Sakata la Kocha: Singida tumechagua kukaa kimya, tuna kazi kubwa mbele yetu

Sakata la Kocha: Singida tumechagua kukaa kimya, tuna kazi kubwa mbele yetu

Hussein Massanza

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
1,016
Reaction score
2,195
Salaam,

Nimeona mijadala mingi humu ikizungumzia sakata la kocha wetu ambaye amenukuliwa na vyombo vya habari nchini Afrika Kusini kuhusu sababu za yeye kuondoka kambini.

Kwa upande wa klabu bado hatujasema chochote, taarifa yetu ya awali tulitoa kuhusiana na yeye kuondoka kambini kwa sababu zake binafsi. Ni kweli aliondoka bila kueleza sababu kwahiyo kwetu bado tunaziona ni sababu binafsi.

Maswali machache yakinifu ya kujiuliza;

1. Je, kwanini ndani ya muda mfupi baada ya kuondoka kambini akakimbilia kujieleza kwenye vyombo vya habari? Lengo ni nini?

2. Je, ana uthibitisho wowote wa tuhuma alizozitoa? Ni kipi kinathibitisha kuwa aliyoyasema yote ni ya ukweli?

3. Amekiri hakupangiwa kikosi kabla na wakati wa mechi, kwanini alalamike kupangiwa kikosi? Kipi?

4. Madai ya kupangiwa kikosi yanachekesha: Amecheza mechi moja tu na kikosi si alipanga mwenyewe, aliingiliwa wapi?

5. Kama ni kweli aliitwa kikaoni na waajiri wake kuhojiwa, kwanini asitoe majibu ya kiufundi yeye akiwa kama mtaalamu?

6. Anasema ameutaarifu uongozi kuwa ameacha kazi, kwanini anakuwa mgumu kuandika barua rasmi kama anaamini ana sababu za msingi?

Kimsingi Sisi bado tunasubiri barua yake ya kuacha kazi au kujieleza kwanini hayupo kambini. Mambo ya utoro kazini hatutaki. Kama amepata kazi sehemu nyingine aseme, sio kwenda kutuchafua kwenye vyombo vya habari kutafuta visingizio. Kwa sasa tumechagua kakaa kimya, tuna mechi ngumu na Future FC Oktoba Mosi kule Misri. Autumie muda huu vizuri kujitafakari na kufanya maamuzi kwa kufuata utaratibu rasmi.

Pakiwa na jambo lolote klabu itatoa taarifa rasmi!
 
Ok, Nani ni mmiliki wa timu? Maana tunasikia maneno kuwa kocha aliwekwa mtu kati na Watu wazito. Hebu fafanua kidogo ndugu Massanza maana ndio majukumu yako haya kutupasha habari na kujibu maswali mbalimbali

Mmiliki wa timu anafahamika ni Japhet Makau, Mkurugenzi wa Fountain Gate. Ndio sababu hata timu imebadili umiliki wa jina na kuitwa Singida Fountain Gate. Kumtaja mtu mwingine ni katika kutafuta attention tu nadhani ndio sababu akakimbilia kwenye vyombo vya habari. He is not stupid!
 
Ok, Nani ni mmiliki wa timu? Maana tunasikia maneno kuwa kocha aliwekwa mtu kati na Watu wazito. Hebu fafanua kidogo ndugu Massanza maana ndio majukumu yako haya kutupasha habari na kujibu maswali mbalimbali
singida fg inamilikiwa na mwanachama wa yanga mwigulu nchemba, huyu ndio anaepanga kikosi cha timu
 
Mmiliki wa timu anafahamika ni Japhet Makau, Mkurugenzi wa Fountain Gate. Ndio sababu hata timu imebadili umiliki wa jina na kuitwa Singida Fountain Gate. Kumtaja mtu mwingine ni katika kutafuta attention tu nadhani ndio sababu akakimbilia kwenye vyombo vya habari. He is not stupid!
Acha uongo huyo makau ameinunua singida kwa tsh ngapi? Hana hela ya kununua , mmiliki ni mwigulu
 
Salaam,

Nimeona mijadala mingi humu ikizungumzia sakata la kocha wetu ambaye amenukuliwa na vyombo vya habari nchini Afrika Kusini kuhusu sababu za yeye kuondoka kambini.

Kwa upande wa klabu bado hatujasema chochote, taarifa yetu ya awali tulitoa kuhusiana na yeye kuondoka kambini kwa sababu zake binafsi. Ni kweli aliondoka bila kueleza sababu kwahiyo kwetu bado tunaziona ni sababu binafsi.

Maswali machache yakinifu ya kujiuliza;

1. Je, kwanini ndani ya muda mfupi baada ya kuondoka kambini akakimbilia kujieleza kwenye vyombo vya habari? Lengo ni nini?

2. Je, ana uthibitisho wowote wa tuhuma alizozitoa? Ni kipi kinathibitisha kuwa aliyoyasema yote ni ya ukweli?

3. Amekiri hakupangiwa kikosi kabla na wakati wa mechi, kwanini alalamike kupangiwa kikosi? Kipi?

4. Madai ya kupangiwa kikosi yanachekesha: Amecheza mechi moja tu na kikosi si alipanga mwenyewe, aliingiliwa wapi?

5. Kama ni kweli aliitwa kikaoni na waajiri wake kuhojiwa, kwanini asitoe majibu ya kiufundi yeye akiwa kama mtaalamu?

6. Anasema ameutaarifu uongozi kuwa ameacha kazi, kwanini anakuwa mgumu kuandika barua rasmi kama anaamini ana sababu za msingi?

