Sakata la BANDARI ZETU na DPW linataka kuliingiza Taifa kwenye umwagaji wa damu!?


Ndugu yangu umeona mbali.
Itafika mahali watu watajitoa ufahamu.
 
Nimekumbuka tuliambiwa hata tule nyasi ila ndege ya Rais itanunuliwa tuu

Wakaja na vijisenti hela za mboga nk watu wapo kimyaaa

Haikutosha wakagawa fedha kila mkoa 50m ili kututoa kwenye reli

Nchi yetu hii kila Kona kuna ukakasi fulani
Kwa hili la sasa watu wanataka uwekezaji Ila ulio na maslahi kwa watanganyika si vinginevyo
 


Sent using Jamii Forums mobile app
 
mshana toa account namba utakuwa kibopa sasahivi maana Mbarawa ana fungu kabisa la kuhakikisha wanaopinga wanalainishwa kwa mijihela ,ikishindikana wanakuua maana hawana chakupoteza yeye na dadake hangaya. kuna mtu anajiita balile yaani nimemshangaaa kweli kweli jamaa alikua anajifanya critical sasahivi kalooowaaaaaaa kisa hela, kajamaa kalikua kanajifanya nunda kumbe njaa tu.
 
kuna mtu anajiita balile yaani nimemshangaaa kweli kweli jamaa alikua anajifanya critical sasahivi kalooowaaaaaaa kisa hela, kajamaa kalikua kanajifanya nunda kumbe njaa tu.[emoji419][emoji375]
Nasikia kala dollar 100,000

Sent using Jamii Forums mobile app
 
lazima maana sio kwa povu lile alilokua anatoa yani hata la foma gold haliko vile , uzuri wenye akili walishamshtukia siku nyingiiii umbwa yule
 
Hali ni tete

Hali ni tete lakini Samia anataka kujifanya yeye ni Marie Antonnette wa ufaransa ; wakati watu wanalalamika juu ya mkataba yeye anacheza taarab!! Mfundisheni historia kitu gani kiliwapata Mfalme yule wa Ufaransa na mkewe!!

Huyo Waziri wa mambo ya ndani Masauni naye anayetoka Zanzibar inafaa aache mara moja humo uijnga wa kutoa amri ya kuwashuhulikia waTanaganyika [ kama alivyosema Kingai] wanaopinga huo mkataba kwani ndio anakoleza moto!
 
Shida kubwa zaidi walishatoa na kishika uchumba na kilishapokelewa na kuliwa chote

Sent using Jamii Forums mobile app
Hili ndilo tatizo kubwa na haliongelewi.
Hili linafanya hata D.P World kushindwa kujibu hili sakata.
Imewaachia walichukua 50% wajibu.
Katu hatukubali kutawaliwa na yeyote kisa mikataba feki na njaa za udalali.
 
Mwarabu anaweza kuanza maandalizi ya kuleta silaha za kuua watu weusi wanaopinga kutawaliwa. Tujifunze ya kule Sudan na Darfur
Watu wanajazwa matumaini ya Mapesa Kisha wanauza uhuru wao na taifa lao.

Waarabu na Wazungu SIO Wajinga . Walishajua kuwa Afrika Kuna rasilimali nyingi sana ila hakuna watu wenye akili ya Kuzilinda Wala kutumia. Kwa Karne nyingi wanapora rasilimali za bara la Afrika Kwa kushirikiana na watawala Wala rushwa na wabinafsi na waoga .

Wazungu na Waarabu kamwe hawajawahi kuwapenda WAAFRIKA zaidí ya kutamani rasilimali zetu na kutumia hila kuzipata wakishirikiana na watawala.

Dawa ya Hawa watawala na Chama chao ni kuwatoa madarakani Kwa sanduku la kura 2025 .
CCM na familia zao wamejisahau wanaona hii nchi ni Mali Yao wanafanya wanachotaka.

Kuna Siku watawauzia Waarabu Mlima Kilimanjaro Ili wajenge miundo ya kisasa ya kupanda na kushuka na kutunza mazingira.
Hawa nadhani wanawekaga mikataba ya kuuza nchi WAKIWA wamekeweshwa na pesa au madawa ya kulevya mana haiingii akilini MTU auze bandari iliyotumika kupitisha misaada ya kijeshi kuzikomboa nchi zote za kisini Mwa Afrika .

Kilichotuunganisha na Zanzibar ni woga Wa kuvamiwa na masalia ya Sultani ambao walikua Wana Miliki ukanda Wa Afrika Mashariki tangu Karne ya Kumi na mbili.

Wakoloni hawajawahi kujali damu za watu Wa makoloni Yao zaidí ya rasilimali.

Sadam hakuwahi kukubaliana na Falme za Kiarabu Kwa sababu ni wasaliti walioungana na Marekani.
Gadaf hakukubaliana na Falme za Kiarabu Kwa sababu ni wasaliti walioungana na Wamarekani.
Dubai ni mawakala Wa Wazungu. Pesa zitamwagwa Kila MAHALI na vikundi Vya kihalifu vitazagaa Kila MAHALI ikiwemo ugaidi.
 
Aisee!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…