OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 53,868
- 121,001
Siasa hizo hizo ndio zimempa pesa bosi wako, anapiga hela kupitia siasaWewe ushaharibika na porojo za siasa. Nakusamehe bure.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Siasa hizo hizo ndio zimempa pesa bosi wako, anapiga hela kupitia siasaWewe ushaharibika na porojo za siasa. Nakusamehe bure.
hii timu inatumia tozo za watanzania wanyonge, tunaomba mfungwe na mtolewe na hao future wasengerema nyieeee.Hapo hakuna jibu hata moja. Tumechagua kukaa kimya!
umamaliza kila kitu mkuu, with due respect.1. Kaenda kujieleza ili kuondoa upotoshaji uliotolewa kuwa ameenda kutatua matatizo ya kifamilia sababu uliyoitoa wewe wakati si kweli meidndrop hana matatizo ya kifamilia. Unadhani huyo ni kocha wa ndondo mpaka aache kazi atatue matatizo ya kifamilia.
2.Jamaa hajatoa tuhuma zozote zile zaidi ya kueleza ukweli wa mambo kwanini within 2 weeks ameamua kuachana na timu ambazo kaeleza kabisa sababu wewe unaziita tuhuma.
3.Amelalamika kuingiliwa majukumu yake ya ukocha kwa kuulizwa kwanini kagoma na chukwu hawajaanza match na kwanini gadiel kacheza DCM wakati ni beki akaona hapo mbele wanapoelekea watamwambia huyu acheze na huyu asicheze kitu ambacho kwa taaluma yake as profesional coach hawezi kukubali ni bora aondoke na ndicho alichofanya .
4. Wewe ndo unakuja kuchekesha humu ndani unadhani wote wana iramba kila analosema mwigulu tunaitikiaa ndio sio?. Aliingiliwa pale ambapo paliitishwa kikao akajua ni kikao cha pongezi kumbe anaenda kuulizwa kwanini kamchezesha Gadiel na si chukwu na kwanini kawaacha kina kagoma nje , ikabidi ashangaee wakina mwingulu na wengine hawapo mazoezini lakini bado wanalazimisha kupanga timu akaona hawa maboya vipi wanadhani wapo kwenye kikao cha chama hapa[emoji23]
5.Unaposema kama ni kweli aliitwa kwenye kikao unamaanisha kwamba meidndrop amedanganya kuwa kulikua hamna kikao. Sababu kazitoa yeye ndiyo kocha na muda wote anakuwa na wachezaji mazoezini na as a coach anajua how to approach the game na ndicho alichokifanya.
6. Hana haja ya kuandika barua mbona ameshajibu hilo kwenye interview aliyofanya amesema aliwaambia palepale kwenye kikao anaacha kazi na sababu ni kuingiliwa majukumu yake kama kocha na issue sio hela .
Sasa unakuja wewe pupet wa mwigulu unayepewa laki 2 na vi memo upeleke huku na kule unataka tukuamini wewe kuliko kocha ambaye alikuwa anachukua mpunga mrefu lakini amejali taaluma yake kuliko fedha , unataka tukuamini wewe kijana wa mwigulu .
7. Unaulizwa timu ni ya nan unakuja kutuletea uongo uongo na unatafuta kuaminiwa wakati meidndrop amekaa wiki 2 na anaeleza kabisa alivyopigiwa simu na kuongea na waziri wa fedha ambaye ndo real owner wa hio timu . Tatizo mmliki wa team ni specialist in failure alianza na sgd utd akafeli na sasa hii singida sijui big star sijuii fountain gate ni swala la muda tu itafeli .
Mwambie ajikite na kuitafuta dollar na si kugombania kupanga kikosi na kocha .