Saed Kubenea amburuza Paul Makonda Mahakamani, kupanda kizimbani Desemba 3, 2021 kwa makosa ya jinai

Mimi nikizoom naona tarehe 24 na siyo tarehe 27, Tarehe 27 ndo gazeti lilitoka
 
Mle tungwa
 
Waliomtuma wana kila nyenzo ya kumlinda, kubwa zaidi majaji ni wa kwao, na hao watakaotakiwa kutoa ushahidi wanaweza wakaogopa kufunguka ipasavyo kwa kuhofia "usalama" wao na vitega uchumi vyao.
Aliyemtuma Sabaya ndo alimtuma Makonda .Vipi usalama na uchumi wa.....
..
 
Reactions: Lee
kwani huyo Kubenea ni lini atawapeleka mahakamani wale waliomwagia tindikali
 
Wacha upepo uvume tuzione nyeti za kuku. Kuna maovu mengi sana Makonda alifanya na hayakuwa kuripotiwa popote,sasa huko mahakamani ndiyo tutayajua mengi kama ambavyo tumejua upuuzi mwingi unaofanywa na Polisi kuwabambikia wapinzani kesi ili kuinusuru CCM katika kesi ya kishetani ya kumsingizia Mbowe kuwa ni gaidi. Na pia kupitia kesi ya Mbowe Watanzania tumejionea wenyewe jinsi Mahakama inavyonajisiwa na watawala wabovu,Jaji anafanywa kama houseboy kuendesha kesi kiboya ili ilingane na hukumu aliyokwisha andikiwa na mtawala.Wacha mvua inyesha tuone wapi panavuja.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Kesi iko mahakamani,tuaichie Mahakama ifanye kazi yake,kama haina mashiko itatupiliwa mbali

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
[emoji3] [emoji3] [emoji3] Nole kivipi Sasa, wakati kesi haijafunguliwa na Dpp... Yeye anamamlaka na kesi anazoshtaki yeye na kifungu ni 91
 
Huyo saed kubenea wana ugomvi na makonda toka ikiwa mbunge wa jimbo mojawapo la dar na yeye makonda akiwa mkuu wa wilaya hapo dar....

Ilikuwa hivi, kulitokea tatizo kwenye eneo lao, kubenea akawahi kufika na kuitisha mkutano kwa wananchi..watu wakaitikia kweli...ila ghafla mkuu wa wilaya makonda akaingia na gari zake...akamkuta kubenea anaendesha mkutano kama mwenyekiti.....makonda akawa anabaniwa nafasi ya kuongea....sasa makonda akauliza ww mbunge unasikiliza matatizo na unatoa solution , nani utamwagiza kutekeleza hiyo solution yako? Mbele ya wananchi kubenea, akasema na mkuu wa mkoa....makonda akamuuliza ww una serikali? Kubenea akaanza kufoka na kurushiana maneno mbele za watu....unajua kilitokea nini?

Makonda akatoa amri kwa askari wakamkamata kubenea hovyohovyo wakampeleka sero hahahahaha....kwahiyo hao jamaa hawapatani kabisa
 
Wewe ni MJ#NG@ unajua mateso aliyowapatia watu nyakati yuko kwenye cheo au wee ndio mshtakiwa mwenyewe
 
Kubenea anaenda kukata kiu ya mamilioni nikiwepo mimi. Bila kujali mahakama itaenda kuamuaje, lakini tu kufika viunga vya mahakama inatosha.

Jah Bles
 
Kubenea anaenda kukata kiu ya mamilioni nikiwepo mimi. Bila kujali mahakama itaenda kuamuaje, lakini tu kufika viunga vya mahakama inatosha.
Nilichokuwa sifahamu ni kuwa lengo la ule uvamizi lilikuwa kushinikiza kurushwa picha zinazomdhalilisha mch Gwajima.

Madaraka ni zaidi ya kilevi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…