Serikali acheni kujifanya hamtuoni wahitimu, tupeni ajira, hali ni mbaya mtaani

Serikali acheni kujifanya hamtuoni wahitimu, tupeni ajira, hali ni mbaya mtaani

umenena vyema. Kunawatu sio wahitimu wa vyuo( vya Kati wala vikuu) wapo mtaani maisha yanasonga.
Ila wasomi wetu( wahitimu) wanalalama kila uchwao.
Inawezekana vyeti vyao ni leseni ya kuilaumu Serikali na ambao hawajaenda chuo leseni hiyo hawana ndio maana wamekaa kimya.
Wana haki ya kulalamika unajua kwanini, psychology ni kitu very strong wala sio jambo la kuli overlook!

Toka umezaliwa ukajitambua unamuona baba anaamka asubuhi anawasha pikipiki au gari anaenda kazini. Au anafatwa na gari kila asubuhi. Ukipeleleza unaambiwa baba yako ni mhasibu anafanya kazi bandarini baba yako ni msomi, ukicheki kwa wajomba system ni hio hio, baba wadogo system ni hio hio.

Mama unayeshinda nae muda mwingi anakwambia ukianza shule usome ili upate ajira nzuri kama kaka yako si unaona anajenga nyumba yake sahizi. Its been a recurring statement for years na kweli unaona kaka na dada zako wamesoma wakamaliza shule wakapata kazi na maisha wana full control mara paap wana magari mara wameoa life linaendelea wana kila wanachokitaka kupitia kazi.

Katika situation kama hii hiki kitu kimejengeka kwenye saikolojia ya mtoto toka mdogo kwamba kumbe the right path ni kusoma kwa bidii! Inafikia wakati mtoto ametimiza wajibu wake vizuri kashakuwa mtu mzima sasa muda wa kupata ajira ili nae aanze kumenye ghafla hajira hazipo? Omba huku na kule hola serikali haitoi ajira.

Hivi unafikiri ni jambo jepesi kumwambia mtu wa hivi ajiajiri? Wengine hata talanta ya kuuza pipi hawana ghafla umwambie eti ajiajiri maanake aanze kuuza ice cream na karanga barabarani kitu ambacho hakikuwahi kupita hata kwa bahati mbaya kichwani mwake? Hii ni kansa ambayo matibabu yake ukifosi kuiunguza umeua mgonjwa straight away!

Mtu kasoma ili afanye kazi ofisini hati ghafla ajiria hamna easily tu mkajiajiri vijana?
 
Waziii mkuu.

Yaani Mimi huwa nashangaa, mtu ana miaka zaidi ya sitini lakini bado yupo ofisi fulani!!! eti yeye ni mzoefu kwahiyo hakuna haja ya replacement, mtu akifikisha miaka sitini Kama ilivyo kwa watumishi wengine basi astaafu apishe wengine.

Kuna lingine unakuta mtu alikuwa mbunge kipindi fulani, baadaye huyohuyo anakuwa DC mahali fulani, akitoka huko utasikia mara RC mahali, haitoshi utasikia balozi mahali fulani, kumbe huyu alipokuwa mbunge alitumikia taifa na kula cake yake kabisa, Basi uDC apewe mwingine.

Mwisho, kuna hili la watu wa ukoo fulani wenyewe ndo viongozi miaka yote, anatoka babu anamwachia mwanae, mwanae naye anamwachia mjukuu wa babu.

Kama taifa lazima tuyaangalie mambo haya, hili taifa ni la watanzania wote.
Hivi vipengele nilishawahi kutoa muongozo wa katiba uweje miongoni mwa mapendekezo lilikuwa hilo la utaratibu wa kurithishana madaraka.

Maana familia zile zile ndio zinazungukia kwenye system ya nchi. Wazee kwa watoto kama vile watanzania wengine hawana haki. Hili lazma lifanyiwe mabadiliko kisheria.
 
