Salma Kikwete ataka Sheria ya Stahiki za wake wa Viongozi Wakuu

Salma Kikwete ataka Sheria ya Stahiki za wake wa Viongozi Wakuu

Habari!
Hii taarifa imenipata nikaona niilete kama ilivyo.

My Take: Yani wanataka kila kitu serikali iwaandalie yani hadi Future yao kweli?

Mbunge wa Mchinga (CCM), Salma Kikwete ameishauri Serikali kutengeneza utaratibu ama sheria ya kuwahakikishia stahiki zao wake na wenza wa viongozi wa juu, akiwemo Rais, mara baada ya wenzi wao kuchaguliwa kushika nafasi hizo.

Mbunge huyo ambaye ni mke wa Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete ameyasema hayo leo Ijumaa Aprili 22,2022 Bungeni Jijini Dodoma wakati akichangia katika makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora mwaka 2022/2023.

Amesema wake wa viongozi akiwemo rais, makamu wa rais na Waziri Mkuu mara baada ya wenza wao kushika nafasi hizo wanatakiwa kustaafu na kuendelea na shughuli nyingine.

Amesema kitendo hicho kinamaanisha kuwa utaalamu wake unatoweka.

“Ukiwiwa sana unaweza kusema hebu nianzishe Ngo (mashirika yasiyo ya kiserikali) lakini hata ukianzisha hakuna mtu anayeku suport ni wewe mwenyewe uhangaike ili kuhakikisha unapata raslimali ili uweze kuendesha Ngo,”amesema.

Ameomba Serikali kutengeneza utaratibu wa kisheria ambao mke wa kiongozi anapomaliza muda wake ajue ni nini anachotakiwa kukifanya.

“Ni imani yangu mtatengeneza utaratibu ama sheria inayomuhusu mke wa Rais ama wenza nini bada ya hapo kiendelee kufanyika ni jambo muhimu sana na si kwangu bali ni kwa vizazi vijavyo kujua haki zao,”amesema.

Chanzo: MWANANCHI
Du anataka bunge lijadili na kutunga sheria kwa watu kama watano hivi?
Mama Salma anajisahau sana.
Na watu wa jimbo lake wanafaidika vipi?.
Mfadhili mmoja nchini Kenya aliwahi kusema, watu wanakula na kufsidi misaada na hatimaye kuvimbiwa na kutapikia viatu vya wafadhili.
Naona hii ndio picha naiona ya mama Salma.
 
Wanataka sijui wawe wanapewa kiinua mgongo nao?
Kiinua mgongo cha viongozi wastaafu huwa kinajumuisha na familia zao!! It’s assumed their wife’s cater for their families full time!!

Mke wa Kikwete anatakiwa aelimishwe!
Yeye Salma mafao yake yameunganishwa na mafao anayopata mumewe hivyo asitubebeshe Mzigo mwingine; hata hivyo yeye anapata mara mbili hivi sasa kule kwa mumewe na bungeni!! Atosheke na anachopata.
 
Hii Nchi ya ajabu sana yani Kijana Anakaa CHUO miaka 3 au 4 hadi Mi 5 akisoma anatoka pale anaambiwa na SERIKALI aji AJIRI Leo Mke wa Rais amekua na Mme wake 10 Years kwenye position yenye Fursa kibao za kufanya na za kumwingizia Mamilion ya Hela ila anataka Serikali imuandalie Mazingira mazuri ya yeye kama mke baada ya Mme wake kuacha Urais wapewe Posho hii inaingia akilini kweli?🤔
 
Hii Nchi ya ajabu sana yani Kijana Anakaa CHUO miaka 3 au 4 hadi Mi 5 akisoma anatoka pale anaambiwa na SERIKALI aji AJIRI Leo Mke wa Rais amekua na Mme wake 10 Years kwenye position yenye Fursa kibao za kufanya na za kumwingizia Mamilion ya Hela ila anataka Serikali imuandalie Mazingira mazuri ya yeye kama mke baada ya Mme wake kuacha Urais wapewe Posho hii inaingia akilini kweli?🤔
Narudia tena.
Mama Salma kachafua hali ya hewa.
 
Si wanasema familia ya marehemu rais itakuwa inachukua mshahara wa asilimia 80 ya rais aliyekuwa madarakani miaka yote?
mama Janet sidhani Kama Ana shida ya hela labda kama account za magufuli zimechukuliwa.
Hivi magufuli angekubali aondoke hivi hivi bila kuwatengenezea mazingira mazuri familia yake?
mama Salma mwenyewe kanufaika Sana na hii nchi kwa misamaha ya kodi na miradi ya kumwaga.
Kama mama Salma analia na mama Maria afanye Nini?
Au umemsikia mama Anne mkapa akilia ?
Labda ukute alikua anamlenga mama Janet asaidiwe huenda Serikali imemtupa Ila nawaza tu but sidhan kama ilikua sahihi?
 
