Kuna wimbi limezuka yakwamba wagombea wa chadema wanatekwa na kunyang'anywa form za kugombea nafasi za ubunge na udiwani wanapoelekea kuzikabidhi kwa tume ya uchaguzi.
Kwanini ni chadema pekee na si vyama vingine?,jibu ni kwamba chadema inatafuta attention kwa nguvu, ndani ya nchi na nje katika jumuiya ya kimataifa kujionyesha wanaushawishi wakati si kweli hata kidogo.
Hili la kujiteka lipo ndani ya Chadema wenyewe.
Chadema hakina fedha za uchaguzi kuweka wagombea na wasimamizi au mawakala nchi nzima ,hili liko wazi, wanachofanya ni kutaka kuvuruga uchaguzi huu tu.
Hawakufanya vetting ya kutosha kwa wateule wa nafasi za udiwani ,ubunge na hata urais,wamekurupuka na hilo liko wazi kabisa.
Utachukuaje wagombea bila mchakato makini?, haya ndio matokeo yake . Wagombea wao Wanatelekeza nafasi zao kwa ukata ,chama hakina fedha ya uchaguzi , wakijua hawatashinda.
Wakitumia njia ya kujitoa wataonekana wasaliti kwa wafuasi wao
Njia wanayoitumia kwa sasa ni kuingia mitini kwa kisingizio cha kujiteka na huu ni upumbavu wa hali ya juu sana.
Naviomba vyombo vya ulinzi na usalama kwa kushirikiana na TCRS kubaini mwenendo huu ambao unaharibu taswira ya nchi yetu kwa makusudi kabisa.
Hili likiendelea kuachwa madhara yake ni makubwa huko mbeleni.