Saa zingine vaa vizuri ingia town ulizia bei za magari ili uushtue "umasikini" sio kukaakaa kizembe?

Saa zingine vaa vizuri ingia town ulizia bei za magari ili uushtue "umasikini" sio kukaakaa kizembe?

tatizo wafanyabiashara wetu wa bongo ni wakarimu[emoji23] unaenda kuulizia kitu anataja bei unamwambia basi siku nyingine lakini yeye anazidi kukupunguzia tu bei.kuna siku jamaa alinipunguzia laki nzima kwenye fridge
Mimi: hii fridge bei gani ?
muuzaji: hii laki nne na nusu boss wangu
Mimi: oh basi nitarudi (huku naanza kuondoka)
muuzaji:boss nipe nne kamili (huku ananishika mkono)
mimi:hapana,parefu sana
Muuzaji:basi nipe tatu na nusu
Zilikua zangu hizo ila sijaacha nimepunguza tu.Sina hata hela nimezurura mjini vya kutosha nikiona kitu kizuri na ninajua kwamba bei yake imechangamka ,basi naulizia ilhali najua sina hata hela.. Hapo bei itapunguzwa hadi najuta kwa nini niliuliza na hela sina.

Sent from my Redmi 8 using JamiiForums mobile app
 
Nenda ulizia viwanja, matrekta, nyumba na n.k unaona kabisa hii kuipata sio leo lakini jitahidi muda fanya hivyo acha kukaa kizembe unafikiri hela zinakujaje.

Inatakiwa uuchangamshe umaskini wako na watu mijini humo unapoishi wawe kidogo na wasi wasi na wewe waone huyu mtu sio mchezo mchezo kumbe ata anaweza kununua hiki, acha kushangaa shangaa mjini hapa kuku we🤣 😅

Weka imani na kitu flani zungukia kukiulizia acha kumzungukia kila siku Mwajuma wa Mtaa wa pili bata we😜 Route zako ziamishie Kwenye jambo lako lenye tija,

Sasa kama nimefoka shauli yenu mimi naenda na niwatakie siku njema na jumapili njema 🙏

🤦🤪🏃
Kuushitua umasikini ujiandae kupigwa chini na wajumbe🤣🤣🤣
 
kuna siku nlienda UBP kuulizia frem wanapangisha bei gani... nlikutana na mhindi dogo janja tu pale mapokezi, akaniambia ngoja niongee na boss kubwa. mara akaniita "njoo huku mkuu uongee na boss kubwa." kufika yule boss wake ni mhindi ana nyusi kazichonga hatari, udevu km wote akaniangaliaaa... akanitazamaaa... akaniambia "karibu kijana" ila bado ananithaminisha tu! nkamchana "frem ngapi bei?" akawa km amekunja ndita hv yaan bado haamini! ikabidi anijibu... "hapa frem zinapangishwa kwa wenye makampuni na frem kwa mwezi ni mil3 na unalipa kwa miaka3."
kilichofwata baada ya hapo ni kuagana naye nkasepa.

kupata exposure ni kitu kizuri sana, unaondoa ushamba.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]unaona bwana
Umenifurahisha sana hapo mbagala kichem chem.


Kuna siku nilitoka na mshikaji wangu nait kali....tukaenda night club moja ya kishua. Tukanywa Virgin Mohito glass 2 kila mmoja...nikalipa elfu 40 tukasepa.

Sasa demu wake akawa amekuja getto kwake (ana funguo) demu akawa mkali usiku ule anatoka wapi?

Akanipigia simu nikaenda. Nikasolve msala na katika kutia mbwembwe nikamwambia shem sisi hatujafanya jambo baya tumekunywa tu VIRGIN MOHITO tukarudi. Utata ukaanza hicho ndio kinywaji gani? Mnanidanganya...waongo nyie....hehehe nikacheka.

Nikamwambia siku moja mwambie bro akupeleke kisha agiza hiyo kitu na ulipe. Pale pale nikagundua demu hana exposure.

Kuna kisa kingine....kuna demu nilikua namfukuzia anasoma chuo by then. Nikampeleka hotel moja hivi tukapata late lunch. Tumemaliza kula nikachukua toothpick nikawa nasafisha meno. Akaniomba na mimi naomba toothpick, nikamuonesha kwa ishara hizo hapo maana zilikua upande ule aliokaa yeye. Kumbe hajazijua, akakaa tena akanikumbusha toothpick....ikabidi nimchukulie nifungue nimpe. Toothpick za hotel zinakuwa covered kama straws za juice vile. Yeye hajazoea hizo mambo.

