Sababu za kiroho kwanini watu wengi walitamka kwamba utawala wa Mwendazake hautafika mbali

Hakuna cha unabii wala sauti za kiroho. Kuna hulka ya mtu hubainisha mustakabali wake kirahisi. Kuishi kihasara hasara, ubishi na dharau nyingi dhidi ya hatari zinazokuzunguka.

Soma kisa cha Abunuwasi alipokuwa akikata tawi la mti huku kalikalia. Mpita njia akampa tahadhari kuwa ataanguka na tawi. Yeye akampuuza. Ilipotokea kweli na kwa bahati hakujeruhiwa akamkimbilia yule mtu akiona ni nabii na kumuomba amtabirie siku yake ya kufa!
 
U have a point mkuu
 
Takataka tu umeandika.


Bila jpm hii tz ulishakuwa mali ya wahuni, shukuru sana huyo mtu alikomboa mambo mengi na kuweka siri nyngi za viongozi wetu jinsi wanavyoharibu hii nchi.

Hata hivyo hakuna mwanachadema mwenye akili timamu anaweza kukili mazuri ya yule bwana.

Sas huyu samia na kikwete wana mazuri gan mpka wamshinde Magu kiasi kwamba mpka mbingu zimchukie mwendazake.

Watu wengi walkuwa wana hofu ya huyo bwana kutofika mbali sababu ya kuharibu mianya ya wahuni Full stop, kwanza huyo mzee alipendwa na watu wengi, kwanzia watoto, wamam na wazee, shahid mtaani kwako, japo unakaza fuvu lkn ukweli unao.

Lile nyomi la mafuriko ya watu walpokuwa wakimuaga halijawahi tokea tangu Baba wa taifa mpaka mwendazake,afu utokee wew mpuuzi mmoja usiejielewa wala kuwa na mchango wowote nchini kuanza kutuandikia upumbavu wako humu.

SHAME ON YOU
 
Wakati WA uchaguzi WA 2020 Kuna siku Alisikika akisema " MZEE MWINYI KAONGOZA VIPINDI VIWILI, MZEE MKAPA VIPINDI VIWILI, MZEE KIKWETE VIPINDI VIWILI, MIMI NDIO MNATAKA NIONGOZE KIPINDI KIMOJA"

Hapo mwendazake hakuwa akizungumza na wewe Wala Mimi Wala MTU yoyote Yule katika ulimwengu WA nyama . Hapo mwendazake alikuwa akizungumza Na sauti ya Mungu iliyo kuwa ikiendelea kumwambia kwamba yeye sio Rais..

Hapo nimekuelewa
 
Uongo wako unaanzia ulipo sema hakukuwa na shamrashamra za mzee kuwa Rais, huo sio ukweli hata kidogo, tulikuwepo mwaka 2015, wala haikuwa mbali, kikwete aliandaa shamrashamra kubwa ambazo hakuwahi kufanyiwa Rais yoyote, madege yalipaishwa taifa pale utadhani ni siku ya muungano ama uhuru, na siku hiyo ilitangazwa sikukuu

Sasa hiyo kusema hakukuwa na shamrashamra sijui mwezetu ilikuwa ulaya hukushuhudia, we don't know and we are not sure of that
 
Halafu hilo neno 'mwendazake' mnataka muambiwe mara ngapi kuwa kwa kiswahili chetu Tanzania sio neno sahihi hilo. Hilo ni kama tusi, huku mtu aliyefariki huitwa marehemu ama hayati. Hayo maneno ya matusi Eti "mwendazake" mmeyaokota wapi

Mnaotumia neno mwendazake, hebu muimagine baba zenu au mama zenu shangazi na mababu na mabibi zenu wawe wanaitwa mmwaendazao hivi mtajisikiaje??

Mtaacha lini kutumia matusi kumuaddress mzee wa watu kajipumzikia mbele za haki

Maana hilo neno haitwi Rais mwengine aliyefarki wala mtu mwengine yoyote zaidi yake, mnataka muelewekeje, na neno lenyewe linasound kama tusi kwa sisi wazawa wa kiswahili
 
Nani asiekingoja kifo?

Hakuna utawala wowote utakaodumu zaidi ya miaka 10, tumejipangia wenyewe.

Miaka 10 ni mifupi sana kwa maisha ya utawala na kibinadam na ni muda mrefu sana kwa maisha ya kutawala Ki-Mungu mtu.
 
Madai ya kitoto sana haya..ok currently sauti ya nature inasemaje..hebu tupe bashiri yako leo ili kesho yakitimia ukumbukwe. maana si nature hukujuza ya sirini.
Saizi nature inaseme pesa zimetapakaa mtaani, kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake πŸ˜€πŸ˜€
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…