Rufiji: Vijiji 23 vimekumbwa na mafuriko makubwa kutoka Bwawa la Umeme la JNHPP. Je, Tathmini ya athari kwa mazingira ilipuuzwa kabla ya ujenzi?

Rufiji: Vijiji 23 vimekumbwa na mafuriko makubwa kutoka Bwawa la Umeme la JNHPP. Je, Tathmini ya athari kwa mazingira ilipuuzwa kabla ya ujenzi?

Acha ujinga,ungesoma hata mada uelewe.

Tatizo lilikuwepo na mojawapo ya sababu za kujenga bwawa tuliambiwa litadhibiti Mafuriko badala yake limeongeza Ukubwa wa tatizo.

Yote hii ni Kwa sababu ya kukurupuka ,wangefanya EIA wangejua namna Bora ya kulijenga Ili li save purpose zote.
Wewe mwenyewe unasemaje tatizo lilikuwepo, Kwa hiyo chanzo chake sio uwepo wa Bwawa.
La kujiuliza sasa ni kwanini uwepo wa Bwawa hakujatatua tatizo.
Na ukumbukmbe matarajio ya awamu ya Tano na matarajio ya awamu ya February yalikuwa tofauti, mpaka kumalizika Kwa Bwawa Hilo na kuanza uzalishaji .
Sasa watu wenye uelewa huanza kufanya ulinganishona tofauti za taarifa za Awamu ya Tano na za Awamu ya February.akisaidiwa na Nepi Nawea
 
Wewe mwenyewe unasemaje tatizo lilikuwepo, Kwa hiyo chanzo chake sio uwepo wa Bwawa.
La kujiuliza sasa ni kwanini uwepo wa Bwawa hakujatatua tatizo.
Na ukumbukmbe matarajio ya awamu ya Tano na matarajio ya awamu ya February yalikuwa tofauti, mpaka kumalizika Kwa Bwawa Hilo na kuanza uzalishaji .
Sasa watu wenye uelewa huanza kufanya ulinganishona tofauti za taarifa za Awamu ya Tano na za Awamu ya February.akisaidiwa na Nepi Nawea
Soma mada wewe mjinga
 
Inasikitisha sana kusoma kwamba Zaidi ya Vijijini 23 Wilayani Rufiji vilivyopo kwenye blonde la mto Rufiji Vimekumbwa na Mafuriko Makubwa ya maji kutoka bwawa la umeme la Nyerere.

Vijiji hivyo viko kwenye kata 12 Zenye kaya zaidi ya 1,000 ambapo makazi,mashamba,mazao na Mali nyingine vimegaribiwa vibaya na Mafuriko hayo.

Ikumbukwe njia ya mwongo Huwa ni fupi.Wakati wa Ujenzi wa bwawa hili tuliambiwa pamoja na mambo mengine eti ujenzi wake utadhibi Mafuriko ya mara Kwa mara huko lower Rufiji basin lakini imekuwa kinyume chake kwani Mafuriko ndio yameongezeka na Haki kuwa mbaya zaidi maana maji yanakuja Kwa Wingi na Kasi kubwa.

Ni vyema ikaeleweka kwamba kabla ya kufanya mradi wowote ni vyema athari Kwa mazingira ikafanyika ila Kwa bwawa hili inaelekea jambo hili lilipuuzwa.

Ikumbukwe kwamba miradi yeyote iwe ya kiuchumi au kijamii Huwa inalenga kuleta ustawi Kwa jamii husika ila ikiwa kinyume chake haifai au njia mbadala lazima zitafutwe.

View attachment 2953636
View attachment 2953637
View attachment 2953638
---========

MCHENGERWA ATOA MIL.40/- KUSAIDIA WANANCHI WA RUFIJI WALIOKUMBWA NA MAFURIKO

Na Projestus Binamungu

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji mkoani Pwani Mhe. Mohamed Mchengerwa, ametoa Sh.milioni 40 kwa ajili ya kusaidia ununuzi wa mbegu kwa zaidi ya wakazi 1,000 wa maeneo mbalimbali ya wilaya ya Rufiji ambao mali, mashamba na makazi yao yameathiriwa na mafuriko ya maji, yaliyofunguliwa kutoka bwawa la uzalishaji umeme la Mwalimu Nyerere.

