Sarakasi za Mbunge kijana na somo kwa vyama vya siasa wakati wa uteuzi majina ya wabunge

Sarakasi za Mbunge kijana na somo kwa vyama vya siasa wakati wa uteuzi majina ya wabunge

Imekuwa ni kawaida kwa vyama katika baadhi ya maeneo kuchagua watu wasio na weledi. Wakati mwingine waliokosa difa kabisa.

Tatizo hili hijitokeza pia hata kwa nafasi za wagombea wenza. Vyama vingi hufanya makosa katika hili
 
Kumuita mbunge kijana,wakati ni wa mwaka 72,sijui inakuaje?

Nadhani ana miaka 50 sasa.

Inaonyesha ni mtu wa mazoezi sana huyu mtu hasa ukizingatia umri.
 
Hizi ni athari za wabunge
Yah. Uchafuzi ule ungekuwa uchaguzi huru na wa haki, mbunge wa mbeya mjini angekuwa Sugu, zitto angekuwa bungeni, Mdee angekuwa mbunge halali wa kuchaguliwa, kina Mbowe, Heche, Mbatia etc wangekuwamo. Na bunge lingekuwa na heshima yake. Hakungekuwa na 'covid19', sarakasi wala kulia bungeni.

Maana pale pangekuwa na mapambano yenye tija, ya hoja dhidi ya hoja.

Hawa wanafiki wengine kina gambo hawangekuwamo. Lissu na Lema hawangekuwa ubelgiji/Canada, tungekuwa tunasikilizia nyundo zao huo Dodoma.
 
Nimeiangalia video ya Mheshimiwa mbunge wa Arumeru namna alivyopanda juu ya meza yake na kusimama miguu kichwa chini. Siwezi kusema sikushangazwa sana kama wengi walioiona video hiyo kwa mara ya kwanza. Wanaonekana wabunge waliokaa jirani yake wanashangaa wakicheka kwa kustaajabishwa. Hata sauti ya kucheza ya Mheshimiwa Spika akimkataza mbunge huyo wa Arumeru asifanye kituko hicho, na yenyewe ni ya kucheka akiwa anashangaa haamini kile kinachokwenda kufanyika ndani ya ukumbi wa bunge.

Inaonekana mheshimiwa Mbunge amenyimwa kule kukua kisawasawa kabla hajapewa nafasi ya kuwa mbunge, ni kama vile kuna hatua maishani mwake imerukwa na akapewa ubunge kabla hajaipitia hiyo hatua. Bungeni ameingia mtu mzima wa umbo lakini ni mtoto wa kimaamuzi sawa sawa na mahali pale. Amefanya mpaka wataalam wa kutengeneza vibonzo wakitengeneza kimoja akiwa amesimama miguu juu kichwani pembeni ya viti vya Samia na Mzee Greenburg wa Royal Tour, eti wanamtazama wakimshangaa.

Naliona kosa linalofanyika mara kwa mara wakati wa teuzi za wagombea ubunge wa vyama vya siasa. Anachaguliwa kugombea aina ya mtu anayependwa na uongozi wa juu lakini hakubaliki miongoni mwa wajumbe wanaoteua. Anayeteuliwa mgombea asiyekubalika au asiyeenda sambamba na hulka za wapiga kura wanaomchagua!. Wajumbe wanaishia kupiga makofi ya kinafiki siku wanapotajiwa kuwa ndio anayekwenda kuwawakilisha katika uchaguzi mkuu na baadae bungeni.

Mbunge anayecheza sarakasi ndani ya ukumbi wa bunge sio tu ni aibu ya CCM bali pia ni aibu ya mifumo yetu ya kisiasa. Kwamba anakuwepo mgombea anayependwa na kukubalika miongoni mwa wapiga kura na pia anakuwepo yule anayekubalika miongoni mwa wanaokaa meza kuu. Ni hapa unapomuangalia mbunge huyu licha ya kuwasilisha hoja za msingi kwa mheshimiwa Spika lakini bado anazo hulka za ujana, hulka za mtu ambaye hajakomaa sawa sawa kichwani mwake. Bado mwili wake unachemkwa na damu ya ujana.

Hapa lipo la kujifunza na kulifanyia kazi. Kwamba sauti ya wengi siku zote huwakilisha maoni sahihi ya watu wa sehemu husika. Kwamba maoni na vionjo vya watu ni vya kuheshimiwa na sio kuwapelekea aina ya mbunge kwa kutazama vigezo vya wachache wanaokaa meza kuu.

