Tetesi: Sakata la Makonda, Clouds na Nape kutua Bungeni na kupotelea huko

Tetesi: Sakata la Makonda, Clouds na Nape kutua Bungeni na kupotelea huko

apolycaripto

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2011
Posts
644
Reaction score
225
Vyanzo vinadai kuwa kulipeleka swala hili mahakamani, litanyima fursa ya Bunge kulizungumzia. Binafsi sitegemei jipya kupitia Bunge hili na kama ikitokea basi utakuwa muujiza wa kwanza wa Bunge letu katika Serikali hii "tata". Hoja ya "collective responsibility" ni changamoto katika mhimili huu mzito kuliko yote (Sauti ya Wananchi yenye Mamlaka kamili) kutokana na maslahi ya kivyama na hofu.

Nashauri mjadala huu ufungwe ama wenyekuhitaji kupata haki ama maamuzi sahihi yasiyo na shaka basi angalau waelekee kwenye mhimili wa "Mahakama"....kwa hoja kuu tatu:-

1. Kufungua shauri linalomtaka Makonda kuwasilisha vyeti vyake vya elimu hasa kidato cha nne (Wanasheria wapo na wanaweza kusaidia)

2. Clouds kumfungulia kesi ya jinai Ndugu Makonda kwa kuvamia kituo cha habari (Hili linahusu kituo cha habari chenyewe hasa katika wakati huu ambao Jamhuri inaona si kosa)

3. Nape kufungua shauri juu ya kutishiwa maisha na Askari kanzu (Hili lina muhusu Nape hasa ukizingatia mazingira ya Jamhuri kutokuona kama ni kosa)

Ndugu wanabodi, pamoja na madhaifu makubwa ya katiba yetu, bado katiba hii ya mwaka 1977 haijanyima haki kwa Wananchi wake. Bunge lina mamlaka kamili lakini aliwezi kutekeleza majukumu yake kikamilifu kutokana na sababu nilizozieleza hapo juu. Mahakama kama chombo chakutoa haki, bado kina fursa ya kutafsiri sheria, kukutanisha pande zote mbili ama kuchukua hatua (kutoa hukumu ama kuachia huru).

Wito wangu: " Kwa Bunge hili tulilonalo, Mahakama ni bora zaidi"
 
Je kuna uhakika gani kama alivamia au alikwenda? Clouds wenyewe wanasema Makonda pale palikuwa kama kwake alikuwa anaweza kuja au kukaa mpaka saa 9 usiku je ni uharibifu gani umefanyika Clouds wanasema hakuna sasa utasemaje hapo?

Kwanza nipe tafasiri ya kuvamia na kutembelea kuhusu kutembea na Police wenye silaha hyo ni kawaida yule ni kiongozi na kuna OPS anaweza kuzifanya usiku usiku
 
Umenifumbua macho sasa kwanini kumbe hata suala la daudi bashite watu hawajaenda mahakamani sababu ni moja tu kuwa wakienda mahakamani watashindwa lizungumzia vizuri saw sawa ngoja tuone
 
Blackmail zote za makonda kumbe huwa anatumwa na Msukuma mwenzake hata GSM sasa wanapewa Tenda kimya kimya wapate pesa za kulea nyumba ndogo za msukuma mkubwa na msukuma mdogo, zile ndege zilizonunuliwa kwa cash GSM walipata 10% kubwa na kuna tenda kibao za kimya kimya ipo pesa nyingi ya kuwanunua wabunge wa CCM pia Ruge wa clouds ili wasitoe ushirikiano kwenye Dhambi zote zilizotendwa na Daudi Albert Bashite, ni vigumu bungeni hoja kupenya hasa endapo Tulia Naibu Spika atakuwa mjengoni, njia pekee ya kumaliza Tatizo ni kwenda Pemba watafutwe wazee wamsomee Elbadili Daud ingawa na mchawi sana lakini kwa kuwa dhambi zake ni za kweli lazima Elibadili itamshika tu na kumpa fundisho kama yule makamu wa Rais kule Zanzibar
 
kama ushahidi ungekuwepo, tungeshauwona au ungekuwa umewasilisha kwenye vyombo husika. Watu wana clock mileage na hizi issue, watu wanataka kuvuna umaarufu kwa vitu visivyo na tija kwa taifa hili.
 
Umenifumbua macho sasa kwanini kumbe hata suala la daudi bashite watu hawajaenda mahakamani sababu ni moja tu kuwa wakienda mahakamani watashindwa lizungumzia vizuri saw sawa ngoja tuone
DPP kapewa mkwara kuwa kesi zote za Daud Bashite zikipelekwa mahakamani lazima ashinde na endapo mlalamikaji atashinda kesi dhidi ya Daud atambue kuwa jaji mkuu na DPP watatumbuliwa Jipu
 
kama ushahidi ungekuwepo, tungeshauwona au ungekuwa umewasilisha kwenye vyombo husika. Watu wana clock mileage na hizi issue, watu wanataka kuvuna umaarufu kwa vitu visivyo na tija kwa taifa hili.
Chanzo cha yote ni blackmail za makonda Daudi kama kuna wa kulaumiwa ni hiyo ndoa ya wasukuma wawili wanaowabambikia watu kesi na kutumana kwenda clouds kufanya fujo kisha wanataka ushahidi, cctv zipo, walioporwa magari wapo, waliobambikiwa kesi wapo, na ushahidi wa mali zote za Daud upo, lakini kwa kuwa amefunga ndoa na msukuma mkubwa ni vigumu haki kutendeka popote Tanzania.
 