Akizungumza na wakazi hao mara baada ya kufanya ziara ya kukagua athari ya mafuriko hayo katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo, Waziri Mchengerwa amesema analazimika kutoa kiasi hicho cha pesa ili kuwatia moyo wakazi hao kurejea shambani kulima upya baada ya mazao yao kusombwa na mafuriko hayo.

“Hili ni janga letu sote mimi na nyinyi, tuliamini kwamba ujenzi wa JNHPP utakuwa mkombozi wa mafuriko ambayo yamekuwa yanatukumba mara kwa mara lakini kwa bahati mbaya bado imejitokeza, tuendelee kuwa na Imani kwamba mradi ukikamilika uwenda changamoto hii ikawa imetatuliwa” alisema Waziri Mchengerwa.
View attachment 2953643
Aliongeza kuwa “ Ninafahamu fika namna wakazi wa Rufiji mlivyokuwa mmelima kwelikweli mwaka huu, ninaomba turejee shambani tulime tena vilevile kwa kiwango kikubwa, mimi ninamkabidhi Mkuu wa wilaya shilingi milioni 40 kwa kuanzia kwa ajili ya kusaidia ununuzi wa mbegu ili turejee shambani tupande tena tusije kufa kwa njaa.”

Alikadhalika Waziri Mchengerwa ametoa wito kwa taasisi na mashirika ya misaada ya kibinadamu Pamoja na wasamalia wema kuguswa na hali ya Warufiji kwa kuwashika mkono kwa namna moja au nyingine katika kipindi hiki ambacho serikali ya wilaya inaendelea na ufuatiliaji na tathimini ya athari za mafuriko hayo kwa ujumla.

“Ukweli niseme kiasi hiki cha milioni 40 nilikuwa nimekidunduliza kutoka kwenye mshahara wangu kwa ajili ya kuhakikisha tunakuwa na futari ya Pamoja katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhan kama tunavyofanya kila mwaka, lakini kwa hali hii ya mafuriko niseme tu kwamba futari si kitu nalazimika kutoa kiasi hiki kwa ajili ya ununuzi wa mbegu na nitaenda kuwaomba marafiki zangu wanichangie angalau tufikishe milioni …..

========

My Take
Kwa hili la Rufiji, Serikali ihamishe Wananchi na iwalipe fidia kama inavyofanya Ngorongo Kwa Masai Kwa sababu maslahi na Haki zao zilikiukwa Kwa kutofanya EIA kama sheria za Nchi na Kimataifa zinavyotaka.

Tunapenda Umeme ila sio Kwa utaratibu huu.
Serikali ilete mafuriko halafu taasisi na watu binafisi tuguswe?
Serikali iguswe tu kivyake.
 
Hilo Dubwasha siku liseme lijambe tu kidogo.Kuna story zitapigwa miaka na miaka na Vilembwekeze wa Nchi.

Vilembwe wa Kina Mwijaku,Mashalavu watasimulia sana huko mbeleni.
 
Mamia ya wananchi hawana mahali pa kuishi, huku wengine 55 kutoka Kaya 15 wakihifadhiwa katika Shule za Msingi wilayani Rufiji Mkoa wa Pwani.

Ni baada ya nyumba zao kufunikwa na maji yanayotoka katika bwawa la Mradi wa Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP).

Mbali na kukosa makazi, watu hao wako hatarini kukumbwa na njaa baada ya mazao yao kuzama kwenye maji mashambani.

Akizungumza na Mwananchi Digital leo Alhamisi Aprili 4, 2024 katika Kijiji cha Mohoro wilayani humo, Diwani wa Mohoro ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rufiji, Abdul Chobo amesema tathmini za kila siku zinaonyesha maafa yanaendelea kuongezeka.

