Safari za Rais Samia nje ya nchi

Safari za Rais Samia nje ya nchi

Sidhani kama Rais anajipangia safari. Ana timu ya wataalamu wabobezi; mabingwa wa nyanja zote ambao hupanga safari zake. All options, possibilities, pros and cons; advantages and disadvantages zinakuwa zimezingatiwa by the time Rais anapokuwa anaelekea airport. Take that!
Hao unaowaita wataalamu ndiyo watu wa hovyo kabisa kuwahi kutokea.

Kama ndiyo hao wanao engineer safari za nje basi kama taifa tunapigwa sana.

Niliwah kusikia kipindi cha Jiwe kuwa kuna watu walikuwa wanamuandalia ziara ili nyuma wapige deal zao. Na walikuwa wanafurah akiwa ziaran huko kwan walijipigia kadri wawezavyo.

Naunganisha dots. Hii isije ikawa ni mbinu yao ya kuendelea kupiga deal na actually wanakula kodi mambo ya Per diem si hatar hiyo mkuu...

Enewei hizo safari za nje sioni tija yake kabisa. Maji hakuna , umeme ndo usiseme kwa saa moja unakuta unakatika hata mara 10 halafu mtu unamhie habar za safari za nje???????


Tuamke!
 
Kwanza naona umeonyesha wasiwasi wako wa kuona kama ziara za Mheshimiwa Rais pengine hazina tija nje ya nchi.ningependa kukuhakikishia na kukuambia kuwa safari za Mheshimiwa Rais zimekuwa na tija kubwa sana kiuchumi , kibiashara.kuongeza watalii, wawekezaji na kujenga mahusiano mazuri na nchi mbalimbali, hasa kwa kuzingatia sera yetu ya mambo ya nje ambayo inahusu mambo ya uchumi.

Mfano ziara ya Mheshimiwa Rais ya hivi majuzi kule nchini Indonesia imepelekea na kusaidia kupata fursa ya uwekezaji utakao leta kicheko na tabasamu kwa mamilioni ya wakulima.kwa kuwa kuna kiwanda cha mbolea kinakuja kujengwa hapa nchini. Jambo litakalofanya mbolea kupatikana hapa hapa nchini na kwa bei nafuu zaidi itakayochochea uzalishaji kwa mkulima na hivyo kuongeza kipato na kuondoa umaskini wa kaya.

Ziara ya Mheshimiwa Rais kule china ilifungua ukurasa mpya katika mambo mbalimbali ya kiuwekezaji na kidiplomasia ,ambapo ni katika ziara hiyo tuliweza kusamehewa deni la takribani billion 31 fedha ambazo zinaweza kujenga zaidi ya km 30 za barabara au vituo vya afya takribani 61 vya millioni mia tano tano au kutoa Ruzuku katika mbolea au kununua vifaa tiba mahospitalini n.k.

Ziara ya Mheshimiwa Rais kule Marekani ilifungua pia fursa mbalimbali ambapo pia alipata kuonana na makampuni mbalimbali ya utalii akafanya nayo mazungumzo ,jambo ambalo kwa sasa limepelekea kupata mafuriko ya watalii wanaomiminika na kupishana angani kuja Tanzania kama mwewe na sasa tunapokea watalii zaidi ya milioni moja na laki nane..lakini pia ni katika ziara hizo na kujenga mahusiano mazuri tumeweza kurudishwa katika mpango wa mapesa ya millenium challenge.

Amekwendaa pia huko india ambako tumepata soko kwa ajili ya mbaazi na korosho zetu ambapo hapo awali bei ya mazao hayo ilikuwa imeporomoka kama jiwe lililodondoka toka darini.lakini pia hospitali ya Apollo itajenga hapa hospitali nyingine ambapo badala ya wagonjwa kusafirishwa kwenda india watakuwa wanapatiwa matibabu hapa hapa na hivyo kuokoa matumizi ya dollar ambayo itatumika katika manunuzi ya bidhaa zingine muhimu nje ya nchi.

Amekwenda kule Ufaransa nako tumeweza kusainiana mikataba yenye manufaa makubwa sana kiuchumi na kibiashara.