Kwa maisha ya sasa hapa bongo, Ili uwe tajiri inabidi uwe mbele ya muda na ili uwe mbele ya muda inabidi uwe tayari kupita njia za panya ilimradi utoboe...hilo ndio somo wengi tunachelewa kulipata hakuna tena maisha ya mstari ulionyooka eti usome chuo, ufaulu,uajiriwe , upige kazi, upande daraja, ustaafu....hayo maisha hayapo tena
Kweli nafikiria ni kuvaa mabomu tu mzee maana hamna namna! Yani maisha yamekaa kisengelenyuma sana mkuu!

Kuna haja ya ku temper na system maana ukiifata system haikupi matokeo instantly. Get rich or Die Trying ndio falsafa ambayo pengine itatuokoa vijana wa leo.
 
Mkuu naona kama unamfokea mdau!

Embu twende pole pole sababu tunajadili jambo la muhimu hapa.

Kudai kitu kama haki, ni lazima uwe na kifungu cha sheria unanukuu kusapoti hoja yako.

Kuandika tu bila kunukuu kifungu chochote cha sheria kinachoilazimisha serikali kukupa haki unayoidai, nami nitasema ni malalamiko yasiyo na mashiko.

Uzi wako una point za msingi sana, isipokuwa umeuandika kibaguzi saazingine kwa kujua ama bila kujua.

Ipo hivii: kundi lenu la vijana wa kTz mnaochipuka kila mwaka ambao ndiyo nguvu kazi inayotegemewa ni kubwa sana.

Kuna waliomaliza vyuo na wengine kuishia elimu ya chini ambao sijasikia mahali popote ukiwasemea namna gani serikali imewaandalia kutumia nguvu kazi yao kujiletea maendelea yao na ya nchi kwa ujumla .

Je ni kweli kabisa kila mhitimu sheria inasema aajiriwe na serikali?

Je takwimu ya kila mwaka ya wasomi wanaozalishwa ni kiasi gani, inalingana na soko la ajira?

Je kama soko la ajira likiwa chini na idadi ya wahitimu ipo juu, serikali isitishe kusomesha watoto kwanza hadi waliomaliza masomo wapate ajira?

Je serikali isomeshe watoto kwa idadi ya nafasi za ajira zitakazo kuwepo nk nk?

Je ni nini kifanyike?

Ninajua ukijibu maswali haya, nitapata msingi wa kujadili hoja yako kwa hekima
idadi ya wahitimu waliopo mtaani ni kubwa kutokana na hali ya utoaji wa ajira iliyopo tangu mwaka 2015, to make it simple, chukua idadi ya wanao maliza kila mwaka kotoka vyuo vilivyosajiliwa na serikali katika ngazi ya cheti hadi elimu ya juu.

kuhusu sheria inayoitaka serikali kuajiri unaweza kuniambia ni kifungu gani cha sheria kilichotumika kuwaajiri waajiriwa waliopo makazini? ukishapata jibu la hapa utagundua kuwa ni wajibu wa serikali kusimamia raslimali za nchi na kuhakikisha zinawafaidisha wanachi katika nyanja mbali mbali ikiwepo kutoa ajira kwa wale walio na taaluma kama sehemu ya kurudisha kodi iliyokusanywa kwa wananchi.

kuhusu ambao wameishia ngazi za chini, sijawabagu ila ni kwamba katika andiko langu nimekusudia kupaza sauti ya wahitimu, nao wanayo nafasi ya kupaza sauti zao, uzi mmoja hautoshi kuwasemea wadau wote walio waathirika wa elimu

kuhusu kufuta shule, si busara, ila kinachotakiwa ni kubadilisa mfumo wa elimu uliopo ili kumsaidia mwanafunzi aweze kukabiri mazingira kupitia taaluma anayoipata akiwa shule, kwani mfumo uliopo ni wa nadharia kwa asilimia zaidi ya 80 kuliko vitendo hii ni kwa maslahi mapana ya kizazi kilichopo na kijacho ikiwa serikali itaamua kufumbia macho suala la ajira kama ilivyofanya hivi sasa.

sijaweza kutoa takwimu mahususi kwa njia ya namba kwenye swala la idadi ya wahitimu waliopo mtaani lakini kwa faida ya wote kama taifa, unaweza kwenda kwenye mamlaka husika kuomba idadi hiyo ambayo ni kubwa sana, na kuileta hapa na hivyo kusaidia mjadala kuwa na mashiko zaidi.

tulijege taifa pamoja
 
Kweli nafikiria ni kuvaa mabomu tu mzee maana hamna namna! Yani maisha yamekaa kisengelenyuma sana mkuu!