Hata hivyo, amesema wamewataka watu hao watafute sehemu nyingine ya kuhamia kwa sababu Jumatatu Aprili 8, 2024 shule zinafunguliwa.

Amesema hakuna kifo kilichotokea tangu mafuriko yalipoanza na jitihada za kuwaokoa zinaendelea.
 
Wazungu walipokataa huu mradi waliyajua yote haya.

Mungu wabariki Wazungu
 
Inasikitisha sana kusoma kwamba Zaidi ya Vijijini 23 Wilayani Rufiji vilivyopo kwenye blonde la mto Rufiji Vimekumbwa na Mafuriko Makubwa ya maji kutoka bwawa la umeme la Nyerere.

Vijiji hivyo viko kwenye kata 12 Zenye kaya zaidi ya 1,000 ambapo makazi,mashamba,mazao na Mali nyingine vimegaribiwa vibaya na Mafuriko hayo.

Ikumbukwe njia ya mwongo Huwa ni fupi.Wakati wa Ujenzi wa bwawa hili tuliambiwa pamoja na mambo mengine eti ujenzi wake utadhibi Mafuriko ya mara Kwa mara huko lower Rufiji basin lakini imekuwa kinyume chake kwani Mafuriko ndio yameongezeka na Haki kuwa mbaya zaidi maana maji yanakuja Kwa Wingi na Kasi kubwa.

Ni vyema ikaeleweka kwamba kabla ya kufanya mradi wowote ni vyema athari Kwa mazingira ikafanyika ila Kwa bwawa hili inaelekea jambo hili lilipuuzwa.

Ikumbukwe kwamba miradi yeyote iwe ya kiuchumi au kijamii Huwa inalenga kuleta ustawi Kwa jamii husika ila ikiwa kinyume chake haifai au njia mbadala lazima zitafutwe.

View attachment 2953636
View attachment 2953637
View attachment 2953638
---========

MCHENGERWA ATOA MIL.40/- KUSAIDIA WANANCHI WA RUFIJI WALIOKUMBWA NA MAFURIKO

Na Projestus Binamungu

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji mkoani Pwani Mhe. Mohamed Mchengerwa, ametoa Sh.milioni 40 kwa ajili ya kusaidia ununuzi wa mbegu kwa zaidi ya wakazi 1,000 wa maeneo mbalimbali ya wilaya ya Rufiji ambao mali, mashamba na makazi yao yameathiriwa na mafuriko ya maji, yaliyofunguliwa kutoka bwawa la uzalishaji umeme la Mwalimu Nyerere.

Akizungumza na wakazi hao mara baada ya kufanya ziara ya kukagua athari ya mafuriko hayo katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo, Waziri Mchengerwa amesema analazimika kutoa kiasi hicho cha pesa ili kuwatia moyo wakazi hao kurejea shambani kulima upya baada ya mazao yao kusombwa na mafuriko hayo.

“Hili ni janga letu sote mimi na nyinyi, tuliamini kwamba ujenzi wa JNHPP utakuwa mkombozi wa mafuriko ambayo yamekuwa yanatukumba mara kwa mara lakini kwa bahati mbaya bado imejitokeza, tuendelee kuwa na Imani kwamba mradi ukikamilika uwenda changamoto hii ikawa imetatuliwa” alisema Waziri Mchengerwa.
View attachment 2953643
Aliongeza kuwa “ Ninafahamu fika namna wakazi wa Rufiji mlivyokuwa mmelima kwelikweli mwaka huu, ninaomba turejee shambani tulime tena vilevile kwa kiwango kikubwa, mimi ninamkabidhi Mkuu wa wilaya shilingi milioni 40 kwa kuanzia kwa ajili ya kusaidia ununuzi wa mbegu ili turejee shambani tupande tena tusije kufa kwa njaa.”

