Sanamu ya Amani iliyowekwa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa ina maana gani? Je, inauhusiano gani na utabiri wa siku za mwisho?

Kwani shida ya samu hiyo ni nini!?
Kama unaogopa sanamu tu iliyotengenezwa kwa plastic, chuma na udongo mapepo yakija utaweza kupambana nayo kweli!?
Kumbe unajua kuna mapepo?

Na hapo hapo unakataa uwepo wa mashetani?

Wewe ni bwege ama?
 
Yaani hawa watu sijui wanadhani sisi ni mbumbumbu sana,dubwasha hili litaletaje amani kama sio extermination ya humanity.
 
Aisee!! Mbona tunazunguka zunguka ndugu. Nimekuambia imani ni kitu binafsi kina nihusu mimi. Kama wewe umeamua kuweka imani yako public basi is up to you. Unaweza kutuambia imani yako!?
Huna haja ya kuficha, jina lako la kimtandao na avatar yako tells it all.Na kama imani yako haina shida,kwa nini ufiche?
 
Wazungu wanawavuruga msiojielewa kwelikweli. Siku mkiamka mtakuta washaihama hii sayari.
 
Wazungu wanawavuruga msiojielewa kwelikweli. Siku mkiamka mtakuta washaihama hii sayari.
Wewe unayejielewa mwenzetu tuambie hilo sanamu usoni linalofanana na Chui mwenye hasira kali lina-maanisha nini?
 
Wewe Unaezani unaelewa na sisi wengine mambumbumbu ndo utuelewesha sasa
Hapo unaposema kueleweshwa umenena vyema; sawa!?
Kwanza unatakiwa kuandika "Unaedhani" sio Unezani.
Neno dhani, dhana, dhania nk.

Sasa unataka nikufundishe kitu gani!?
 
Na hapa ndipo mazezeta kama nyie mlipokamatwa na walioleta hizo dini. Eti Biblia haisomwi kama Alfu lela ulela,
Kwani mkikubali tu kwamba mavitabu yenu yamejaa mapungufu kuna shida gani?

Yaani eti Mungu huyohuyo aandae Moto wa Jehanamu mwenyewe ili wadhambi awachome,

Halafu yeye huyohuyo Mungu/Yesu anakuja kuwafia watu ili awaokoe na moto aliouandaa yeye mwenyewe.

Sasa hizi kama si hadithi za kijinga ni nini?
 
Kwanza kabisa MUNGU alimuumba mwanadamu kwa mfano wake (yani Umungu) , akampa nafasi ya kuchagua kuishi katika mabaya ambao mshahara wake ni motoni na kuishi katika mema ambapo mshahara wake ni mbingu

Motoni haikutengenezwa kwa ajili ya binadamu , motoni ilikuwa ni kwa ajili ya shetani. Adam ndiye aliyesabisha wanadamu kuingia motoni baada ya kuchagua mabaya yaani pale alipodanganywa na shetani ale tunda na afanane na MUNGU , na ikumbukwe shetani (malaika walioasi) nao walifukuzwa mbinguni na kuhukumiwa kwenda motoni kwa sababu ya kutaka kuwa MUNGU na kuupinduwa utawala wa MUNGU

Pili swala la Biblia , Hakuna kitu kwenye Biblia kitafutika , yale yalioandikwa yatatimia .

Na nimeona pia hujui tofauti kati ya MUNGU na Yesu , Yesu ni mwana wa kwanza wa MUNGU , ndiye wa kwanza kuumbwa na MUNGU kabla hajaumba chochote kile kati ya mbingu na malaika . Na Yesu ndiye aliyefanya uumbaji , kwa kupitia nguvu ya MUNGU . Na yeye ndiye Masiha . Na kila goti litapigwa siku ya mwisho kwa sababu MUNGU amemfanya kuwa mfalme

Jina La Yesu , likitajwa Mapepo(Majini) yanapiga kelele za maumivu. Jina La Yesu likitajwa wenye imani wanapona UKIMWI , KISUKARI , KANSA na magonjwa yalioshindikana. HAKUNA JINA LENYE NGUVU KAMA JINA LA YESU
 
Mwenyezi Mungu yupi!?
1. Wa wayahudi
2. Wa wakristo
3. Wa waislam
4. Wa wahindu
5. Wa wabudha
6. Wa confuism
7. Wa Taoism
Yupi unayemuongelea anakuja kufufua mifupa iliyooza na mingine decayed, imeliwa na funza!? Na kuwa mbolea.
Hao wote MUNGU WAO MMOJA.
Kwani dunia na vilivyomo vimeumbwa na Mungu wangapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…