Rwanda wamepiga marufuku "Adhana" Alfajiri

Rwanda wamepiga marufuku "Adhana" Alfajiri

Maana ya Adhana kwa wakati huu ishapitwa na wakati.
Wakati ule kulikuwa hakuna saa, wala, alarm, wala simu.
Ndio maana waliona waitane kwa kutumia sauti ya mtu.

Sasa hivi teknolojia imekuwa na adhana haina maana nyingine zaidi ya kupigiana kelele na kuyafurahisha Majini.

Mbona hamchelewi Kumka kwenda kazini hata kama hakuna adhana.
 
Adhana piga nyumbani kwako
Tukipiga nyumbani ndio zitakuwa nyingi zaidi.Lakini kwa madhumuni yake inatakiwa iwe moja katika eneo fulani kwenye msikiti. Wako wanaojaza maneno yao machache kidogo kuliko inavyotakiwa.Pamoja na hivyo haizidi dakika 5.Hapo kuna kero gani la kufikiria kuizuia.
 
Nadhani tuishie hapa kwani tunazunguka tu.

Adhana sio kelele kama jinsi mlio wa honi, gari, mbwa, jogoo anayewika, radi nk, honi, gari, mapikipiki, watoto, jogoo nk, milio yao inayosababu na faida katika jamii--- labda uniambie hakuna sababu na vinatoa milio kiwendawazimu!!

Adhana ni mwito kwa waumini kwenda kufanya ibada, ibada ni mafundisho ya hulka njema (morals) ---hutanielewa kama wewe ni ethiest, naamini wewe unaamini Mungu.

Imani za dini ndizo huweka misingi ya morals kwa watu na ndio maana utasikia marakadhaa viongozi wa kisiasa wakiwahimiza viongozi wa kidini kuwasaidia kuwajenga waumini wao kimaadili nk, ili kujenga jamii bora, hapo sasa utaona dini ina take part katika kujenga jamii, utawala kuzuia adhana ni kuweka kizingiti indirectly kwa dini kujenga hulka kwa waumini ambao ni sehemu ya jamii ya watu wote, unless tukubaliane kwamba nchi husika inafuata misingi ya Communism hapo ni kesi nyingine.

Ninachotaka kukuambia ni hiki; Dini ni imani ndani ya jamii na utawala bora ni ule unao Compromise imani, utamaduni, mila nk, za jamii husika ili kuleta amani, maelewano kati ya jamii na utawala nk.

Chuki ya adhana isiwapofusheni mkawa shortsighted msione mbali zaidi ya hapo juu ya kitu kinachoweza kutokea, suala hili ni mtambuka.
Kwanza,Mimi sijazungumzia adhana pekee,nimejjmuisha kelele zote zinazosumbua watu zinazosababishwa na hizi dini zetu!
Pili,hata wewe unaelewa kuwa hiyo ni compromise!Lakini inapozidi a kuwa kero zaidi inaweza kuondolewa!Mimi naamini Rwanda sio kwamba wamekurupuka tu,miaka yote hiyo kwanini basi wamevumiliwa ni ije kuwa Leo?Kwanini tusijikite kujua sababu ya uamuzi huo wa serikali ya Rwanda na badala yake mjadala uko kwingine kabisa!
 
Maana ya Adhana kwa wakati huu ishapitwa na wakati.
Wakati ule kulikuwa hakuna saa, wala, alarm, wala simu.
Ndio maana waliona waitane kwa kutumia sauti ya mtu.

Sasa hivi teknolojia imekuwa na adhana haina maana nyingine zaidi ya kupigiana kelele na kuyafurahisha Majini.

Mbona hamchelewi Kumka kwenda kazini hata kama hakuna adhana.
kwanini utuchagulie mambo yanayotuhusu kwenye dini yetu.Na kwanini utuongezee kazi ya kutafuta alarm kwa ajili ya swala.Kumbe kazi hiyo inafanywa na mtu mmoja katika eneo kubwa.
 
