Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
wakulima hewa wapo wengi sana kwa nje wanafanya kilimo ila kwa ndani wanabiashara za hatari sana kwa taifa wanapenyeza mizigo yao bandarini kwa vibali vya kilimo hawalipi kodi na biashara zinaendelea wakulima hewa wapo sanahis excellency Magufuli anashangaa kwa nini hakuna wakulima hewa, bali kuna wafanyakazi hewa.........
daaaaaaaaahhh............hii ni noma sana mkuu.........na kuna watu watakuwa wanajua sana sema wapo wametuliaaaaaaa kama sio wao vile.wakulima hewa wapo wengi sana kwa nje wanafanya kilimo ila kwa ndani wanabiashara za hatari sana kwa taifa wanapenyeza mizigo yao bandarini kwa vibali vya kilimo hawalipi kodi na biashara zinaendelea wakulima hewa wapo sana
Jasusi ni mtu anayechukua au kukusanya taarifa za nchi nyingine zinazochukuliwa kuwa ni siri bila ya ruhusa. Kwa upande wa anakopeleka taarifa hizo huwa ni faida lakini kwa upande anakozichukua huwa ni hasara kulingana na taarifa ziilizochukuliwa.
Jasusi huyo anaweza kuwa wakigeni, yaani kutoka nje ya nchi au wanyumbani yaani wa nchi husika ambaye hugeuka kuwa Double agent na huyu ndio huwa hatari zaidi hasa anapokuwa katika nafasi ambazo zinamuwezesha kuzipata taarifa mbalimbali kwani anakuwa ameaminiwa na huwa vigumu kumgundua japo hupatikana kulingana na ubora wa counter-intelligence measures za nchi husika, lakini kama hakuna tips au viashiria vyovyote kumgundua mwingine anaweza hadi kufa au kustaafu na asijulikane.
Tabia ya majasusi kuiba siri za nchi nyingine ni sehemu ya maisha yenyewe ya ujasusi, jinsi gani upo smart kupata taarifa za mwenzako either adui, au jirani au mshindani ndio jinsi utakavyokuwa bora.
Hawa double agent wanapatikana kwa kuwa spotted na maadui kwa kuchunguzwa vizuri na kisha kufuatwa au wenyewe ku-offer service kwa kujipeleka kwa sababu mbalimbali. Sehemu nyingie ambazo hawa double agent hupatikana ni pale nchi zetu zinazoendelea zinavyopeleka watu wetu nje kupata mafunzo zaidi kama vile MAREKANI, UINGEREZA n.k kwa vile wao ndio wanaendesha mafunzo ni rahisi kuwa-spot wale ambao ni the best kisha kuwa-approach wakijua watakuja kupata nafasi nzuri na nyeti sana katika taasisi zetu.
Hawa wa nje wapo tu hawazuliki, wengine wafanyabiashara, wanafunzi, wanadiplomasia, kwenye mashirika ya kimataifa, NGO's n.k. hakuna jinsi ya kuwazuia wakija kwa njia hii suala huwa ni kulimit tu wasipate taarifa za ndani, hawa wanaweza kupata taarifa za kawaida kupitia vyanzo vya wazi kama kupitia mitandao, magazeti, midahalo, bunge, n.k mfano yanayoendelea sasa kuhusu mijadala ya muungano wetu n.k ni wazi yanajulikana tu.
Sasa hawa wa ndani, ambao huigeuka nchi yao na kuisaliti kwa kutoa siri ndio hatari zaidi kulingana na nafasi aliyopo, kiasi cha muda wa usaliti wake na uwezo wake wa kujificha asijulikane. Hizi ni baadhi ya sababu zinazopelekea jasusi kuisaliti nchi yake.
