Ruvuma: Ajali yaua Watu 6 wakiwemo Walimu 4 wa Shule moja

Ruvuma: Ajali yaua Watu 6 wakiwemo Walimu 4 wa Shule moja

Mtoa Taarifa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2024
Posts
213
Reaction score
671
Screenshot_2024-12-28-15-58-17-184_com.instagram.android-edit.jpg

Watu sita wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wanasafiria kutoka kijiji cha Lumalu kata ya Upolo - Kilosa wilayani Nyasa kuanguka katika mteremko wa Chunya wilayani Mbinga mkoani Ruvuma.

Waliofariki kati yao ni walimu wanne wa shule ya msingi Lumalu ya mkoani humo, Mfamasia mmoja na dereva wa gari hilo walilolitumia kuelekea Nyasa katika shule ya sekondari Limbo, kikazi.

Akizungumza katika eneo la ajali, Salumu Ismail, Katibu Tawala Wilaya ya Nyasa, amewashukuru wananchi kwa kujitokeza katika eneo ilipotokea ajali na kutoa msaada.

Amewaomba ndugu wa marehemu kwenda kupima DNA kwa ajili ya utambuzi wa miili hiyo ambayo imehifadhiwa katika hospitali ya Mbinga mkoani humo.

Ajali hiyo imetokea leo Desemba 28, 2024 ambapo chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika.

TBC
Screenshot_2024-12-28-15-58-01-763_com.instagram.android-edit.jpg

Screenshot_2024-12-28-15-57-45-145_com.instagram.android-edit.jpg
 
Mungu azipokee roho za marehemu wapate pumziko jema.

Ila maisha ni ya ajabu sana,kimahesabu hapa kuna familia tano zinalia na kuhuzunika kwa uchungu wa kuondokewa na jamaa zao then kuna familia nyengine tano zitapona kwa jamaa zao kushika nafasi walizokuwa wakizitumikia hawa waliotangulia.
 
We utakufa bila uzembe bro. So subiria umauti wako.
Hua unaandika posts na comments nyingi za kutafuta attention boss nasi tunakupa tena attentively. So subiria ufe bila uzembe.
Siko hapa kutafuta attention you idiot!

Vifo vingi vya wanadamu vinatokana na ujinga, uzembe, umaskini na ukosefu wa maarifa.
 
Back
Top Bottom