Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 21,470
- 40,593
Simba Jumamosi saa 10 jioni itacheza mchezo wake wa Nusu Fainali dhidi ya Wydad. Simba itashinda mechi hiyo kwa sababu zifuatazo.
1. Simba haina cha kupoteza kwenye mechi hiyo kwa ivo itacheza kwa kila njia bila ya kuwa na hofu ya kufungwa.
2. Simba haina tena shinikizo kwenye Ligi ya ndani kwani kwa vyovyote vile mwakani tena itashiriki kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.
3. Wachezaji wa Simba wengi sana sasa hivi wana dhamira ya dhati kabisa kupambana kwa ajili ya timu yao.
4. Kucheza uwanja wa Nyumbani kunawapa Simba deni la kuzuia kuaibika mbele ya Mashabiki wake.
5.Kocha wa Simba ameonekana kuwa na uwezo mkubwa sana wa kutumia mbinu kucheza kitimu kuliko kumtegemea mchezaji mmoja mmoja.
6. Simba ndiyo Klabu Pekee ya Soka Tanzania ambayo ina rekodi nzuri sana ya kuzishinda timu ngumu za Uarabuni kwenye wakati wa shinikizo. Kadri shinikizo linavyokuwa kubwa ndivyo simba inavyokuwa imara zaidi kupambana na timu toka Afrika ya Kaskazini.
1. Simba haina cha kupoteza kwenye mechi hiyo kwa ivo itacheza kwa kila njia bila ya kuwa na hofu ya kufungwa.
2. Simba haina tena shinikizo kwenye Ligi ya ndani kwani kwa vyovyote vile mwakani tena itashiriki kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.
3. Wachezaji wa Simba wengi sana sasa hivi wana dhamira ya dhati kabisa kupambana kwa ajili ya timu yao.
4. Kucheza uwanja wa Nyumbani kunawapa Simba deni la kuzuia kuaibika mbele ya Mashabiki wake.
5.Kocha wa Simba ameonekana kuwa na uwezo mkubwa sana wa kutumia mbinu kucheza kitimu kuliko kumtegemea mchezaji mmoja mmoja.
6. Simba ndiyo Klabu Pekee ya Soka Tanzania ambayo ina rekodi nzuri sana ya kuzishinda timu ngumu za Uarabuni kwenye wakati wa shinikizo. Kadri shinikizo linavyokuwa kubwa ndivyo simba inavyokuwa imara zaidi kupambana na timu toka Afrika ya Kaskazini.