Kuna haja ya ku temper na system maana ukiifata system haikupi matokeo instantly. Get rich or Die Trying ndio falsafa ambayo pengine itatuokoa vijana wa leo.
Kujilipua ndio njia iliyobaki, ndio maisha halisi ya soko la kibepari bora ufe katika harakati za kujaribu kujitoa kwenye umasikini vinginevyo tutaishia kupoteza muda na kuwa frustrated na mfumo tulioaminishwa ni sahihi wakati haupo tena...hizo ajira zenyewe zinazoliliwa ni mizinguo unakuta hela unayolipwa inaishia kutumika kama nauli na kununulia maji ili uendelee kupiga kazi, ukipata msala mdogo tu mpaka uanze kukopa na kuchangisha kwa majamaa na rafiki.
 
hizi siasa za kutuaminisha eti mnakopa ma trioni kwa ajili ya miradi ya maendeleo na kujifanya hamuoni hali zetu sisi tuliozingatia kitabu kama mlivyotuagiza ni uzandiki mtupu.

Leo hii tunaonekana kama mizigo kwa wazazi na ndugu nyie mko bize kulumbana kisa uchu wa madaraka, tunakoelekea tutakuwa tukikutana na viongozi tunapiga mawe mpaka kufa kama sheria za wayahudi wa zamani maana sheria mnazotunga zinawalinda wenyewe ili tusiwaguse, kuna faida gani kuendelea kuzalisha kundi la wasomi na kuwatelekeza.

Nchi ina gesi, madini, vivutio vya utalii, tozo, mikopo na misaada kibao, lakini wahitimu wanaachwa kana kwamba sio wale mnaowapa vipaumbele kwenye sera zenu wanapokuwa shuleni.

tufike mahali tuache kujisahau, fukuto la chuki mnalolijaza kwetu hakika halitawaacha salama.

"when I grow up I will carry a gun" remains my all time favourite line among the lines I have learned in school.

CCM is corrupt
CDM wana tamaa iliyokithiri ya uchu wa madaraka kiasi cha kulichukua fisadi eti wamelitakasa kuwawakilisha kwenye uchaguzi kisa lina upepo wa kisiasa
vyama vingine vya kisiasa, sio tu havina nguvu, vinatumika kama mitaji ya kisiasa kwa chama tawala.

Ndugu wahitimu, amkeni acheni kulia ndani ya moyo, wanatuambia tuigeuze elimu kuwa hela huku wao wakiwa wanategemea mishahara kupitia kodi zetu ni zaidi ya kututukana tena matusi ya nguoni.

kazi za wahitimu;
1)kuuza movie
2)kuuza liquid protector
3)kuuza pedi za kufua
4)kutumika madukani kwa ndugu na wazazi (wachache)
5)kujiuza (wanaita kudanga)
kuuza juice
6)kulima small scale agriculture kwa sababu ya mitaji midogo
7)wizi
na nyingine kibao ambazo hazina hadhi ya elimu waliyo nayo.

serikali ikitangaza ajira utasikia "awe na uzoefu kazini kianzia miaka miwili" kwa kazi gani mlizo tupatia? Hakika wanasiasa wametudharau sana ni wakati sasa wa kuwakataa na tamaa zao za kujifaidisha wao na koo zao.

