Sadaka ya kujimaliza ya kwa Mwamposa inatia watu umasikini

Sadaka ya kujimaliza ya kwa Mwamposa inatia watu umasikini

Natoa Rai kuw msingatieni Sana mwamposa msimpuuze Kuna kitu ndani yake ambayo wengi hawana

Mm Sina neno nao Kama Ni wa mungu bas sawa Kam si nabii wake ni tapeli ila nijuacho mm anakitu ndani yake
Shuhuda zake azielezeki maelfu humfata je Ni Nani huyu
Hivi Yesu alikuwa anachangisha waumini wake na kuishi kwa anasa kama hawa wa sasa?
 
Ila pale kwa Mwamposa kuna baadhi ya vitu havipo sawa. Kuna mzee alipata ajali Musoma akavunjika mguu. Ndugu yake akaamua kumleta Dar kwa matibabu zaidi. Alipofika huku akiwa katika matibabu ya hospitali (ikiwa anatumia magongo kutembelea) akasikia kuhusu Mwamposa.
Akaamua kwenda kuombewa huko. Alipofika akaitwa mbele kwenye ibada maalum akaambiwa atupe magongo keshapona. Sasa sijui ilikuwa mzuka wa imani akaweza kutembea mpaka nje ya kanisa. Kufika kituo cha daladala kwa kuchechemea mguu ukamchachia hakuweza kutembea tena na pesa yote katoa sadaka ya kujimaliza. Ikabdi apigie simu ndugu waende kumchukua. Na mpaka kupona kwake ilibidi kutumia fimbo ya fagio maana magongo aliacha kanisani.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Juzi Bi. mkubwa wangu kanitembelea nyumbani, sasa yeye ni mmoja wa waumini wa kwa Mwamposa.

Baada ya salamu za hapa na pale akaomba awekewe channel ya Mwamposa aangalie ibada.

Wakati tukiangalia kulikuwa ni kipindi cha sadaka, kilichonishanga ni hii sadaka ya kujimaliza yaani toa chote ulichonacho ili ubarikiwe zaidi.

Nikamuuliza Bi mkubwa na wewe huwa unajimaliza? Akanijibu ndio kuna siku nilijimaliza nikakosa mpaka nauli nikachoka.
Bi mkubwa alijimaliza.
 
Niliwahi forciwa wakati fulani na B mkubwa kwenda kwenye mahubiri ya Jamaa, saaa mimi ikabidi nibebe bible ndogo, na lengo ni kwamba anapo tanka kitabu fulani basi nisome, Day ya kwanza hakuna sehemu alitamka Fungu zaidi ya yeye kufika na kuanza kuita watu watoe ushuhuda, nikajisemea labda ratiba ndo iko hivgo, Day 2 pia hivyo hivyo, nikajikaza nikaenda day 3 navyo hivyo, tangu siku hio sikwahi kanyaga kwa jamaaa tena. Siku tatu hakuna kusoma fungu,
Uwa unasoma bwana vifungu ...usipotoshe watu, kwenye ukweli useme
 
Natoa Rai kuw msingatieni Sana mwamposa msimpuuze Kuna kitu ndani yake ambayo wengi hawana

Mm Sina neno nao Kama Ni wa mungu bas sawa Kam si nabii wake ni tapeli ila nijuacho mm anakitu ndani yake
Shuhuda zake azielezeki maelfu humfata je Ni Nani huyu
Kama ni nabii WA kweli aombee maji yatoke na umeme usiwe unakata hovyo
 
ili uishi miaka mingi ya uzima na amani ;zishike amri za Mungu mkuu na wala usisahau sheria zake..

ukienda kujimaliza huo ni uzwazwa wako.. password ya mafanikio ushapewa vitabuni.
 
Yaan wanaopaswa kupimwa afya ya akili ni waumini wa hayo makanisa wanaweza kukuta wote wameshadumazwa akili!
 
Kuna vijana wanaokoka wanashawishi na wazee wao waache makanisa mama waambatane nao! Wazee walioishi na kuwalea hadi mmekuwa na familia mnawachomoa kwenye makanisa yao! Mwisho wengi wanavurugwa na imani yenyewe while walikuwa na amani!

Waacheni wazee wenu kwenye makanisa yao mnawaharibu na mihemuko yenu mkishaokoka! Wameishi miaka kibao kwa amani kwenye makanisa mama then mnawavuruga uzeeni na makanisa ya mwendokasi. Mzee anaugua magonjwa ya uzee unaanza kumzungusha kwenye makanisa kutafuta uponyaji! Mwisho anafariki kwa uchovu wa mengi.
 
WAIHUBIRIO INJIRI. WATAPATA MKATE KWA HIYO INJIRI
Watu washenzi sana hawafahamu kuwa makuhani watakula madhabahuni..wanesahau kua kabila la walawi hawakupewa ardhi kaanani kwasababu kazi yao kuu ilikua kuhudumu madhabahuni.

Leo hii watu wakiona wachungaji na maaskofu wanaishi vzr kupitia madhabahu wanaanza kuropoka.

Madhabahuni ndio ofsini mwao.

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom