Sera ya Elimu Bure ni mtaji wa kisiasa unaopunguza uwajibikaji kwa wananchi

Sera ya Elimu Bure ni mtaji wa kisiasa unaopunguza uwajibikaji kwa wananchi

G.Man

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2014
Posts
1,040
Reaction score
2,157
Mambo vipi,

Moja kwa moja kwenye mada. Juzi nikiwa kwenye daladala nikasikia watu wakilaumu Serikali kwamba ''Heri Magufuli alivyo kuwepo, saivi watoto wametakiwa kulipa michango ya kama 22k shuleni'', sikuweza kuchangia neno lakin niliwaza sana, Seriously! mchango kama huo kwa mwaka kwaajili ya mwanao kupata elimu unaonekana ni uonevu!

Naishauri Serikali kama ina nia njema ya kuwapa wananchi maendeleo ya Kifikra bila kuangalia mtaji wa kura, irudishe ada shuleni na kutumia hizo pesa kuboresha mifumo ya kielimu kama kuajiri walimu wa kutosha. Kulikoni mpaka leo kuendelea kutegemea mikopo na wahisani hata kujenga vyoo. Tunabembelezana sana kwenye mambo ya msingi kisa tu wanasiasa wanataka Kura. Nafahamu kuwa zipo kaya Masikini sana lakini kunaweza kukawa na mpango maalumu kwa ajili ya watu kama hao.

Kuna wakati nilimsikia Waziri wa TAMISEMI akisema wanafunzi waruhusiwe kwenda shule bila Uniform.! Siku nyingine hawa si watasema hawana kalamu alafu waambiwe hata wasipoandika hamna shida?! Sasa kwa hali kama hiyo kwanini serikali isichukue tu ada alafu wa provide wenyewe Uniform na vitendea kazi kama madaftari?

Hivi wale watoto wanaolipiwa 30mil kwenye International Schools ndo unataka wawe na soko sawa la ajira na wanetu hawa wa kajamba nani?

Si bure tunasoma ili tu kuhitimu na ndio maana hatuna uwezo wa kufikiri kwa kina na kuhoji mambo yanayohitaji uwezo mdogo tu wa akili, zaidi tunafata mkumbo.

Mungu atusaidie!
 
'Every time your mind shifts, your World shifts'
 
Wakati wa miaka ya katikati ya 1980 serikali hii hii ya CCM ilishauriwa na IMF iachane na suala la kutoa huduma za kijamii bure ili iweze kuimarisha uchumi wake. Chini ya "Stractural Adjustment Programs (SAPs) serikali ikakubaliana na ushauri huu.

Baada ya ushauri huo kukubalika, huduma muhimu za kijamii kama vile afya na elimu zilikaanza kulipiwa na watu, huku serikali ikiendelea kuwekeza zaidi katika miundombinu ya kimkakati. Lakini cha ajabu zaidi tulipofika mwaka 2015 serikali ile ile ya CCM ikaamua kuanza kutoa elimu ya msingi bure, kisa eti suala hili liliwapa CDM kiki katika ilani yao ya uchaguzi wa mwaka 2010.

Kurukia gari moshi kwa mbele likiwa katika mwendo ni uamuzi wa kukurupuka na kiubabaishaji. Ikiwa elimu ya juu inatolewa kwa mikopo, inashindikana nini pia kaa elimu ya msingi kutolewa kwa mkopo!?

Ni dhahiri kabisa maadui wakuu wa maendeleo katika awamu ya kwanza ya utawala wa nchi yetu waliokuwa ni ujinga, maradhi na umaskini. Lakini naona sasa imefanyika "U-turn" na badala yake serikali ya CCM ina "capitalize" katika hayo ili iendelee kubakia madarakani kwa gharama yoyote ile.

