Sarakasi za Mbunge kijana na somo kwa vyama vya siasa wakati wa uteuzi majina ya wabunge

Sarakasi za Mbunge kijana na somo kwa vyama vya siasa wakati wa uteuzi majina ya wabunge

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Nimeiangalia video ya Mheshimiwa mbunge wa Arumeru namna alivyopanda juu ya meza yake na kusimama miguu kichwa chini. Siwezi kusema sikushangazwa sana kama wengi walioiona video hiyo kwa mara ya kwanza. Wanaonekana wabunge waliokaa jirani yake wanashangaa wakicheka kwa kustaajabishwa. Hata sauti ya kucheza ya Mheshimiwa Spika akimkataza mbunge huyo wa Arumeru asifanye kituko hicho, na yenyewe ni ya kucheka akiwa anashangaa haamini kile kinachokwenda kufanyika ndani ya ukumbi wa bunge.

Inaonekana mheshimiwa Mbunge amenyimwa kule kukua kisawasawa kabla hajapewa nafasi ya kuwa mbunge, ni kama vile kuna hatua maishani mwake imerukwa na akapewa ubunge kabla hajaipitia hiyo hatua. Bungeni ameingia mtu mzima wa umbo lakini ni mtoto wa kimaamuzi sawa sawa na mahali pale. Amefanya mpaka wataalam wa kutengeneza vibonzo wakitengeneza kimoja akiwa amesimama miguu juu kichwani pembeni ya viti vya Samia na Mzee Greenburg wa Royal Tour, eti wanamtazama wakimshangaa.

Naliona kosa linalofanyika mara kwa mara wakati wa teuzi za wagombea ubunge wa vyama vya siasa. Anachaguliwa kugombea aina ya mtu anayependwa na uongozi wa juu lakini hakubaliki miongoni mwa wajumbe wanaoteua. Anayeteuliwa mgombea asiyekubalika au asiyeenda sambamba na hulka za wapiga kura wanaomchagua!. Wajumbe wanaishia kupiga makofi ya kinafiki siku wanapotajiwa kuwa ndio anayekwenda kuwawakilisha katika uchaguzi mkuu na baadae bungeni.

Mbunge anayecheza sarakasi ndani ya ukumbi wa bunge sio tu ni aibu ya CCM bali pia ni aibu ya mifumo yetu ya kisiasa. Kwamba anakuwepo mgombea anayependwa na kukubalika miongoni mwa wapiga kura na pia anakuwepo yule anayekubalika miongoni mwa wanaokaa meza kuu. Ni hapa unapomuangalia mbunge huyu licha ya kuwasilisha hoja za msingi kwa mheshimiwa Spika lakini bado anazo hulka za ujana, hulka za mtu ambaye hajakomaa sawa sawa kichwani mwake. Bado mwili wake unachemkwa na damu ya ujana.

Hapa lipo la kujifunza na kulifanyia kazi. Kwamba sauti ya wengi siku zote huwakilisha maoni sahihi ya watu wa sehemu husika. Kwamba maoni na vionjo vya watu ni vya kuheshimiwa na sio kuwapelekea aina ya mbunge kwa kutazama vigezo vya wachache wanaokaa meza kuu.

Na ni hapa tunaweza kuuona uhalali wa malalamiko ya baadhi ya watanzania wanaposema kwamba uchaguzi wa 2020 hawana kabisa imani nao, wakimaaanisha rafu za kisiasa zilikuwa ni nyingi na za wazi. Sijawahi kukaa na watu wa jimbo lililomchagua mheshimiwa huyu kwenda bungeni, lakini nahisi kuna ile hali ya unyonge wa kuona liwalo na liwe kama wameamua kwenda na huyu kijana kama mbunge kwa miaka hii mitano inayomalizika 2025.
 
  • Thanks
Reactions: Qwy
Nimeiangalia video ya Mheshimiwa mbunge wa Arumeru namna alivyopanda juu ya meza yake na kusimama miguu kichwa chini. Siwezi kusema sikushangazwa sana kama wengi walioiona video hiyo kwa mara ya kwanza. Wanaonekana wabunge waliokaa jirani yake wanashangaa wakicheka kwa kustaajabishwa. Hata sauti ya kucheza ya Mheshimiwa Spika akimkataza mbunge huyo wa Arumeru asifanye kituko hicho, na yenyewe ni ya kucheka akiwa anashangaa haamini kile kinachokwenda kufanyika ndani ya ukumbi wa bunge.