Kwa namna alivyokuwa sikutarajia kuwa hajui kama zile ni toothpick....nikagundua hana exposure.
Mwenzio wanajuaga kwetu mambo safi mtoto wa kishua au nna sponsor [emoji2][emoji2]
kumbe nikiwa bored natazama ramani naangalia Wapi nataka kutembelea na nikagundue nini?
-Kama ni restaurant naingia website yao nachukua PDF ya Menu naisoma najua kabisa wanauza Tsh ngapi na ntaenda kula nini ntatumia usafiri gani kufika.
-Sasa kuna Rafiki yangu mmoja tukiwa off ananiambia naomba tukatembee mahala,tunaeza kwenda mahala wote ndio siku ya kwanza tunafika ila mimi nakua kama mwenyeji kwanzia mazingira nayajua kabla sijafika sina haja hata ya kuangalia menu zao naagiza tu lete Ken forrester na yy ananiambia nichagulie. Akimaliza anamuita muhudumu Tsh ngapi nambadilishia kauli Mwambie alete bill binti Basi ananionaga mtu fulani kumbe basi tu experience za maisha[emoji23][emoji23][emoji23] Tunalipa wote ila yeye anaonekana Chawa
 
Saf kabsa inapendeza hyoo mie nlimaliza chuo sina kaz sina hata mia lkn nlkuwa naenda kuulizia magar kila siku na tunakubariana had bei mara niende kwa madalali naulizia nyumba [emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji3590]
 
Zilikua zangu hizo ila sijaacha nimepunguza tu.Sina hata hela nimezurura mjini vya kutosha nikiona kitu kizuri na ninajua kwamba bei yake imechangamka ,basi naulizia ilhali najua sina hata hela.. Hapo bei itapunguzwa hadi najuta kwa nini niliuliza na hela sina.

Sent from my Redmi 8 using JamiiForums mobile app

hahaha[emoji23] lazima ujute na unamuonea huruma muuzaji maskini,unajua wale jamaa wa Electronics anaweza maliza siku mbili hajauza kitu ndio maana wanatuchangamkiaga mno kwenye bei
 
Nenda ulizia viwanja, matrekta, nyumba na n.k unaona kabisa hii kuipata sio leo lakini jitahidi muda fanya hivyo acha kukaa kizembe unafikiri hela zinakujaje.

Inatakiwa uuchangamshe umaskini wako na watu mijini humo unapoishi wawe kidogo na wasi wasi na wewe waone huyu mtu sio mchezo mchezo kumbe ata anaweza kununua hiki, acha kushangaa shangaa mjini hapa kuku we[emoji1787] [emoji28]

Weka imani na kitu flani zungukia kukiulizia acha kumzungukia kila siku Mwajuma wa Mtaa wa pili bata we[emoji12] Route zako ziamishie Kwenye jambo lako lenye tija,

Sasa kama nimefoka shauli yenu mimi naenda na niwatakie siku njema na jumapili njema [emoji120]

[emoji1751][emoji2957][emoji125]
hahahahaha salut mkuuu,umenena
 
Ni kweli mkuu
tena siku moja moja unaenda pale lugalo unamkamata mjeda mmoja unamnyang'anya bunduki yake then una ji karanga fotooo......
Sio kila siku bunduki washike wao tu, ng'ombe we!!!
 
[SUB]
IMG-20200830-WA0002.jpg
[/SUB]
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Nenda ulizia viwanja, matrekta, nyumba na n.k unaona kabisa hii kuipata sio leo lakini jitahidi muda fanya hivyo acha kukaa kizembe unafikiri hela zinakujaje.

Inatakiwa uuchangamshe umaskini wako na watu mijini humo unapoishi wawe kidogo na wasi wasi na wewe waone huyu mtu sio mchezo mchezo kumbe ata anaweza kununua hiki, acha kushangaa shangaa mjini hapa kuku we🤣 😅

Weka imani na kitu flani zungukia kukiulizia acha kumzungukia kila siku Mwajuma wa Mtaa wa pili bata we😜 Route zako ziamishie Kwenye jambo lako lenye tija,

Sasa kama nimefoka shauli yenu mimi naenda na niwatakie siku njema na jumapili njema 🙏

🤦🤪🏃
wakati nasoma shule nilienda kwenye maonyesho ya sabasaba nikaingia banda la scania nikakuta horse mpya iko display nikauliza bei yake majibu niliyopata sina hamu hadi leo,
 
Ndo maana mimi sipendi kabisa kuitwa mnyonge tena anayeniita hivyo anatembelea li V8 lenye kiyoyozi.Ukipenda kuishi kinyonge kamwe huwezi kua na mawazo yakujikwamua kifikra hadi kiuchumi.
 
Back
Top Bottom