Safari za Rais Samia nje ya nchi

Safari za Rais Samia nje ya nchi

Safari za Samia [na watangulizi wake] zitaonekanaje zina ilhali huduma za msingi kama maji, umeme, n.k., bado ni changamoto?

Wamekaa madarakani zaidi ya miaka 60 lakini hadi leo bado tunahangaika na ukosefu wa umeme!

utanishawishije mimi Mnyantuzu wa Ikungulyabashashi kwamba safari zao zina tija ilhali huduma za msingi tu zimewashinda?

Ungeniambia labda Samia anaenda kutafuta power companies huko nchi za nje waje kuanza kutoa huduma ya umeme maana serikali imeshindwa, na kweli hao watu wakaja na kuanza kutoa huduma ya uhakika, guess what?

Nisingelalamika!
Nimeona Lucas Mwashambwa aliwajibu tija za safari lakini sijaona kama mmemjibu.

Tena nimesikitika kuona mtu mmoja baada ya kujibiwa ameponda majibu kwa kusema "nani atasoma gazeti hili?".

Hapa kuna siasa na uchumi. Kuongelea siasa kwa hisia ni rahisi.

Kuongelea uchumi kwa namba ni kazi ngumu.

Wengi tunapenda kuongelea siasa kwa hisia kuliko kuongelea uchumi kwa namba.

Na kwa kweli siwezi kuwalaumu sana mnaoongelea siasa kwa hisia, kwa sababu, kama nilivyosema hapo awali, serikali yenyewe haitoi data za kuwawezesha kufanya uchambuzi wa uchumi kwa namba.

Bila ya granular cost benefit analysis reports ni vigumu sana kuibishia serikali, kwa sababu wao wanaweza kukuambia tumeenda kuweka mazingira mazuri ya biashara na serikali za ughaibuni, kwingine kuna mikataba wafanyabiashara watasaini.

Na hata wakisaini hatujui tofauti ya MoU na a binding contracts.
 
Akae atulie ashulikie swala la upatikanaji wa sukari nnchin umekuwa si wakurudhisha hata kwa wananchi wa nchin kwa kilo.1 sukari kupanda mkuu wa.nnchi kulisemea.

Waliominiwa Kama mawakala na viwanda vya sukari wanangalia maslah.yao binafs
 
Kuwaongoza Watanzania ni tabu sana.

1. JK alisafiri sana, Watanzania wakakereka.

2. JPM alikataa safari, pia Watanzania wakadai nchi inakosa fursa.

3. Samia anasafiri, wamerudi kule kwa JK kulaumu.

Ni ajabu!
 
Mjinga mimi nina swali. Ni swali kumhusu Rais Samia [baadhi yenu ni mama yenu].

Sina takwimu wala taarifa zingine zozote za kuufuta huu ujinga wangu.

Na hata sijui niende wapi ili kuzipata takwimu na taarifa hizo.

Hivyo basi, JamiiForums ndiyo kimbilio langu nitakapo kupata baadhi ya taarifa.

Kwa namna fulani, JF imekuwa ni injini ya utafutaji wa baadhi ya taarifa.

Sasa ni hivi; huyu Rais wetu tokea achukue madaraka, ameshakaa nchini kwa hata mwezi mzima [mmoja] bila kusafiri kwenda nje ya nchi?

Nauliza hivyo kwa sababu naona kama vile kila baada ya wiki mbili hivi huwa ni lazima asafiri kwenda nje ya nchi, jambo ambalo sidhani kama lina tija sana kitaifa.

Wajuzi nijuzeni, tafadhalini sana.
anaitwa Flying president
 
Nimeona Lucas Mwashambwa aliwajibu tija za safari lakini sijaona kama mmemjibu.

Tena nimesikitika kuona mtu mmoja baada ya kujibiwa ameponda majibu kwa kusema "nani atasoma gazeti hili?".

Hapa kuna siasa na uchumi. Kuongelea siasa kwa hisia ni rahisi.

Kuongelea uchumi kwa namba ni kazi ngumu.

Wengi tunapenda kuongelea siasa kwa hisia kuliko kuongelea uchumi kwa namba.

Na kwa kweli siwezi kuwalaumu sana mnaoongelea siasa kwa hisia, kwa sababu, kama nilivyosema hapo awali, serikali yenyewe haitoi data za kuwawezesha kufanya uchambuzi wa uchumi kwa namba.