Inaonekana mheshimiwa Mbunge amenyimwa kule kukua kisawasawa kabla hajapewa nafasi ya kuwa mbunge, ni kama vile kuna hatua maishani mwake imerukwa na akapewa ubunge kabla hajaipitia hiyo hatua. Bungeni ameingia mtu mzima wa umbo lakini ni mtoto wa kimaamuzi sawa sawa na mahali pale. Amefanya mpaka wataalam wa kutengeneza vibonzo wakitengeneza kimoja akiwa amesimama miguu juu kichwani pembeni ya viti vya Samia na Mzee Greenburg wa Royal Tour, eti wanamtazama wakimshangaa.

Naliona kosa linalofanyika mara kwa mara wakati wa teuzi za wagombea ubunge wa vyama vya siasa. Anachaguliwa kugombea aina ya mtu anayependwa na uongozi wa juu lakini hakubaliki miongoni mwa wajumbe wanaoteua. Anayeteuliwa mgombea asiyekubalika au asiyeenda sambamba na hulka za wapiga kura wanaomchagua!. Wajumbe wanaishia kupiga makofi ya kinafiki siku wanapotajiwa kuwa ndio anayekwenda kuwawakilisha katika uchaguzi mkuu na baadae bungeni.

Mbunge anayecheza sarakasi ndani ya ukumbi wa bunge sio tu ni aibu ya CCM bali pia ni aibu ya mifumo yetu ya kisiasa. Kwamba anakuwepo mgombea anayependwa na kukubalika miongoni mwa wapiga kura na pia anakuwepo yule anayekubalika miongoni mwa wanaokaa meza kuu. Ni hapa unapomuangalia mbunge huyu licha ya kuwasilisha hoja za msingi kwa mheshimiwa Spika lakini bado anazo hulka za ujana, hulka za mtu ambaye hajakomaa sawa sawa kichwani mwake. Bado mwili wake unachemkwa na damu ya ujana.

Hapa lipo la kujifunza na kulifanyia kazi. Kwamba sauti ya wengi siku zote huwakilisha maoni sahihi ya watu wa sehemu husika. Kwamba maoni na vionjo vya watu ni vya kuheshimiwa na sio kuwapelekea aina ya mbunge kwa kutazama vigezo vya wachache wanaokaa meza kuu.

Na ni hapa tunaweza kuuona uhalali wa malalamiko ya baadhi ya watanzania wanaposema kwamba uchaguzi wa 2020 hawana kabisa imani nao, wakimaaanisha rafu za kisiasa zilikuwa ni nyingi na za wazi. Sijawahi kukaa na watu wa jimbo lililomchagua mheshimiwa huyu kwenda bungeni, lakini nahisi kuna ile hali ya unyonge wa kuona liwalo na liwe kama wameamua kwenda na huyu kijana kama mbunge kwa miaka hii mitano inayomalizika 2025.
Hizi ni athari za wabunge kuteuliwa na mtu mmoja ili baadae waje wamsifu na kumwamudu. Hizi ni kazi ya mwendazake na ndiyo legacy aliyoiacha. Huyu mbunge aliingia bungeni baada ya watu wenye busara akili kuporwa kura zao na huyu akaingia kwa nguvu za dola. Wala usishangae kwani wako wengi kweli kweli bungeni. Tena wengine ni wajinga kuliko huyu.
 
Kwa sasa ethics za uongozi haziangaliwi bali inategemea hasa kwenye circle anakujua nani
Ndo sababu tunapata hawa vijana wanaopiga sarakasi mahala ambapo kimsingi ndipo panapotungwa sheria za nchi, hata ule uwoga hawana .
Unaweza kudhani upo kwenye big gambling casino ! Kumbe unaangalia bunge tukufu.
 
Heri hamsini kama yeye ambao angalau ana-sense of homour na kuchekesha na pia yupo Unique kuliko wanaopewa posho kwa kulala au walio serious huku wanapitisha mikataba ya ajabu ajabu...

Ustaarabu pekee ninaotaka kwa hao watunga sheria ni kutokutunga sheria mbovu au kutetea waliowatuma..., hayo mengine kwangu ni immaterial...
 
Nimeiangalia video ya Mheshimiwa mbunge wa Arumeru namna alivyopanda juu ya meza yake na kusimama miguu kichwa chini. Siwezi kusema sikushangazwa sana kama wengi walioiona video hiyo kwa mara ya kwanza. Wanaonekana wabunge waliokaa jirani yake wanashangaa wakicheka kwa kustaajabishwa. Hata sauti ya kucheza ya Mheshimiwa Spika akimkataza mbunge huyo wa Arumeru asifanye kituko hicho, na yenyewe ni ya kucheka akiwa anashangaa haamini kile kinachokwenda kufanyika ndani ya ukumbi wa bunge.