Kwa ufupi ni kuwa Rais samia Amekuwa ni Rais mwenye shabaha ambaye anafanya ziara kwa shabaha maalumu ya kupata na kulenga kitu fulani chenye manufaa kwa Taifa letu Rais Samia hasafiri tu ilimradi. Lakini pia Mheshimiwa Rais amekuwa akihudhuria vile vikao muhimu ambavyo huwakutanisha wakuu wa nchi na serikali mbalimbali hapa Duniani.mfano kama vikao vya umoja wa mataifa.vikao vilivyowakutanisha wakuu wa nchi na serikali katika kujadili matumizi ya nishati safi na salama badala ya matumizi ya kuni .vikao vilivyowakutanisha wakuu wa nchi na serikali pamoja na umoja wa falme za kiarabu kule Dubai n.k.

Usiangalie gharama linapokuja suala la kukutana na viongozi wenzako bali angalia tija ya vikao na ziara hizo itakayopatikana kwa Taifa lako. Ziara za Mh Rais zimeleta matokeo chanya sana kwa Taifa letu.imeifungua nchi yetu na sasa fursa za kiuchumi zinatiririka nchini kama maji ya mafuriko.

Tanzania siyo kisiwa na kama Taifa hatuwezi kujifungia ndani wenyewe na mambo yetu wenyewe utafikiri watu wenye ukoma au wagonjwa wa corona au kipindupindu .ni lazima mkuu wetu wa nchi afanye ziara za kuonana na wenzake katika kujadili masuala mbalimbali yatakayoleta na kuchochea fursa za biashara.hatuwezi tukasema tutalima sana kila aina ya zao wakati hujaweka mikakati ya wapi utauza bidhaa zako pamoja na wapi utapata mbolea au fedha za kuwekeza katika ujenzi wa viwanda au kuvutia watu wakija kujenga viwanda vya bidhaa fulani lakini ukitoka nje ya nchi au kualika wenzako basi utapata fursa mbalimbali zenye matokeo chanya kwa Taifa lako.

Tupo katika Dunia ya ushindani,Dunia ambayo kila mtu anatafuta fursa kwa ajili ya Taifa lake.ndio maana hakuna anayetulia na kujifungia ndani tu kama kipofu wakati wenzako wanakulika fursa hadi kwa tochi.
Najiskia vibaya sana nikiona maandiko yako wa jina. Najikuta mwenye aibu sana nikiona jina la kitume linaandika habari za kichawa.

Rekebika. Nchi haina maji wala umeme, sukari ndo kabisa halafu ww unahangaika kusifia watu walioshindwa kutatua kero hizo?

Huenda una shida kubwa tumboni mwako lkn nakuhakikishia, dawa ya maumivu haiwezi kuponesha hilo tumbo lako. Unahitaji kumuona daktari bingwa wa magonjwa kama hayo aweze kukufanyia matibabu ya haraka kama ikiwezekana hata kwa opareshen. Hayo madawa ya kutuliza maumivu yatakuletea shida kwenye utumho mpana kaka.

Tafuta daktari bingwa atakayeponesha hilo tumbo lako na siyo kuhangaika na famasi na duka za dawa ya maumivu ya tumbo.

( Wanafasihi watakuwa wamenielewa vyema! )
 
Enewei hizo safari za nje sioni tija yake kabisa. Maji hakuna , umeme ndo usiseme kwa saa moja unakuta unakatika hata mara 10 halafu mtu unamhie habar za safari za nje???????


Tuamke!
Nadhani ni Tanzania tu ambapo watu wanaweza kuwavumilia watu waliokaa madarakani kwa zaidi ya miaka 60 na kushindwa kabisa kutatua changamoto nyepesi kama hizo ulizozianisha hapo.

Na ni aibu sana kwa kweli.
 
Mjinga mimi nina swali. Ni swali kumhusu Rais Samia [baadhi yenu ni mama yenu].

Sina takwimu wala taarifa zingine zozote za kuufuta huu ujinga wangu.

Na hata sijui niende wapi ili kuzipata takwimu na taarifa hizo.

Hivyo basi, JamiiForums ndiyo kimbilio langu nitakapo kupata baadhi ya taarifa.

Kwa namna fulani, JF imekuwa ni injini ya utafutaji wa baadhi ya taarifa.

Sasa ni hivi; huyu Rais wetu tokea achukue madaraka, ameshakaa nchini kwa hata mwezi mzima [mmoja] bila kusafiri kwenda nje ya nchi?

Nauliza hivyo kwa sababu naona kama vile kila baada ya wiki mbili hivi huwa ni lazima asafiri kwenda nje ya nchi, jambo ambalo sidhani kama lina tija sana kitaifa.

Wajuzi nijuzeni, tafadhalini sana.
Siku ambazo anakuwa hajasafiri huwa unapata tija gani? Tuanzie hapo.
Mambo mengine yana wivu wa kike
 
Najiskia vibaya sana nikiona maandiko yako wa jina. Najikuta mwenye aibu sana nikiona jina la kitume linaandika habari za kichawa.

Rekebika. Nchi haina maji wala umeme, sukari ndo kabisa halafu ww unahangaika kusifia watu walioshindwa kutatua kero hizo?

Huenda una shida kubwa tumboni mwako lkn nakuhakikishia, dawa ya maumivu haiwezi kuponesha hilo tumbo lako. Unahitaji kumuona daktari bingwa wa magonjwa kama hayo aweze kukufanyia matibabu ya haraka kama ikiwezekana hata kwa opareshen. Hayo madawa ya kutuliza maumivu yatakuletea shida kwenye utumho mpana kaka.

Tafuta daktari bingwa atakayeponesha hilo tumbo lako na siyo kuhangaika na famasi na duka za dawa ya maumivu ya tumbo.

( Wanafasihi watakuwa wamenielewa vyema! )
Huna akili
 
🤣

Leo yuko Namibia kuhudhuria mazishi!

Mwezi huu kasafiri kwenda nje mara ngapi vile?

This woman is worthless.
 
🤣

Leo yuko Namibia kuhudhuria mazishi!

Mwezi kasafiri kwenda nje mara ngapi vile?

This woman is worthless.
Diplomasia ya kimataifa inaendeshwa kwa kanuni za reciprocity.

Kanuni za kurudishiana fadhila, kurudishiana madhila.

Rais wetu alifariki, watu wa nje wakaja kuzika. Marais.

Rais wa Namibia amefariki. Kwa nini rais wetu asiende?

Yani tunataka watu waje Tanxania kwenye misiba lakininsisi tusiende kwenye misiba yao?

Samia kuna safari za kumsema, lakini si safari za misiba.

Hao Wanamibia wengi wamekulia Upanga tunawajua, wengi wamekulia kwenye kambi za wakimbizi Tanzania wakati wanapigania uhuru.

Tumekuwa nao karibu miaka mingi sana mpaka wanapata uhuru, leo wamepata uhuru ndiyo tuwatupe mkono?

Hata kwenye diplomasia za uchumi hilo litakuwa ni ujinga.
 
Diplomasia ya kimataifa inaendeshwa kwa kanuninza reciprocity.

Rais wetu alifariki, watu wa nje wakaja kuzika. Marais.

Rais wa Namibia amefariki. Kwa nini rais wetu asiende?

Yani tunataka watu waje Tanxania kwenye misiba lakininsisi tusiende kwenye misiba yao?
Marais wote wa dunia walikuja? Marais wote wa Afrika walikuja? Marais wote wa SADC walikuja?

Kazi za kuhudhuria misiba mara nyingi huwa ni za makamu wa Rais.

Ndani ya miezi miwili iliyopita huyu bibi anasafiri tu.

Lini anakaaga ofisini?
 
Marais wote wa dunia walikuja? Marais wote wa Afrika walikuja? Marais wote wa SADC walikuja?

Kazi za kuhudhuria misiba mara nyingi huwa ni za makamu wa Rais.

Ndani ya miezi miwili iliyopita huyu bibi anasafiri tu.

Lini anakaaga ofisini?
Namibia si some random country, kuna uhusiano mkubwa kati ya Tanzania na Namibia, wa Namibia wamekaa sana Tanzania wakipigania uhuru.