Bila ya granular cost benefit analysis reports ni vigumu sana kuibishia serikali, kwa sababu wao wanaweza kukuambia tumeenda kuweka mazingira mazuri ya biashara na serikali za ughaibuni, kwingine kuna mikataba wafanyabiashara watasaini.

Na hata wakisaini hatujui tofauti ya MoU na a binding contracts.
Takwimu kwenye makaratasi na uhalisia wa maisha waishiyo watu vikiwa tofauti sana, hata takwimu ziwe nzuri kiasi gani, utapata shida sana kuwashawishi watu kwamba mambo ni mazuri.

Ni biashara ngapi ndogo ndogo zilizoathirika na huu mgao wa umeme uliodumu kwa zaidi ya mwaka sasa?

Halafu kweli takwimu za serikali ya CCM zinaaminika?
 
Takwimu kwenye makaratasi na uhalisia wa maisha waishiyo watu vikiwa tofauti sana, hata takwimu ziwe nzuri kiasi gani, utapata shida sana kuwashawishi watu kwamba mambo ni mazuri.

Ni biashara ngapi ndogo ndogo zilizoathirika na huu mgao wa umeme uliodumu kwa zaidi ya mwaka sasa?

Halafu kweli takwimu za serikali ya CCM zinaaminika?
Hata kama takwimu haziaminiki, ni bora ziwepo iki kuonesha ni za uongo.

Zisipokuwepo tunarudi kubishana bila namba katika jambo linalohitaji namba.

Pia, serikali mara zote inaweza kukujibu kwamba kama huko nyuma tulikosea, sisi awamu yetu inarekebisha makosa.

Hoja hiyo huwezi kuipangua objectively mpaka ukokotoe namba na kuonesha kuwa kwa namba hizi, hata nyie mnarudia makosa yaleyale tu.

Tatizo serikali ina usiri mkubwa hata kwenye mambo ya haki za kikatiba za wananchi kujua.
 
Hata kama takwimu haziaminiki, ni bora ziwepo iki kuonesha ni za uongo.

Zisipokuwepo tunarudi kubishana bila namba katika jambo linalohitaji namba.

Pia, serikali mara zote inaweza kukujibu kwamba kama huko nyuma tulikosea, sisi awamu yetu inarekebisha makosa.

Hoja hiyo huwezi kuipangua objectively mpaka ukokotoe namba na kuonesha kuwa kwa namba hizi, hata nyie mnarudia makosa yaleyale tu.

Tatizo serikali ina usiri mkubwa hata kwenye mambo ya haki za kikatiba za wananchi kujua.
Ukitaka kujua usiri wa serikali, ulizia mshahara wa Rais ni kiasi gani.

Kwanza, raia tu wa kawaida watakwambia hilo wewe halikuhusu kwa sababu mshahara wa mtu ni siri ya mtu.

Sasa unakuta hata huko serikalini kuna watu wenye ujinga kama huo.

Hawaelewi kwamba utumishi wa umma kuna mambo huwa si ya siri.

Leo miaka 17 sasa hapa JF mimi nimeulizia mshahara wa Rais wa Tanzania ni kiasi gani na hakuna jibu lililonyooka.

Kila ajibuye anakuja na kiasi chake, jambo linaloashiria kwamba hakuna chanzo cha uhakika cha hizo taarifa.

Magufuli kafa na watu hata hatuna uhakika kafa lini, achilia mbali kutokujulishwa kuugua kwake!

Usiri huo wa serikali unawezeshwa na ujinga ulio wa kukithiri wa Watanzania.

Hatujui kudai haki zetu. Haki zilizo zetu tunadhani ni hisani ya walio madarakani.

Hapo unategemea kupata taarifa gani za kuaminika toka serikalini?
 
Mfano ziara ya Mheshimiwa Rais ya hivi majuzi kule nchini Indonesia kuna kiwanda cha mbolea kinakuja kujengwa hapa nchini. Jambo litakalofanya mbolea kupatikana hapa hapa nchini na kwa bei nafuu zaidi itakayochochea uzalishaji kwa mkulima na hivyo kuongeza kipato na kuondoa umaskini wa kaya.
Kiwanda cha Mbole Tanga kilikufa kwasababu gani?
Ziara ya Mheshimiwa Rais kule china ilifungua ukurasa mpya... tuliweza kusamehewa deni la takribani billion 31 fedha ambazo zinaweza kujenga zaidi ya km 30 za barabara au vituo vya afya takribani 61 vya millioni mia tano tano au kutoa Ruzuku katika mbolea au kununua vifaa tiba mahospitalini n.k.
Skiupenda !! nasema sipendi lakini nalazimika kusema pumbavu kabisa nikiwa na sababu.
1. COVID 19 kwa miezi 20 tu wamelipwa zaidi ya Bilioni 32, leo unashangilia Taifa kusamehewa peremende na China