Na ni hapa tunaweza kuuona uhalali wa malalamiko ya baadhi ya watanzania wanaposema kwamba uchaguzi wa 2020 hawana kabisa imani nao, wakimaaanisha rafu za kisiasa zilikuwa ni nyingi na za wazi. Sijawahi kukaa na watu wa jimbo lililomchagua mheshimiwa huyu kwenda bungeni, lakini nahisi kuna ile hali ya unyonge wa kuona liwalo na liwe kama wameamua kwenda na huyu kijana kama mbunge kwa miaka hii mitano inayomalizika 2025.
Aibu kwa taifa.
IMG_20220524_183533.jpg
 
Umeandika meengi lakini na wewe unaongozwa na mihemko binafsi na imepelekea hata kutotambua yule mbunge hakuwa wa Arumeru bali mbunge wa Mbulu....
Sarakasi ya kujiaibisha ime-overshadow kile alichokuwa anakizungumzia, ndiyo pale unapotumia njia za kipuuzi kuwasilisha jambo la maana na kusababisha huo upuuzi ukalifunika hilo jambo.

Mleta uzi yuko sahihi kabisa kwa namna alivyolifafanua tukio zima.
 
... kama jiwe alivyokuwa akipiga pushups kwenye majukwaa. Utimamu wa mwili wa mwanadamu ni fumbo.
Naamini amekuelewa, big up GT kwa jibu mujarabu kabisa.
 
Hizi ni athari za wabunge kuteuliwa na mtu mmoja ili baadae waje wamsifu na kumwamudu. Hizi ni kazi ya mwendazake na ndiyo legacy aliyoiacha. Huyu mbunge aliingia bungeni baada ya watu wenye busara akili kuporwa kura zao na huyu akaingia kwa nguvu za dola. Wala usishangae kwani wako wengi kweli kweli bungeni. Tena wengine ni wajinga kuliko huyu.
Hakika mkuu, tutashuhudia mengi, tuombe uzima tu,
 
Aaaaagh picha iko wapi sasa,wengine tupo Kandahar tuone MPalievunja records za mjengoni
 
Nimeiangalia video ya Mheshimiwa mbunge wa Arumeru namna alivyopanda juu ya meza yake na kusimama miguu kichwa chini. Siwezi kusema sikushangazwa sana kama wengi walioiona video hiyo kwa mara ya kwanza. Wanaonekana wabunge waliokaa jirani yake wanashangaa wakicheka kwa kustaajabishwa. Hata sauti ya kucheza ya Mheshimiwa Spika akimkataza mbunge huyo wa Arumeru asifanye kituko hicho, na yenyewe ni ya kucheka akiwa anashangaa haamini kile kinachokwenda kufanyika ndani ya ukumbi wa bunge.

Inaonekana mheshimiwa Mbunge amenyimwa kule kukua kisawasawa kabla hajapewa nafasi ya kuwa mbunge, ni kama vile kuna hatua maishani mwake imerukwa na akapewa ubunge kabla hajaipitia hiyo hatua. Bungeni ameingia mtu mzima wa umbo lakini ni mtoto wa kimaamuzi sawa sawa na mahali pale. Amefanya mpaka wataalam wa kutengeneza vibonzo wakitengeneza kimoja akiwa amesimama miguu juu kichwani pembeni ya viti vya Samia na Mzee Greenburg wa Royal Tour, eti wanamtazama wakimshangaa.

Naliona kosa linalofanyika mara kwa mara wakati wa teuzi za wagombea ubunge wa vyama vya siasa. Anachaguliwa kugombea aina ya mtu anayependwa na uongozi wa juu lakini hakubaliki miongoni mwa wajumbe wanaoteua. Anayeteuliwa mgombea asiyekubalika au asiyeenda sambamba na hulka za wapiga kura wanaomchagua!. Wajumbe wanaishia kupiga makofi ya kinafiki siku wanapotajiwa kuwa ndio anayekwenda kuwawakilisha katika uchaguzi mkuu na baadae bungeni.

Mbunge anayecheza sarakasi ndani ya ukumbi wa bunge sio tu ni aibu ya CCM bali pia ni aibu ya mifumo yetu ya kisiasa. Kwamba anakuwepo mgombea anayependwa na kukubalika miongoni mwa wapiga kura na pia anakuwepo yule anayekubalika miongoni mwa wanaokaa meza kuu. Ni hapa unapomuangalia mbunge huyu licha ya kuwasilisha hoja za msingi kwa mheshimiwa Spika lakini bado anazo hulka za ujana, hulka za mtu ambaye hajakomaa sawa sawa kichwani mwake. Bado mwili wake unachemkwa na damu ya ujana.

