Sababu 3 muhimu kwanini mwanaume mwenye hela humvutia mwanamke kirahisi

Sababu 3 muhimu kwanini mwanaume mwenye hela humvutia mwanamke kirahisi

Infinite_Kiumeni

JF-Expert Member
Joined
Jan 23, 2023
Posts
382
Reaction score
687
Mwanamke yeyote anahitaji usalama kutoka kwa mwanaume wake, ndicho kitu cha kwanza wanakiangalia kabla ya kuwa kwenye mahusiano, japo huwa halisemwi waziwazi.

Usalama wanaotaka ni usalama wa kiakili, kiroho na kimwili ilii aweze kujiachia kwa mwanaume. Usalama wa kimwili mwanamke huupata pale anapojua mahitaji yake ya kimwili yanaweza kutimizwa, na mahitaji ya mtoto wake yataweza kutimizwa.

Hela inatimiza mahitaji makuu ma 3 ya kimwili. Mwanamke anakua na uhakika anaweza kuvaa, kula na kulala sehemu nzuri na salama, ukiwa na pesa hivyo vitu vinakua rahisi kwako kutimiza. Sehemu pakiwa na uhakika wa kula basi mtu hujisikia salama kuishi, haijalishi ni mwanamke au mwanaume.

Pia hela inaepusha migogoro midogo midogo, Mfano, unakuta mwanaume anamlalamikia mwanamke anamaliza sabuni ya kuogea, huyo mwanamke atajisikia usalama kuishi na mwanaume anayemuacha ajisafishe kwa amani bila kulalamikiwa kuhusu sabuni.

Hela inawezesha kusafiri na kufurahia sehemu tofauti. Ukiwa na pesa ni rahisi kumtoa mwanamke wako kwenda kutembea (ni jambo muhimu).

Wanawake wanapenda kuweka kumbukumbu tofauti tofauti pamoja na watu wawapendao. Usije ukakaa na mwanamke sehemu moja tu siku zote 365, utachokwa. Panga siku za kutoka. Haijalishi una hela kiasi gani, ila hakikisha mnabadili mazingira angalau mara moja kwa wiki.

Hela inasaidia kupata huduma za kiafya kirahisi. Atajiona yupo salama kwako unapokua na hela ya kumhudumia anapoumwa. Wanawake ni rahisi kukubali kuwa ni wagonjwa (sisi wanaume tunaona kuumwa ni udhaifu) ndo mana mara kwa mara atakuambia anaumwa, sio jambo baya sababu inabidi wawe na afya nzuri ili waweze kuleta uhai mpya wenye afya hapa duniani.

Mahitaji mengine kama vocha, vipodozi na manukato unaweza msaidia kadri uonavyo sawa, hakikisha mwanamke unayetaka kujenga naye maisha anayaweza hayo mahitaji madogo, pia unaweza mfundisha jinsi ya kupangilia matumizi ili asikuelemee kwenye hivyo vitu vidogo.

Ila usije ukadhani ni hela pekee ndio itakuwezesha kumtunza mwanamke wako. Wapo wanaowatimizia wanawake mahitaji ya kifedha na wamewashindwa wanawake, sababu wameshindwa kutimiza mahitaji mengine.

Bali uwezo wako wa kumridhisha kimwili, kiakili na kiroho, na kuwa kiongozi wake mzuri unakuwezesha kumtunza mwanamke unayetaka kujenga naye maisha, ndio maana katika kundi la infinite kiumeni utajifunza kila siku jinsi ya kumvutia na kumtunza mwanamke unayetaka kujenga naye maisha.
 
Write your reply...Najua suala la ngono lipo kimwili zaidi ila umekataa kulizungumzia kbsa umebase kwenye pesa tu.

Unaweza ukampa mwanamke kila kitu ila ukishindwa kumridhisha kingono na happy ndipo utaanza kuchapiwa na wahuni wa mtaani wasio na mbele Wala nyuma.
 
Mwanamke yeyote anahitaji usalama kutoka kwa mwanaume wake, ndicho kitu cha kwanza wanakiangalia kabla ya kuwa kwenye mahusiano, japo huwa halisemwi waziwazi.

