Seba aliyeandika meseji kwa rafiki yake amtunzie mwanae na anakata roho kwenye ghorofa ya Kariakoo lililoanguka, akutwa amefariki

Seba aliyeandika meseji kwa rafiki yake amtunzie mwanae na anakata roho kwenye ghorofa ya Kariakoo lililoanguka, akutwa amefariki

Hivi kumbe Wanajeshi kazi zao zote huwa ni za kutumia nguvu tu peke yake bila akili??
Hilo eneo halikuhitaji watu elfu moja kwanza ni eneo lililokua linahitaji kuwepo na hewa ili watu waliofukiwa wapate Oxygen, alafu kitendo cha kujaza watu elfu moja kama unavyotaka ni hatua nyingine ilikua inaenda kuhatarisha uhai wa watu, kazi isingefanyia kwa uangalifu, narudia tena ni eneo lililokua linahitaji akili na siyo nguvu, kama Front loader zipo za kutosha wangehitaji nguvu kifusi kingezolewa ndani ya siku 1 ila asingetoka hata mmoja hai
 
Its painful 😣

Hiv kam jengo moja ndio limeanguk tena ndan ya jiji kubwa na karbu krbu na fire (waokozi) lakn zoez la ukoaji watu halijakamilika itakuwaje siku magorofa 5/20 yakiangukia watu huko mikoa ya pembezon 😐😐
Jengo moja siku 10..
Majengo 10 = siku 100.
Survival chance ni 0.0% kwa siku 100 undergroud.
 
Hilo eneo halikuhitaji watu elfu moja kwanza ni eneo lililokua linahitaji kuwepo na hewa ili watu waliofukiwa wapate Oxygen, alafu kitendo cha kujaza watu elfu moja kama unavyotaka ni hatua nyingine ilikua inaenda kuhatarisha uhai wa watu, kazi isingefanyia kwa uangalifu, narudia tena ni eneo lililokua linahitaji akili na siyo nguvu, kama Front loader zipo za kutosha wangehitaji nguvu kifusi kingezolewa ndani ya siku 1 ila asingetoka hata mmoja hai
Je, kwenye hiyo comment yangu ya awali uliyonukuu hukuona kwamba nimegusia suala la kuletwa Mitungi ya Gesi za Oxygen kwa ajili ya kuwapatia hewa safi Watu waathirika waliokuwepo chini ya jengo kwenye basement floor? Ni kweli kwamba haukuona kitu hicho nimeeleza kwenye comment yangu hiyo?
 
Deep sorrow!

But all in all, vifo vya Watu hawa kamwe havikusababishwa kwa kudra ya Mungu, Bali ni kutokana na kuwepo kwa janga la rushwa, uzembe wa makusudi, ufisadi na kushindwa kuwajibika ipasavyo.
Vifo vingi nchini ni uzembe wa siasa na mfumó wa uongozi Tanzania. Wakulaumiwa ni Nyerere (mnayemuita baba wa Taifa) alieruhusu janga hili ccm iendelee kwenye mfumo wa vyama vingi. Ilitakiwa ccm ife ipotee kwa sababu ni chama dola kilichokuea na matawi mpaka jeshini[ yaani majeshi yote na watu wote katika usalama wa Taifa walikuwa ccm],
katiba mpya ingeanzishwa na vyama mbadala vipya kukiwa na masharti laini kwa wanachama.
Sio eti viongozi wote lazima wawe ccm. Najua wachache sn watanielewa, machawa wata-dislike. Waliruhusu vyama vingi wakijua kuna namna ya kuviangamiza
 
Apumzike kwa amani
Kijana Seba aliyeandika message kwa rafiki yake amtunzie mwanae na anakata roho siku mbili zilizopita.

View attachment 3158342

Mwili wake umeopolewa mda huu ukiwa tayari umeshaanza kuaribika kwenye jengo la Kariakoo.. Tayari mwili wake umepelekwa kwenye hospitali ya Amana kwa kwa taratibu nyingine za kuhustili..Roho ya marehemu ipumzike mahara pema peponi 😭😭 Inasikitisha sana jamani Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un💔🙏
 
Hilo jengo la Kariakoo halijaporomoka kutokana na sababu za kuwepo kwa tetemeko la Ardhi..
Anyway, Ukweli unabaki kuwa Serikali inapaswa kuwa na taasisi imara na madhubuti kabisa za kuweza kupambana na majanga mbalimbali kama haya. Taasisi hizo zinapaswa kuwezeshwa kikamilifu kwa Mafunzo ya Utayari wa Kupambana na Majanga sambamba na kuwezeshwa kwa Vifaa vya Uokozi kwa ajili ya utayari wa kupambana na majanga mbalimbali.

Wananchi nao pia wapewe mafunzo ya utayari wa kuweza kupambana au mafunzo ya mbinu za kuweza kujihami na majanga mbalimbali, Mamlaka zinazohusika na masuala ya kupambana na majanga ziwe zinatoa mafunzo ya namna hii kwa umma.

Aidha, Watu wote waliozembea na kusababisha ajali hii huko Kariakoo wanapaswa kuwajibishwa kwa kufikishwa Mahakamani kwa makosa ya kusababisha vifo vya Watu kwa makusudi. Uwazi unatakiwa sana kwenye suala hili. Wahusika wafikishwe Mahakamani na wawajibishwe. Wafuatao ni Watu wa kuanza nao:-
1.Mmiliki wa Jengo.
2. Mhandisi wa Ujenzi Manispaa ya Ilala, pamoja na Maafisa wengine wote kabisa waliohusika na mchakato wa Kutoa Kibali cha Ujenzi na/au Ukaguzi wa Jengo.
3. Contractor.
4. Consultant.
5. Wahusika wa Usalama Mahali pa kazi (OSHA).,n.k, n.k.
HATUWEZI KUACHA KUIMARISHA VIKUNDI VYA KUMSIFU CHURA KIZIWI ETI ILI TUFANYE HAYO UNAYOTAKA,HAYO FANYA WEWE.
 
Deep sorrow!

But all in all, vifo vya Watu hawa kamwe havikusababishwa kwa kudra ya Mungu, Bali ni kutokana na kuwepo kwa janga la rushwa, uzembe wa makusudi, ufisadi na kushindwa kuwajibika ipasavyo.
Mfumo ovu na wakishetani chini ya CCM ndiyo chanzo cha vifo hivyo.

Kuna mahali Mkuranga huko nilipita nikaona wamama na watoto migongoni wamejazana nnje ya duka la dawa,nilipouliza kunani, nikaambiwa wanatibiwa.

Nikamuuliza huyo mwenyeji,wamatibiwaje kwenye duka la dawa muhimu ( DLDM)!!??
Uongozi wa mtaa unajua, nikaambiwa wanapelekewa fungu lao mpaka Wilayani na Halmashaurini.
 
Its painful 😣

Hiv kam jengo moja ndio limeanguk tena ndan ya jiji kubwa na karbu krbu na fire (waokozi) lakn zoez la ukoaji watu halijakamilika itakuwaje siku magorofa 5/20 yakiangukia watu huko mikoa ya pembezon 😐😐
Raia wa gaza wakituona watashangaa sans
 
Back
Top Bottom