"Mungu awatembelee mmoja baada ya mwingine, awafundishe kula kwa jasho kama watu wengine"_kwa sauti ya kala jeremiah.View attachment 2061370
Serikali gani duniani inaweza kutoa ajira kwa wahitinu wote?,acha ujinga pambana na hali yako

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Wana haki ya kulalamika unajua kwanini, psychology ni kitu very strong wala sio jambo la kuli overlook!

Toka umezaliwa ukajitambua unamuona baba anaamka asubuhi anawasha pikipiki au gari anaenda kazini. Au anafatwa na gari kila asubuhi. Ukipeleleza unaambiwa baba yako ni mhasibu anafanya kazi bandarini baba yako ni msomi, ukicheki kwa wajomba system ni hio hio, baba wadogo system ni hio hio.

Mama unayeshinda nae muda mwingi anakwambia ukianza shule usome ili upate ajira nzuri kama kaka yako si unaona anajenga nyumba yake sahizi. Its been a recurring statement for years na kweli unaona kaka na dada zako wamesoma wakamaliza shule wakapata kazi na maisha wana full control mara paap wana magari mara wameoa life linaendelea wana kila wanachokitaka kupitia kazi.

Katika situation kama hii hiki kitu kimejengeka kwenye saikolojia ya mtoto toka mdogo kwamba kumbe the right path ni kusoma kwa bidii! Inafikia wakati mtoto ametimiza wajibu wake vizuri kashakuwa mtu mzima sasa muda wa kupata ajira ili nae aanze kumenye ghafla hajira hazipo? Omba huku na kule hola serikali haitoi ajira.

Hivi unafikiri ni jambo jepesi kumwambia mtu wa hivi ajiajiri? Wengine hata talanta ya kuuza pipi hawana ghafla umwambie eti ajiajiri maanake aanze kuuza ice cream na karanga barabarani kitu ambacho hakikuwahi kupita hata kwa bahati mbaya kichwani mwake? Hii ni kansa ambayo matibabu yake ukifosi kuiunguza umeua mgonjwa straight away!

Mtu kasoma ili afanye kazi ofisini hati ghafla ajiria hamna easily tu mkajiajiri vijana?
Mambo yakibadilika inatakiwa mtu ndio abadilike ilikuendana na uhalisia.
Kusubiri mambo yabadilike yarudi kama zamani ama yawekama unavyowaza wewe( fantasy) huko nijitoa kafara bila agano.

Kwa ishu uliyoiweka mezani kwenye hii comment yako ipo sawa kabisa.
Ila ikumbukwe sio kila familia inabahati ama ilibahatika kuwa na mema ya aina hiyo kwa kuwa na ndugu ama wazazi waliopata ajira Serikalini na sehemu zozote zile zenye maana. Tuachane na hii kwa sababu sio moral of the story.
Kitu kikubwa ambacho kinatakiwa kifanyike kwa kijana uyo aliepigwa chuma kizito ni
Kubadilisha paradigm
Inatakiwa abadili mtazamo wake ( maisha, kipato, mafanikio) kutoka kwenye fantasy na kwenda kwenye uhalisi wa wakati ulipo mana mkeka wake ushachanika njia ya kupata ajira yakuridhisha moyo wake ni nyembamba sana.
Muhimu ni kurudi kwenye basics za maisha, yakutafuta mia 2 mia 2.
Muda mwengine kikubwa uhai🤣🤣😂
 
Mi nilishauri kipindi flani hizi kazi pia ziwe za mkataba sio za kudumu ambapo mtu anajiachia tu kwakuwa anajua ataondoka ofisini akiwa mzee [emoji28]!

Mikataba iwe ya muda mfupi 3-5 yrs kulingana na productivity na malipo yawe mazuri ili watu wakiondoka maofisini wakajiajiri mtaani maana wanaondoka na mitaji mizuri. Kuna watu wengi walipinga sana hili sababu ya kuprotect mkate wao eti ooh ufanisi utakuwa hamna sijui uzoefu utapatikana vipi? Training si zipo ama internsihip programs!