2. Taarifa ya CAG ina zaidi ya Trilioni moja imepotea, yaani mara 30 , leo unashangilia kusamehewa bilioni 31

3. Kodi ya Kiwanda cha BIA ya miezi 5 tu ni sawa na msamaha wa China.

4. Kuna magari 500 ya serikali yamekaa tu yakisubiri dili la kuuzwa, leo unakuja kushangilia bilioni 31

5. Kuna Mikataba 30 imesainiwa China. Hatujui ilihusu nini na kwanini ni siri. Unaweza kuuza ng'ombe ununue kuku halafu useme umefanikiwa

Halafu mtu anakuja kushangalia upuuzi wa Taifa la watu milioni 60 kusamehewa pesa ya peremende

Nauliza, hivi nani anajua BAJETI ya Bunge! lini uliwahi kusikia .


 
Mjinga mimi nina swali. Ni swali kumhusu Rais Samia [baadhi yenu ni mama yenu].

Sina takwimu wala taarifa zingine zozote za kuufuta huu ujinga wangu.

Na hata sijui niende wapi ili kuzipata takwimu na taarifa hizo.

Hivyo basi, JamiiForums ndiyo kimbilio langu nitakapo kupata baadhi ya taarifa.

Kwa namna fulani, JF imekuwa ni injini ya utafutaji wa baadhi ya taarifa.

Sasa ni hivi; huyu Rais wetu tokea achukue madaraka, ameshakaa nchini kwa hata mwezi mzima [mmoja] bila kusafiri kwenda nje ya nchi?

Nauliza hivyo kwa sababu naona kama vile kila baada ya wiki mbili hivi huwa ni lazima asafiri kwenda nje ya nchi, jambo ambalo sidhani kama lina tija sana kitaifa.

Wajuzi nijuzeni, tafadhalini sana.
Kama ana afya na hana woga wa kupanda ndege sioni shida. Yule dikteta marehemu alikuwa hasafiri kwa kuwa aliwekewa kibiriti kifuani na siyo sababu ya kubana matumizi.
 
na wasipoalikwa kwenye mikutano ya wababe wa dunia kama davos au club of rome wanafura hadi wanamtuma mwanajeshi kuita watu wakimbizi, isitoshe sehemu nyingi wanajipeleka wala hawaalikwi, mambo ya nje wanaorganize tu hizo safari.

anyway 2025 tuna raisi mpya …
Nani wa kumbabaisha Mwenyekiti Chamani ??!!
Nguvu ya Mamba kumayi !!
 
Kiwanda cha Mbole Tanga kilikufa kwasababu gani?

Skiupenda !! nasema sipendi lakini nalazimika kusema pumbavu kabisa nikiwa na sababu.
1. COVID 19 kwa miezi 20 tu wamelipwa zaidi ya Bilioni 32, leo unashangilia Taifa kusamehewa peremende na China

2. Taarifa ya CAG ina zaidi ya Trilioni moja imepotea, yaani mara 30 , leo unashangilia kusamehewa bilioni 31

3. Kodi ya Kiwanda cha BIA ya miezi 5 tu ni sawa na msamaha wa China.

4. Kuna magari 500 ya serikali yamekaa tu yakisubiri dili la kuuzwa, leo unakuja kushangilia bilioni 31

5. Kuna Mikataba 30 imesainiwa China. Hatujui ilihusu nini na kwanini ni siri. Unaweza kuuza ng'ombe ununue kuku halafu useme umefanikiwa

Halafu mtu anakuja kushangalia upuuzi wa Taifa la watu milioni 60 kusamehewa pesa ya peremende

Nauliza, hivi nani anajua BAJETI ya Bunge! lini uliwahi kusikia .
Duh 🙄 !
 
Mjinga mimi nina swali. Ni swali kumhusu Rais Samia [baadhi yenu ni mama yenu].

Sina takwimu wala taarifa zingine zozote za kuufuta huu ujinga wangu.

Na hata sijui niende wapi ili kuzipata takwimu na taarifa hizo.

Hivyo basi, JamiiForums ndiyo kimbilio langu nitakapo kupata baadhi ya taarifa.

