TANZIA Said Akachube (Akachube Road) ambaye ni muuza magari maarufu DSM afariki dunia

TANZIA Said Akachube (Akachube Road) ambaye ni muuza magari maarufu DSM afariki dunia

Muuza magari maarufu jijini Dar es Salaam, Akachube afariki dunia usiku wa kuamkia leo.

Ndugu wa karibu wamesema amefariki kwa ugonjwa wa Nimonia.

Umaarufu wake ulipelekea mpaka kupewa barabara ya Akachube iliyopo Kijitonyama

Mungu ailaze pema peponi roho yake
Kupewa barabara si umaarufu, hata wewe unaweza ukapewa. Tangu mfumo wa anuani za makazi (postal code) ulipoanzishwa TCRA ilitoa tangazo kuwakaribisha wakazi kupeleka majina ya kupewa mitaa yao, tatizo la mitaa msingi kuendelea kutokuwa na majina ambalo pia linakwamisha mambo mengi kama Uber kushindwa kuingia mitaani ni watanzania kutokuwa wafuatiliaji wa taarifa na matangazo.
Nakushauri kama mtaa wako hauna jina nenda TCRA kawape jina unalopendekeza, hata la babu yako mzaa bibi mzaa shangazi.
 
Kila mtu apambane anavyojua mwenyewe.
Kama
Magonjwa yapo kibao.kwanini Corona ndo.tumpe lawama magufuli?.
huu NI ugonjwa Kama magonjwa mengine usingoje uambiwe na rais ufanye nini.
Unatakiwa ujiongeze mwenyewe

Unaweza kujadili hoja na si kunyooshea vidole mtu?
Nani kakwambia hii inamhusu yeye binafsi?
Unaijua nguvu ya kutokuwa na kauli thabiti kwa jambo lolote kweye jamii hata kama wewe si kiongozi wa juu.
 
Hiyo kauli itatuharibia uchumi kwa sasa tuko kwenye right track hauitaji Rais aje akwambie majukumu yako ya kuchukua tahadhari we kaa kizembe ikukule kichwa ukisubili kauli ya Rais au nasema uongo ndugu zanguuuuu mitano tena
Tatizo watu wakivaa barakoa viongozi wa serikali wanazuia, rejea kilichotokea moshi
 
nyumonia kali eee - tuendelee tu kuficha maradhi !!!
 
Kila mtu apambane anavyojua mwenyewe.
Kama
Magonjwa yapo kibao.kwanini Corona ndo.tumpe lawama magufuli?.
huu NI ugonjwa Kama magonjwa mengine usingoje uambiwe na rais ufanye nini.
Unatakiwa ujiongeze mwenyewe

Unaweza sema vyovyote, lakini sina uhakika kama unajua thamani ya magonjwa ya mlipuko hata kama yana dawa au hayana dawa. Ni masuala yanayohitaji umakini na si kauli nyepesi kama hizi zako.
 
Inamaana mungu kashindwa situliaminishwa ktk maombi?

Wewe unaonaje?

Ulishawahi fikiria siku yako ikifika kama wewe binafsi unaweza ku negotiate na kumshawishi Mungu ili asikuchukue?

Imani zetu wengine zinatuambia tujifunze kuomba kwa imani kwa tunachota tutapewa, na ikitokea hatujapewa hicho basi tumshukuru Mungu kwa kila jambo
 
Muuza magari maarufu jijini Dar es Salaam, Akachube afariki dunia usiku wa kuamkia leo.

Ndugu wa karibu wamesema amefariki kwa ugonjwa wa Nimonia.

Umaarufu wake ulipelekea mpaka kupewa barabara ya Akachube iliyopo Kijitonyama

Mungu ailaze pema peponi roho yake
Duh kumbe huu mtaa ni jina lake...nilikua sijui...mitaa yangu hii daily
Mitaa yako, Mimi nimezaliwa hapo na kukulia hapo mtaa wa mzee jarufu,kwasasa ukijulikana kama Broocklin street na mpaka sasa bado tuna mjengo hapo ingawa watoto tuko maeneo mbalimbali kupambana na maisha. Jamaa alikuwa powa sana. Nakumbuka last time niliposhindana nae pool table baada ya kuniambia nikimfunga ataninunulia mzinga wa konyagi hapo CCM Knyama kiwanja cha nyumbani😊
Huo mzinga ndio ulionifanya niichukie Konyagi. Wakuu Kuna Raha sana kunywa viwanja vya nyumbani ambapo kila mtu anakufahamu. Mdogo wangu Imu (Akachube's son) pole sana
Rest in peace bro
 
Mitaa yako, Mimi ndio nimezaliwa hapo na kukulia hapo na mpaka sasa bado tuna mjengo hapo ingawa watoto tuko maeneo mbalimbali kupambana na changamoto za maisha. Jamaa alikuwa powa sana. Nakumbuka last time niliposhindana nae pool table baada ya kuniambia nikimfunga ataninunulia mzinga wa konyagi hapo CCM Knyama kiwanja cha nyumbani😊
Huo mzinga ndio ulionifanya niichukie Konyagi. Wakuu Kuna Raha sana kunywa viwanja vya nyumbani ambapo kila mtu anakufahamu.
Rest in peace bro
Pole kwa kupoteza rafiki jirani
 
Kila mtu apambane anavyojua mwenyewe.
Kama
Magonjwa yapo kibao.kwanini Corona ndo.tumpe lawama magufuli?.
huu NI ugonjwa Kama magonjwa mengine usingoje uambiwe na rais ufanye nini.
Unatakiwa ujiongeze mwenyewe
Ni kiherehere chake tu,mbona kipindupindu kipo,malaria ipo,ukimwi upo,sukari ipo,kansa ipo,lakini asihusishwe navyo? Mtu huyu anahukumiwa kwa maneno yake!! Si kwa ukimya wake,anasema hakuna corona tanzania,na anajua kabisa kuwa kuna wajinga wengi sana tanzania ambao wataweza kumwamini na kuishi kama vile kweli hakuna corona,matokeo yake ni kuwa wataambukizwa na kuwaambukiza wengine,ni kama vile anavyosemaga kuwa tanzania ni nchi tajiri sana wakati tulishafundishwa kuwa tanzania ni nchi masikini na tukaridhika na kuishi kama masikini,sasa anavyotuambia kuwa sisi ni matajiri huku matumbo yana njaa na nguo zina viraka hapo ndiyo anatuamsha usingizini tuanze kudai mgao wa utajiri wa nchi yetu,ambao kiukweli wanasiasa ndiyo wanaougawana, mtu kama magufuli aliyekaa kwenye madaraka kwa zaidi ya miaka 25 akituita matajiri tunajua tu anatudhihaki,akisema hakuna corona ni kama anatutukana kwa kutuona hatuna akili na mwenye akili ni mmoja tu ambaye ndiye yeye
 
Umakini upi unaoutaka wewe?.
Ina maana nchi nyingine wanaokufa na Corona hawana huo UMAKINI?
Unaweza sema vyovyote, lakini sina uhakika kama unajua thamani ya magonjwa ya mlipuko hata kama yana dawa au hayana dawa. Ni masuala yanayohitaji umakini na si kauli nyepesi kama hizi zako.
 
Back
Top Bottom