Inaonekana mheshimiwa Mbunge amenyimwa kule kukua kisawasawa kabla hajapewa nafasi ya kuwa mbunge, ni kama vile kuna hatua maishani mwake imerukwa na akapewa ubunge kabla hajaipitia hiyo hatua. Bungeni ameingia mtu mzima wa umbo lakini ni mtoto wa kimaamuzi sawa sawa na mahali pale. Amefanya mpaka wataalam wa kutengeneza vibonzo wakitengeneza kimoja akiwa amesimama miguu juu kichwani pembeni ya viti vya Samia na Mzee Greenburg wa Royal Tour, eti wanamtazama wakimshangaa.

Naliona kosa linalofanyika mara kwa mara wakati wa teuzi za wagombea ubunge wa vyama vya siasa. Anachaguliwa kugombea aina ya mtu anayependwa na uongozi wa juu lakini hakubaliki miongoni mwa wajumbe wanaoteua. Anayeteuliwa mgombea asiyekubalika au asiyeenda sambamba na hulka za wapiga kura wanaomchagua!. Wajumbe wanaishia kupiga makofi ya kinafiki siku wanapotajiwa kuwa ndio anayekwenda kuwawakilisha katika uchaguzi mkuu na baadae bungeni.

Mbunge anayecheza sarakasi ndani ya ukumbi wa bunge sio tu ni aibu ya CCM bali pia ni aibu ya mifumo yetu ya kisiasa. Kwamba anakuwepo mgombea anayependwa na kukubalika miongoni mwa wapiga kura na pia anakuwepo yule anayekubalika miongoni mwa wanaokaa meza kuu. Ni hapa unapomuangalia mbunge huyu licha ya kuwasilisha hoja za msingi kwa mheshimiwa Spika lakini bado anazo hulka za ujana, hulka za mtu ambaye hajakomaa sawa sawa kichwani mwake. Bado mwili wake unachemkwa na damu ya ujana.

Hapa lipo la kujifunza na kulifanyia kazi. Kwamba sauti ya wengi siku zote huwakilisha maoni sahihi ya watu wa sehemu husika. Kwamba maoni na vionjo vya watu ni vya kuheshimiwa na sio kuwapelekea aina ya mbunge kwa kutazama vigezo vya wachache wanaokaa meza kuu.

Na ni hapa tunaweza kuuona uhalali wa malalamiko ya baadhi ya watanzania wanaposema kwamba uchaguzi wa 2020 hawana kabisa imani nao, wakimaaanisha rafu za kisiasa zilikuwa ni nyingi na za wazi. Sijawahi kukaa na watu wa jimbo lililomchagua mheshimiwa huyu kwenda bungeni, lakini nahisi kuna ile hali ya unyonge wa kuona liwalo na liwe kama wameamua kwenda na huyu kijana kama mbunge kwa miaka hii mitano inayomalizika 2025.
Umeandika meengi lakini na wewe unaongozwa na mihemko binafsi na imepelekea hata kutotambua yule mbunge hakuwa wa Arumeru bali mbunge wa Mbulu.

Alilazimika kuonyesha kukerwa kwake na ukimya wa serikali yake ya CCM kwa kutoanza kutimiza ahadi ya ujenzi wa Barabara kwa kiwango cha lami.
Licha ya kuwa kwenye bajeti kwa muda wa miaka mitatu mfululizo.

Kwa wananchi wake wa mbulu wanaoishi katika eneo husika wanamuelewa vizuri kutokana na uzito wa kero ya barabara hasa kipindi cha mvua.

Na kwa sababu hiyo tu.huyo mtu anapata Political mileage ya kutosha na ameweka rekodi ya msisitizo.

Kuna vituko vingi sana katika mabunge mbalimbali Duniani ikiwemo hata kuzichapa ngumi kavukavu.

Mngeangalia zaidi uzito wa hoja yake kuliko kuangalia mambo ya sarakasi ile.
 
Huyo ni mbunge wa Mbulu vijijini,ameonyesha ana utimamu wa mwili hasa,kwani kuruka sarakasi zile siyo mchezo,utimamu mwingine wa akili,sijajua.Ila hata utimamu wa akili anaonekana yuko vizuri kwa namna alivyochangia hoja zake.All in all yuko vizuri kiuwakilishi.
 
Mbunge anayecheza sarakasi ndani ya ukumbi wa bunge sio tu ni aibu ya CCM bali pia ni aibu ya mifumo yetu ya kisiasa.
... yakifanywa mambo ya aibu na CCM ndipo mnapohusisha "mifumo yote" ya siasa! Yangefanywa na upande mwingine mngelaani Chadema kwa nguvu zote pengine hata UVCCM kuandamana kumshinikiza Msajili akifutie usajili! Ila kwa sababu yamefanywa na mtu wenu imekuwa "mifumo yote" ya kisiasa! Wanafiki wakubwa ninyi!
 