Mishahara iwe standardized tu kuendana na hali ya maisha na iwe flat kulingana na level ya elimu! Degree au zaidi wale 6M, Diploma 3M kila mwezi! Mtu akipiga 3 yrs lazma atakuwa ana pension nzuri tu ya kuendeleza maisha apishe wengine. Sio kumkalisha mtu miaka 60 ofisini kisha hataki kuondoka anaogopa moto wa mtaani[emoji28]ila ndio kinara wa kuwaambia watoto wa wenzie wajiajiri wakati yeye kamchomeka mwanae kwenye system.
Hii ni sahihi kabisa,ajira ziwe za muda mfupi na zenye ujira mzuri, ili wengine waingie kwenye system nao .Hata bungeni Iwe miaka 5 mtu anaondoka.
 
Hii ni sahihi kabisa,ajira ziwe za muda mfupi na zenye ujira mzuri, ili wengine waingie kwenye system nao .Hata bungeni Iwe miaka 5 mtu anaondoka.
hili linaweza kufanyika kuanzia ajira zijazo (if only zitatolewa) na kuendelea.

watu wanaopinga utasikia wanakuambia eti hakuna nchi iliyoendelea inayofanya hivi, sijui ni nani alitufunga akili na kutuambia kila kinachofanywa na nchi nyingine ni muafaka na kwetu.
 
hizi siasa za kutuaminisha eti mnakopa ma trioni kwa ajili ya miradi ya maendeleo na kujifanya hamuoni hali zetu sisi tuliozingatia kitabu kama mlivyotuagiza ni uzandiki mtupu.

Leo hii tunaonekana kama mizigo kwa wazazi na ndugu nyie mko bize kulumbana kisa uchu wa madaraka, tunakoelekea tutakuwa tukikutana na viongozi tunapiga mawe mpaka kufa kama sheria za wayahudi wa zamani maana sheria mnazotunga zinawalinda wenyewe ili tusiwaguse, kuna faida gani kuendelea kuzalisha kundi la wasomi na kuwatelekeza.

Nchi ina gesi, madini, vivutio vya utalii, tozo, mikopo na misaada kibao, lakini wahitimu wanaachwa kana kwamba sio wale mnaowapa vipaumbele kwenye sera zenu wanapokuwa shuleni.

tufike mahali tuache kujisahau, fukuto la chuki mnalolijaza kwetu hakika halitawaacha salama.

"when I grow up I will carry a gun" remains my all time favourite line among the lines I have learned in school.

CCM is corrupt
CDM wana tamaa iliyokithiri ya uchu wa madaraka kiasi cha kulichukua fisadi eti wamelitakasa kuwawakilisha kwenye uchaguzi kisa lina upepo wa kisiasa
vyama vingine vya kisiasa, sio tu havina nguvu, vinatumika kama mitaji ya kisiasa kwa chama tawala.

Ndugu wahitimu, amkeni acheni kulia ndani ya moyo, wanatuambia tuigeuze elimu kuwa hela huku wao wakiwa wanategemea mishahara kupitia kodi zetu ni zaidi ya kututukana tena matusi ya nguoni.

kazi za wahitimu;
1)kuuza movie
2)kuuza liquid protector
3)kuuza pedi za kufua
4)kutumika madukani kwa ndugu na wazazi (wachache)
5)kujiuza (wanaita kudanga)
kuuza juice
6)kulima small scale agriculture kwa sababu ya mitaji midogo
7)wizi
na nyingine kibao ambazo hazina hadhi ya elimu waliyo nayo.

serikali ikitangaza ajira utasikia "awe na uzoefu kazini kianzia miaka miwili" kwa kazi gani mlizo tupatia? Hakika wanasiasa wametudharau sana ni wakati sasa wa kuwakataa na tamaa zao za kujifaidisha wao na koo zao.

"Mungu awatembelee mmoja baada ya mwingine, awafundishe kula kwa jasho kama watu wengine"_kwa sauti ya kala jeremiah.View attachment 2061370

Kwenye sufuria watakusikia kwa maneno tu kweli mjomba?

IMG_20211119_091739_123.jpg
 
Back
Top Bottom