Alikadhalika Waziri Mchengerwa ametoa wito kwa taasisi na mashirika ya misaada ya kibinadamu Pamoja na wasamalia wema kuguswa na hali ya Warufiji kwa kuwashika mkono kwa namna moja au nyingine katika kipindi hiki ambacho serikali ya wilaya inaendelea na ufuatiliaji na tathimini ya athari za mafuriko hayo kwa ujumla.

“Ukweli niseme kiasi hiki cha milioni 40 nilikuwa nimekidunduliza kutoka kwenye mshahara wangu kwa ajili ya kuhakikisha tunakuwa na futari ya Pamoja katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhan kama tunavyofanya kila mwaka, lakini kwa hali hii ya mafuriko niseme tu kwamba futari si kitu nalazimika kutoa kiasi hiki kwa ajili ya ununuzi wa mbegu na nitaenda kuwaomba marafiki zangu wanichangie angalau tufikishe milioni …..

My Take
Kwa hili la Rufiji, Serikali ihamishe Wananchi na iwalipe fidia kama inavyofanya Ngorongo Kwa Masai Kwa sababu maslahi na Haki zao zilikiukwa Kwa kutofanya EIA kama sheria za Nchi na Kimataifa zinavyotaka.

Tunapenda Umeme ila sio Kwa utaratibu huu.

View: https://www.instagram.com/p/C5S-mCZiN5p/?igsh=aWpqb2Vkbzl3cmFn


View: https://twitter.com/MwananchiNews/status/1775954878486954481?t=KzTuuvW3q_kKLhd_QOXebA&s=19
 
Wajenge crown dams--maji extra yajaze vibwawa vidogo vidogo--wakodishie wavuvi wa samaki--walime kambale kibiashara---changamoto ni fursa!
Sasa kwa nn wasitengeneze bwawa lingine ambalo litakuwa lipokea maji yaliyozid kwenye bwawa la mwalimu nyerere
Kama kabla ya ujenzi wangefanya EIA haya yote yangezingatiwa ila Kwa sababu Kuna mtu alikuwa mjuaji sana basi ndio matokeo yake haya Sasa

View: https://twitter.com/MwananchiNews/status/1775954878486954481?t=KzTuuvW3q_kKLhd_QOXebA&s=19
 
Mtu mweusi anahitaji ukombozi wa kifikra na kiroho.
Blackman
 
Inasikitisha sana kusoma kwamba Zaidi ya Vijijini 23 Wilayani Rufiji vilivyopo kwenye blonde la mto Rufiji Vimekumbwa na Mafuriko Makubwa ya maji kutoka bwawa la umeme la Nyerere.

Vijiji hivyo viko kwenye kata 12 Zenye kaya zaidi ya 1,000 ambapo makazi,mashamba,mazao na Mali nyingine vimegaribiwa vibaya na Mafuriko hayo.

Ikumbukwe njia ya mwongo Huwa ni fupi.Wakati wa Ujenzi wa bwawa hili tuliambiwa pamoja na mambo mengine eti ujenzi wake utadhibi Mafuriko ya mara Kwa mara huko lower Rufiji basin lakini imekuwa kinyume chake kwani Mafuriko ndio yameongezeka na Haki kuwa mbaya zaidi maana maji yanakuja Kwa Wingi na Kasi kubwa.

Ni vyema ikaeleweka kwamba kabla ya kufanya mradi wowote ni vyema athari Kwa mazingira ikafanyika ila Kwa bwawa hili inaelekea jambo hili lilipuuzwa.

Ikumbukwe kwamba miradi yeyote iwe ya kiuchumi au kijamii Huwa inalenga kuleta ustawi Kwa jamii husika ila ikiwa kinyume chake haifai au njia mbadala lazima zitafutwe.

View attachment 2953636
View attachment 2953637
View attachment 2953638
---========

MCHENGERWA ATOA MIL.40/- KUSAIDIA WANANCHI WA RUFIJI WALIOKUMBWA NA MAFURIKO

Na Projestus Binamungu

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji mkoani Pwani Mhe. Mohamed Mchengerwa, ametoa Sh.milioni 40 kwa ajili ya kusaidia ununuzi wa mbegu kwa zaidi ya wakazi 1,000 wa maeneo mbalimbali ya wilaya ya Rufiji ambao mali, mashamba na makazi yao yameathiriwa na mafuriko ya maji, yaliyofunguliwa kutoka bwawa la uzalishaji umeme la Mwalimu Nyerere.

