Saa ya Rais Samia yadaiwa kuwa na thamani ya Tsh. Milioni 111,601,22/=

Sasa kama matoto ni mavivu kila uchao kunungunika kazi hayafanyi....! Ni mbio mbio tu kila mkoa, Ninachosema mshahara wake unamruhusu, we just measure unto salary!
 
😁😁 Na wewe unakunywa bia na misosi ya bar kila weekend, lakini kuna ndugu katika ukoo wako anakosa hela ya ada, wanakuomba 50k unagoma hauna.

Tujadili mambo ya msingi, urembo na mambo yake binafsi tumuachie, kwa nafasi alizoshika na biashara zake kupata vitu kama hivyo ni kawaida kabisa.
 
Naona wengi wanamshambulia mtoa mada, mtoa mada yuko sahihi ila shida ni ndogo tu ametumia hisia zaidi ya fikra yakinifu.

Ukitumia hisia lazima uumie pale ambapo nchi ni masikini sijui ya ngapi huko kutoka chini, na kiongozi/viongozi wake wanaficha umasikini kwa kujipamba na kujivika vito vya thamani na anasa za hapa na pale.

Ukitumia fikra pembuzi utagundua ni fursa na utukufu kufanya wafanyayo kwa nafasi zao.
 
Mjinga wewe, Rais ni kiongozi sio boss, anawaongoza watu masikini wa Tanzania, nchi masikini alafu anavaa saa ya milioni 100?? Kiongozi lazima aonyeshe unyenyekevu na aishi maisha ya wale anaowaongoza
Acha hasira, umaskini ni wa kwako sio wote maskini. Rais sio mzazi wako ni kiongozi wa nchi. Kwahiyo ulitaka avae saa ya elfu 3 na yeboyebo kama wewe? Aliyekuloga amekufa.Hama mabondeni mvua zinakuja.
 
Kuna uhakika gani kama ndio yenyewe jamani? Labda mama is faking till she makes it je?

Ila mimi sijui hizo saa watu huwa wanazipendea nini? Niache kuvaa apple smart nivae mshale dunia hii ya sasa? Na uwezo upo?
Mishale ni urembo, Nina uhakika wala haangalii muda kwa hiyo saa, ila ni sehemu ya vidani (jewelry) zake, na ukizingatia hiyo bei, hadhi ya juu!

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
Sahihi kbsa
 
Hatutaki unafiki wa kujifanya raisi hana uwezo ilihali upo, raisi ni tajiri mpaka watoto na wajukuu huenda wakarithi huo utajiri, sasa asiishi kitajiri sababu nchi ina raia masikini? Ok, Nchi inawavuta bange hiì, raisi anatakiwa afanane na wananchi wake naye apulize mibange.
 
Bibi yako huyu

USSR
we! angekuwa bibi yangu usingenikuta huku bata wangepata shida sana! natafuta nini huku kuchakutwa kumsimanga na kumpa sifa asizostahili karibia mtamlaumu kwa joto na kumpongeza kwa mvua zinazonyesha?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…