ERoni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2013
- 48,052
- 104,677
Nakubaliana na wewe kwamba serikali iwekeze sana kwenye mbinu za uokozi, majanga kama haya yanakuja kwa namna tofauti tofauti hivyo mbinu tofauti zinahitajika ili kuwaezesha waokozi, pamoja na hayo serikali inches kuwekeza kwenye mambo yasiyo ya msingi, vifaa vya kisasa ni muhimu, posho na maslahi kwa watu wanaofanya hizo kazi pia.Hilo jengo la Kariakoo halijaporomoka kutokana na sababu za kuwepo kwa tetemeko la Ardhi..
Anyway, Ukweli unabaki kuwa Serikali inapaswa kuwa na taasisi imara na madhubuti kabisa za kuweza kupambana na majanga mbalimbali kama haya. Taasisi hizo zinapaswa kuwezeshwa kikamilifu kwa Mafunzo ya Utayari wa Kupambana na Majanga sambamba na kuwezeshwa kwa Vifaa vya Uokozi kwa ajili ya utayari wa kupambana na majanga mbalimbali.
Wananchi nao pia wapewe mafunzo ya utayari wa kuweza kupambana au mafunzo ya mbinu za kuweza kujihami na majanga mbalimbali, Mamlaka zinazohusika na masuala ya kupambana na majanga ziwe zinatoa mafunzo ya namna hii kwa umma.
Aidha, Watu wote waliozembea na kusababisha ajali hii huko Kariakoo wanapaswa kuwajibishwa kwa kufikishwa Mahakamani kwa makosa ya kusababisha vifo vya Watu kwa makusudi. Uwazi unatakiwa sana kwenye suala hili. Wahusika wafikishwe Mahakamani na wawajibishwe. Wafuatao ni Watu wa kuanza nao:-
1.Mmiliki wa Jengo.
2. Mhandisi wa Ujenzi Manispaa ya Ilala, pamoja na Maafisa wengine wote kabisa waliohusika na mchakato wa Kutoa Kibali cha Ujenzi na/au Ukaguzi wa Jengo.
3. Contractor.
4. Consultant.
5. Wahusika wa Usalama Mahali pa kazi (OSHA).,n.k, n.k.
Lakini pamoja na hayo, bado tukumbuke hilo ni janga kama majanga mengine, ni ngumu sana kufukua vifusi ndani ya 72hrs na kuweza kuokoa watu walifukiwa, kwa kiasi fulani kama kuna vifaa wanaweza kupunguza ila sio rahisi na wala tusiwe watu wa kulalamika kuwa kwa nini kwa nini...