeshi gani halifuati miiko? Hata kama lengo la polisi ni kumfungulia kesi ya ugaidi, huyo rpc ni kielelezo cha mdudu ndani ya polisi. Unawezaje kutamka jambo kama hilo kwa style hiyo.....anaweza akatunza siri za polisi n anchi huyo?
 
Jukumu namba moja la police ni kuilinda ccm isianguke.
 
Wakuu wa vyombo vyote vya ulinzi wakistaaafu urudi kupewa fadhila kwa nafasi za kisiasa kama asante ya kuilinda ccm isianguke.
 
Katiba imekaa vibaya ndiyo maana hatuna maendeleo
Maendeleo hayatokuwepo ni hadi Yale maagano na shetani mapangoni bagamoyo yavunjwe na mwenge utupwe baharini kabisa Ili usiendelee kupumbaza watz,karne ya 21 bado tunazungusha uchawi wa moto.
 
Wanazidiwa hata na police wa Malawi Katu huwezi kuta wanatumwa na chama,wale wanalindana nchi na sio kulinda chama.
 
Hivi hawa polisi wanaofanya uonevu kwa watu wengine wana familia kweli hawa? Na je, familia zao wanazificha kwenye safety vaults au?

Hawa askari hawajiulizi ni kwa kiasi gani wanaziumiza hisia za wanafamilia au ndugu wa hawa wanaowatesa sasa?

Je, hawajui kuwa kuna kitu kinaitwa vendetta? Vendetta inaweza isitokee leo lakini inaweza kutokea 10 years to come. Je wakati huo askari hawa watesaji watakuwa na uwezo wa kuzilinda familia zao dhidi ya vendetta?

They should always remember - what goes around.......................
 
Tatizo sio CCM Wala Chadema au hyo katiba mpya unayoitaka, kumbuka unatakiwa kuwa na familia Bora ili wanaowasije kuwa watu wakulalamika lalamika kila wakati.

Amka acha ujinga fanya kazi kwa juhudi tafuta hela na ukishapata pesa utakuja kugundua kuwa kumbe Kuna mtaji mkubwa Sana kwenye nchi hii nao Ni watu wasiojitambua wanataka Nini sio wengine Bali Ni vijana waliowengi wakitanzania.

Tafuta pesa uipate, ili upate pesa au uishi maisha mazuri na familia yako na wanaokuzunguka hayaitaji katiba mpya Wala usaidizi wa CCM au chadema Bali n kujituma katika kutafuta pesa.

Ukipata pesa haya Mambo ya makato ya simu hutayaona makubwa Bali utaona n nafasi nyingine ya kupata zaidi kwa namna moja au nyingine. (Uamue usitumie simu kwa malipo ubaki na benki tuu au utumie simu kwa kunufaika wewe na wateja wako.)
Mkuu uko sawa we huoni hata hao wenye hela wanavyo sumbuliwa mara account zao zifungiwe waporwe pesa zote mara wabikiziwe kodi kubwa yaani ni tafrani hii nchi ipo siku japo siombei itokeee lile lilitokea nchi za kiarabu litatokea na huku ndipo amani hata hii ya uoga tuliyonayo haitarudi mpaka yesu arudi
 
Uzi wako utachezea figusi si mda utabaki wewe tu.maana ya moyoni kutoa ukweli humu ni kosa jf
Askari wetu na familia zao wakipatwa na tatizo kama hilo tunaanza na mwenye kiti wenu ye sio ndio kiongozi mkuu na muhamasishaji vurugu halafu tunafata mmoja mmoja kama nyie ni kazi ndogo sana ndani ya wiki mmoja kazi imeish.
 
Kumbe huyu RPC ambaye alimtolea maneno mabaya Mbowe kuwa "this time huchomoki tutakupiga na kesi ya ugaidi(kwa maneno ya John Mrema) "vile vile aliwahi kumwambia Lema akiwa RCO Arusha kuwa hatashinda uchaguzi kwa sababu yeye ni Kada. Maneno haya aliyasema ndugu Godbless Lema mbunge mstaafu Arusha mjini kupitia kipindi cha mtandaoni cha Maria Space.

Hili ndio jeshi letu la polisi, kiongozi wake anafanya kazi kwa kusukumwa na siasa kuumiza wengine makusudi. Jeshi linaendeshwa kwa misukumo ya kisiasa tuseme kuwa Tanzania tunailinda upendo na mshikamano wetu? Hawa si ndio polisi wavuruga amani?

IGP Simon Siro hili ndio jeshi lako linalofanya kazi na kujawa kibri kufikia hatua hii. Si ajabu hii taarifa iliyosomwa na jeshi la polisi ilikua na maneno ya huyu RPC.

Ni dhambi kubwa sana kumtuhumu mtu kesi nzito kiasi hicho ikiwa hajawahi hata kutishia mtu mabati.

Itakuwa ni a aibu sana kwa Jeshi la Polisi siku akigundulika hana hatia maana kesi yoyote ile ni ushahidi.
Polisi wetu wapo juu ya Sheria Hakuna cha kuwafanya

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Katiba ni tatizo kubwa sana na ni chanzo cha kutokupata maendeleo, madaraka yote yamehodhiwa na viongozi na sii wananchi.

Centralized economy-ujamaa bado ni kitendawili kigumu. Hizi Siasa zilishindikana China na Russia. Sisi tumezingangania.
 
Sio jeshi la polisi tu, vyombo vyote vya usalama vimejazwa ma CCM.

View attachment 1868427

View attachment 1868428
Afisa mstaafu wa jeshi kuwa mwanachama wa chama cha siasa si dhambi wala si kosa.
Tena ni kawaida sana kwa nchi zilizo endelea kidemokrasia kama Marekani.
Unajuwa kama Raisi Bush ni veteran wa jeshi pia ni mwanachama wa Republican.
Unajuwa maraisi wangapi wa Marekani walikuwa askari zamani kabla ya kuingia kwenye vyama vya siasa?

Msikariri mambo mtafute maarifa na taarifa.
 
Mkuu uko sawa we huoni hata hao wenye hela wanavyo sumbuliwa mara account zao zifungiwe waporwe pesa zote mara wabikiziwe kodi kubwa yaani ni tafrani hii nchi ipo siku japo siombei itokeee lile lilitokea nchi za kiarabu litatokea na huku ndipo amani hata hii ya uoga tuliyonayo haitarudi mpaka yesu arudi
Nchi hii wanaolipa Kodi kwa wakati Ni wafanyakazi tuu sababu inakatwa pale mshahara unapowekwa kwenye account huko kwenye Biashara Kuna Mambo Sana naomba niishie hapa
 
Wakati wanajifurahisha kukomoa na kubambikizwa kesi way sehemu Fulani wanawachabo na kuondoa Imani nao kimataifa
 
Basi hata mwenyekiti hataweza kuchomoka katika hili cz ndiye aliyemwakikishia Rema kustaafu kwakwe.


#fikrahuru
 
Afisa mstaafu wa jeshi kuwa mwanachama wa chama cha siasa si dhambi wala si kosa.
Tena ni kawaida sana kwa nchi zilizo endelea kidemokrasia kama Marekani.
Unajuwa kama Raisi Bush ni veteran wa jeshi pia ni mwanachama wa Republican.
Unajuwa maraisi wangapi wa Marekani walikuwa askari zamani kabla ya kuingia kwenye vyama vya siasa?

Msikariri mambo mtafute maarifa na taarifa.
Tatizo sio Afisa Mstaafu, tatizo ni professionalism. Wenzetu wamefikia kiwango kikubwa cha weledi kiasi kwamba mara nyingi hawafanyi maamuzi kwa kufuata itikadi zao.

Huku kwetu hali sio hiyo. Siasa ziliingizwa kwenye vyombo kwa makusudi. Inakuwaje RPC wa Arusha anatoa salamu ya chama? Huoni shida hapo. Tunataka vyombo viwe nje ya siasa kweli kweli. Na huko Marekani ulikotoa mfano, wengi wa former officer wanapitakana vyama vyote. Mbona huku kwetu, kila former wanakuwa CCM tu?
 
Back
Top Bottom