Hapa lipo la kujifunza na kulifanyia kazi. Kwamba sauti ya wengi siku zote huwakilisha maoni sahihi ya watu wa sehemu husika. Kwamba maoni na vionjo vya watu ni vya kuheshimiwa na sio kuwapelekea aina ya mbunge kwa kutazama vigezo vya wachache wanaokaa meza kuu.

Na ni hapa tunaweza kuuona uhalali wa malalamiko ya baadhi ya watanzania wanaposema kwamba uchaguzi wa 2020 hawana kabisa imani nao, wakimaaanisha rafu za kisiasa zilikuwa ni nyingi na za wazi. Sijawahi kukaa na watu wa jimbo lililomchagua mheshimiwa huyu kwenda bungeni, lakini nahisi kuna ile hali ya unyonge wa kuona liwalo na liwe kama wameamua kwenda na huyu kijana kama mbunge kwa miaka hii mitano inayomalizika 2025.
Hakika huyu munger anaakili sana amekuwa mbunifu wa hali ya just sana ni miongoni mwa wabunge wachache wa chama cha kijani (green party) wanaojitambua na wenye ability ya kiwango cha juu katika kupeleka ujumbe HONGERA SANA MBUNGE FLATEI MASSAY KAZI NZURI
 
Nimeiangalia video ya Mheshimiwa mbunge wa Arumeru namna alivyopanda juu ya meza yake na kusimama miguu kichwa chini. Siwezi kusema sikushangazwa sana kama wengi walioiona video hiyo kwa mara ya kwanza. Wanaonekana wabunge waliokaa jirani yake wanashangaa wakicheka kwa kustaajabishwa. Hata sauti ya kucheza ya Mheshimiwa Spika akimkataza mbunge huyo wa Arumeru asifanye kituko hicho, na yenyewe ni ya kucheka akiwa anashangaa haamini kile kinachokwenda kufanyika ndani ya ukumbi wa bunge.

Inaonekana mheshimiwa Mbunge amenyimwa kule kukua kisawasawa kabla hajapewa nafasi ya kuwa mbunge, ni kama vile kuna hatua maishani mwake imerukwa na akapewa ubunge kabla hajaipitia hiyo hatua. Bungeni ameingia mtu mzima wa umbo lakini ni mtoto wa kimaamuzi sawa sawa na mahali pale. Amefanya mpaka wataalam wa kutengeneza vibonzo wakitengeneza kimoja akiwa amesimama miguu juu kichwani pembeni ya viti vya Samia na Mzee Greenburg wa Royal Tour, eti wanamtazama wakimshangaa.

Naliona kosa linalofanyika mara kwa mara wakati wa teuzi za wagombea ubunge wa vyama vya siasa. Anachaguliwa kugombea aina ya mtu anayependwa na uongozi wa juu lakini hakubaliki miongoni mwa wajumbe wanaoteua. Anayeteuliwa mgombea asiyekubalika au asiyeenda sambamba na hulka za wapiga kura wanaomchagua!. Wajumbe wanaishia kupiga makofi ya kinafiki siku wanapotajiwa kuwa ndio anayekwenda kuwawakilisha katika uchaguzi mkuu na baadae bungeni.

Mbunge anayecheza sarakasi ndani ya ukumbi wa bunge sio tu ni aibu ya CCM bali pia ni aibu ya mifumo yetu ya kisiasa. Kwamba anakuwepo mgombea anayependwa na kukubalika miongoni mwa wapiga kura na pia anakuwepo yule anayekubalika miongoni mwa wanaokaa meza kuu. Ni hapa unapomuangalia mbunge huyu licha ya kuwasilisha hoja za msingi kwa mheshimiwa Spika lakini bado anazo hulka za ujana, hulka za mtu ambaye hajakomaa sawa sawa kichwani mwake. Bado mwili wake unachemkwa na damu ya ujana.

Hapa lipo la kujifunza na kulifanyia kazi. Kwamba sauti ya wengi siku zote huwakilisha maoni sahihi ya watu wa sehemu husika. Kwamba maoni na vionjo vya watu ni vya kuheshimiwa na sio kuwapelekea aina ya mbunge kwa kutazama vigezo vya wachache wanaokaa meza kuu.

Na ni hapa tunaweza kuuona uhalali wa malalamiko ya baadhi ya watanzania wanaposema kwamba uchaguzi wa 2020 hawana kabisa imani nao, wakimaaanisha rafu za kisiasa zilikuwa ni nyingi na za wazi. Sijawahi kukaa na watu wa jimbo lililomchagua mheshimiwa huyu kwenda bungeni, lakini nahisi kuna ile hali ya unyonge wa kuona liwalo na liwe kama wameamua kwenda na huyu kijana kama mbunge kwa miaka hii mitano inayomalizika 2025.
Aibu kubwa sana
 
Back
Top Bottom