1.PESA
Hii ndio motivating factor kubwa kabisa ya jasusi kuisaliti nchi yake kwa nchi nyingine, ndio maana hawa jamaa hulipwa vizuri kadri inavyowezekana. Sasa ikitokea either haridhiki na anachokipata kwa sababu zake binafsi kama vile kutaka kuishi maisha ya gharama au tu anahisi mshahara haumtoshelezi hivyo wakitokea watu wakamuahidi kiasi kikubwa cha pesa anaona atoe siri apate hizo pesa. Mfano ni jamaa mmoja John Walker alikuwa mtaalamu wa mawasiliano mwenye cheo cha Warrant Officer katika jeshi la maji la Marekani ambaye alipatikana na hatia ya ku-spy kwa ajili ya Soviet( Russia ya zamani) kuanzia mwaka 1968-1985. Motive yake ilikuwa pesa kwani alikuwa na matatizo ya kiuchumi.
2. MTIZAMO, UZALENDO,IMANI NA UTAMADUNI
Kutofautiana kimtazamo na either jinsi nchi inavyoongozwa au sera zinazoongoza nchi mfano Kim Philby alikuwa agent wa shirika la kijasusi la uingereza MI6 aliamua ku-spy kwa ajili Soviet union kwa kuwa alikuwa akiamini katika ukomunist, mwingine ni Fritz Kolbe alikuwa mwanadiplomasia katika wizara ya mambo ya nje ya ujerumani, aliamua ku-spy kwa ajili ya wamarekani katika vita ya pili ya dunia kwa kuwa hakukubalina na sera za u-nazi.
Jonathan Pollard mmarekani mwenye asili ya uyahudi aliamua kuiba siri kuhusu jeshi la marekani kuzipeleka Israel akiwa katika kitengo cha intelijensia ya jeshi mwaka 1987, alipewa kifungo cha maisha ila anatarajiwa kutolewa mwakani.
Pia hii ya uzalendo, imani na utamaduni ndio silaha kubwa iliyotumiwa na Isreal kupata majasusi wengi katika nchi nyingi maadui zake hasa nchi za kiarabu ambao walikuwa wakipeleka taarifa na ikawa moja ya sababu ya kushinda kwa urahisi kabisa vita vile vya siku sita, kwani wahusika walijihisi wayahudi zaidi kuliko utaifa wa mataifa waliyozaliwa na ndio sababu pia Israel ilikuwa ikiwachunguza sana waisrael waarabu kiasi cha kutengeneza kikosi maalum kilichopelekwa kujipenyeza katika jamii hizo za kiarabu, japo ni raia waisreal lakini walihofiwa kutumiwa na mataifa ya kiarabu kutokana na uarabu wao.
Nadhani ndio maana kipindi fulani tulikuwa na uhusiano wa kusuasua na nchi moja jirani watu walianza kuhoji wale wenye asili ya huko walio sehemu nyeti kama ikulu, ni kwa sababu kama hii.
3.KULAZIMISHWA KWA KUTISHWA
Kutishiwa maisha ya familia yake au uhai wake, akaambiwa alete taarifa au siri juu jambo fulani ili yeye au familia iwe salama. mfano Mathilde Carre alikuwa member wa french resistance waliokuwa wakipamabana ufaransa uvamizi wa wa-nazi wakati wa vita ya pili ya dunia alikamatwa na nazis wamtishia maisha na akatakiwa akachukue taarifa awaletee wao.
4.KUTOKUTHAMINIWA
Inaweza kujitokeza pale mtu anajihisi anafanya kazi nzuri na kubwa akihitaji kuthaminiwa lakini hawi appreciated akionekana mtu mdogo tu huku yeye akijiona bora kuliko wanaomzunguka. Anaweza kuamua kwenda kwa mshindani ku-offer his service. mfano ni Robert Hanssen, alikuwa agent wa FBI akaamua ku-spy kwa ajili ya Warusi kuanzia mwaka 1979-2001. Huyu ni katika doube agent aliyeiumiza sana marekani kwa kuiba siri nyingi na kupeleka Urusi, mfano kipindi hicho Warusi walijua siri nyingi za kijeshi kiasi kama wangeingia vitani basi ilikuwa shughuli nzito sana kwa marekani, warusi walijua kila submarine ya marekani ilipo.
Karibuni kwa michango
Ahsante Mkuu kwa maelezoMkuu, imeeleza vizuri sana katika huo ulimwengu wa ujasusi.