Akizungumza na wakazi hao mara baada ya kufanya ziara ya kukagua athari ya mafuriko hayo katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo, Waziri Mchengerwa amesema analazimika kutoa kiasi hicho cha pesa ili kuwatia moyo wakazi hao kurejea shambani kulima upya baada ya mazao yao kusombwa na mafuriko hayo.

“Hili ni janga letu sote mimi na nyinyi, tuliamini kwamba ujenzi wa JNHPP utakuwa mkombozi wa mafuriko ambayo yamekuwa yanatukumba mara kwa mara lakini kwa bahati mbaya bado imejitokeza, tuendelee kuwa na Imani kwamba mradi ukikamilika uwenda changamoto hii ikawa imetatuliwa” alisema Waziri Mchengerwa.
View attachment 2953643
Aliongeza kuwa “ Ninafahamu fika namna wakazi wa Rufiji mlivyokuwa mmelima kwelikweli mwaka huu, ninaomba turejee shambani tulime tena vilevile kwa kiwango kikubwa, mimi ninamkabidhi Mkuu wa wilaya shilingi milioni 40 kwa kuanzia kwa ajili ya kusaidia ununuzi wa mbegu ili turejee shambani tupande tena tusije kufa kwa njaa.”

Alikadhalika Waziri Mchengerwa ametoa wito kwa taasisi na mashirika ya misaada ya kibinadamu Pamoja na wasamalia wema kuguswa na hali ya Warufiji kwa kuwashika mkono kwa namna moja au nyingine katika kipindi hiki ambacho serikali ya wilaya inaendelea na ufuatiliaji na tathimini ya athari za mafuriko hayo kwa ujumla.

“Ukweli niseme kiasi hiki cha milioni 40 nilikuwa nimekidunduliza kutoka kwenye mshahara wangu kwa ajili ya kuhakikisha tunakuwa na futari ya Pamoja katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhan kama tunavyofanya kila mwaka, lakini kwa hali hii ya mafuriko niseme tu kwamba futari si kitu nalazimika kutoa kiasi hiki kwa ajili ya ununuzi wa mbegu na nitaenda kuwaomba marafiki zangu wanichangie angalau tufikishe milioni …..

My Take
Kwa hili la Rufiji, Serikali ihamishe Wananchi na iwalipe fidia kama inavyofanya Ngorongo Kwa Masai Kwa sababu maslahi na Haki zao zilikiukwa Kwa kutofanya EIA kama sheria za Nchi na Kimataifa zinavyotaka.

Tunapenda Umeme ila sio Kwa utaratibu huu.

View: https://www.instagram.com/p/C5S-mCZiN5p/?igsh=aWpqb2Vkbzl3cmFn

Tuna viongozi wengi wasiozingatia taaluma za watu.

Mungu awanusuru wananchi wenzetu huko Rufiji
 
Kila project kubwa duniani huwa inachangamoto. Fuatilia Mega projects youtube Utagundua hilo.

Maji yangechepushwa mapema mngeanza kupika kelele kuwa maji yanafunguliwa ili mitambo ishindwe kujiendesha shida ya umeme iendelee.

Ishu ina control mechanism. Naamini miaka ya mbeleni itaisha. Faida za bwawa ni nyingi kuliko hasara. Kazi indelee
 
Siyo tathmini ya maziningira kupuuzwa bali ni kutokana na kufungulia bwawa hilo pole pole wakati likiwa limejaa na kusababisha lifurike. Juzi bwawa wamfungulia, halafu etiu wakalifunga na hivyo kusababisha overflow. Iwapo lingefunguliwa njia zake zote sawasawa kulingana na design, kusingekuwa na tatizo lolote.
 
Back
Top Bottom