Usikute hi nchi ni tajiri sana ila wananchi tu ndio hatuambiwi, watu wanamlaumu JPM kumbe alikua anatwambia UKWELI! Haiwezekani viongozi wetu kila wakati wanawaza kutumia tu na sio kuzalisha, hi nchi ni TAJIRI sana, wananchi tunadanganywa
 
Huyu mama nilikuwa namuheshimu lakin kumbe ni mtu wa hovyo sana. Yaani haoni hata masikini waliojaa huko Lindi anakowakilisha hawana dawa wala maji safi. Puuuaa! Puuuaa!
 
Ukute katumwa na mumewe, hayo ndiyo wameyaona ya maanaaaa!!
Na unakuta watu wanamwona JK alikuwa bonge la rais![emoji2297]
Hayo mambo lazima wateja dili na mumewe kabla ya kuja kulopoka bungeni!! Ulafi mtupu.
 
Sijaona ubaya ya aliyoyasema, lakini sijui watu wamechukulia kwa mtazamo upi.

Kawaida mtu ukistaafu lazima ulipwe mafao yako.

Mfano Mama janeth alikuwa mwalimu lakini baada ya Magufuli kuwa raisi yeye anastaafishwa kazi. Sasa kwanini asilipwe mafao yake kama mwalimu.
Una kichwa kizito mno mafao yao waldau hata Kesho watalipwa aliyekwambia hawalipwi nano nenda kaangalie sheria za mifuko ya Pension

Hujaelewa kabisa alichoongea huyo anachotaka wake wa hao viongozi wawe na mafao kama waume zao wakishaondoka kwenye ajira zao
Hao viongozi wa juu wanachpewa kina cover hadi wake zao .Aende akaombe kwa mumewe ampe kama hampi hayo matatizo yao ya chumbani asituletee mitaani

Mume akifariki yeye anaendelea kupokea shida nini? Ndio maana unaona Maria Nyerere, Janet Magufuli maisha Yao yanaenda bila shida
 
Mama salama ana hojamani ya Msingi, mama Janet alikuwa mwalimu mama salma alikuwa mwalimu walistaafishwa kwa nguvu mafao yao inakuwaje?
Hiyo pension wanayopata kwa kuwa tunza waume zao ni mara Mia moja ya pension yao ya ualimu!!

Huyu Salma anadai hiyo pension pengine ameachika kwa Vasco Dagama?
 
Una hakika haangaliwi leo kama mke wa Rais? Tuache kuwatukana watanzania. Anachotafuta ni kupata legal status ili impe milage!!! Nachojiuliza ni milage ya nini sasa? Tujifunze kula na kushiba. Binadamu wote wana midomo. Imagine wawe wanashinda njaa, halafu wachache ndio wanakula...kitatokea nini???
Swala hapo kulipwa stahiki zake kama mwalimu mstaafu pale ambapo alistaafishwa kazi mbona simple tu
 
Mama salama ana hojamani ya Msingi, mama Janet alikuwa mwalimu mama salma alikuwa mwalimu walistaafishwa kwa nguvu mafao yao inakuwaje?
Si ndo hapo sasa

Namimi naona sio wao tu hata raisi akiwa mwanamke na mume wake kustaafishwa naye alipwe stahiki zake.

Hivi ikitoke mafanyakazi labda mwalimu akachaguliwa na raisi kuwa waziri

Vipi stahiki zake za ualimu asilipwe ?
 
Hii Nchi ya ajabu sana yani Kijana Anakaa CHUO miaka 3 au 4 hadi Mi 5 akisoma anatoka pale anaambiwa na SERIKALI aji AJIRI Leo Mke wa Rais amekua na Mme wake 10 Years kwenye position yenye Fursa kibao za kufanya na za kumwingizia Mamilion ya Hela ila anataka Serikali imuandalie Mazingira mazuri ya yeye kama mke baada ya Mme wake kuacha Urais wapewe Posho hii inaingia akilini kweli?[emoji848]
Sio apewe posho kama mke wa raisi.
naona bado hujaelewa
 
Una kichwa kizito mno mafao yao waldau hata Kesho watalipwa aliyekwambia hawalipwi nano nenda kaangalie sheria za mifuko ya Pension

Hujaelewa kabisa alichoongea huyo anachotaka wake wa hao viongozi wawe na mafao kama waume zao wakishaondoka kwenye ajira zao
Hao viongozi wa juu wanachpewa kina cover hadi wake zao .Aende akaombe kwa mumewe ampe kama hampi hayo matatizo yao ya chumbani asituletee mitaani

Mume akifariki yeye anaendelea kupokea shida nini? Ndio maana unaona Maria Nyerere, Janet Magufuli maisha Yao yanaenda bila shida
Ndo maana amezingumzia hayo maana hawalipwi hayo mafao yao na kisheria inatakiwa ulipwe pale unapostaafu kazi
 
Back
Top Bottom