Usalama wanaotaka ni usalama wa kiakili, kiroho na kimwili ilii aweze kujiachia kwa mwanaume. Usalama wa kimwili mwanamke huupata pale anapojua mahitaji yake ya kimwili yanaweza kutimizwa, na mahitaji ya mtoto wake yataweza
Ukimaliza hili nakuomba baadae uje na Sababu Kuu Tatu ( 3 ) za Kwanini Wanawake ( hasa Wake za Watu ) hupenda Kutoka ( Kubanduliwa ) na Wanaume wa Kawaida sana na hata wasio na Pesa?

Nitakushukuru ukija na Jibu Kiongozi.
 
Mwanamke yeyote anahitaji usalama kutoka kwa mwanaume wake, ndicho kitu cha kwanza wanakiangalia kabla ya kuwa kwenye mahusiano, japo huwa halisemwi waziwazi.

Usalama wanaotaka ni usalama wa kiakili, kiroho na kimwili ilii aweze kujiachia kwa mwanaume. Usalama wa kimwili mwanamke huupata pale anapojua mahitaji yake ya kimwili yanaweza kutimizwa, na mahitaji ya mtoto wake yataweza kutimizwa.
Asikudanganye mtu huwezi kumridhisha mwana mke hata ukitimiza hayo yote atabuni jipya tu, hao viumbe acha tu.....nikama ma trafiki wabongo hata gari ikiwa nzima na imekamilika atakutafutia tatizo jingine jipya, eti kwanini umeva sando wakati uneendesha gari.
 
Punguzeni kuwapandikizia ujinga hawa mabinti, waelimisheni kutafuta, kuzalisha na kujitegemea.

Saivi mabinti wanaingia kwenye mahusiano wakijua kunalipa kuliko kufanya kazi.

Binti mwenye uwezo wa kujitegemea kuna vitabia vya kishenzi na vitamaa vinakaa mbali na yeye
 
Ukimaliza hili nakuomba baadae uje na Sababu Kuu Tatu ( 3 ) za Kwanini Wanawake ( hasa Wake za Watu ) hupenda Kutoka ( Kubanduliwa ) na Wanaume wa Kawaida sana na hata wasio na Pesa?

Nitakushukuru ukija na Jibu Kiongozi.
Sawa.
 
Write your reply...Najua suala la ngono lipo kimwili zaidi ila umekataa kulizungumzia kbsa umebase kwenye pesa tu.

Unaweza ukampa mwanamke kila kitu ila ukishindwa kumridhisha kingono na happy ndipo utaanza kuchapiwa na wahuni wa mtaani wasio na mbele Wala nyuma.
Ndiyo ni kweli.
Hizo ni sababu zisizo za kingono...
 
Nilivyokuwa binti nilikuwa nikitongozwa na mwanaume mwenye pesa natoka mbio, yaani hata kumsikiliza nilikuwa staki...
Now natamani nitongozwe na mwenye pesa ndo hawanitongozi kama sio gundu hili ni nini
Maana yake motisha yako ni kumpata mwanaume kama kitega uchumi?
 
Nilivyokuwa binti nilikuwa nikitongozwa na mwanaume mwenye pesa natoka mbio, yaani hata kumsikiliza nilikuwa staki...
Now natamani nitongozwe na mwenye pesa ndo hawanitongozi kama sio gundu hili ni nini
Kwanini ulikuwa ukiwaona hao wanaume unawakimbia? Demi
 
Kwanini ulikuwa ukiwaona hao wanaume unawakimbia? Demi
Kwanza nilikuwa naamini ya kwamba wanaume wote wenye pesa wana ukimwi.
Halafu sijui kwanini walikuwa hawanivutii kabisa.
Hata sasa hivi mwanaume akiwa na pesa sana hanivutii namuona wa ajabu ajabu wa kula nae starehe tu.
Ila huyu wa kwangu namuombea azidi kupata pesa aje kuwa tajiri😅😅
 
Nilivyokuwa binti nilikuwa nikitongozwa na mwanaume mwenye pesa natoka mbio, yaani hata kumsikiliza nilikuwa staki...
Now natamani nitongozwe na mwenye pesa ndo hawanitongozi kama sio gundu hili ni nini
Oshey mr 💰
 
Back
Top Bottom