Kumsaidia mtoto wa maskini asome bure, unamfanya mzazi wake azidi kuzaa watoto zaidi, aongeze idadi ya wake, apate kipato cha kunywa pombe za kienyeji, na zaidi ya yote azidi kubakia na kubobea ndani ya "vicious circle of poverty"
 
Wakati wa miaka ya katikati ya 1980 serikali hii hii ya CCM ilishauriwa na IMF iachane na suala la kutoa huduma za kijamii bure ili iweze kuimarisha uchumi wake. Chini ya "Stractural Adjustment Programs (SAPs) serikali ikakubaliana na ushauri huu.

Baada ya ushauri huo kukubalika, huduma muhimu za kijamii kama vile afya na elimu zilikaanza kulipiwa na watu, huku serikali ikiendelea kuwekeza zaidi katika miundombinu ya kimkakati. Lakini cha ajabu zaidi tulipofika mwaka 2015 serikali ile ile ya CCM ikaamua kuanza kutoa elimu ya msingi bure, kisa eti suala hili liliwapa CDM kiki katika ilani yao ya uchaguzi wa mwaka 2010.

Kurukia gari moshi kwa mbele likiwa katika mwendo ni uamuzi wa kukurupuka na kiubabaishaji. Ikiwa elimu ya juu inatolewa kwa mikopo, inashindikana nini pia kaa elimu ya msingi kutolewa kwa mkopo!?

Ni dhahiri kabisa maadui wakuu wa maendeleo katika awamu ya kwanza ya utawala wa nchi yetu waliokuwa ni ujinga, maradhi na umaskini. Lakini naona sasa imefanyika "U-turn" na badala yake serikali ya CCM ina "capitalize" katika hayo ili iendelee kubakia madarakani kwa gharama yoyote ile.

Kumsaidia mtoto wa maskini asome bure, unamfanya mzazi wake azidi kuzaa watoto zaidi, aongeze idadi ya wake, apate kipato cha kunywa pombe za kienyeji, na zaidi ya yote azidi kubakia na kubobea ndani ya "vicious circle of poverty"
Tunadekezana sana bila kujua kuwa tunajichimbia shimo
 
Serikali imefanya wazazi wawe wazembe kupindukia, ili mzazi awe na uchungu wa elimu kwa mtoto wake ni lazima turudishe ada shuleni, tena iwe 40000/ kwa mwaka. Wazazi wamekaa kizembezembe sana.
 
Serikali imefanya wazazi wawe wazembe kupindukia, ili mzazi awe na uchungu wa elimu kwa mtoto wake ni lazima turudishe ada shuleni, tena iwe 40000/ kwa mwaka. Wazazi wamekaa kizembezembe sana.
Viongozi wanawaza kura, lakin sio maslahi mapana ya taifa
 
Wakati wa miaka ya katikati ya 1980 serikali hii hii ya CCM ilishauriwa na IMF iachane na suala la kutoa huduma za kijamii bure ili iweze kuimarisha uchumi wake. Chini ya "Stractural Adjustment Programs (SAPs) serikali ikakubaliana na ushauri huu.

Baada ya ushauri huo kukubalika, huduma muhimu za kijamii kama vile afya na elimu zilikaanza kulipiwa na watu, huku serikali ikiendelea kuwekeza zaidi katika miundombinu ya kimkakati. Lakini cha ajabu zaidi tulipofika mwaka 2015 serikali ile ile ya CCM ikaamua kuanza kutoa elimu ya msingi bure, kisa eti suala hili liliwapa CDM kiki katika ilani yao ya uchaguzi wa mwaka 2010.

Kurukia gari moshi kwa mbele likiwa katika mwendo ni uamuzi wa kukurupuka na kiubabaishaji. Ikiwa elimu ya juu inatolewa kwa mikopo, inashindikana nini pia kaa elimu ya msingi kutolewa kwa mkopo!?

Ni dhahiri kabisa maadui wakuu wa maendeleo katika awamu ya kwanza ya utawala wa nchi yetu waliokuwa ni ujinga, maradhi na umaskini. Lakini naona sasa imefanyika "U-turn" na badala yake serikali ya CCM ina "capitalize" katika hayo ili iendelee kubakia madarakani kwa gharama yoyote ile.