Kwa namna fulani, JF imekuwa ni injini ya utafutaji wa baadhi ya taarifa.

Sasa ni hivi; huyu Rais wetu tokea achukue madaraka, ameshakaa nchini kwa hata mwezi mzima [mmoja] bila kusafiri kwenda nje ya nchi?

Nauliza hivyo kwa sababu naona kama vile kila baada ya wiki mbili hivi huwa ni lazima asafiri kwenda nje ya nchi, jambo ambalo sidhani kama lina tija sana kitaifa.

Wajuzi nijuzeni, tafadhalini sana.
Wewe Sukuma gang unawashwa na kitu gani?
Kwanini msikubali kuwa Rais Samia sasa ndiyo kiongozi wa nchi hii ya JMT?

Jiwe alishaondoka mjomba ebu funga mkanda tusonge mbele na mama Samia.
 
Sidhani kama Rais anajipangia safari. Ana timu ya wataalamu wabobezi; mabingwa wa nyanja zote ambao hupanga safari zake. All options, possibilities, pros and cons; advantages and disadvantages zinakuwa zimezingatiwa by the time Rais anapokuwa anaelekea airport. Take that!
Mimi ni mpinzani mkubwa wa CCM lkn linapokuja suala la kiongozi wa nchi kusafiri sina tatizo naye.
 
Kwanza naona umeonyesha wasiwasi wako wa kuona kama ziara za Mheshimiwa Rais pengine hazina tija nje ya nchi.ningependa kukuhakikishia na kukuambia kuwa safari za Mheshimiwa Rais zimekuwa na tija kubwa sana kiuchumi , kibiashara.kuongeza watalii, wawekezaji na kujenga mahusiano mazuri na nchi mbalimbali, hasa kwa kuzingatia sera yetu ya mambo ya nje ambayo inahusu mambo ya uchumi.

Mfano ziara ya Mheshimiwa Rais ya hivi majuzi kule nchini Indonesia imepelekea na kusaidia kupata fursa ya uwekezaji utakao leta kicheko na tabasamu kwa mamilioni ya wakulima.kwa kuwa kuna kiwanda cha mbolea kinakuja kujengwa hapa nchini. Jambo litakalofanya mbolea kupatikana hapa hapa nchini na kwa bei nafuu zaidi itakayochochea uzalishaji kwa mkulima na hivyo kuongeza kipato na kuondoa umaskini wa kaya.

Ziara ya Mheshimiwa Rais kule china ilifungua ukurasa mpya katika mambo mbalimbali ya kiuwekezaji na kidiplomasia ,ambapo ni katika ziara hiyo tuliweza kusamehewa deni la takribani billion 31 fedha ambazo zinaweza kujenga zaidi ya km 30 za barabara au vituo vya afya takribani 61 vya millioni mia tano tano au kutoa Ruzuku katika mbolea au kununua vifaa tiba mahospitalini n.k.

Ziara ya Mheshimiwa Rais kule Marekani ilifungua pia fursa mbalimbali ambapo pia alipata kuonana na makampuni mbalimbali ya utalii akafanya nayo mazungumzo ,jambo ambalo kwa sasa limepelekea kupata mafuriko ya watalii wanaomiminika na kupishana angani kuja Tanzania kama mwewe na sasa tunapokea watalii zaidi ya milioni moja na laki nane..lakini pia ni katika ziara hizo na kujenga mahusiano mazuri tumeweza kurudishwa katika mpango wa mapesa ya millenium challenge.

Amekwendaa pia huko india ambako tumepata soko kwa ajili ya mbaazi na korosho zetu ambapo hapo awali bei ya mazao hayo ilikuwa imeporomoka kama jiwe lililodondoka toka darini.lakini pia hospitali ya Apollo itajenga hapa hospitali nyingine ambapo badala ya wagonjwa kusafirishwa kwenda india watakuwa wanapatiwa matibabu hapa hapa na hivyo kuokoa matumizi ya dollar ambayo itatumika katika manunuzi ya bidhaa zingine muhimu nje ya nchi.

Amekwenda kule Ufaransa nako tumeweza kusainiana mikataba yenye manufaa makubwa sana kiuchumi na kibiashara.

