Sakata la DP WORLD: Rais Samia asema Serikali itatafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar, sasa kuchangia robo tatu ya bajeti ya nchi

Sakata la DP WORLD: Rais Samia asema Serikali itatafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar, sasa kuchangia robo tatu ya bajeti ya nchi

Siyo atakuwa ameshapatikana..

Alishapatikana wiki 2 zilizopita Rais alipokwenda ziara Dubai..

Mwekezaji huyo anaitwa DP WORLD
Upo sahihi mkuu Raisi alikutana na wakurugenzi wa DP World alipokuwa ziarani Dubai.

Hili suala la ubia tayari tunalo ambapo yupo na TICTS ambao wamepewa gati namba 7-11 wanahudumia meli za containers na Hawa wapo chini ya Hutchinson Holding ya Hong Kong China.

Miaka 2 nyuma Kipindi Cha Mh. Dr Magufuli kulikuwa na tetesi za kuwa mkataba wa TICTS ukiisha ilikuwa hakuna kuongeza na angeleta vifaa huko kurudi serikalini.

Nchi nyingi wamewapa Wabia Port Operators bandari zao Kwa mikataba tofauti, Msumbiji na Somalia wamewapa DP world.

Hii hapa ni list ya port Operators wakubwa Duniani
Tayari sisi tunae Hutchinson Holding (TICTS).Bandari nzima asipewe mbia apewe gati hizo hizo za container hizo nyingine TPA iongeze maboresho kwenye vifaa vya kisasa na technology mpya.
 
Nimeona Rais akisema Serikali kutafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar es Salaam ili kuleta ufanisi na kuongeza mapato.

Ni kweli tunahitaji mbia wa kuiendesha bandari ya Dar? Sisi wenyewe imeshindikana kabisa?

Tumewahi kufanya hivi kwenye reli, shirika la ndege lakini tunajua kilichotukuta.

Hii haiwezi kuja kuiua hii bandari kwa maana tunajuana vizuri sisi hasa linapokuja suala la maslahi.

--
Rais Samia Suluhu amesema maboresho yanafanyika kwenye Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kupata mbia wa kuiendesha, kubadili uongozi na miundombinu ili kuongeza ufanisi.

Amesema robo tatu ya bajeti ya nchi inaweza kutegemea bandari endapo zitafanya kazi inavyotakiwa.

Waliwang'oa viongozi wabunifu wakawekwa wa kwao wakaanza kutafuna wameshindwa kuwarejesha wa zamani kwa aibu ndio wanaonelea kuja na mawazo ya mbia!!!
 
Tuna watanzania wazalendo wa kutosha kuendesha bandari zetu zote na zikaleta tija. watu type ya Mchechu NHC wapo tuwatumie kwanza kabla ya kuwapa wageni chakula mezani.
 
I absolutely support this. TPA wameshindwa kuendesha hiyo bandari bora watu wengine wajaribu hatuwezi kuendelea kupoteza muda, nguvu na mapato kwa kigezo cha uzalendo. Ikiwezekana hata TRA wapewe wabia maana wabongo tumeshindwa kazi ndo ukweli mchungu.
 
Wewe ukifanya mwenyewe unakusanya Bil 90 lets say kwa mwezi hapo Bandari - Mwekezaji anakuja anakwambia atakusanya Bil 400 afu wewe atakupatia Bil 300. Mkataba wa miaka 10 with uplift ya 5% kila mwaka , je utakataa ama utakubali ?
Tatizo lao huwa wanasema hivyo hivyo, nitakupa Bilioni 300 lakini nifanye maboresho then nipe Grace period ya 5 years kisha naanza kukulipa, baada ya huo muda anakwambia napata hasara tu siendelei na mkataba. . . akili kumkichwa
 
I absolutely support this. TPA wameshindwa kuendesha hiyo bandari bora watu wengine wajaribu hatuwezi kuendelea kupoteza muda, nguvu na mapato kwa kigezo cha uzalendo. Ikiwezekana hata TRA wapewe wabia maana wabongo tumeshindwa kazi ndo ukweli mchungu.
Wapigaji tu
 
Siku hizi bandari zote kubwa duniani zinaendeshwa kibiashara. Kuna makampuni mahsusi yaliobobea kazi hizo.

Kuingia ubia ndio njia sahihi kwa dunia ya leo.