Kwanza,Mimi sijazungumzia adhana pekee,nimejjmuisha kelele zote zinazosumbua watu zinazosababishwa na hizi dini zetu!
Pili,hata wewe unaelewa kuwa hiyo ni compromise!Lakini inapozidi a kuwa kero zaidi inaweza kuondolewa!Mimi naamini Rwanda sio kwamba wamekurupuka tu,miaka yote hiyo kwanini basi wamevumiliwa ni ije kuwa Leo?Kwanini tusijikite kujua sababu ya uamuzi huo wa serikali ya Rwanda na badala yake mjadala uko kwingine kabisa!
Kama wamevumilia au hawajavumilia Rwanda sio kigezo cha dini za watu na hasa Uislamu.Uislamu umetangulia mbali kabla hakujawa na Rwanda. Hivyo uvumilivu wao hautakiwi kuwa na kikomo kwa kusikiliza hoja za mashoga.
 
Kupiga kelele saa 10 alfajiri na kuamsha watu wote hata ambao siyo wa imani yako, siyo sahihi kabisa. Nina raha sana kuishi sehemu ambayo hakuna mtu ananiamsha kila siku alfajiri kabla ya muda wa kawaida wa binadamu kuamka. Usingizi wa kutosha ni muhimu kwa afya. Nina uhakika kuna Waislamu ambao hawataki kuamshwa saa 10 usiku. Rwanda oyeeee...
Uvivu tu, watu hiyo Adhana inatukuta kwe shughuli zetu tayari
 
Tukipiga nyumbani ndio zitakuwa nyingi zaidi.Lakini kwa madhumuni yake inatakiwa iwe moja katika eneo fulani kwenye msikiti. Wako wanaojaza maneno yao machache kidogo kuliko inavyotakiwa.Pamoja na hivyo haizidi dakika 5.Hapo kuna kero gani la kufikiria kuizuia.
Dakika 5 nyingi,mnaasha hata ambao hiyo adhana haiwahusu!
Halafu mbaya zaidi,kwanini Spika zile Huwa zinaumiza masikio?Hivi Huwa Zina decibel ngapi?Maana kila msikiti ikipigwa adhana hapo lazima usikilizie kukereketwa
na Ile sauti inayotoka!
 
Kama wamevumilia au hawajavumilia Rwanda sio kigezo cha dini za watu na hasa Uislamu.Uislamu umetangulia mbali kabla hakujawa na Rwanda. Hivyo uvumilivu wao hautakiwi kuwa na kikomo kwa kusikiliza hoja za mashoga.
Duuuh,nahisi siwezi kufanya mjadala na wewe!
 
Kwanza,Mimi sijazungumzia adhana pekee,nimejjmuisha kelele zote zinazosumbua watu zinazosababishwa na hizi dini zetu!
Pili,hata wewe unaelewa kuwa hiyo ni compromise!Lakini inapozidi a kuwa kero zaidi inaweza kuondolewa!Mimi naamini Rwanda sio kwamba wamekurupuka tu,miaka yote hiyo kwanini basi wamevumiliwa ni ije kuwa Leo?Kwanini tusijikite kujua sababu ya uamuzi huo wa serikali ya Rwanda na badala yake mjadala uko kwingine kabisa!


Case study hapa ni Adhana, Adhana haina mbadala na ukiizuia ni sawa na kuingilia na kuvuruga imani tena nguzo muhimu katika imani ya dini, leo ukianza KUTOMASA adhana kesho utatomasa sherehe ya Idd, Kesho kutwa utasema sio ruhusa kuoa mwanamke zaidi ya mmoja, mtondo goo-----, inakuwa ni kizungumkuti.

Unakataza adhana hapo hapo unataka shk akusaidie kuwapa maadili watu??-- sii wehu huo!!?
 
Case study hapa ni Adhana, Adhana haina mbadala na ukiizuia ni sawa na kuingilia na kuvuruga imani tena nguzo muhimu katika imani ya dini, leo ukianza KUTOMASA adhana kesho utatomasa sherehe ya Idd, Kesho kutwa utasema sio ruhusa kuoa mwanamke zaidi ya mmoja, mtondo goo-----, inakuwa ni kizungumkuti.

