Safari ya gari Cape Town, Afrika Kusini mpaka Dar es Salaam, Tanzania

Safari ya gari Cape Town, Afrika Kusini mpaka Dar es Salaam, Tanzania

Hii ni picha umedownload, ila hata ingekuwa ni bajaj haiongezi wala kupunguza millage.

Cape town mpaka Dar ni zaidi ya kilometer 5000 inategemea unapitia njia gani, kuna njia zaidi ya tatu.

Ukipitia Johannesburg maana yake mpaka Dar si chini ya kilometer 6000. Pili kuna vitu vya kuzingatia kibali cha interpol na border ya kuingia Tanzania ili gari iingie kwa kulipia transit tu ni lazima gari iingizwe na mgeni yani siyo Mtanzania kwamba anakuja kutembea, sidhani kama utaratibu umebadirika, ila kama upo vizuri ujiandae kulipa ushuru wa hiyo gari border kama unaingia nayo mwenyewe kwa passport ya Tanzania, kitu ambacho najuwa hiyo gari utaiacha tu border na kupanda basi kwenda Dar na huenda hiyo gari ukaiuzia hapohapo border. Unawajuwa TRA?

Nimekufumbuwa macho kidogo, wajuzi watakueleza zaidi.
Ataiuza kweli sio poa
 
Hii ni picha umedownload, ila hata ingekuwa ni bajaj haiongezi wala kupunguza millage.

Cape town mpaka Dar ni zaidi ya kilometer 5000 inategemea unapitia njia gani, kuna njia zaidi ya tatu.

Ukipitia Johannesburg maana yake mpaka Dar si chini ya kilometer 6000. Pili kuna vitu vya kuzingatia kibali cha interpol na border ya kuingia Tanzania ili gari iingie kwa kulipia transit tu ni lazima gari iingizwe na mgeni yani siyo Mtanzania kwamba anakuja kutembea, sidhani kama utaratibu umebadirika, ila kama upo vizuri ujiandae kulipa ushuru wa hiyo gari border kama unaingia nayo mwenyewe kwa passport ya Tanzania, kitu ambacho najuwa hiyo gari utaiacha tu border na kupanda basi kwenda Dar na huenda hiyo gari ukaiuzia hapohapo border. Unawajuwa TRA?

Nimekufumbuwa macho kidogo, wajuzi watakueleza zaidi.
Ahsante kwa maoni yako. Kuhusu TRA ni mahesabu ya kawaida hakuna tofauti ya uingiza gari kupitia bandari.
 
Mateso yote ya nini mtoa post panda ndege hizo gharama za gari,,border,service na risk, zingine za njiani achana nazo unless kama mko kifamilia zaidi ya 4 people
Asante kwa ushauri. Ila kila mmoja ana matamanio, mipango yake katika maisha. Hata utokapo nyumbani kwenda kazini asubuhi hujui litakalo kukuta barabarani (hiyo ni risk pia) ila unaenda kazini na kurudi.

Kama pesa inaruhusu, hivyo ndivyo kufurahia maisha na kuona mazingira tofauti.
 
Wakuu vp experience ya basi ya abiria kutoka Cape town kuja Tanzania, nauli imekaaje na uchukuwa siku ngap

na kama kuna details zinazohitajika zaid ya Passport, ningependa ufafanuzi kwa anayefaham
Hakuna basi kutoka Capetown hadi Dar.
Hapo itabidi uunge uunge.
Capetown hadi Johburg kisha Johburg hadi Lusaka kisha Lusaka hadi Tunduma/Nakonde.
 
Hata ukiwa na residence permit document yako kama imekua declared kama EX1 -Permanent Export maana yake hio gari imekua deregistered na hairudi South Africa kwaio ikifika border inakua IM4( import for home use) kwaio itatakiwa ulipie ushuru labda ufanye mchakato ila kama itatoka kwa Temporary Export utakata tu ile Temporary Import Permit - TIP ambayo utapewa either mwezi mmoja...
Gari ninayo hapa natumia na sijalipia kodi na ikitoka hapa inaenda Malawi ndio ntalipia kodi mbona unalazimisha vitu visivyokuwepo ni kama navyopita Botswana au Zambia bila kulipia Kodi unaweza kukaa Zambia muda unaotaka na ukaamua kuondoka ili mradi ulipie kibali cha kutumia gari kwa muda pale ila kama gari destination yake ni hapa na nimeamua kulipa nalipa tuu maana kodi yake haijachangamka kama gari za kutoka Japan..
 
Gari ninayo hapa natumia na sijalipia kodi na ikitoka hapa inaenda Malawi ndio ntalipia kodi mbona unalazimisha vitu visivyokuwepo ni kama navyopita Botswana au Zambia bila kulipia Kodi unaweza kukaa Zambia muda unaotaka na ukaamua kuondoka ili mradi ulipie kibali cha kutumia gari kwa muda pale ila kama gari destination yake ni hapa na nimeamua kulipa nalipa tuu maana kodi yake haijachangamka kama gari za kutoka Japan..
Sawa mkuu gari unayo South Africa au Tanzania?
 
Ila msinunue gari mtandaoni SA watu wametapeliwa sana matrekta na gari mnaambiwa sijui bank repo pana utapeli sana hapo siku ntaanzisha uzi wake njia salama ya kununua na kusafirisha gari kutoka ZA...
Mkuu siku ukishusha huu uzi naomba unitag, halafu vipi na kuhusu spare kwa kununua online pia si salama kwa sasa pia?.
 
Mkuu siku ukishusha huu uzi naomba unitag, halafu vipi na kuhusu spare kwa kununua online pia si salama kwa sasa pia?.
SA imeingiliwa ila naweza kukupa address mara ya kwanza ukifika hapo Nugget parts au Bumper to Bumper trip zinazofatia unachukua wanakupa simu zao unawasiliana nao kwa whatsAap tu ukishafanya manunuzi kwa mara moja ni rahisi kufanya nao manunuzi mtandaoni au unaenda trip moja ni kuchukua mawasiliano na truck za kusafirisha mizigo yako...
 
SA imeingiliwa ila naweza kukupa address mara ya kwanza ukifika hapo Nugget parts au Bumper to Bumper trip zinazofatia unachukua wanakupa simu zao unawasiliana nao kwa whatsAap tu ukishafanya manunuzi kwa mara moja ni rahisi kufanya nao manunuzi mtandaoni au unaenda trip moja ni kuchukua mawasiliano na truck za kusafirisha mizigo yako...
Sawa mkuu mie kwa sasa sina mpango wa kwenda nilikuwa nikitembelea platforms tofauti za huko hivyo nikaona huu usumbufu wa wafanyabiashara wetu kutupiga bei ya ajabu ndio nikaona siku moja nijaribu na huko.

Ila nikiwa sawa nitafata tuu nitaanza na Msumbiji halafu katika na huko.
 
Kwamba una temporary permit ya zaidi mwezi mmoja?
Wewe jamaa unauliza ufundishwe au nina miaka zaidi ya 20 nafanya kazi za magari na vitu vingine SA matakataka yote na sheria nyingi zinabadilika tupo kwenye gemu...humu nipo kuwaeleza wengine wasione ugumu wewe unaleta mambo yenu ya Kitanzania kuwa haiwezekani unafaidika nini wakati gari za Gauteng zipo nyingi Daslm na mikoa mingine..
 
Back
Top Bottom