John Wickzer Mulholland
JF-Expert Member
- Apr 13, 2023
- 6,656
- 14,403
Ni ngumu mkuu,
Ukisema utumie machinery, unaweza kuua watu zaidi maana linaweza kuporomoka zaidi. Ukisema ufukue taratibu kuna watu wanakosa hewa ndani na wanahitaji uokozi wa haraka. Sio rahisi hata kidogo.
Kifusi kingewezekana kabisa kufukuliwa kwa muda mfupi, tatizo lililokuwepo ni kwamba hapakuwa na mpaka Sasa bado Hakuna taasisi imara iliyo madhubuti yenye Utayari na nyenzo sahihi za kuweza kupambana na majanga Kama hayo. Hakuna watu/waokozi wenye mafunzo sahihi ya kushughulikia majanga ya namna hiyo na Wala Hakuna nyenzo au vifaa sahihi kwa kazi ya uokozi wa namna hiyo.Nakubaliana na wewe kwamba serikali iwekeze sana kwenye mbinu za uokozi, majanga kama haya yanakuja kwa namna tofauti tofauti hivyo mbinu tofauti zinahitajika ili kuwaezesha waokozi, pamoja na hayo serikali inches kuwekeza kwenye mambo yasiyo ya msingi, vifaa vya kisasa ni muhimu, posho na maslahi kwa watu wanaofanya hizo kazi pia.
Lakini pamoja na hayo, bado tukumbuke hilo ni janga kama majanga mengine, ni ngumu sana kufukua vifusi ndani ya 72hrs na kuweza kuokoa watu walifukiwa, kwa kiasi fulani kama kuna vifaa wanaweza kupunguza ila sio rahisi na wala tusiwe watu wa kulalamika kuwa kwa nini kwa nini...
Kuna uzembe uliopitiliza kwenye suala hili.
Mathalani, hivi kwa mfano AMRI ingetolewa haraka mara tu ajali ilipotokea ya kuwaleta Wanajeshi wapatao elfu Moja (1000) kwa ajili ya kazi hiyo ya Uokoaji, Je, kweli kwamba kifusi cha jengo hilo tangu ajali ilipotokea hadi leo hii tarehrle 22 Novemba 2023 kingekuwa bado tu hakijaisha??
Vile vile, vifo vya Watu wengi kwenye jengo hilo inaonekana vilisababishwa na ukosefu wa hewa safi (suffocation), jaribu kujiuliza: Je, Serikali ilikuwa na mipango gani ya dharula ili kuhakikisha kwamba Watu waliokuwa chini kwenye basement floor wanapatiwa hewa safi ili wasife kwa kukosa hewa huku zoezi la uokozi likiwa linaendelea? Je, uliona Serikali ilileta mitungi ya kuzalisha gesi ya Oxygen ya dharula hapo kwenye eneo la ajali ili kuwapatia hewa safi Waathirika wa janga hilo waliokuwepo chini ya vifusi kwenye basement floor??
Hosea 4:6
Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa.