SATIVA adhibitiwe kwa matusi ya nguoni anayotoa mitandaoni

SATIVA adhibitiwe kwa matusi ya nguoni anayotoa mitandaoni

Ndiyo maana Babu yangu Mchungaji alinizuia kabisa baada ya kuhitimu kidato cha sita kujiunga na upolice.

Kazi ya upolice ni ngumu mno iliyojaa vishawishi na amri kutoka kwa wakuu wako uitii hata kama ni ya hovyo.

RIP babu.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kiwango alichofikia huyu kijana ni kibaya sana,ni kiwango ambacho hakihitaji kuvumiliwa wala kuachwa hivi hivi pasipo kudhibitiwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Kwa sasa anatukana matusi ya nguoni mpaka mtu mwenye hekima na akili timamu unabaki unaona aibu na fedheha kubwa.Ni matusi na lugha ambazo yeyote mwenye akili Timamu,mwenye hofu ya Mungu na mcha Mungu na aliyepata malezi mazuri ya wazazi wake hawezi kutukana wala kutoa iwe hadharani au mafichoni.

Sielewi huyu kijana kama wazazi wake wapo hai au walishatangulia mbele za haki.sielewi ikiwa huyu kijana ana ndugu wa karibu au viongozi wa Dini . sielewi huyu kijana kama amewahi hata kujua kama Mungu yupo na kwamba kuna siku sisi wanadamu tutakufa na kwenda kutoa hesabu mbele za Mwenyezi Mungu.sielewi kama huyu Kijana amewahi kuishi na wazazi wake na kulelewa katika ukuaji wake.

Anatoa lugha na matusi makubwa na yenye kuibua hasira,chuki na ghadhabu kubwa sana . Ni matusi na lugha ambazo hazikubaliki mbele ya jamii iliyostaarabika. Ni matusi na lugha ambazo haziwezi na hazipaswi kufumbiwa macho na kuachwa zipite hivihivi.

Huyu kijana anapaswa kudhibitiwa haraka sana.hawezi kuachwa aendelee kutukana matusi ya Nguoni.ni lazima akamatwe na kuwajibishwa kisheria.ni lazima afundishwe adabu ,ni lazima aambiwe huo siyo utamaduni wetu na siyo maadili yetu ya kitanzania. Ni lazima aambiwe wazi kwa vitendo kuwa popote pale Duniani hakuna uhuru wa kutukana matusi kama kichaa au mwendawazimu mbele ya watu waliostaarabika na ukaachwa hivi hivi.

Kama kuna mtu anaweza kuunga mkono matusi ya huyu kijana basi atakuwa ni mtu wa ajabu sana,mwenye matatizo ya akili,mwenye kukosa hofu ya Mungu na aliyekosa malezi ya wazazi wake na mwenye matatizo kichwani na asiyejitambua.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Hayo matusi ya huyo Sativa, japo hatuyajui wala hujayataja, yanafanalingana kwa namna yoyote ile na vitendo vile vilivyofanywa na shetani mafwele na hao mashetani wengine, waliaoamua kumteka na kumwua? Huyo Sativa, anamtukana nani? Kama anawatukana hao waliotaka kumwua, ni halali kwani waliyomtendea yanapita viwango vya uhayawani wote.

Mambo hayo ya wazazi wa Sativa, ungeachana nayo tu. Humu watu wengi wenye uelewa wanawaonea huruma wazazi wa chawa mbobezi Lucas aliyeamua kuudhalilisha ubinadamu wake ili tu watawala wamrushie makombo. Yaani a.eamua tumbo liufute ubinadamu na utu wake.
 
Gentleman,
kinachomsumbua moyoni si matusi au kuna kingine?

kwamba bangi anazovuta na wengine watumie right ili wawe kama yeye kwa faida, hasara na maumivu ya nani kwa mfano?🐒
wewe inakuhusu nini sativa akitukana..kati ya mambo ya kipumbavu ni kutetea wanaofanya matendo ya kuumiza wengine, hakuna sabab hata moja kujustfy uharamia na ushenzi wa kuteka watu kwa sababu yoyote ile! those dark days r gone my friend..serikali kwenye jamii iliyostaarabika inaelewa tofauti ya mawazo na matarajio ndani ya jamii na hivyo you don't silence people who challenge the government by abducting and killing them..let them say what they see r not correct! God didn't create a super man..!
 
Saliva hayupo vizuri mentally kutokana na magum aliyopitia, nadhan anahitaji tiba!
Anahitaji justice, tiba ya kwanza kumponya ni justice, kitu ambacho kwa Tanzania hii hawezi kukipata. Mtu aliywkufa akafufuka hana ha kupoteza.
 
...siku zinavyokwenda anaudhihirishia umma kwamba yeye ni liability kiasi gani kwa hili taifa la watu wastaarabu
Taifa gani la "watu wastaarabu"?
Maana kama unaongelea hiyo Tanzania ambayo kwa sasa watawala ndo watekelezaji wa utekaji na mauaji, wizi wa kura, ufisadi wa raslimali za umma, ubakaji wa demokrasia, uminywaji wa haki za raia, na maovu mengine mengi.. hakuna ustaarabu wowote hapo, ni uhayawani mtupu!
 
Anahitaji justice, tiba ya kwanza kumponya ni justice, kitu ambacho kwa Tanzania hii hawezi kukipata. Mtu aliywkufa akafufuka hana ha kupoteza.
Kwa hiyo anatafuta kifo au sijakuelewa? unaongea utasema unayaweza akianza kubanwa huko msianze kulia humu.
 
Kwani hao waliomteka na kumtupa pori la katavi hawakujua kama mungu yupo? Acha ufala we KIMA chawa mkubwa wewe kujipendekeza tuu mtoto wa kiume na teuzi hupewi, na sativa ashasema hataki ushauri wowote wa kima kama wewe.
Mkono wa sheria utamfikia popote pale alipo .huku Ninyi Mkiendelea kujificha kwa fake ID huku jukwaani.
 
Back
Top Bottom