Lakini kila sehemu ni lazima pawepo na hii counter intelligence yaani ujasusi kinzani.
Hii ni kwa sababu kama taarifa zisizo sahii zinapatikana ni lazima pawepo na double agent ili azipitie na kuhakiki kisha kuthibitisha kwa wakubwa.
Mfano ili kufahamu kinachoendelea TRA basi ni lazima TRA wawe na majasusi wao lakini wanaweza kuwa wanafanya kazi moja na majasusi kutoka nje ya TRA.
Lakini pia hali hii ya kufanya kazi sehemu mbili tofauti inapelekea majasusi kuja kuwa double agents kwa kubadili kabisa waajiri yaani "vice-versa" na hii ndio hali inatokea wachina wananyonga au Iran na kwingine wasipopenda upuuzi huo.
Hivyo kuna counterintelligence yaani kuchunguza majasusi kutoka nje waliopo ndani ya nchi ambao wana nia ya kuharibu kwenye uchumi, kufanya mauaji kwa niaba ya nchi au taasisi za nje.
Halafu kuna counter-espionage ambapo majasusi wa ndani pia wanalinda taarifa maalum au za siri kuhusu nchi kama vile miundo mbinu, mitambo ya mawasiliano zisidukuliwe na majasusi wa kutoka nje mbao wanawakilisha nchi zao.
Nilikuwa nasikitika sana pale nilipoona wachina wanauza karanga, mitumba na CDs mitaani nikasema kweli vijana wenzetu wapo kazini kweli, lakini nina imani sasa hivi wapo imara.
Hawa walikuwa hawauzi tu hivyo vitu mitaani walikuwa na malengo yao.
Sasa ni double agents wangapi wameisaliti nchi yetu maana situ kwenye kusaliti kutoa taarifa bali hata kusafirisha nje ya nchi wanyama kama Twiga, meno ya tembo, na Tumbili ni nyara za serikali.
Je wanastahili adhabu gani hawa?
Lakini dhamira kuu ni uroho na tamaa.
Ahsante Mkuu. TinkerTaylorSoldierSpy nimeiona.Mkuu Mngony, kuna movie moja itafute inaitwa "The Double" ya 2011.
Kuna jamaa Mrusi humo anaitwa code name yake -Cassius ambae ilidhaniwa na CIA kwamba alikuwa amekufa na alikuja kumuua mbunge au senator na kukawa na mtafutano.
Sasa kazi ya kumtafuta Cassius inakolea pale bosi wa CIA anapompa kazi hiyo jasusi aliestaafu Richard Gere ambae anaungana na binti kutoka FBI na wenzie kumsaka Cassius.
Hii ni moja ya movie nzuri za kazi ya ujasusi ulotukuka pamoja na ile ya The Good Sherpard ambayo inasisitiza zoezi la kutafuta majasusi hodari.
Pia zipo movie zingine nzuri tu za kujifunza na kuelewa mbinu mbalimbali za kazi hii ngumu.
Kuna ingine inatwa Tinker, Taylor, Solder, Spy pia ya 2011.
HIVI WAKUU HAWA WAJOMBA KWA NINI WANA VAA MIWANI NYEUSI?KWA TANZANIA NAWAONA SANA WAKIWA KATIKA HAFLA WAKIWA WAME VAA KAUNDA SUTI ZA MIKONO MIFUPI NA VEST NDANI....hapa namkumbuka @EdwardSnowden alipowachuuza NASA kwa kutoa siri zao za udukuzi kwa viongozi wa mataifa mengine,japo si wa kumwamini kwa sababu spy-agent yeyote si rahisi kutambua anatumika upande ule ule au la
ndugu sidhani......wale jamaa huwa ni wazelendo sana kwa nchi yao,..then wanalipwa vizuri sanahivi kuna jasusi anaweza kuwa double agent wa CIA na TISS? Yan TISS wamtumie kupata taarifa za USA?
ah mkuu hii hbr imenitachi sana ila umeficha vingi kweli......Sio suala la pesa tu kama rushwa ya barabarani kuna kuchungwa na kufuatiliwa mienendo kwa hali ya juu kabisa!!!!