Unakataza adhana hapo hapo unataka shk akusaidie kuwapa maadili watu??-- sii wehu huo!!?
Nimeshamwambia Hilo la kuoa ni suala binafsi,halimuathiri mtu mwingine hivyo ni mfano mfu!
Naona Rwanda kimeeleweka,hizi dini wakati mwingine zinajihisi zinaogopwa na serikali!Rwanda wameonesha njia,kama huwezi kwenda kuswali bila kupigia watu makelele basi acha!Kama unaona hutapata thawabu bila kupiga makelele nenda nchi ambazo ni Ruksa ukaishi huko!
Serikali inawaomba mashekhe wawape maadili waumini wao Ili waepuke kukutana na mkono wa Dola!Dini isipowapa maadili basi maadili watayapata gerezani!Habari za kubembelezana zimepitwa na wakati!
Tii sheria bila shuruti,Rwanda imeshakuwa hivyo!
 
Nimeshamwambia Hilo la kuoa ni suala binafsi,halimuathiri mtu mwingine hivyo ni mfano mfu!
Naona Rwanda kimeeleweka,hizi dini wakati mwingine zinajihisi zinaogopwa na serikali!Rwanda wameonesha njia,kama huwezi kwenda kuswali bila kupigia watu makelele basi acha!Kama unaona hutapata thawabu bila kupiga makelele nenda nchi ambazo ni Ruksa ukaishi huko!
Serikali inawaomba mashekhe wawape maadili waumini wao Ili waepuke kukutana na mkono wa Dola!Dini isipowapa maadili basi maadili watayapata gerezani!Habari za kubembelezana zimepitwa na wakati!
Tii sheria bila shuruti,Rwanda imeshakuwa hivyo!



Eti wawape maadili waumini wasikutane na mkono wa dola!!!, hoja dhaifu kwelikweli!!

Nchi ikijaa wahalifu hata wakuu wa vyombo vya dola nao watakuwa wahalifua au huoni hilo?!?--- nchi hiyo itakuwa ni failed state.

Nchi haifundishi maadili, maadili ni spiritual essence nayo inaanzia kwenye dini ndipo inakwenda kwa jamii na kwenye utawala kwani watawala nao ni Jamii au hujui hilo nalo??!

The subject matter ni Adhana, Swala ni nguzp muhimu katika uisilamu na kabla ya swala kuna; Adhana, Kutawadha, Iqama na hatimaye Swala yenyewe, sasa utaondoaje kipengele cha adhana??

Katika Adhana kuna maneno; Hayya ala swalaa, yaani njooni kuswali, pia kuna maneno; Hayya ala fallaaa, yaani njooni kwenye ufaulu,kukataza adhana maana yake maneno hayo na mengine hayatosikika tena kwa watu/waislamu , sasa akatokea Mwendawazimu ikamkera na akaenda kuwalipua watu??!---watu wengine ni vichaa!!🤣

Rwanda have taken the wrong way let's wait and see God rulings.
 
Eti wawape maadili waumini wasikutane na mkono wa dola!!!, hoja dhaifu kwelikweli!!

Nchi ikijaa wahalifu hata wakuu wa vyombo vya dola nao watakuwa wahalifua au huoni hilo?!?--- nchi hiyo itakuwa ni failed state.

Nchi haifundishi maadili, maadili ni spiritual essence nayo inaanzia kwenye dini ndipo inakwenda kwa jamii na kwenye utawala kwani watawala nao ni Jamii au hujui hilo nalo??!

The subject matter ni Adhana, Swala ni nguzp muhimu katika uisilamu na kabla ya swala kuna; Adhana, Kutawadha, Iqama na hatimaye Swala yenyewe, sasa utaondoaje kipengele cha adhana??

Katika Adhana kuna maneno; Hayya ala swalaa, yaani njooni kuswali, pia kuna maneno; Hayya ala fallaaa, yaani njooni kwenye ufaulu,kukataza adhana maana yake maneno hayo na mengine hayatosikika tena kwa watu/waislamu , sasa akatokea Mwendawazimu ikamkera na akaenda kuwalipua watu??!---watu wengine ni vichaa!!🤣

Rwanda have taken the wrong way let's wait and see God rulings.
Kwanza maadili huanzia Kwa wazazi/walezi,ndio maana wanasema asiyefunzwa na mamaye atafunzwa na ulimwengu!Mtoto akiwa mdogo hata hajajua dini na masuala ya Imani,kwanza anaanza kujifunza kutoka Kwa wazazi!Hizi dini huja baadaye kuongezewa alipoacha Mzazi!Kabla ya hizi dini kuja,inamaana watu walikuwa hawana maadili?Wakati mwingine hizi dini zinafundisha watu kuwa ma-extremist!
Nakazia,mitaa wanayokaa masikini ndio utakuta makanisa na misikiti inayopiga makelele Iko katikati ya makazi ya watu,sehemu za matajiri hakuna kitu kama hicho!Wanalala usingizi wa pono bila bughudha na kanisani na msikitini wanaenda kuswali!
Sisi masikini ndio tunakomaa tuamshwe na adhana!
 
