Sauti za waliofukiwa na Ghorofa Kariakoo: "Tuko hai lakini tunateseka, tusaidieni tutakufa"

Sauti za waliofukiwa na Ghorofa Kariakoo: "Tuko hai lakini tunateseka, tusaidieni tutakufa"

20241117_053636.jpg
 
Ayo TV imeongea kwa njia ya simu na mtu aliyepo chini na wenzake tangu asubuhi Novemba 16,2024 ghorofa lilipoporomoka ambapo amesema yeye na wenzie 10 wapo hai lakini hali zao ni mbaya.


Pia, Soma: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Majeruhi 63 kati ya 70 waruhusiwa, uokozi bado unaendelea, zoezi halijasitishwa


"Tupo chini tupo 10 toka asubuhi, tuko upande wa Don Touch, piga hata kwa Mama Samia, tuko toka jana,"

Kwa upande mwingine amesikika Mwanamke mmoja akisema wana hali mbaya.
View attachment 3154074
 
Daaaaaa nimeskiliza iyo video adi jasho linanitoka..
Kwanza uyo mtangazaji ni mpumbavu eti anauliza mnahaligani huko?
Watu wapo njia panda ya uhai na kifo yeye anauliza swali la kichoko.

Huo muda anaompotezea chaj kupga nae story ni ilibidi atafute kiongozi wa jeshi la uokoaji na mwenyeji wa mitaa iyo( anaejua maduka) Kisha uyo muhanga awape maelezo wapo chini sehem gani maana naona alitaja upande waliopo adi jina la duka..
Na wangepata content km kawaida ya muokozi akiongea na muhanga sio mtangazaji aongee na muhanga..

Hao watu kadri muda unavyozidi kwenda miili inaishiwa nguvu wapo wengi na wanapambania hewa(oxygen) kidogo sana inayopenya huko, mwsho ataanza kuzima mmoja mmoja😭😭😭😭.

Hadi nawaza au sjui waandishi wanapenda kutangaza vifo kuliko manusura??
Taarifa alizotoa mhanga zinatosha kabisa kumfanya msikilizaji yeyote anaejua hilo eneo akapafahamu wahanga walipo.Huo muda wa kumtafuta muokoaji ndio asikilize maelezo una uhakika simu ingeendelea kuwa hewani?Ingekata chaji?Tuache kukosoa kila kitu. Mwandishi ametekeleza wajibu wake ipasavyo. Hawa watu kumi wakiokolewa hizi ni moja kwa moja juhudi binafsi na ubunifu wa mwandishi. Sisi kazi yetu kukosoa tu tukiwa nyuma ya keyboard.
 
Kama jengo halijabomoka pande Zote watu wa kikosi Cha uokoaji wangetafuta namna ya kupata vifaa watoboe vimashimo vidogo vidogo ktk kila jengo Kwa ajili ya kusaidie kuwaingizia hewa wahanga walioko ndani ya jengo na kupitia hayo vinafasi waingize maji Yale madogo madogo Kwa ajili ya wahanga
 
So sad,Mungu awape neema wawe salama na watoke katika hali ya afya njema Nachukua nafasi hii kuwapa pole wale wote waliopatwa na janga hili na walipoteza maisha wapate pumziko la amani
 
Mimi usingizi umeshindikana kbs Kwa Leo!Kuna yule dada Instagram anaitwa bintimohammed28 ameniliza Kwa jinsi walivyo banwa!Hivi ule muda waziri mkuu anapoteza kuhutubia si ungefaa kuendelea na kazi?Yaan mtu anakuja kwenye majanga badala apige kazi ndio kwanza anakuja na msafara wa maV8 na kupoteza muda tu!Tunaongozwa na watu wa ajabu sana
Ilipaswa na yy awe kwenye magwanda ya uokozi kuhamasisha. Hakuna point ya kuhutubia tena uhai na uchovu wa mwili ausubiri kwa watu walionaswa.
 
Ayo TV imeongea kwa njia ya simu na mtu aliyepo chini na wenzake tangu asubuhi Novemba 16,2024 ghorofa lilipoporomoka ambapo amesema yeye na wenzie 10 wapo hai lakini hali zao ni mbaya.


Pia, Soma: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Majeruhi 63 kati ya 70 waruhusiwa, uokozi bado unaendelea, zoezi halijasitishwa


"Tupo chini tupo 10 toka asubuhi, tuko upande wa Don Touch, piga hata kwa Mama Samia, tuko toka jana,"

Kwa upande mwingine amesikika Mwanamke mmoja akisema wana hali mbaya.
View attachment 3154074
Dah,ya Allah watilie wepesi waja wako wapate kuokolewa salama watoke kwenye ilo janga lililowafika huko chini ya vifusi, kwa hakika baada ya uzito upo wepesi inshall'ah
 
Leo nimesema silali, nawaombea wawe hai. Ninalia, namshukuru Mungu kuwa wako hai kweli 🙏
Jamani kila mmoja kwa Imani yake, tuwaombee. Wako wamechoka, kiu, hewa hakuna, giza na hofu. 💔

Mimi naona watu wengi, watakuwa pale kushoto kwenye kifusi kikubwa. Kama hatuwezi uwokozi, tungeomba hata mataifa mengine, waje waokoe jahazi. Wana vifaa na watu wenye uzoefu na majanga ya aina hii. Tufanye chochote, waokolewe. Tuna la kujifunza, tuwekeze vifaa vya kisasa vya uokozi, tuache kununua magari ya anasa serikalini.
CCM hawana hiyo akili. Akili zao ni kununua mashangingi na magoli ya Simba na Yanga.
 
Idara ya zima moto na uokoaji, haina vifaa vya kufanya uokoaji. Crane kubwa na zenye nguvu zinahitajia eneo la tukio kuinua nguzo nzito zilizolaliana, Bulldozers za kutosha zifike eneo la tukio ziweze kuzoa kifusi, pia tunahitaji malori makubwa ya kubeba mchanga ili kuondoa vifusi eneo la tukio ili kurahisisha zoezi la uokoaji.

Tunahitaji kituo cha kuchukuli na kutolea taarifa, na tunahitaji kituo cha huduma ya kwanza chenye wahudumu wa kada zote za afya wanaohitajika kwenye majanga, na ambulace za kusafirisha wagonjwa kupelewa hospitali kwa waokolewaji.

Mwisho Jeshi la polisi lifukuze watu eneo la tukio au lipange utaratibu wa namna ya kufanya uokoaji kwa kushirikiana na wataalamu wa majanga, majengo ili kuzuia hatari kwa waokoaji na waokolewaji.

Mlundikano wa watu eneo la tukio bila utaratibu mzuri ni tatizo kwenye eneo la uokoaji, iwe majini au nchi kavu. Kuna paswa kuwe na utaratibu mzuri ili kufanikisha zoezi husika.

Watanzania waeleweshwe, hili ni tatizo siyo movie kila mtu anapaswa kushuhudia.

Wananchi wakae mbali, wachaguliwe watu wenye afya na uwezo wa kusaidia tu, wanawake na watoto wakae mbali.
Wananchi wameokoa watu wengi kuliko hao unaowaita Wataalamu.
 
Inshu ni namna tunavyodili na matatizo,kama nchi bado kuna tatizo sana hasa yanapotokea majanga,just imagine jana kuna watu walijitolea tu kuwaokoa wenzao..kana kwamba vyombo husika havipo..na hata walipofika ilikua ni kuanza kuhutubia wanachi kwanza badala ya kuwahi kuokoa.
 
Back
Top Bottom