Kwa ufupi ni kuwa Rais samia Amekuwa ni Rais mwenye shabaha ambaye anafanya ziara kwa shabaha maalumu ya kupata na kulenga kitu fulani chenye manufaa kwa Taifa letu Rais Samia hasafiri tu ilimradi. Lakini pia Mheshimiwa Rais amekuwa akihudhuria vile vikao muhimu ambavyo huwakutanisha wakuu wa nchi na serikali mbalimbali hapa Duniani.mfano kama vikao vya umoja wa mataifa.vikao vilivyowakutanisha wakuu wa nchi na serikali katika kujadili matumizi ya nishati safi na salama badala ya matumizi ya kuni .vikao vilivyowakutanisha wakuu wa nchi na serikali pamoja na umoja wa falme za kiarabu kule Dubai n.k.

Usiangalie gharama linapokuja suala la kukutana na viongozi wenzako bali angalia tija ya vikao na ziara hizo itakayopatikana kwa Taifa lako. Ziara za Mh Rais zimeleta matokeo chanya sana kwa Taifa letu.imeifungua nchi yetu na sasa fursa za kiuchumi zinatiririka nchini kama maji ya mafuriko.

Tanzania siyo kisiwa na kama Taifa hatuwezi kujifungia ndani wenyewe na mambo yetu wenyewe utafikiri watu wenye ukoma au wagonjwa wa corona au kipindupindu .ni lazima mkuu wetu wa nchi afanye ziara za kuonana na wenzake katika kujadili masuala mbalimbali yatakayoleta na kuchochea fursa za biashara.hatuwezi tukasema tutalima sana kila aina ya zao wakati hujaweka mikakati ya wapi utauza bidhaa zako pamoja na wapi utapata mbolea au fedha za kuwekeza katika ujenzi wa viwanda au kuvutia watu wakija kujenga viwanda vya bidhaa fulani lakini ukitoka nje ya nchi au kualika wenzako basi utapata fursa mbalimbali zenye matokeo chanya kwa Taifa lako.

Tupo katika Dunia ya ushindani,Dunia ambayo kila mtu anatafuta fursa kwa ajili ya Taifa lake.ndio maana hakuna anayetulia na kujifungia ndani tu kama kipofu wakati wenzako wanakulika fursa hadi kwa tochi.
Umeandika pumba kama zote
 
Sidhani kama Rais anajipangia safari. Ana timu ya wataalamu wabobezi; mabingwa wa nyanja zote ambao hupanga safari zake. All options, possibilities, pros and cons; advantages and disadvantages zinakuwa zimezingatiwa by the time Rais anapokuwa anaelekea airport. Take that!
lbdaa maraisi wa developed state ndio wanafanyiwa izo analysis sio kwetu wachumia tumbo, kikwete alikuwa hivi hivi faida gan unaweza kuzipima kwenye maendeleo ya watu kipindi chake ?
 
Sidhani kama Rais anajipangia safari. Ana timu ya wataalamu wabobezi; mabingwa wa nyanja zote ambao hupanga safari zake. All options, possibilities, pros and cons; advantages and disadvantages zinakuwa zimezingatiwa by the time Rais anapokuwa anaelekea airport. Take that!
Anaweza kukaata, Rais sio robot. Wakati mwingine hao wanaoitwa wataalamu, mabingwa na wabobezi huwa wanafanya mambo kwa maslahi yao. Ian Khama wa Botswana alikuwa haudhurii vikao vya Umoja wa Africa(AU) akisema ni kupoteza muda tu huko.
 
Exactly, bottom line ni Mtanzania Afaidike, what's the point mtu akae ndani kama tupo kisiwani wakati anaweza kutengeneza Connection nyingi nje?

Mfano Kariakoo sasa hivi kuna ongezeko kubwa la wa Congo, Zambia, Wamalawi na Wacomoro, wengi walikimbia awamu iliopita wameanza kurudi kwa kasi Baada ya Raisi kupitia Nchi za jirani na kuwahimiza warudi.

Ndio maana hata wafanyabiashara walivyogoma Tra na Polisi kuharass hawa wageni na kudai Rushwa za Dola fasta fasta wakapigwa marufuku wasiwaguse.
kariakoo kwa wakimbia kodii? apo sokoni kila nikidai risiti naambiwa sio lazima kununua apa nafukuzwa maduka karibu kumi toka mwaka juzi December till leo
 
Urais ni taasisi; taasisi ni watendaji. Hata Marekani ni hivyo even more!
Mbona Rais wa Marekani ni nadra sana kumsikia akisafiri kwenda nje ya nchi? Au watendaji wake hawamshauri hivyo?
 
Back
Top Bottom