Kimsingi Sisi bado tunasubiri barua yake ya kuacha kazi au kujieleza kwanini hayupo kambini. Mambo ya utoro kazini hatutaki. Kama amepata kazi sehemu nyingine aseme, sio kwenda kutuchafua kwenye vyombo vya habari kutafuta visingizio. Kwa sasa tumechagua kakaa kimya, tuna mechi ngumu na Future FC Oktoba Mosi kule Misri. Autumie muda huu vizuri kujitafakari na kufanya maamuzi kwa kufuata utaratibu rasmi.

Pakiwa na jambo lolote klabu itatoa taarifa rasmi!
Nafurahi kusikia hili kutoka kwako mseamji wetu .
Hakika jambo liliniumiza sana na jana Azam wakashindilia maumivu zaidi ila muda utaongea najua tutarudi tukiwa imara zaidi.

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Je wewe ndio msemaji rasmi wa Singida Fountain Gate?
 
Mmiliki wa timu anafahamika ni Japhet Makau, Mkurugenzi wa Fountain Gate. Ndio sababu hata timu imebadili umiliki wa jina na kuitwa Singida Fountain Gate. Kumtaja mtu mwingine ni katika kutafuta attention tu nadhani ndio sababu akakimbilia kwenye vyombo vya habari. He is not stupid!
Umeeleweka, tumeshukuru wewe kutumia jukwaa hili.... !

Jambo moja ni Ombi kwa kuwa mvumilivu,humu wapo watu Wenye akili tofauti tofauti.
Sasa kuna Vichwa vikichemka vinatoa maneno utadhani kwenye fuvu hakuna Ubongo.! Uvumilie ,ugangamale kweli kweli.
Na Usipotee ndugu yetu massage.!
 
Umeeleweka, tumeshukuru wewe kutumia jukwaa hili.... !

Jambo moja ni Ombi kwa kuwa mvumilivu,humu wapo watu Wenye akili tofauti tofauti.
Sasa kuna Vichwa vikichemka vinatoa maneno utadhani kwenye fuvu hakuna Ubongo.! Uvumilie ,ugangamale kweli kweli.
Na Usipotee ndugu yetu massage.!
Mimi mkongwe humu 😃
 
1. Kaenda kujieleza ili kuondoa upotoshaji uliotolewa kuwa ameenda kutatua matatizo ya kifamilia sababu uliyoitoa wewe wakati si kweli meidndrop hana matatizo ya kifamilia. Unadhani huyo ni kocha wa ndondo mpaka aache kazi atatue matatizo ya kifamilia.

2.Jamaa hajatoa tuhuma zozote zile zaidi ya kueleza ukweli wa mambo kwanini within 2 weeks ameamua kuachana na timu ambazo kaeleza kabisa sababu wewe unaziita tuhuma.

3.Amelalamika kuingiliwa majukumu yake ya ukocha kwa kuulizwa kwanini kagoma na chukwu hawajaanza match na kwanini gadiel kacheza DCM wakati ni beki akaona hapo mbele wanapoelekea watamwambia huyu acheze na huyu asicheze kitu ambacho kwa taaluma yake as profesional coach hawezi kukubali ni bora aondoke na ndicho alichofanya .

4. Wewe ndo unakuja kuchekesha humu ndani unadhani wote wana iramba kila analosema mwigulu tunaitikiaa ndio sio?. Aliingiliwa pale ambapo paliitishwa kikao akajua ni kikao cha pongezi kumbe anaenda kuulizwa kwanini kamchezesha Gadiel na si chukwu na kwanini kawaacha kina kagoma nje , ikabidi ashangaee wakina mwingulu na wengine hawapo mazoezini lakini bado wanalazimisha kupanga timu akaona hawa maboya vipi wanadhani wapo kwenye kikao cha chama hapa[emoji23]

5.Unaposema kama ni kweli aliitwa kwenye kikao unamaanisha kwamba meidndrop amedanganya kuwa kulikua hamna kikao. Sababu kazitoa yeye ndiyo kocha na muda wote anakuwa na wachezaji mazoezini na as a coach anajua how to approach the game na ndicho alichokifanya.

6. Hana haja ya kuandika barua mbona ameshajibu hilo kwenye interview aliyofanya amesema aliwaambia palepale kwenye kikao anaacha kazi na sababu ni kuingiliwa majukumu yake kama kocha na issue sio hela .
Sasa unakuja wewe pupet wa mwigulu unayepewa laki 2 na vi memo upeleke huku na kule unataka tukuamini wewe kuliko kocha ambaye alikuwa anachukua mpunga mrefu lakini amejali taaluma yake kuliko fedha , unataka tukuamini wewe kijana wa mwigulu .

7. Unaulizwa timu ni ya nan unakuja kutuletea uongo uongo na unatafuta kuaminiwa wakati meidndrop amekaa wiki 2 na anaeleza kabisa alivyopigiwa simu na kuongea na waziri wa fedha ambaye ndo real owner wa hio timu . Tatizo mmliki wa team ni specialist in failure alianza na sgd utd akafeli na sasa hii singida sijui big star sijuii fountain gate ni swala la muda tu itafeli .

Mwambie ajikite na kuitafuta dollar na si kugombania kupanga kikosi na kocha .
 
Back
Top Bottom