Rais Museveni wa Uganda alihadithia jinsi alivyokaa Upanga wapigania uhuru wa SWAPO.

Samia ana kazi ya ku repair some of the damage done by Magufuli during his isolationist era.

Rais wa nchi ana kazi yenye sura ya ndani ya nchi na nje ya nchi.

Na hata kama anatakiwa apunguze safari, si busara kukata safari za mazishi kwenye nchi yenye uhusiano mzuri nasi kama Namibia.

Aliyefariki Namibia ni head of state, ni rais, si VP. Ki itifaki rais anatakiwa kuzikwa na ma rais wenzake, ukimpeleka VP ni kama umem slight.
 
Namibia si some random country, kuna uhusiano mkubwa kati ya Tanzania na Namibia, wa Namibia wamekaa sana Tanzania wakipigania uhuru.

Rais Museveni wa Uganda alihadithia jinsi alivyokaa Upanga wapigania uhuru wa SWAPO.

Samia ana kazi ya ku repair some of the damage done by Magufuli during his isolationist era.

Rais wa nchi ana kazi yenye sura ya ndani ya nchi na nje ya nchi.

Na hata kama anatakiwa apunguze safari, si busara kukata safari za mazishi kwenye nchi yenye uhusiano mzuri nasi kama Namibia.

Aliyefariki Namibia ni head of state, ni rais, si VP. Ki itifaki rais anatakiwa kuzikwa na ma rais wenzake, ukimpeleka VP ni kama umem slight.
Haya, sawa. Aende tu.
 
Haya, sawa. Aende tu.
Kwenye msiba mimi sina lawama.

Na hata hizo safari nyingine zinazoweza kuwa na tija, zikifanywa vizuri, siwezi kumlaumu.

Rais hatakiwi kutapanya fedha kwa safari zisizo na tija.

Lakini pia, rais si mwali ajifungie nyumbani tu.

Unaweza kulalamika rais kafanya safari ya kutumia dola milioni moja, ukasema hizo ni pesa nyingi sana. Lakini, kama hiyo safari imeleta faida ya dola bilioni moja, then it is justified.

Kuna namna ya ku balance kusafiri na kukaa ndani.

1. Safari ziwe na cost benefit analysis nzuri. Tujue rais anaenda kufanya nini, anaenda ku represent intetests gani za kiuchumi, kisiasa, kidiplomasia.

2. Safari ziwe na uwazi. Tujue gharama, tujue sababu, tuweze kupima.

3. Safari ziwe na jumbe ndogo zinazolipiwa na serikali, zikiruhusu wajumbe wengine watakaoandamana na rais, kama wafanyabiashara walioidhinishwa, kuwa katika msafara wa rais, kwa kujilipia wenyewe gharama zote.

Mimi huwa namsema sana Magufuli, vibaya. Lakini, katika hili la tatu, Magufuli aliweza kudhibiti vizuri sana ukubwa wa jumbe za Tanzania hususan kwenye mikutano ya UN New York City.

Jumbe za Tanzania nje kabla ya Magufuli zilikuwa zinafanya kufuru.

Nakumbuka niliona ripoti moja ya TV ya New York City (local news), walifanya expose ya mabalozi wa nchi/ UN delegations za kiafrika walivyokuwa wanatanua kwenye hoteli za bei mbaya za New York City, na kufanya shoppings za kufa mtu.

Lakini, walitoa mfano mmoja mzuri wa ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Waziri Augustine Mahiga ulivyokuwa mdogo na ulivyokaa kwenye hoteli za bei nafuu sana.

Tunaweza kufanya hizi safari kwa tija tukakataa rais kutokuwa na safari kabisa kwa upande mmoja na kusafiri sana kwa upande mwingine.

Tatizo moja naliona Tanzania tunakuwa sana watu wa "all or nothing at all".

Mtu kama Magufuli aliona tatizo la rais kusafiri sana, akatuletea tatizo lingine la rais ambaye hasafiri kabisa.
 