Kumsaidia mtoto wa maskini asome bure, unamfanya mzazi wake azidi kuzaa watoto zaidi, aongeze idadi ya wake, apate kipato cha kunywa pombe za kienyeji, na zaidi ya yote azidi kubakia na kubobea ndani ya "vicious circle of poverty"
Hii elimu bure ni moja ya Sera za kipuuzi sana na tunabebeshana mizigo kwenye tozo bila sababu yeyote.

Kiukweli mie nahangaika wanangu wasome shule nzuri sana na alhamdulillah so Hana. Ila hii kutulipisha tozo ili wengine waliobweteka tuwasomeshee watoto wao bure kabisa naona haiwezekani kabisa.

Moja ya mambo yanayochangia umasikini ni hii elimu bure, mtu anaona mzigo wa kusomeshwa Hana anaamua kuzaa tu Kama kuku hajali.

Ukikaa na watu tunaosomesha watoto kwa shule za gharama utaona kabisa mtu anapiga hesabu ya watoto wakiwa wengi sana no wanne. Jaribu kupiga hesabu mtoto anasoma Ada kwa mwaka mzima ni milioni 5.7 hujaweka makorokocho mengine humo plus mahitaji yake binafsi huwezi kufikiria kubweteka hata kidogo lakini Kama mtoto anaenda shule ya mguu, halipo Ada Yani anakula jioni akirudi huna gharama yeyote ukiweka uniform na viatu kwa mwaka humalizi elfu 30 unatarajia nini?

Hiyo inawafanya wanaongeza watoto bila kujua wanaongeza umasikini maana huyu mtoto alimaliza la Saba anarudi kulima apambane kujitoa kwenye vicious cycle of poverty na Kama wa kike anaona akiolewa atakuwa amejikomboa kukaa kwa wazazi ndio imeisha hiyo hakuna kipya.

Nakubaliana na wanaosema hii elimu bure ni kutengeneza umasikini maana tunashushana kimapato unanikata tozo ambayo unaenda kumsomesha kijana ambaye akifika la saba Hana mpango wa kuendelea na masomo sababu mzazi wake ana watoto 11 na wote wanasoma elimu bure sasa ikifika juu hawezi kuwasomesha maana hajazoea huo utaratibu wa kukusanya hela kwa ajili ya Ada ya mtoto.
 
Ccm wana sera ya Ujamaa wa kinafiki sana! Wanajifanya kutoa elimu bure kwa Watanzania, halafu watoto wao wanawapeleka kusoma shule za kulipia, na zenye gharama kubwa!

Wako busy kujenga madarasa, lakini huwezi kusikia huo ujenzi ukienda sambamba na utoaji wa maelfu ya ajira za ualimu kwa watoto wa maskini ili wakawafundishe maskini wenzao!

Chama cha hovyo kabisa!
 
Ccm wana sera ya Ujamaa wa kinafiki sana! Wanajifanya kutoa elimu bure kwa Watanzania, halafu watoto wao wanawapeleka kusoma shule za kulipia, na zenye gharama kubwa!

Wako busy kujenga madarasa, lakini huwezi kusikia huo ujenzi ukienda sambamba na utoaji wa maelfu ya ajira za ualimu kwa watoto wa maskini ili wakawafundishe maskini wenzao!

Chama cha hovyo kabisa!
Hakuna nia ya dhati ya kukomboa fikra za wananchi
 
Habari,

Baada ya pendekezo hilo kufuatwa, wananchi walianza kulipia huduma muhimu za kijamii kama vile afya na elimu, huku serikali ikiendelea kuwekeza katika miundombinu muhimu. Hata hivyo tulipofika 2015, utawala huohuo wa CCM ulichagua kuanza kutoa elimu ya msingi bure, kesi ambayo inasemekana iliwaingizia CDM kiki kwenye jukwaa lao la uchaguzi wa 2010.
real estate istanbul
 
Back
Top Bottom