Safari yangu ya Dar-Njombe-Iringa-Dodoma-Tabora-Kigoma-Kasulu-Kibondo-Nyakanazi-Kahama-Singida-Dom-Dar

Siku ukipita Sitalike- Majimoto( maji ya moto) zamani waliita hivyo, uniambie nikuagizie kitu kinaitwa (MADIMU) ila angalizo mmm

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahahaahahah ulivyosikia umeme ukajua Tanesco.....haya
Ukisikia gari inatumia umeme 100% ujue haitumii mafuta, mfano Kenya wanazo 50% umeme, yaani inaanza na umeme kisha inaendelea na mafuta, gari zinazotengenezwa siku hizi ni 100% umeme, unaanza na umeme na utamaliza kwa umeme haina injini ya mafuta japo unaichaji fasta kwenye kituo cha mafuta, hizo ndiyo gari za umeme na wanachaji kwa kutumia umeme wa Tanesco.
 
Daaaa bwana PGO ulichofanya ni Zaidi ya yaliyo katika PGO
(People General Order)
ya kitaa yaani umeupiga mrefu sana mpaka umepitiliza
Jambo ambalo wengi linawashinda,
Hongera mkuu wangu!
You are
Inspiration!
 
Hebu soma Tena nilichoandika
 
Kwanza hongera kwa safari ya kuona ukubwa wa nchi.

Watanzania wengi kutembea wanaona kama wanapoteza hela. Ndio maana maswali Yao niende Serengeti kufanya nini? Kumwona Simba tu? Ananisaidia nini?

Wapo wengi watanzania hawaijui nchi hii. Anafika sehemu kwa sababu ametumwa kikazi. Yeye mwenyewe hawezi kufanya adventure.

Mimi likizo yangu Septemba na octoba nilitembea Peke yangu kwa xtrail. Nilizunguka robo kipande Cha Tanzania. Nilivyosoma andiko lako ni kama nilikuwa najiona vile. Kasoro uliamua kuacha njia ya Mbeya, Sumbawanga, Katavi hadi Kigoma. Ungepita ungejua nchi hii ni kubwa sana.

Nimezunguka njia hiyo. Kigoma-Kasulu-Kibondo-Nyakanazi-Runzewe- Bwanga-Katoro-Geita-Mwanza. Mwanza - Geita- Katoro- Runzewe- Nyakanazi- Kakonko- Kibondo- Kasulu- Kigoma- Mpanda-Sitalika nikapitia mbugani- Namanyere- Sumbawanga- Tunduma-Mbeya - Ubaruku-Makambako-Njombe-Songea. Songea-Njombe-Iringa-Moro-Dar. Dar-Dodoma- Manyoni-Itigi - Tabora- Kaliua-Uvinza-Kigoma. Mwaka huu nimezunguka kwa private hadi raha halafu Peke yangu. Lakini nilichoka sana.

Nawahamasisha wengine kufanya route za kujionea nchi. Nahitaji kuifanya route ya Musoma to Arusha nikipumzika Serengeti panapo majaliwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…