Wakitaka hili swala lifanikiwe, wahakikishe ule mchepuko wa pale bungeni aidha wamweke kitandani au wamtengezee zengwe asiwepo wakati hii hoja ikiwa inaongelewa mjengoni.... Nje ya hapo hakutakuwa na jipya
 
Mungu mbariki mkuu wa mkoa mh Paul makonda
hiyo baraka inamwendea mwenye jina hilo lakini Daud Albert bashite yupo kama unataka kumtakia heri muombee kwa jina lake hilo usiliombee jina bandia, pia kunbuka kuwa Mungu hapendi tabia za wivu, kukomoa watu kuwabambikia kesi, Udikteta na unyanyasaji.
 
Wakitaka hili swala lifanikiwe, wahakikishe ule mchepuko wa pale bungeni aidha wamweke kitandani au wamtengezee zengwe asiwepo wakati hii hoja ikiwa inaongelewa mjengoni.... Nje ya hapo hakutakuwa na jipya
Yule watamwendea Uganda wakapate mbinu za kuwatuliza watu wenye Tabia mbovu za kulea maovu.
 
Je kuna uhakika gani kama alivamia au alikwenda? Clouds wenyewe wanasema Makonda pale palikuwa kama kwake alikuwa anaweza kuja au kukaa mpaka saa 9 usiku je ni uharibifu gani umefanyika Clouds wanasema hakuna sasa utasemaje hapo?

Kwanza nipe tafasiri ya kuvamia na kutembelea kuhusu kutembea na Police wenye silaha hyo ni kawaida yule ni kiongozi na kuna OPS anaweza kuzifanya usiku usiku
Kimtazamo wa kwenda au kuvamia, kama alikwenda tu, ni kwa nini alitishia kuwafunga vijana bila kupitia mahakamani?, na ni kwa nini alifyonza ile video clip na kuondoka na flash yenye content za mahojiano? Huo ni mtazamo tu!
 
Kesi dhidi ya Daud kungekuwa na uwezekano ingefunguliwa mahakama za kimataifa huko haki ingetendeka lakini huku Tanzania ukimfungulia kesi Daud utakuwa unapoteza mda na pesa bure kwani DPP kwanza atahujumu upande wa walalamikaji hata jaji lazima atoe hukumu ya kushangaza lakini ya kuwafurahisha wakoloni wapya toka chato na koromije.
 
Kimtazamo wa kwenda au kuvamia, kama alikwenda tu, ni kwa nini alitishia kuwafunga vijana bila kupitia mahakamani?, na ni kwa nini alifyonza ile video clip na kuondoka na flash yenye content za mahojiano? Huo ni mtazamo tu!
Nchi imerejea kwenye Ukoloni kama ule wa 1961 ni wakati wa kupigania uhuru toka kwa wasukuma wawili waliofunga ndoa haramu.
 
kama ushahidi ungekuwepo, tungeshauwona au ungekuwa umewasilisha kwenye vyombo husika. Watu wana clock mileage na hizi issue, watu wanataka kuvuna umaarufu kwa vitu visivyo na tija kwa taifa hili.

Tuongelee CCTV video, ndo ilikuwa movie ya maigizo tu au?
 
Kimtazamo wa kwenda au kuvamia, kama alikwenda tu, ni kwa nini alitishia kuwafunga vijana bila kupitia mahakamani?, na ni kwa nini alifyonza ile video clip na kuondoka na flash yenye content za mahojiano? Huo ni mtazamo tu!
Hakuna ushahidi wa moja kwa moja wa hayo unayosema lakini ushahidi tulioona wote ni kumuona Makonda anaingia kituo cha Clouds tu
 
Au mzee warioba afungue mashitaka ya kuzabuliwa vibao na huyu bashite
 
Unamzungumzia Makonda yupi? Huyu aliyeitwa na bunge akakataa, huyu aliyeitwa mahakamani akakataa, huyu aliyekimbia tume natokeo yake nape akafukuzwa
 
Maisha yanaendelea tu naona negativity strategy ni kila kona sasa,watu wa media nao,watu wa law nao.

But Serikali haiwezi kupangiwa wala kuendeshwa kwa matakwa ya watu wenye nia ovu kwa wanyonge.

Serikali naamini itaendelea kupigania kuhakikisha huduma kwa wanainchi zinakuwa bora zaidi
 
Back
Top Bottom