Nnamini bandari ya Dar ilivyokaa vizuri geographically, na nchi landlocked zinavyotuzunguka, bandai ya Dar pekee inaweza kuendesha budjet ya serikali kwa Tanzania nzima.

Nchi kama Singapore na Dubai hazina zinachojivunia zaidi ya badari zao nandio vyanzo vyao vyote vya mapato vinatokea hapo. Kwanini sisi tusindwe? Wizi mtupu banadarini Dar. Wizi wa Bandarini ni kansa iliyopo kila idara (each and every department).

Kama yalivyokufa mashirika yote umma na badari haipo salama tukiedelea kuiedesha wenyewe. Apewe tajiri mmoja aiendeshe tujionee mabadiliko.

Wala haina haja ya kuwa rocket science kuelewa kuwa bandari kwa Tanzania ina faida kubwa sana ikiendeshwa ipasavyo. Mfano mzuri ni Bagamoyo, nchi na wafanya biashara matajiri wa nje wapo tayari kuingiza na kuwekeza pesa kibao kujenga banadari na mji mpya kabisa wa kisasa, ili waingie ubia wakuiendesha bandari tu. Watafanya hivyo kama hawajaiona faida kwenye upembuzi wao?

Mama hata polisi ingia ubia iendeshwe professionally, maana imeshindwa kabisa kulinda mali za Watanzania na badala yake wanaua raia kwa thamani ndogo tu.
Faiza nakuelewa vizuri sana. Ubarikiwe. Hata Polisi waingie ubia na mashirika mahili ya ulinzi.
 
Siku hizi bandari zote kubwa duniani zinaendeshwa kibiashara. Kuna makampuni mahsusi yaliobobea kazi hizo.

Kuingia ubia ndio njia sahihi kwa dunia ya leo.

Nnamini bandari ya Dar ilivyokaa vizuri geographically, na nchi landlocked zinavyotuzunguka, bandai ya Dar pekee inaweza kuendesha budjet ya serikali kwa Tanzania nzima.

Nchi kama Singapore na Dubai hazina zinachojivunia zaidi ya badari zao nandio vyanzo vyao vyote vya mapato vinatokea hapo. Kwanini sisi tusindwe? Wizi mtupu banadarini Dar. Wizi wa Bandarini ni kansa iliyopo kila idara (each and every department).

Kama yalivyokufa mashirika yote umma na badari haipo salama tukiedelea kuiedesha wenyewe. Apewe tajiri mmoja aiendeshe tujionee mabadiliko.

Wala haina haja ya kuwa rocket science kuelewa kuwa bandari kwa Tanzania ina faida kubwa sana ikiendeshwa ipasavyo. Mfano mzuri ni Bagamoyo, nchi na wafanya biashara matajiri wa nje wapo tayari kuingiza na kuwekeza pesa kibao kujenga banadari na mji mpya kabisa wa kisasa, ili waingie ubia wakuiendesha bandari tu. Watafanya hivyo kama hawajaiona faida kwenye upembuzi wao?

Mama hata polisi ingia ubia iendeshwe professionally, maana imeshindwa kabisa kulinda mali za Watanzania na badala yake wanaua raia kwa thamani ndogo tu.
Mtuonee huruma jamani khaa!
 
Mkuu Hilo kwa Tanzania hii limewahi kutokea shirika gani?
Mwinyi aiwahi kutafuta mwekezaji wa Kilimanjaro hotel kwa story Kama hizo, mwishowe unajua kilichotokea.

Mkapa nae akaja kubinafsisha mashirika kwa story Kama hizo unazosema, TTCL, Tanesco, Reli zinapotea

JK nae akaja na story hizohizo kwenye Reli na ATCL mwisho wote unajua ilikuaje.

Hakuna shirika hapa bongo liliwahi kutafutiwa mbia likafanya vizuri, yote yalifilisika na mengine kufa kabisa
Wamekuwa kama mamba hasikii mpaka damu zimtoke...Hakuna hata kimoja chakuonyesha kilifanikiwa kwa mawazo haya mufislisi lakini bado wanataka tu kutuaminisha...Watu wasiojiamini wala kuwa na uthubutu kwa jambo lolote!
 
Nimeona Rais akisema Serikali kutafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar es Salaam ili kuleta ufanisi na kuongeza mapato.

Ni kweli tunahitaji mbia wa kuiendesha bandari ya Dar? Sisi wenyewe imeshindikana kabisa?

Tumewahi kufanya hivi kwenye reli, shirika la ndege lakini tunajua kilichotukuta.