Adhana siyo tatizo maana inachukua dk2 hivi. Tatizo NI maneno yanayoongezwa. Utasikia Acha kung'ang'ania Shukla, Mungu anakuona unavyosikia adhana, aki na Baba nyote hili NI sharti siyo ombi amkeni......hapo unakuta shehe hana tofauti na mchungaji.
 
Mimi ni Uislam namuunga mkono Kagame kwa hili la zuio..

Uislam ni dini ya hekima,dini iliyojaa busara,lakini kuna baadhi ya Waislam wanazidisha mambo na kuifanya hii dini iwee dini ya kelele

Sala ni moja ya nguzo za kiislam,ni njia moja ya kuwa karibu na Mungu,sasa kuna misikiti mingine utasikia Imam anasalisha na yale yote anayosalisha unayasikia kwenye vipaza sauti

Sheikh anasoma sura na mambo mingine, yanasikika nje kwa kutumia vipaza sauti...bila ya kujali jamii iliyomzunguka,wagonjwa,wazee,watoto wadogo nk

Huu utamaduni wa kutumia vipaza sauti kwenye misikiti umeanzia mashariki ya mbali na sisi huku tukaiga..

Bora Tanzania nayo iige mfano wa Rwanda,turudi kama zamani,Adhana zote ziwe za sauti ya muadhini bila ya kutumia Vipaza sauti
 
Kwanza maadili huanzia Kwa wazazi/walezi,ndio maana wanasema asiyefunzwa na mamaye atafunzwa na ulimwengu!Mtoto akiwa mdogo hata hajajua dini na masuala ya Imani,kwanza anaanza kujifunza kutoka Kwa wazazi!Hizi dini huja baadaye kuongezewa alipoacha Mzazi!Kabla ya hizi dini kuja,inamaana watu walikuwa hawana maadili?Wakati mwingine hizi dini zinafundisha watu kuwa ma-extremist!
Nakazia,mitaa wanayokaa masikini ndio utakuta makanisa na misikiti inayopiga makelele Iko katikati ya makazi ya watu,sehemu za matajiri hakuna kitu kama hicho!Wanalala usingizi wa pono bila bughudha na kanisani na msikitini wanaenda kuswali!
Sisi masikini ndio tunakomaa tuamshwe na adhana!


Niliposoma tu kwamba eti maadili yanaanzia kwa wazazi hata hamu ya kuendelea kusoma ikaniisha,, Hayo maadili wazazi wameyapata wapi??

Usizini, usiibe, usiseme uongo, usiue nk,, hizo ni hukumu/nasaha kutoka kwa binadamu??!!--- hayo sio maandiko ya Mungu binadamu ndiye amepewa na kuyafanya kuwa maadili ?!!

Maadili msingi wake ni Mungu na kawapa mitume wake na ndio hayo tunayapata kupitia dini.

Piga ua maadili msingi wake ni dini,
Hakuna nchii itakayopinga mafundisho ya dini na taratibu zake kwa njia yoyote ikastawi, tusubiri ya Rwanda tutakuja hapa kuelezana tuombe uhai tu.
 
Tukipiga nyumbani ndio zitakuwa nyingi zaidi.Lakini kwa madhumuni yake inatakiwa iwe moja katika eneo fulani kwenye msikiti. Wako wanaojaza maneno yao machache kidogo kuliko inavyotakiwa.Pamoja na hivyo haizidi dakika 5.Hapo kuna kero gani la kufikiria kuizuia.
Bilal(rehema za Allah ziwe juu yake) alitumia maspika ya dB200 kuita watu kwenda kuswali?

Hata Misri adhana zimepigwa marufuku siyo Rwanda tu.
 
Back
Top Bottom