Unadhani uhaba wa dola unatokea wapi?
Unatokana na hizi safari, mamilioni ya dola yanatumika.
Hatuna raisi, tulipigwa
 
Unadhani uhaba wa dola unatokea wapi?
Unatokana na hizi safari, mamilioni ya dola yanatumika.
Hatuna raisi, tulipigwa
Mkuu,

Kama nchi inamaliza dola zake kwa safari za rais tu, hiyo nchi haistahili kuwa nchi.
 
Kwenye msiba mimi sina lawama.

Na hata hizo safari nyingine zinazoweza kuwa na tija, zikifanywa vizuri, siwezi kumlaumu.

Rais hatakiwi kutapanya fedha kwa safari zisizo na tija.

Lakini pia, rais si mwali ajifungie nyumbani tu.

Unaweza kulalamika rais kafanya safari ya kutumia dola milioni moja, ukasema hizo ni pesa nyingi sana. Lakini, kama hiyo safari imeleta faida ya dola bilioni moja, then it is justified.

Kuna namna ya ku balance kusafiri na kukaa ndani.

1. Safari ziwe na cost benefit analysis nzuri. Tujue rais anaenda kufanya nini, anaenda ku represent intetests gani za kiuchumi, kisiasa, kidiplomasia.

2. Safari ziwe na uwazi. Tujue gharama, tujue sababu, tuweze kupima.

3. Safari ziwe na jumbe ndogo zinazolipiwa na serikali, zikiruhusu wajumbe wengine watakaoandamana na rais, kama wafanyabiashara walioidhinishwa, kuwa katika msafara wa rais, kwa kujilipia wenyewe gharama zote.

Mimi huwa namsema sana Magufuli, vibaya. Lakini, katika hili la tatu, Magufuli aliweza kudhibiti vizuri sana ukubwa wa jumbe za Tanzania hususan kwenye mikutano ya UN New York City.

Jumbe za Tanzania nje kabla ya Magufuli zilikuwa zinafanya kufuru.

Nakumbuka niliona ripoti moja ya TV ya New York City (local news), walifanya expose ya mabalozi wa nchi/ UN delegations za kiafrika walivyokuwa wanatanua kwenye hoteli za bei mbaya za New York City, na kufanya shoppings za kufa mtu.

Lakini, walitoa mfano mmoja mzuri wa ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Waziri Augustine Mahiga ulivyokuwa mdogo na ulivyokaa kwenye hoteli za bei nafuu sana.

Tunaweza kufanya hizi safari kwa tija tukakataa rais kutokuwa na safari kabisa kwa upande mmoja na kusafiri sana kwa upande mwingine.

Tatizo moja naliona Tanzania tunakuwa sana watu wa "all or nothing at all".

Mtu kama Magufuli aliona tatizo la rais kusafiri sana, akatuletea tatizo lingine la rais ambaye hasafiri kabisa.
Mimi sina tatizo kabisa na safari za nje. Sipingi Rais kusafiri kwenda nje.

Ila kwa huyu mama naona kumezidi.

Si majuzi tu hapa alikuwa Norway, Indonesia, Ethiopia,Vatican, sijui Congo, na leo yupo Namibia…..in a span of maybe 2 months.

Hata kwenye uapisho wa Bola Tinubu alienda 😀.

Alishindwa hata kumtuma Dkt. Mpango?

Kuna safari zingine unaona kabisa makamu wa Rais angetosha.

Btw, Rais Magufuli alipokufa, Rais wa Namibia hakuja kwenye msiba.

Just thought I’d throw that in there since you mentioned reciprocity.

Narudia tena, sipingi safari za nje kwa Rais. Lakini kutumia busara na kuchagua safari zipi za kwenda na zipi za kutuma mwakilishi, maamuzi mazuri.
 
Mimi sina tatizo kabisa na safari za nje. Sipingi Rais kusafiri kwenda nje.

Ila kwa huyu mama naona kumezidi.

Si majuzi tu hapa alikuwa Norway, Indonesia, Ethiopia,Vatican, sijui Congo, na leo yupo Namibia…..in a span of maybe 2 months.

Hata kwenye uapisho wa Bola Tinubu alienda 😀.

Alishindwa hata kumtuma Dkt. Mpango?