Huyo ni mbunge wa Mbulu vijijini,ameonyesha ana utimamu wa mwili hasa,kwani kuruka sarakasi zile siyo mchezo,utimamu mwingine wa akili,sijajua.Ila hata utimamu wa akili anaonekana yuko vizuri kwa namna alivyochangia hoja zake.All in all yuko vizuri kiuwakilishi.
... kama jiwe alivyokuwa akipiga pushups kwenye majukwaa. Utimamu wa mwili wa mwanadamu ni fumbo.
 
Kwa sasa ethics za uongozi haziangaliwi bali inategemea hasa kwenye circle anakujua nani
Ndo sababu tunapata hawa vijana wanaopiga sarakasi mahala ambapo kimsingi ndipo panapotungwa sheria za nchi, hata ule uwoga hawana .
Unaweza kudhani upo kwenye big gambling casino ! Kumbe unaangalia bunge tukufu.
na hicho ndo kizazi tunachokitegemea kuleta mabadiliko katika nchi.kizazi cha nyoka na yule mwovu ibilisi.
 
Huyo ni mbunge wa Mbulu vijijini,ameonyesha ana utimamu wa mwili hasa,kwani kuruka sarakasi zile siyo mchezo,utimamu mwingine wa akili,sijajua.Ila hata utimamu wa akili anaonekana yuko vizuri kwa namna alivyochangia hoja zake.All in all yuko vizuri kiuwakilishi.
Labda bangi inahusika,maana yenyewe Ile Kwa kurahisisha mambo na kuona yote Sawa ni kawaida Sana.Ubongo ambao haujasisimuliwa na chochote,hujua kipi kifanyike wapi na lini.kipi kisemwe sasa na kipi kisubiri.
 
Hizi ni athari za wabunge kuteuliwa na mtu mmoja ili baadae waje wamsifu na kumwamudu. Hizi ni kazi ya mwendazake na ndiyo legacy aliyoiacha. Huyu mbunge aliingia bungeni baada ya watu wenye busara akili kuporwa kura zao na huyu akaingia kwa nguvu za dola. Wala usishangae kwani wako wengi kweli kweli bungeni. Tena wengine ni wajinga kuliko huyu.
Hao hawakuchaguliwa,waliletwa na mwendazake.
 
... yakifanywa mambo ya aibu na CCM ndipo mnapohusisha "mifumo yote" ya siasa! Yangefanywa na upande mwingine mngelaani Chadema kwa nguvu zote pengine hata UVCCM kuandamana kumshinikiza Msajili akifutie usajili! Ila kwa sababu yamefanywa na mtu wenu imekuwa "mifumo yote" ya kisiasa! Wanafiki wakubwa ninyi!
Huko CHADEMA kuna wabunge wa underwear wa Mheshimiwa Mbowe. Nao ni tatizo kwani malalamiko yanayotolewa na wanachama ni mengi haswa ya watu wa nyanda za juu kusini, waliolalamika mwaka 2015 Mbowe kujichagulia vimwana kuwa ndio wagombea rasmi.

Kusema mfumo mzima wa kisiasa nadhani sijakosea, ni sawa kabisa.
 
Umeandika meengi lakini na wewe unaongozwa na mihemko binafsi na imepelekea hata kutotambua yule mbunge hakuwa wa Arumeru bali mbunge wa Mbulu.

Alilazimika kuonyesha kukerwa kwake na ukimya wa serikali yake ya CCM kwa kutoanza kutimiza ahadi ya ujenzi wa Barabara kwa kiwango cha lami.
Licha ya kuwa kwenye bajeti kwa muda wa miaka mitatu mfululizo.

Kwa wananchi wake wa mbulu wanaoishi katika eneo husika wanamuelewa vizuri kutokana na uzito wa kero ya barabara hasa kipindi cha mvua.

Na kwa sababu hiyo tu.huyo mtu anapata Political mileage ya kutosha na ameweka rekodi ya msisitizo.

Kuna vituko vingi sana katika mabunge mbalimbali Duniani ikiwemo hata kuzichapa ngumi kavukavu.

Mngeangalia zaidi uzito wa hoja yake kuliko kuangalia mambo ya sarakasi ile.
Well said ,ndio maana bunge sidhani kama ataitwa kwenye kamati ya maadili .
Ukweli hoja yake ndio tuijadili hapa
 
Back
Top Bottom