Sahihi kusema Arusha ndio Jiji bora Tanzania?

Sijajua kwa nini Arusha ni jiji. Ukiona nyumba yoyote imeangalia lami nenda nyuma ya hizo nyumba utakuta nyumba za udongo, tena sio mbali we anzia Sanawari, mianzini, Kwa Iddi kote huko nyuma ya nyumba nzuri unakutana na za udongo na hii hali huwezi kuikuta Dar wala Mwanza. Hivi hiyo barabara ya clock tower kwenda Kisongo unaiweka kwenye viwango vya barabara za Dar na Mwanza?

Hizo Hotel zinazoongelewa zinadaiwa maana zilishafilisika ni majengo yamebaki. Si unajua anguko la Snow crest, Impala, Ngurdoto, ile ya Sanawari yenye vioo vya bluu. Nenda Mwanza uone jinsi wenye Hotel na guest house walivyo wakarimu wanakupeleka hotelini au guest house na kukurudisha stand kwa gharama zao. Hili huwezi kulikuta Arusha wala Dar na hakuna hoteli iliyofilisika.

Hivyo viwanja vya Ndege angalia takwimu za abiria kwenye viwanja vya Tanzania uone ni uwanja gani unaingiza pesa nyingi.

Angalia stendi ya mabasi ya Singida na ya Arusha ipi bora, Soko la Kilombero na la Magomeni lipi bora?

Nafikiri ungeangalia takwimu na kutembelea nchi hii kwanza la sivyo hoja bila takwimu ni kufurahisha jukwaa.
 
Uko sahihi. Mkoa wa Arusha ulitakiwa kujengwa zaidi lakini naona kama mashamba ya kahawa yamesogelea sana jiji. Mji ulitakiwa upanuke kuelekea Ilboru, Elkinding'a n.k. Tatizo ni kwamba watu wengi wanafikiri wanaojenga mji ni wazawa wa lile eneo lile. Mji unajengwa kwa kuwekewa miundombinu na Serikali halafu wanakuja wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi.
 
Point zote za juu ni kanjanja. Bora ungebaki na ile hali ya hewa na foreign community katika jiji ilo.

Ukweli kaskazini mmejaliwa hali ya hewa nzuri. Arusha wakae makini dom ikiendelea kuwezeshwa itamkuta hapo.

Jiji bora litabaki dar, mwanza
Hiyo hali ya hewa nzuri unayoiona ni kwa sababu ya mji kuwa chini ya vilima vyenye uoto wa asili. Ukitaka kujua miji yenye hali ya hewa nzuri nenda mikoa yenye mvua mbili kwa mwaka.Ukitoka kwenye eneo la vilima ni majanga matupu. Angalia hali ya hewa ya ukitoka mjini kidogo tu mfano Mbuguni, Monduli, Bwawani, Kwa mrombo mwisho wa lami kuelekea Olkesumeti ni ukame wa hatari. Kwa sasa vilima hivyo vimevamiwa na shughuli za kibinadamu ambao ni mwanzo wa kukaribisha athari za mabadiliko ya tabianchi. Ukisimama Chekeleni upande mmoja kilima kinakwanguliwa kupata gravel, upande mwingine watu wanalima na kujenga. Muda si mrefu utasikia land slide au maporomoko.
Nchi hii ni yetu sote si ya Waarusha, ni vema serikali ikalinda vilima na mazingira yake.
 
Ni kweli. Ole Sabaya amelambavua ya miaka 30 juzi juzi. Na bado Pilato hajaachana naye. Atamtandika nyingine kama miaka 100 hivi
Ndio sifa ya huko bila kumsahau jambazi mstaafu wa magari aliyepo ughaibuni!
 
Yaani vile vidala vyao ni kero saba
 
Ndio sifa ya huko bila kumsahau jambazi mstaafu wa magari aliyepo ughaibuni!
Namjua huyu aliyethibitishwa na mahakama na kuhukumiwa miaka 30 jela na kazi ngumu. Na bado anasubiri mingine. Huyo mwingine unayemsema wa ugaibuni ni umbeya na majungu yako tu. Huna uthibitisho wowote. Kama unao uweke hapa
 
Mji gani Tzn hii ukiacha sehemu ya Dom umepimwa?
 
Dar es Salaam/Mwanza nk imepimwa kigamboni/ Nyasaka na maeneo mengine kwa njia ya kukopa Bank na limefanyika kwa mafanikio makubwa sana. Serikali ikainingila kati na kulisimamisha.
Sasa Mji gani ambao vimitaa kama hivyo haujapimwa?
 
Sasa watu hapa hawajaelewa
Mtoa mada kasema Arusha ndio jiji bora Tanzania
Na wala hajasema ni mji wenye idadi kubwa ya watu
Naona hapa kuna makanjanja wanarukia kwenye point ya kwamba Dodoma na Mwanza zimeizidi Arusha kwa kigezo cha ukubwa wa mji
Manaje ukisema ukubwa wa mji hakuna mji wowote wa kuifikia Dar hapa nchini
Ila mtoa mada anaongelea balance of social services kati ya watu na huduma zilizopo
Arusha peke yake ina private hospitals zaidi ya 3 zinazotoa vipimo vya kibingwa zamani vilivyokua vinapatikana nje ya nchi
Kila mji una madhaifu yake ila kwa level za kibongo Arusha iko mbali sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…