Kuna safari zingine unaona kabisa makamu wa Rais angetosha.

Btw, Rais Magufuli alipokufa, Rais wa Namibia hakuja kwenye msiba.

Just thought I’d throw that in there since you mentioned reciprocity.

Narudia tena, sipingi safari za nje kwa Rais. Lakini kutumia busara na kuchagua safari zipi za kwenda na zipi za kutuma mwakilishi, maamuzi mazuri.
Naona kuna tatizo la uwazi serikalini, kiasi kwamba inakuwa vigumu kuitetea serikali, hata ikiwa serikali inafanya safari zenye tija.

Mpaka leo kimsingi Ikulu haina bajeti maalum ama bajeti haikaguliwi.

Yale mapesa rais anayogawa ovyo barabarani, au ya kununua magoli, huwa hayana bajeti wala ukaguzi. Anaweza kiyapeleka kununua saa ya $44,000 na watu wasijue.

Na kwa kweli kukosa uwazi huku kunatafsirika kama mbinu maalum ya kuepuka utawala bora na kutaka kufanya mabaya, ikiwa ni pamoja na ubadhirifu wa mali ya umma.

Kuna dhana kwamba kukosa uwazi huku si kwa bahati mbaya, ni mpango maalum wa kuficha matumizi.

Ni vigumu hata kuilaumu serikali objectively with facts and figures, kwa sababu hatupati factual and data driven reports kuhusu safari hizi. Ingawa circumstantial evidence haioneshi kuwa tuna watu wenye akili au hata kujali hapo Ikulu.

Labda tujikite hapo kwanza kwenye data kwanza. Hivi Tanzania hatuna some sort of "Freedom of Information Act" ya kuomba hizi data? Hii ni haki ya kikatiba.

Utaitetea vipi serikali ikiwa serikali yenyewe haina uwazi wa kuonesha cost benefit analysis?

Sishangai Magufuli hata rafiki zetu hawakuja kumzika, he was an ignoble country bumpkin isolationist buffoon. Sasa kampa kazi kubwa sana Samia ku repair damage, inawezekana Samia anaonekana anasafiri sana kwa sababu anafidia mpaka safari za Magufuli.
 
Naona kuna tatizo la uwazi serikalini, kiasi kwamba inakuwa vigumu kuitetea serikali, hata ikiwa serikali inafanya safari zenye tija.

Na kwa kweli kukosa uwazi kinayafsirika kama mbinu maalum ya kuepukanutawala bora na kufanya mabaya, ikiwa ni pamoja na ubadhirifu wa mali ya umma.

Kuna dhana kwamba kukosa uwazi huku si kwa bahati mbaya, ni mpango maalum wa kuficha matumizi.

Ni vigumu hata kuilaumu serikali objectively with facts and figures, kwa sababu hatupati factual and data driven reports kuhusu safari hizi. Ingawa circumstantial evidence haioneshi kuwa tuna watu wenye akili au hata kujali hapo Ikulu.

Labda tujikite hapo kwanza.

Utaitetea vipi serikali ikiwa serikali yenyewe haina uwazi wa kuonesha cost benefit analysis?

Sishangai Magufuli hata rafiki zetu hawakuja kumzika, he was an ignoble country bumpkin isolationist buffoon. Sasa kampa kazi kubwa sana Samia ku repair damage, inawezekana Samia anaonekana anasafiri sana kwa sababu anafidia mpaka safari za Magufuli.
Safari za Samia [na watangulizi wake] zitaonekanaje zina tija ilhali huduma za msingi kama maji, umeme, n.k., bado ni changamoto?

Wamekaa madarakani zaidi ya miaka 60 lakini hadi leo bado tunahangaika na ukosefu wa umeme!

utanishawishije mimi Mnyantuzu wa Ikungulyabashashi kwamba safari zao zina tija ilhali huduma za msingi tu zimewashinda?

Ungeniambia labda Samia anaenda kutafuta power companies huko nchi za nje waje kuanza kutoa huduma ya umeme maana serikali imeshindwa, na kweli hao watu wakaja na kuanza kutoa huduma ya uhakika, guess what?

Nisingelalamika!
 
Back
Top Bottom