Hii haiwezi kuja kuiua hii bandari kwa maana tunajuana vizuri sisi hasa linapokuja suala la maslahi.

--
Rais Samia Suluhu amesema maboresho yanafanyika kwenye Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kupata mbia wa kuiendesha, kubadili uongozi na miundombinu ili kuongeza ufanisi.

Amesema robo tatu ya bajeti ya nchi inaweza kutegemea bandari endapo zitafanya kazi inavyotakiwa.

Haya mawazo ya ovyo ni ya wapigaji tu. Yaani una bandari na kuna mataifa mengine yanatumia ushindwe kuendesha hadi unatafuta ubia? Isitoshe mwenyewe ushagharamika kupanua kwa mabilioni. Haya mawazo ya ovyo kabisa.
Wajinga kama kina madilu nape na makamba ndio watakuja na mawazo kama hayo. Safari za nje za kijinga kwenda kuwafuata eti consultants. Unafikiri washauri wamarekani au waingereza au wengine wowote ukiwauliza siwatawauzia bandari kampuni za kigeni?
Linalotakiwa ni usimamizi mathubuti wa serikali. Rais akiwasikiliza wahuni tutaweka wabia hadi kuendesha jeshi polisi na magereza. Hapo tutakua huru kweli?
 
Eehh kweli kabisa, tukapeleka na Airport ya Kimataifa Chato, sasa wanatua mbayuwayu tu. Tukawaibia na majumba na magari yao matajiri. Tukawatolea bastola kuwatisha mawaziri hadharani waliposema ukweli. Tukafumua utawala wa bandari na kuweka "The" gang ndiyo waiendeshe. Usiyasahau yote hayo.
Hii chuki itakufanya ukose mbingu, angalia dada yangu...Nilikuwa nakuamini sana enzi hizo kwa balanced opinion; haya ya siku hizi daah!
 
Haya mawazo ya ovyo ni ya wapigaji tu. Yaani una bandari na kuna mataifa mengine yanatumia ushindwe kuendesha hadi unatafuta ubia? Isitoshe mwenyewe ushagharamika kupanua kwa mabilioni. Haya mawazo ya ovyo kabisa.
Wajinga kama kina madilu nape na makamba ndio watakuja na mawazo kama hayo. Safari za nje za kijinga kwenda kuwafuata eti consultants. Unafikiri washauri wamarekani au waingereza au wengine wowote ukiwauliza siwatawauzia bandari kampuni za kigeni?
Linalotakiwa ni usimamizi mathubuti wa serikali. Rais akiwasikiliza wahuni tutaweka wabia hadi kuendesha jeshi polisi na magereza. Hapo tutakua huru kweli?

It is not a bad thing to look for a partner or a concessionaire to invest and run the Port.

In 1996, I was in the USA, and witnessed the Port of New York looking for a company to manage it. Do you know who won the tender? It was the Port of Dubai.

However, the US Govt later changed its mind and said it was going to repeat the exercise.
 
Lete usha

Lete ushaidi wa uliloandika kama huna chuki binafsi .mwanzo kama nilianza kukuelewa lkn hapa si sawa.changamoto za uendeshaji wa bandari TPA inashindwa kutokana na vitu kadha wa kadha
gharama za ukarabati
tekinologia ya kisasa
ushindani uliopo kwenye bandar za Africa n.k
ebu lete nn kifanyike sio kama unaleta chuki binafsi
Sijakuelewa nilete ushahidi wa nini?
 
Nimeona Rais akisema Serikali kutafuta mbia wa kuiendesha bandari ya Dar es Salaam ili kuleta ufanisi na kuongeza mapato.

Ni kweli tunahitaji mbia wa kuiendesha bandari ya Dar? Sisi wenyewe imeshindikana kabisa?

Tumewahi kufanya hivi kwenye reli, shirika la ndege lakini tunajua kilichotukuta.

Hii haiwezi kuja kuiua hii bandari kwa maana tunajuana vizuri sisi hasa linapokuja suala la maslahi.

--
Rais Samia Suluhu amesema maboresho yanafanyika kwenye Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kupata mbia wa kuiendesha, kubadili uongozi na miundombinu ili kuongeza ufanisi.

Amesema robo tatu ya bajeti ya nchi inaweza kutegemea bandari endapo zitafanya kazi inavyotakiwa.

Hatari sana ! bandari ya Zanzibar nayo atapeleka Mbia ?
 
Back
Top Bottom