Habari za Kazi wana JamiiForums,
Katika thread hii nategemea tutaangazia ziara mbalimbali(Za nje ya nchi) za Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Suluhu Hassan na manufaa kwa taifa.
Leo tarehe 11 April 2021 Mhe Samia anafanya ziara yake ya kwanza nje ya Tanzania na ziara hii ina lengo la kusaini makubaliano ya ujenzi wa bomba la mafuta.
Tarehe 4 mei2021 Mhe Samia amezuru nchi ya Kenya na kuwahitubia wananchi wa Kenya.
Ni ziara yenye tija kwa uchumi wa Nchi. Aidha ikumbukwe mtangulizi wake Hayati Dr. John Pombe Magufuli hakuwa mpenzi wa ziara za nje ya nchi na mara nyingi alimtuma Mhe Samia Suluhu kumuwakilisha.
TUTAENDELEA KUTOA UPDATES YA ZIARA ZA NJE ZA MH RAIS SAMIA.
=====
1). Rais Samia afanya ziara yake ya kwanza nchini Uganda mnamo 11 Aprili 2021 kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa nchi mbili na kumaliza makubaliano ya mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka nchini Uganda.
2). Rais Samia afanya Ziara ya Siku Mbili Nchini Kenya, kuanzia 04 Mei 2021
3). Rais Samia tarehe 16 Julai, 2021 afanya ziara ya Kitaifa ya siku mbili nchini Burundi kwa mwaliko wa Rais Evariste Ndayishimiye.
4). Rais Samia tarehe 02 Agosti, 2021 afanya ziara ya Kiserikali ya siku mbili nchini Rwanda kwa mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Paul Kagame.
5). Rais Samia tarehe 16 Agosti, 2021 aelekea nchini Malawi kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 41 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) utakaofanyika kuanzia tarehe 17 – 18 Agosti, 2021.
6). Rais Samia Tarehe 24 Agosti, 2021 aelekea nchini Zambia kuhudhuria sherehe za kuapishwa Kwa Rais Mteule wa Zambia Mhe. Hakainde Hichilema.
7). Rais Samia tarehe 18 Septemba, 2021 aondoka nchini kuelekea New York nchini Marekani kuhudhuria Mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambapo tarehe 23 anatarajiwa kulihutubia Baraza hilo.
8). Rais Samia tarehe 30 Oktoba, 2021 aelekea Glasgow, Scotland kuhudhuria Mkutano wa 26 wa Umoja wa Mataifa utakaojadili athari za mabadiliko ya tabianchi (COP 26).
9). Rais Samia tarehe 10 Novemba, 2021 aelekea Cairo nchini Misri kwa ziara ya Kiserikali ya siku tatu.
10). Rais Samia tarehe Januari 28, 2022, atembelea Msumbiji. Akiwa Pemba-Msumbiji, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu ameeleza kuwa lengo ya ziara hiyo ni kudumisha Diplomasia kati ya nchi hizo mbili.
11). Rais Samia afanya ziara ya Kikazi Nchini Ufaransa na Ubelgiji kuanzia tarehe 09-19 Februari 2022.
12). Rais Samia Februari 24, 2022 aelekea Dubai Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kushiriki maonyesho ya Expo 2020
13). Rais Samia Aprili 13, 2022 aenda Marekani kwa ziara ya kikazi. Pamoja na mambo mengine anatarajiwa kushiriki uzinduzi wa filamu ya ‘Tanzania Royal Tour’ itakayozinduliwa Aprili 18, 2022 jijini New York. Alikaa siku 8
14). Rais Samia 10 May 2022 afanya ziara ya Kiserikali nchini Uganda kwa siku mbili
15). Rais Samia 23 Mei 2022 ameondoka Nchini Kuelekea Accra, Ghana kwa ajili ya Ziara ya kikazi ya siku tatu Nchini Humo
16). Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan awasili Muscat nchini Oman kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya Siku tatu tarehe 12 Juni, 2022
17). Leo tarehe 06 Julai, 2022 Rais Samia aelekea Dakar Senegal kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa nchi za Afrika wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kimataifa (IDA Summit for Africa)"
18). Rais Samia 16 Agost 2022, aondoka Nchini kwenda DR Congo kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).
19. Septemba 17, Rais Samia
alifika Uingereza ili kuhudhuria mazishi ya malikia Elizabeth II yaliyopangwa kufanyika September 19.
Rais Samia kuhudhuria mazishi ya malikia Elizabeth II