Adhabu yake iko wazi kabisaaa so ku trade maisha na kukiuka kiapo sio jambo dogo pia!!!! Haswa kwa anayefahamu consequences just in case...
Kumbuka Rais wa nchi jirani katoa salamu gani kwa wasaliti wake???!!! Sasa imagine hadharani kasema hivyo,covert part ikoje???!!!!
Kuna mmoja alihisiwa tu anavujisha alikiwa jeshini nchi fulani ,advertise ya kwanza aliuliwa mkewe na kupigiwa simu aseme kalikisha file gani na kwa nchi gani?!! Kwa kuwa hakuwa amefanya ilibidi ampeleke mwanaye kituo cha polisi say (Oysterbay) akamtelekeza hapo kwa usalama naye akaenda mji mwingine say Arusha na kujisalimisha polisi akaeleza kila kitu isipokuwa tu kazi yake (ya ndani)!!!
Na kusisitiza kuwa kaenda kusalimisha uhai wake sababu akiwa nje ya pale atakufa tu iwavyo vyovyote!!!
So pamoja na donge nono,hatari yake ni zaidi ya hatari!!!!!
mkuu kwani mfano ukiwa nchi jirani lets say kenya/rwana nk ukaona wanapanga mipango mibaya kuhusu kudhuru au kuididimiza nchi yako hautatoa taarifa nchini mwako?Hii makitu mie huwa nayapenda sana,i wish ningekuwa mmoja wao wa hao maspy
Sent from my iPhone using JamiiForums app
kamwe hauwezi kujua mipango ya ndani ya siri unless you are part of the inner cycle of their system. na hao sasa ndio huitwa "double agents" ama "moles". mipango ya hujuma kwamwe hauwezi kukuta ikijadiliwa hadharani kama kwenye vijiwe vya kahawa na kukuwezesha wewe kusikia.mkuu kwani mfano ukiwa nchi jirani lets say kenya/rwana nk ukaona wanapanga mipango mibaya kuhusu kudhuru au kuididimiza nchi yako hautatoa taarifa nchini mwako????????????
We ni jasus tayar na huo ndo uzalendo,...ila huna mafunzo tu,....israel wao kila raia anapita mafunzoni kumjengea uzalendo.......
ni sahihi ila pia sometimes hutokea vitu kuleak hasa kwa officials, unalijua hilo?kamwe hauwezi kujua mipango ya ndani ya siri unless you are part of the inner cycle of their system. na hao sasa ndio huitwa double agents. mipango ya hujuma kwamwe hauwezi kukuta ikijadiliwa hadharani kama kwenye vijiwe vya kahawa na kukuwezesha wewe kusikia...........never ever.
hao central intelligence wananunulika sana tu tena kwa urahisi kweli kweli. mbona iran, north korea, china na hata russian moles wamajaa sana ndani ya CIA? issue inakuja sasa unamuingiaje kama unataka kumnunua moja kati ya hao mawakala wao!ndugu sidhani......wale jamaa huwa ni wazelendo sana kwa nchi yao,..then wanalipwa vizuri sana
sidhani hiyo idea uliyoitoa kma inaezekana...........
mkuu, leakage ya mambo mazito si kitu kidogo ndugu yangu. kumbuka kuna kitu huwa wanaita cycle of information. idara nyingi sana za usalama (kama sio zote) huwa wanaweka limitations za ujuzi wa taarifa kwa kila mfanyakazi kulingana na security clearance aliyonayo. so the more clearance you score, the closer you get to the cycle. hata wanausalama wenyewe hawajuani wote kama hawapo unit moja na majukumu yao hayafanani.ni sahihi ila pia sometimes hutokea vitu kuleak hasa kwa officials,..
unalijua hilo?????
nlichozungumzia hapo sio tu vijiweni hata mtu upo ofisi flani may be ya umma,.nchi nyingine ukapata leaks kuhusu nchi yako nani mambo mabaya,.......lazma ulipoti nchini mwako
ndonlichomaanisha